Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2016

Vitabu 49 Nilivyovisoma Mwaka 2016

Picha
Namshukuru Mungu nimeweza kusoma vitabu 49 kwa mwaka 2016. Nimejifunza mengi. Kusoma ni kama kupata nafasi ya kufanya mazungumzo na watu wa kila namna ya uelewa ambao kwa hali ya kawaida usingeweza kuwasikia vijiweni.  Msisitizo wangu umekuwa kwenye vitabu vinavyochambua tabia katika maeneo mbalimbali ya maisha. Hata hivyo, vipo vichache vya masuala ya imani, falsafa na dini. Sijawa msomaji wa riwaya/novel. Nikutie moyo wewe mwenye ratiba ngumu kwa siku. Unaweza kufanya maamuzi ya kusoma ikiwa utaamua kuweka ratiba yako vizuri. Nijitolee mfano mimi mwenyewe.

Siri za Watu Wanaotekeleza Maazimio ya Mwaka Mpya

Picha
TULIJADILI baadhi ya sababu zinazofanya watu washindwe kutekeleza maazimio wanayoyaweka kila mwaka mpya unapoanza. Tuliona sababu kubwa tatu; kuweka maazimio kwa msisimko tu wa kuingia mwaka mpya usioenda sambamba na tafakari ya kina; kuweka malengo mapana mno yasiyopimika; na pale malengo yanapohusisha mabadiliko ya tabia, kutokujua uliko mzizi wa mabadiliko hayo.

Namna ya Kupunguza Changamoto za Wasichana wa Kazi

Picha
TUMETAJA mambo mawili yanayobadili mfumo wa malezi. Mosi, ni kubadilika kwa majukumu ya kijinsia yaliyozoeleka katika jamii. Mama anapoingia kwenye soko la ajira na kwenda kazini kama ilivyozoeleka kwa baba, changamoto inayojitokeza ni namna wanavyoweza kumlea mtoto wao katika muda wa kazi. Pili ni kufifia kwa utamaduni wa familia tandao unaozorotesha msaada wa kimalezi uliozoeleka kutoka kwa ndugu wa karibu. Mawili haya yanalazimisha familia za sasa kutafuta namna nyingine ya malezi kuwapa fursa wazazi kuendelea na kazi.

Kwa Nini Maazimio Mengi ya Mwisho wa Mwaka Huwa Hayatekelezeki?

Picha
Kila mwaka mpya unapoanza, ni kawaida kwa watu wengi kuweka maazimio fulani ya kutekeleza. Wapo ambao huazimia kubadili tabia wasizozipenda. Wengine huazimia kuanzisha mwenendo mpya wa maisha wanayoyatamani. Wengine hufikiria kutekeleza malengo fulani ya kijamii na kiuchumi yatakayobadili maisha yao kwa mwaka unaoanza. Ingawa ukweli ni kuwa mwaka unapoanza kinachobadilika huwa ni tarehe tu, watu huwa na imani kuwa wanaingia kwenye zama za maisha mapya. Imani hiyo huambatana na jitihada za kujaribu kubadili maisha yao yaendane na zama hizo mpya. Wanasema, ‘mwaka mpya na mambo mapya!’

Jifunze Namna Bora ya Kumzawadia Mwanao

Picha
Watoto wanapenda zawadi. Namna watoto wanavyochukulia zawadi inabadilika kulingana na umri. Katika umri mdogo, mtoto huchukulia zawadi kama haki ya kupata kila akipendacho kwa wakati wowote. Mzazi anaporudi nyumbani jioni, kwa mfano, watoto hutarajia pipi bila kufanya chochote. Lakini kadri mtoto anapoendelea kukua, mtazamo wa zawadi kama haki hupungua. Mtoto huanza kufikiria zawadi kama matokeo ya kufanya kile kinachotarajiwa na mzazi. Mtoto anapofaulu mtihani, mathalani, anatarajia kitu. Unapompa kile anachokitarajia, anajenga hamasa na motisha ya kutia bidii zaidi masomoni.  

Mbinu za Kutengeneza Mtandao wa Ajira

Picha
Changamoto kubwa inayowakabili vijana wanaotafuta kazi ni namna ya kupata taarifa sahihi zitakazowasaidia kupata kazi. Ingawa vipo vyanzo vingi vya kupata taarifa hizo, watafuta kazi wengi hutegemea matangazo rasmi ya ajira pekee kupitia vyombo vya habari. Hata hivyo, tafiti za kazi na ajira zinaonyesha kuwa nafasi nyingi za kazi hasa katika sekta binafsi hazitangazwi hadharani. Waajiri wana tabia ya kutafuta mtu  anayeaminika kupitia vyanzo vinavyoaminika. Tafsiri yake ni kuwa kijana anayetegemea kupata taarifa za kazi kupitia matangazo rasmi, anapitwa na taarifa nyingi muhimu.

Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Anayefanya Vibaya Shuleni

Picha
Si jambo la kufurahisha kwa mzazi unapoona mtoto hajafanya vizuri masomoni. Unapofahamu kuwa maendeleo ya mwanao si kama vile ulivyotarajia, ni rahisi kupatwa na simanzi, wasiwasi na hasira. Ni dhahiri mzazi unatamani mtoto awe na mustakabali mzuri kimaisha. Matumaini hayo yanakufanya uchukulie kushindwa kwake masomo kama kiashiria cha kuharibika kwa maisha yake ya baadae. Hakuna mzazi angependa mtoto awe na maisha yasiyoeleweka.

Mbinu za Kushinda Maswali ya Usaili wa Kazi - 2

Picha
Katika makala yaliyopita tuliona maeneo manne muhimu ya kuzingatia unapoingia kwenye usaili. Kwamba pamoja na maswali mengine, unaweza kuulizwa maswali kuhusu uzoefu wako wa kikazi huko ulikotoka. Tuliona kuwa unapoulizwa maswali kama hayo, lengo ni kupima namna unavyoweza kuwa mkweli.

Mbinu Sita za Kukumbuka Maarifa Unayojifunza

Picha
Mafanikio ya kitaaluma, kwa kiasi kikubwa, yanategemea namna unavyoweza kusoma na kukumbuka kile ulichokisoma. Kusoma kwa bidii na kuelewa unayoyasoma ni muhimu. Lakini kama huwezi kukumbuka ulichokielewa, itakuwa vigumu kufanikiwa. Mitihani, kwa mfano, hupima uwezo wako wa kukumbuka kile unachokijua. Hiyo, hata hivyo, haimaanishi uishie kukumbuka. Unahitaji kuelewa unayojifunza kwa kina lakini pia uwe na uwezo wa kukumbuka.

Mbinu za Kushinda Maswali ya Usaili wa Kazi - 1

Picha
Kama tulivyoona katika makala yajuma lililopita , usaili ni hatua ya mwisho kuelekea kupata kazi. Sehemu kubwa ya usaili ni maswali na majibu yanayolenga kupima uwezo wako wa kukabiliana na changamoto halisi za kazi. Ingawa yapo maswali yanayoweza kukupa wasiwasi wa nia ya mwuulizaji, fahamu kuwa hakuna swali linaulizwa kwa nia mbaya au kwa bahati mbaya. Kila swali linaloulizwa linalenga kutafuta uthibitisho kuwa wewe ni mtu sahihi kwa kazi unayoomba.

Mambo ya Kuzingatia Unapojiandaa na Usaili wa Kazi

Picha
Kuitwa kwenye usaili wa kazi ni hatua ya mwisho kuelekea kupata ajira uipendayo. Mara nyingi, kazi inapotangazwa waombaji wa kazi hiyo huwa ni wengi. Baada ya kupokea maombi ya kazi, shughuli inayofuata ni kufanya uchambuzi wa kuwatambua waombaji wanaokaribia vigezo vinavyohitajika. Matokeo ya uchambuzi ni kupatikana kwa orodha ya watu wachache wanaoitwa kwa hatua ya mwisho ya uombaji wa kazi.

Mambo ya Kuzingatia Unapoandika Wasifu wa Kazi (Curriculum Vitae)

Picha
Katika mchakato wa kuomba ajira baada ya kuona tangazo la kazi, mambo matatu ni dhahiri. Mosi, huombi kazi hiyo wewe mwenyewe. Wapo watu wengi wanaoandika maombi na hivyo kuongeza ushindani wa nani atapata. Pili, nyaraka unazotuma kwa mwajiri mtarajiwa ndizo zinazojenga utambulisho wako kabla wewe mwenyewe hujafahamika. Tatu, afisa mwajiri hatatumia muda mrefu kusoma maelezo yako. Katika hali ya kawaida, atatumia dakika moja kuamua ikiwa amevutiwa na maelezo yako ama la.

Jinsi ya Kukuza Umahiri wa Lugha kwa Mtoto

Picha
Tunahitaji lugha katika maisha yetu ya kila siku. Tunapofikiri mambo yaliyopita, yaliyopo na yajayo, tunatumia lugha. Tunapowasiliana na wengine, tunahitaji lugha. Lugha, katika mukhtadha huu, ni nyezo muhimu inayotuunganisha na watu wanaotuzunguka. Ingawa wataalam wa namna mtoto anavyojifunza lugha hawana jibu moja, ni wazi zipo kanuni za matumizi ya lugha ambazo mtoto huzaliwa nazo. Lakini pia mazingira anayokulia mtoto, nayo yana nafasi kubwa ya kujenga uwezo wake wa kutumia lugha. Ndio kusema, kama mzazi unahitaji kuelewa kuwa unao wajibu mkubwa wa kumsaidia mwanao kuwa mahiri katika lugha. Kujifunza lugha kunafuata hatua kadhaa.

Mpe Mtoto Wako Fursa ya Kujifunza Maisha Halisi

Picha
Katika mazingira yetu, si wazazi wengi wanaweza kuwa tayari kuona watoto hawawezi kufanya kazi za nyumbani kama kupika, kufua nguo, kusafisha vyombo na kutandika kitanda. Lakini kutokuweza kufanya kazi hizi, wakati mwingine kunatokana na mitazamo ya wazazi kuwa kazi za ndani hufanywa na mama peke yake au msichana/kijana wa kazi na hivyo watoto hawaruhusiwi kushiriki kazi ‘zisizo zao’.

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke -2

Picha
Katika makala iliyopita , tuliona kuwa mwanamke anahitaji kujua anavyopendwa na mwenzi wake kwa maneno na vitendo. Kadhalika, tuliona mwanamke anatamani kuwa na uhakika wa nafasi ya kwanza kwa mwenzi wake. Hatamani kuona akishindana kwa umuhimu na chochote kile kinachoweza kuchukua nafasi yake kwa mwenzi wake.

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Picha
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.

Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Aweze Kushirikiana na Wenzake

Picha
Kushirikiana ni uwezo wa mtoto kuelewa watu wengine wanatarajia nini kwake. Mtoto mwenye ushirikiano na watu, ni mwepesi kutoa alichonacho, ni msikivu, hufanya kazi na wenzake, hucheza kwa ushirikiano na wenzake na huwa na uwezo wa kutafuta suluhu pale anapojikuta katika mazingira ya ugomvi.

Mbinu za Kutafuta Ajira Mtandaoni

Picha
Changamoto kubwa inayoweza kukukabili unapotafuta kazi, ni taarifa zitakazokusaidia kujua uelekeze wapi maombi ya kazi. Zamani, ili kupata taarifa za kazi, watu walitegemea radio, magazeti, televisheni na taarifa za marafiki wanaofahamiana nao. Mambo yanazidi kubadilika kwa kasi. Sasa hivi, kwa mfano, matumizi ya mtandao yamerahisisha namna tunavyoweza kupata taarifa hizi. Hata hivyo, pamoja na uwepo wa mtandao, bado kuna changamoto ya wapi hasa waweza kupata taarifa sahihi. Mbinu zifuatazo ni matokeo ya uchambuzi wa tafiti mbalimbali na zinaweza kukupunguzia changamoto ya kupoteza muda na nguvu nyingi kutafuta kazi mtandaoni.

Mambo Matano Yanayoweza Kukusaidia Kupata Muda wa Kuwa Karibu na Mtoto

Picha
Wazazi wengi wanapenda kuwa karibu na watoto  kwa lengo la kuwajengea mazingira ya kujifunza. Changamoto, hata hivyo, ni kukosa muda wa kutosha kufanya hivyo. Kwa mfano, ni kawaida kwa wazazi kutoka nyumbani alfajiri na kurudi usiku wakati ambao tayari watoto wameshalala. Matarajio makubwa ya kikazi yamekuwa kipaumbele na hivyo tunatumia muda mwingi kufanya kazi ambazo kimsingi ndizo zinazotusaidia kuwatunza watoto wetu.  Hata hivyo, majukumu  yetu haya muhimu yanatufanya wakati mwingine tukose muda wa kuwasaidia watoto kihisia, kiufahamu na hata kimahusiano kama tunavyotamani. Makala haya yanajadili hatua tano za kuchukua ili kukusaidia mzazi kupata muda wa kuwekeza katika malezi ya watoto wako.

Unatafuta Kazi? Sifa Sita Unazozihitaji

Picha
Katika makala yaliyopita tuliona takwimu zinazothibitisha kuwa tatizo la ajira ni zaidi ya kukosekana kwa nafasi za kazi. Ingawa watafuta kazi wengi hufanya juhudi za kuthibitisha kuwa wanao ujuzi rasmi waliousomea darasani, si waajiri wengi wanathamini alama za darasani zinazoonekana kwenye vyeti vya waombaji hao. Badala yake, mwajiri kwa kawaida hutafuta ujuzi ambao mara nyingi mtafuta kazi hautegemei. Ujuzi huo, tulioupachika jina la ‘ujuzi mwepesi’, ni pamoja na ule uwezo wa kutumia maarifa ya jumla ya darasani katika kufumbua matatizo halisi yanayomkabili mwajiri katika eneo lake la kazi.

Mambo Sita ya Kufanya Unapotafuta Kazi

Picha
Kutafuta kazi ni kuingia kwenye soko la ajira ambalo kimsingi ni uwanja unaowakutanisha watu wenye mahitaji makubwa ya aina mbili. Upande mmoja, wapo watu wenye ‘bidhaa’ ya ujuzi na weledi, lakini wenye hitaji la kujipatia kipato kwa kutumia ujuzi na maarifa waliyonayo. Hawa wanaitwa watafuta kazi.

Jinsi ya Kumfundisha Mtoto Kuwa Mwuungwana

Picha
Umewahi kumpa mtu kitu anachokihitaji lakini haoni sababu ya kusema, ‘asante’? Mtu anakukosea na hawezi kusema, ‘samahani’, ‘nisamehe’? Wapo wengine hata ufanye vizuri namna gani kusema, ‘hongera umefanya vizuri’ ni kama adhabu na kujishushia hadhi. Hizi ni baadhi ya tabia zinazoweza kuonesha namna mtu asivyo muungwana na zinaweza kumpunguzia thamani yake mbele ya jamii.

Unaweza Kumfundisha Mtoto Adabu Bila Kumchapa

Picha
Mjadala wa fimbo na malezi una historia ya mjadala mkali. Fimbo, kwa hakika, zimekuwa kama sehemu ya maisha yetu . Takwimu zinathibitisha hali hii. Kwa mfano, asilimia zaidi ya 80 ya wazazi wa nchi zinazoendelea wanatumia fimbo angalau mara moja kwa mwezi. Ndio kusema, vipigo kwa watoto vimekuwa sehemu ya malezi katika nchi zetu hizi. Matumizi haya makubwa ya fimbo kwa kiasi fulani yanatokana na imani waliyonayo wazazi kuwa bila mtoto kusikia maumivu hawezi kurekebisha tabia wala kuwa msikivu. Ingawa hakuna ushahidi wowote kuwa viboko vinasaidia kujenga nidhamu kwa watoto, bado wazazi wengi wanaamini adhabu ya fimbo ndiyo jibu la kumnyoosha mtoto.

Namna Michezo Inavyomsaidia Mtoto Kujifunza

Picha
Wazazi wengi wanaichukulia michezo ya watoto kama shughuli isiyo na maana. Kimsingi, ipo imani inajengeka kuwa kucheza ni kupoteza muda. Matokeo yake wazazi hujitahidi kuwazuia watoto wasicheze kwa matumaini ya kuwasaidia wapate muda wa kufanya mambo ya maana zaidi kama vile kusoma na kukamilisha kazi za shule. Pamoja na umuhimu wa kufanya hivyo, hata hivyo, michezo  inabaki kuwa shughuli yenye umuhimu mkubwa katika ukuaji wa jumla wa mtoto kimaarifa, kimahusiano, kimwili na kihisia.

Wajibu wa Mzazi Kama Mwalimu wa Kwanza wa Mtoto

Picha
Tafiti nyingi za mazingira ya kujifunzia zimeendelea kusisitiza kuwa elimu bora kwa mtoto huanzia nyumbani. Kuwepo kwa mazingira rafiki ya kielimu nyumbani kunampa mtoto nafasi ya  kukua kiufahamu na humuandaa vyema kujifunza kabla hajaanza shule rasmi. Kimsingi, mzazi ndiye mwalimu wa kwanza anayemwezesha mtoto kujifunza vizuri. Mtoto hujifunza kutembea, kuongea, kujilisha, kazi za nyumbani na kadhalika kwa msaada wa mzazi. Ikiwa mzazi atatambua wajibu wake kama mwalimu wa mtoto na akautekeleza ipasavyo, kazi ya mwalimu shuleni hurahisishwa.

Mambo ya Manne ya Kufanya Mtoto Akusikilize, Akuheshimu

Picha
Msomaji mmoja wa safu hii aliniandikia hivi majuzi akidai mwanae hamsikilizi. Kwa mujibu wa mzazi huyu, pamoja na kufanya jitihada za kumwelekeza mwanae mambo muhimu ya kimaisha, bado kijana wake huyo haonekani kusikiliza. Anasema, kadri anavyomwadhibu mwanae, ‘ndivyo anavyozidi kuwa mkaidi…’ Mzazi huyu, inavyoonekana, amepoteza mamlaka yake kama mzazi. Mamlaka kimsingi ni uwezo wa kusema kitu na kikasikika bila kulazimika kutoa adhabu. Unapokuwa na mamlaka maana yake unayo nguvu ya ushawishi inayomfanya mtoto awe tayari kukuiga, kukusikiliza, kukuelewa na kufanya kwa hiari yake yale unayomwelekeza.

Mwaka Mmoja Bila Mama, Mkono wa Mungu Haujatuacha…

Picha
Nakumbuka mwezi Juni 2002, nikiwa mwanafunzi wa sekondari, eneo ni stesheni ya gari moshi (treni) mjini Singida nikiwa ninarudi nyumbani nikitokea Dodoma. Ilikuwa ni safari ya kuunga unga iliyoanzia Dar es Salaam kupitia Dodoma na kisha Singida. Wakati huo tulikuwa tunaondoka Dodoma saa nne asubuhi, Singida tunafika saa za jioni kuanzia saa kumi na moja hivi tukiwa taabani kwa uchovu wa kukaa kwenye mabehewa yaliyoonekana kuhangaika mno kupita kwenye mataruma katikati ya vichaka ya Dodoma na Singida. Jioni hiyo ninayoikumbuka vyema tulichelewa kidogo na hatimaye tulifika Singida stesheni saa kumi na mbili unusu hivi za jioni.

Kanuni za Kuongeza Ushawishi wa Hoja Zako

Picha
Kwa nyakati tofauti kila mmoja wetu hutamani kuwa na ushawishi kwa wengine. Ni kawaida, kwa mfano, kutamani hoja tunazozitoa zipokelewe na wale tunaowatumia ujumbe husika. Ili ujumbe upokelewe, inahitajika nguvu inayoweza kuwasukuma wengine kuupenda, kuubali na ikiwezekana kubadilika kwa sababu ya ujumbe husika. Nguvu hii inaitwa ushawishi.

Jenga Fikra Chanya, Uwe na Furaha

Picha
Kuwa na furaha ni uamuzi wako mwenyewe. Furaha ni matokeo ya namna ulivyoamua kufikiri. Kadhalika, kukata tamaa na kukosa amani mara nyingi ni matokeo ya kufikiri mambo yanayokatisha tamaa na wakati mwingine tusiyo na majibu yake. Tunatafsiri vibaya mambo tunayokutana nayo na ndiyo sababu tunapatwa na msongo wa mawazo.

Kumfundisha Mtoto Kuwajibika, Kufanya Kazi

Picha
Kumjengea mtoto uwezo wa kuwajibika ni wajibu muhimu sana wa wazazi. Bila kuweka mkazo mapema katika kukuza uwezo huu, mtoto anaweza kuwa mtu mzima asiyefahamu kufanya majukumu mengi ya msingi na ya kawaida. Mtoto aliyefundishwa kuwajibika hujiona ana wajibu wa kushiriki shughuli za ndani bila kujali jinsia yake.  Katika makala haya, tunaangalia namna unavyoweza kumsaidia mtoto wako kujifunza kuwajibika angali mdogo na hivyo kujenga uwezo wa kumudu majukumu ya msingi kadri anavyoendelea kukua.

Kujenga Uwezo wa Kufanya Maamuzi kwa Mtoto

Picha
Unajisikiaje mzazi unapogundua mtoto ameanza kujifunza tabia zisizofaa? Inaumiza, kwa mfano, kuona mtoto anaanza kujifunza wizi, kudanganya na hata kutokuwa na uwezo wa kujisimamia mwenyewe bila uangalizi wa karibu.   

Kumsaidia Mtoto Kujifunza, Kumudu Lugha -2

Picha
Makala yaliyopita yalipendekeza njia nne za kumsaidia mtoto mdogo kujua kuongea. Kadhalika, tuliona hatua kuu anazopitia mtoto katika kujifunza lugha. Katika makala haya, tunamtazama mtoto anayejua kuongea na tunaangalia mapendekezo kadhaa ya kumsaidia kuwa mtumiaji mahiri wa lugha katika mawasiliano yake ya kila siku.

Tunavyoweza Kuacha Tabia ya Kuhukumu Wengine

Picha
Majuzi nikiwa kwenye mgahawa mmoja mjini, waliingia watu wawili wanaume waliokuwa wamevalia mavazi yanayoashiria imani yao ya kidini. Wote wawili walipamba vichwa vyao kwa vilemba nadhifu, mmoja wao akibeba mfuko mdogo mweusi. Nyuso zao, kwa hakika zilipambwa na tabasamu pana la kirafiki lililofanya ndevu zao ndefu ziwe na mwonekano wa kupendeza. Miguu yao ilivaa viatu vya wazi na juu yake zilining’inia suruali fupi mithili ya kaptula ndefu zilizojitokeza ndani ya kanzu fupi nadhifu.

Kwa Nini Tunapenda Kusikia Habari Mbaya?

Picha
Umewahi kujiuliza kwa nini habari tunazofuatilia kwenye vyombo vya habari mara nyingi ni matukio mabaya? Kwamba ili iwe habari yenye kuvutia watu wengi mara nyingi hulazimu iwe habari ya jambo lisilotarajiwa. Kwa mfano, habari za mbunge kulala wakati kikao cha bunge kikiendelea inaweza kuwa na mvuto kuliko habari ya namna mbunge huyo huyo alivyotekeleza wajibu wake kabla ya ‘kupitiwa na usingizi.’

Kumsaidia Mtoto Kujifunza na Kumudu Lugha

Picha
Lugha ni nyenzo muhimu sana tunayoihitaji katika maisha. Hatuwezi kufikiri vizuri, kuongea kwa ufasaha, kusikiliza, kueleza mambo tuliyokutana nayo na hata tunayoyatarajia siku zijazo bila kuhitaji lugha. Ni wazi tunalazimika kutumia maneno au ishara kuwasiliana na wanaotuzunguka. Mjadala wa namna gani mtoto hujifunza lugha ya mama una historia ndefu. Kwamba mtoto huzaliwa na asili ya lugha inayoongoza namna anavyojifunza lugha au ni mazingira anayokulia ndiyo yanayomwezesha kujifunza, ni vigumu kuhitimisha kwa hakika. Hata hivyo, kuna ukweli kwamba ili mtoto ajifunze lugha ipasavyo anahitaji kuwa na uwezo fulani anaozaliwa nao unaomwezesha kuelewa kanuni muhimu za lugha bila msaada mkubwa. Lakini pia mazingira, anayokulia mtoto, nayo yana nafasi kubwa ya kumwezesha kujifunza na kumudu lugha ya kwanza kirahisi.

Kuanzisha na Kuimarisha Urafiki wa Karibu

Picha
Katika zama hizi za maendeleo ya kidijitali, ni rahisi sana kufahamiana na watu wengi ambao, hata hivyo, wanaweza wasiwe marafiki. Unaweza, kwa mfano, kuwa na ‘marafiki’ elfu tano kwenye mitandao ya kijamii, lakini usiwe na rafiki hata mmoja katika maisha halisi. Marafiki wa kweli na wa karibu ni moja wapo ya mahitaji muhimu katika maisha. Tunaweza kuwa na sababu nyingi kuhalalisha kwa nini hatuna (haja na) marafiki wa karibu.  Hata hivyo, zipo nyakati  hufika tukajikuta katika maisha yenye kujaa upweke  na msongo wa mawazo kwa sababu hatukutumia muda wetu kutengeneza urafiki wa karibu na watu tunaofahamiana nao.

Kujenga Tabia ya Kusoma kwa Watoto Wadogo

Picha
Kusoma si tabia nyepesi kuijenga katika mazingira ambayo masimulizi na mazungumzo ni vyanzo vikuu vya maarifa kuliko maandishi.   Tumelelewa katika utamaduni usiosisitiza sana umuhimu wa kusoma. Lakini, hata hivyo, hatuwezi kukwepa kusoma katika ulimwengu huu unaotulazimisha kuyasaka maarifa kwa njia ya maandishi.

Umuhimu wa Kujenga Tabia ya Kujitolea

Picha
Kujitolea ni kutoa sehemu ya muda wako, ujuzi na maarifa uliyonayo na wakati mwingine nguvu zako kufanya kazi ya watu wengine bila kupata malipo ya moja kwa moja. Kazi unayoifanya kwa kujitolea mara nyingi ungeweza kuifanya kwa kudai ujira lakini unaamua kuifanya bure.  Mathalani, mwajiriwa anayetamani kuleta mabadiliko nje ya ajira yake, anapotumia ujuzi wake kufanya kazi za jamii bila kudai malipo, anakuwa amejitolea. Tuangalie kwa mhutasari kwa nini ni muhimu kujenga tabia ya kujitolea.

Kipimo cha Kujitambua ni Tunavyowatendea Tusiowajua, Wasioheshimika

Picha
Mjema anaandika ripoti inayohitajiwa na mkuu wake wa kazi. Wakati muda wa kukabidhi ripoti hiyo ukikaribia, anapigiwa simu na mtu asiyemfahamu. Mjema hajui ni nani hasa anayemtafuta muda huo hivyo anaamua kupokea simu. Bahati mbaya aliyempigia simu hasikiki vyema. Mjema anahisi labda ni tatizo la mtandao, anaamua kuikata mara moja.

Kujitambua ni Kushinda Ubinafsi, Kujali Mahitaji ya Wengine?

Picha
Tulianza kudodosa suala la kujielewa katika makala yaliyopita . Kama tulivyodokeza, kujielewa kunakwenda sambamba na kuelewa msukumo ulio nyuma ya yale tuyatendayo kila siku. Katika sehemu hii, tutaangalia kwa ufupi kwa nini kujitambua ni zaidi ya ule ‘ubinafsi’ unaoishi ndani yetu.

Makundi Manne ya Tabia za Watoto Kitabia

Picha
Ingawa ni kweli tunazaliwa na sehemu ya tabia tulizonazo, upo ukweli wa kiutafiti unaothibitisha kwamba mazingira ya kimalezi yana nafasi kubwa katika kujenga tabia za mtu. Ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili, mathalani, unatawaliwa zaidi na uasili ambao kwa kiasi kubwa hatuna mamlaka nao. Hata hivyo, ukuaji wa kihisia na kimahusiano unatawaliwa zaidi na mazingira ya kimalezi ambayo tayari tuliyaona kwenye makala iliyopita .

Tuyafanyayo ni Matokeo ya Tujionavyo

Picha
Ungeulizwa swali, ‘wewe ni nani’ ungejibuje? Wengi tungetaja majina yetu kwa kuamini ‘sisi’ ni majina yetu. Wengine tungetaja kazi zetu kwa sababu kwetu majukumu ndio utambulisho wetu. Sisi ni nani basi? Kwa hakika swali hili si jepesi lakini linatuwezesha kuelewa tabia zetu. Karibu kila tunachofanya ni matokeo ya vile tujionavyo. Katika makala haya, tutaangazia  mitazamo michache inayoweza kutusaidia kutafakari swali hilo. 

Mazingira Manne ya Kimalezi Yanayotengeneza Tabia za Watoto

Picha
Watafiti wa makuzi na malezi wanasema mtoto anahitaji mazingira yanayomchangamsha kihisia, kiakili, kimwili na kimahusiano. Anapochangamshwa vyema, tunaambiwa, mtoto hujisikia utulivu wa moyo unaomfanya awe karibu na wazazi na watu wengine wanaomzunguka. Anapokosa kuchangamshwa, mtoto hujenga uduwavu unaojenga tabia za kujilinda na uchungu wa kujiona anapuuzwa. Katika makala haya, tunaangazia mambo manne yanayoweza kumchangamsha mtoto kihisia na kimahusiano na hivyo kutengeneza tabia na mitazamo yake.

Kuanza Kupotea kwa Desturi ya Ukaribu wa Kifamilia Kunavyoathiri Malezi

Picha
Malezi katika mazingira yetu ya ki-Afrika ni suala nyeti. Kwa kutambua umuhimu wa malezi katika kujenga jamii yenye ustawi, wa-Afrika tumekuwa na desturi ya kuelekeza nguvu zetu nyingi katika malezi ya wanetu. Kwa mfano, tangu mtoto anazaliwa, ilikuwa ni lazima alale kitanda kimoja na wazazi wake kwa muda unaozidi miaka miwili. Mtoto mchanga hakuachwa alale kwenye kitanda chake mapema kwa sababu za msingi zilizokubalika katika jamii zetu.

Nani Awezaye Kutuletea Mabadiliko Tunayoyataka?

Picha
Ukisikiliza mazungumzo ya wa-Tanzania  –iwe vijiweni, mitaani, mitandaoni ama kwingineko –ni wazi wengi wetu tunayo hamu ya mabadiliko. Tuna shauku ya zama mpya. Shauku hiyo ya mabadiliko imetufanya wengi wetu tutumie muda mwingi kutafuta watu tunaohisi ‘wanatukwamisha.’ Ni hivyo kwa sababu tumejijengea dhana kwamba ili kupata mabadiliko tunayoyataka tunahitaji watu maalum wenye uwezo wa ‘kutuletea maendeleo’. Kwa hiyo ni kama tunasubiri wakombozi fulani fulani waje kutubadilishia mfumo tunaoamini ndio tatizo.

Madikteta wa Familia Tunaweza Kudai Demokrasia?

Picha
Madai kuwa baadhi ya watawala wetu wa ki-Afrika ni madikteta hayashangazi. Inasemekana watawala hawa  hawasikilizi maoni ya watu wanaowaongoza, hawashauriki wakati mwingine na watu walioteuliwa kuwashauri, wanaminya uhuru wa maoni/kujieleza na kadhalika. Madai haya yanaonekana kuwa ni matamanio ya wananchi kuwa na serikali zinazoheshimu demokrasia -nguvu ya wananchi kushiriki katika uongozi/utawala wa taifa lao kwa kuamua utaratibu gani utatumika kujitawala na nani anaweza kupewa jukumu la kuwaongoza. Haya yote yanadai ushirikishwaji wa wananchi kwa kukuza uhuru wa kila raia kusema/kutoa maoni na kadhalika.