Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2008

Udhaifu wa sayansi (1)

Haya tuendelee. Tunahitaji aya nyingi kufafanua dhana ya sayansi. Kwanza nijitete kwamba sina msamiati wa kutosha kukwepa maneno yanayoitwa ya kisayansi ila nitajaribu kadiri niwezavyo. Kwa uchache sana, na katika lugha rahisi zaidi, sayansi ni namna ya upatikanaji wa maarifa kwa njia ya utafiti. Utafiti hapa humaanisha majaribio ambayo hukusudiwa kuchunguza na hatimaye kuthibitisha ama kukanusha bashiri ya kisayansi. Sayansi hutumia mbinu katika kuchunguza dhana, ili kuongeza maarifa ama kurekebisha maarifa yaliyopo. Huanzia katika ukusanyaji wa ushahidi unaochunguzika, unaopimika, na wenye chanzo mahususi kinachokubaliana na ufahamu wa kawaida. ( Sina masamiati sahihi sana ). Ushahidi huo, ndio kile kinachoitwa data, ambazo hupatikana kwa majaribio ambapo bashiri hujengewa hoja ili kufanyika maelezo ya dhana iliyokuwa ikichunguzwa. Majaribio haya hupangiliwa kitaalamu kwa kutumia vibadiliko (variables) ili kuzijaribu bashiri za awali. Majaribio haya hufanyika katika ma

Utangulizi wa hoja: Tumetokea wapi?

Kujielewa ninakokuzungumzia, kunahusisha na uelewa wa mambo kadhaa yanayoaminika kuongoza maisha ya viumbe katika ulimwengu ( pamoja na dunia) tunamoishi. Kwamba sisi binadamu tulitokea wapi na tunatafuta nini hapa duniani. Huko ni kujielewa. Ulimwengu na viumbe vilitokea wapi? Swali kama hili si rahisi sana, pamoja na umuhimu wake katika kujielewa. Yapo mawazo mengi yanayojaribu kutafuta uhalali wa fikra kadha wa kadha kuhusu chanzo hasa cha ulimwengu wenyewe pamoja na uhai na maisha ya viumbe hai na visivyo hai katika ulimwengu huu. Mawazo haya yanaweza kuganywa katika makundi makubwa mawili: Wanaoamini zaidi pasipo ushahidi, na wanaojaribu kutumia akili zao katika kutafuta ushahidi wa mambo haya. Wale wa kwanza, kwa wingi wa idadi, ni wanadini. Wale wa pili, ni wanasayansi. Mwanadini, anatafuta kujenga imani zaidi hata kama haielezeki. Mwanasayansi anatafuta ushahidi unaoelezeka. Katikati ya hao wawili, wapo wengine ambao kazi yao ni kuhoji uhalali wa mahitimisho yanay

Laiti ningeweza kuisemea nafsi vizuri!

Natamani sana kuandika kila siku. Natamani ningekuwa na shughuli moja tu ya kusema yaujazayo moyo. Kusema na kusema. (Hakuna kitu nafurahia kama kuyatoa yaliyopo moyoni). Huwezi kuyatoa kama hayapo huko yanakodhaniwa kutokea. Huwezi kusema kama huna cha kusema. Huwezi kuandika kama huna cha kuandika. Mimi nina agenda moja kubwa: Kujielewa. Natafuta namna nzuri ya kuiweka agenda hii mahala pale. Kuisema mpaka isemeke. Lakini tatizo kubwa ninalokabiliana nalo ni mwingiliano wa majukumu. Majukumu mengine hayasubiri kama ambavyo wengi wetu tunajua. Majukumu ya kitumwa tumwa hivi, kwamba tuwasikilize wenzetu watujaze yale yanayoitwa maarifa yapatikanayo katika taasisi ziitwazo 'shule'. Nadhani hatujafika mahala tukakubaliana kwamba majukumu haya yanaweza kusubiri. Hivyo ninawajibika kwayo, walau kwa sasa. Pamoja na ukosefu wa muda (hivi kweli ni ukosefu ama udhaifu wa mpangilio wa muda?) wa kubwabwaja hapa, huwa nafidia kwa kujibwabwajia mwenyewe. Nadhani kujisemea kuna nguvu

Unaujua uongo wa Charles Darwin?

Picha
Charles Darwin ni yule jamaa aliyepata kuandika ile nadharia maarufu ya "Natural Selection" . Nadharia hii kwa muda mrefu imekuwa ikiaminika kutoa maelezo ya kweli kuhusu namna viumbe vilivyoweza kuwa hivi vilivyo leo hii (organic evolution). Kwamba viumbe havikuumbwa bali vilibadilika kwa kile kinachoitwa kwa kadiri ya Darwin "struggle for existance" na " survival for the fittest". Katika kuipitia pitia, hatimaye nimebaini uongo uliojikita katika nadharia hiyo inayoonekana kulazimisha kuukana uwepo wa Mungu pasipo hoja inayojitosheleza. Lengo la kuyaandika haya, ni kusema wazi kwamba pamoja na akili alizokuwa nazo huyu jamaa, kwangu mimi (Darwin) ni mwanasayansi mwongo (na wa kuandikiwa kitabu kabisa kabisa). Kwa sababu hiyo, nitaandika baadae uongo huo ulivyo wa wazi.

Mazoezi ya kusikiliza wanafunzi wangu

Miezi kadhaa nilikuwa nawafundisha (soma kuwasikiliza) wanafunzi fulani. Niliwapenda vijana wale. Kuna siku nitasimilia zaidi habari zao. Nilibahatika kuwafundisha ile mada katika Biolojia ambayo (ikifundishwa vyema) huwafanya wanafunzi wajifunze kufikiri. Mada yenyewe inaitwa organic evolution. Basi. Mimi ni kati ya wanaoamini kuwa kazi ya mtu aitwaye mwalimu si kufundisha bali kuongoza mijadala. " Mnafikiri viumbe na kila kilichomo katika dunia pamoja na dunia yenyewe vilitokea wapi?" Niliwauliza. Bila shaka unaweza kuelewa walijibu nini. " Sasa (Mungu) aliumbaje viumbe?" Nikawauliza. Mmoja akajibu kwa haraka: " Kwa nguvu zake(Mungu)...maana anao uwezo wote" Maneno mengine siyakumbuki. Kufupisha ilibidi nijie kwa njia hii: " Kwani huyo mnaye mwita Mungu alitokea wapi?" Wakashangazwa sana na swali la kijinga namna ile. Hawakulitazamia kutoka kwa mtu waliyemheshimu kama mimi. Mwalimu wa mazoezi. Huku nikijua kabisa wanahangaika kunilewa,