Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Sheria ya Mtoto

Je, Shule za Bweni Zinafaa kwa Malezi ya Watoto Wadogo?

Picha
PICHA: SOS Schools Ongezeko kubwa la shule za bweni kwa watoto wadogo ni kiashiria kimoja wapo cha mabadiliko ya kijamii yanayoendelea kuathiri desturi za malezi. Pamoja na changamoto zake, mzazi anapofanya maamuzi ya kumpeleka mwanae shule ya bweni huamini anafanya hivyo kwa faida ya mtoto.

Tunavyoweza Kuboresha Vituo vya Malezi

Picha
PICHA: John-Paul Iwuoha MALEZI katika vituo vya kulelea watoto hayakwepeki. Katika mazingira ambayo wazazi wanafanya shughuli zao mbali na nyumbani kituo cha malezi kinakuwa msaada. Tafiti za malezi zimekuwa zikijaribu kuangalia namna gani huduma hizi zinavyoweza kuboreshwa. Moja wapo ya mashirika maarufu katika eneo hili ni   Taasisi ya Marekani ya Mtandao wa Afya ya Mtoto na Maendeleo ya Utafiti wa Malezi ya Watoto (NICHD) .

Unayopaswa Kuzingatia Unapompeleka Mtoto Wako Katika Vituo vya Malezi -1

Picha
PICHA: Hope for Bukasa UTARATIBU wa wazazi kuwapeleka watoto kwenye vituo vya malezi umeanza kuwa maarufu hapa nchini. Karibu kila mji mdogo katika mikoa yote vipo vituo kadhaa mahususi kwa ajili ya kuwatunza watoto wakati wazazi wao wakiwa kazini. Kinachofanya huduma ya malezi ya vituoni kuwa maarufu ni changamoto za akina dada wa kazi, ambao mara nyingi, huwa ni wadogo kiumri na hawana uwezo wala ari ya kuwalea watoto vizuri.

Wajibu wa Mzazi kwa Mtoto Kisheria -2

Picha
SHERIA ya Mtoto Na. 21 ya 2009 inamtambua mtoto kama mtu yeyote mwenye miaka pungufu ya 18. Sheria hii ilitungwa kukidhi matakwa ya makubaliano na mikataba ya kimataifa inayolenga kulinda haki, maslahi na ustawi wa mtoto.

Wajibu wa Mzazi kwa Mtoto Kisheria

Picha
Tumeshuhudia matukio mengi katika jamii yetu ya watoto kunyanyaswa na kudhalilishwa na watu wazima wakiwemo walezi na hata baadhi ya wazazi wasio waadilifu. Imekuwa kawaida kusikia watoto yatima wakitendewa vitendo vya uonevu baada ya wazazi wao kufariki. Ndugu na jamaa, bila haya, wamekuwa wakifanya maamuzi yanayowahusu watoto bila kuzingatia maslahi na haki za watoto.