Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Usomaji wa Vitabu

Kuuishi Wito Wako, Unahitaji Nidhamu ya Kujifunza

Picha
PICHA: findingmastery.net/ Nimekutana na vijana wengi wanaotaka niwaonyeshe njia ya mkato ya kufanya kazi za ndoto zao. Wanafikiri kupata kazi inayoendana na vipaji na tabia zao ni jambo la siku moja. Ingawa huwa ninawasaidia kujiuliza maswali ya msingi yanayowachochea kugundua hazina iliyolala ndani yao, bado husisitiza umuhimu wa kuwa na mtazamo mrefu wa kuona yasiyoonekana kwa macho. Nitatumia mfano wa Robert Green, mwandishi nimpendaye aliyeandika vitabu maarufu vya ‘The 48 Laws of Power, ‘Mastery’ na ‘The Art of Seduction.’ Ingawa tangu akiwa mdogo aligundua alitaka kuwa mwandishi, Robert hakuwa na uhakika anataka kuandika masuala gani.   Baada ya kumaliza chuo, Robert alianza kufanya kazi kama mwandishi wa habari. Kazi hiyo, hata hivyo, haikumwendea vizuri. Mhariri wake alimshauri, ‘Tafuta kazi nyingine ya kufanya. Wewe si mwandishi. Hujui kupangilia mawazo yakaeleweka. Nakushauri ukatafute maisha mengine.” Robert anasema alijisikia vibaya kwa ...

Vitabu Nilivyosoma kwa Mwaka 2017!

Picha

Mwalimu Anavyoweza Kukuza Udadisi kwa Wanafunzi

Picha
PICHA: OBrown & Associates Education Consulting Mara nyingi tumesikia watu wakilaumu mtalaa wetu kwamba unafunga fahamu za wanafunzi wetu. Wenye madai haya wanafikiri bila mtalaa kufanyiwa marekebisho makubwa, haiwezekani elimu yetu ikamnufaisha mwanafunzi. Hata hivyo, tulisema wiki iliyopita, kazi ya mtalaa ni kutoa diraya jumla ya aina ya raia wanaotarajiwa kufundwa kupitia mtalaa husika.

Wajibu wa Mzazi kwa Mtoto Kisheria

Picha
Tumeshuhudia matukio mengi katika jamii yetu ya watoto kunyanyaswa na kudhalilishwa na watu wazima wakiwemo walezi na hata baadhi ya wazazi wasio waadilifu. Imekuwa kawaida kusikia watoto yatima wakitendewa vitendo vya uonevu baada ya wazazi wao kufariki. Ndugu na jamaa, bila haya, wamekuwa wakifanya maamuzi yanayowahusu watoto bila kuzingatia maslahi na haki za watoto.

Vitabu 49 Nilivyovisoma Mwaka 2016

Picha
Namshukuru Mungu nimeweza kusoma vitabu 49 kwa mwaka 2016. Nimejifunza mengi. Kusoma ni kama kupata nafasi ya kufanya mazungumzo na watu wa kila namna ya uelewa ambao kwa hali ya kawaida usingeweza kuwasikia vijiweni.  Msisitizo wangu umekuwa kwenye vitabu vinavyochambua tabia katika maeneo mbalimbali ya maisha. Hata hivyo, vipo vichache vya masuala ya imani, falsafa na dini. Sijawa msomaji wa riwaya/novel. Nikutie moyo wewe mwenye ratiba ngumu kwa siku. Unaweza kufanya maamuzi ya kusoma ikiwa utaamua kuweka ratiba yako vizuri. Nijitolee mfano mimi mwenyewe.

Kujenga Tabia ya Kusoma kwa Watoto Wadogo

Picha
Kusoma si tabia nyepesi kuijenga katika mazingira ambayo masimulizi na mazungumzo ni vyanzo vikuu vya maarifa kuliko maandishi.   Tumelelewa katika utamaduni usiosisitiza sana umuhimu wa kusoma. Lakini, hata hivyo, hatuwezi kukwepa kusoma katika ulimwengu huu unaotulazimisha kuyasaka maarifa kwa njia ya maandishi.

Unauelezaje utamaduni wa kusainiwa kitabu na mwandishi?

Picha
Profesa Mbele anaeleza vizuri kuhusu utamaduni wa kusainiwa vitabu katika blogu yake:  "...Suala hili la kusaini au kusainiwa vitabu linastahili  kutafakariwa. Naamini lina vipengele kadhaa muhimu, kama vile kiutamaduni, kisoshiolojia, kisaikolojia, na kifalsafa. Hata katika maduka ya vitabu hapa Marekani, aghalabu utaona vimepangwa vitabu vya mwandishi vikiwa na ujumbe "Signed copy." Jambo hili linaisukuma akili yangu kutaka kulielewa zaidi. Ningependa kujifunza zaidi kuhusu suala hili, kwa kusoma maandishi mbali mbali na kufanya tafakari mwenyewe..."  Msomaji wa kitabu cha Profesa Mbele, akifurahia nakala ya kitabu. Picha: @hapakwetu Unaweza kusoma zaidi kwenye blogu yake hapa . Kama mmoja wa wasomaji waliowahi kupata bahati ya kusainiwa kitabu na mwandishi mwenyewe, mmoja wapo akiwa Profesa Mbele, mwandishi wa kitabu kizuri cha " Africans and Americans Embracing Cultural Differences ", nikiri kabisa kwamba suala hili lina muujiza wa aina...

Shukrani za pekee kwa Prof. Mbele kwa zawadi ya thamani!

Picha
'Africans and Americans Embracing Cultural Difference', ni kitabu kizuri nilichokisoma kwa mara ya kwanza Aprili, 2009 nilipokiona katika duka la vitabu KIMAHAMA, Arusha. Ilikuwa ni baada ya kukisikia kikisemwa na rafiki yangu mmoja. Ni miaka mitano imepita, lakini kitabu hiki hakikuwahi kuizoea maktaba yangu tangu wakati huo. Kusoma kitabu chenye saini ya mwandishi, si jambo linalowatokea wengi. Ni muujiza ulionitokea. Picha: Jielewe Kwanza, kwa rafiki zangu wasomaji waliofika kwangu kwa mazungumzo ya vitabu na waandishi, kitabu hiki hakikukosekana kwenye mazungumzo hayo. Na kila aliyesikia sifa zake, alipenda kuthibitisha ikiwa nilisema  kweli kwa kukiazima. Kiliazimwa na wasomi, wasafiri, waongozaji wa watalii (tour guide), wapenda maarifa, kutaja kwa uchache. Ni bahati mbaya sana kwamba hakikuwa kinapatikana katika baadhi ya maeneo. Hivyo, kiliazimwa, na kuazimwa, tena na tena kwa muda wa miaka miwili. Mwaka 2011, kiliondoka rasmi kwenye maktaba yangu. Nilikuja k...

Blogging Revolution: Shubiri kwa wajiitao serikali

Picha
Kitabu kizuri kinachoangazia mabadiliko ya kijamii na kisiasa yaliyoletwa na matumizi ya zana za uandishi wa kiraia hususani blogu.  Kinatazama namna blogu zilivyochangia Mapinduzi yanayoendelea katika nchi za kiarabu –maarufu kama Arab Spring – na jinsi ambavyo blogu hizi zinaanza kuwatia hofu watu wanaojiita serikali.

Umemsoma Dambisa Moyo?

Picha
Kama una mpango wa kusoma kitabu kimoja tu mwaka huu, napendekeza hiki cha Dambisa Moyo kiitwacho "How the West was Lost". Ukikisoma utaelewa zaidi kwa nini hawa watawala wanaoitwa "The darling of the west" wanaopigana vikumbo kuhudhuria mkutano wa G8, wamepotea njia. Anacho kingine alichokiandika kabla ya hiki, kiitwacho cha Dead End, bado nakitafuta. Naambiwa ni moto.

CHANGAMOTO Insha za Jamii - Prof. Mbele

Picha
Natamani sana kukisoma kitabu hiki. Ninakitafuta kwa bidii. Unajua kinakopatikana? Mwandishi Profesa Mbele anasema kakiandika kusahihisha majungu kuhusu Mwalimu Nyerere. Msome hapa halafu uone kama unaweza kujishindia Dola 100! Waweza pia kusoma majadiliano katika Jamii Forums yanayodurusu ikiwa wanaomkosoa Mwalimu Nyerere wana hoja.

Take the Risk cha Ben Carson

Picha
Ndio kwanza nimeanza kukisoma. Take the Risk: learning to identify, Choose and Live with accepatable Risk. Kimeandikwa na Mganga Ben Carson kwa msaada wa Gregg Lewis na kuchapishwa na Zondervan Publishing House mwaka 2008. Kitabu kinaanza na masimulizi ya upasuaji mgumu uliofanyika Julai 2003 kuwatenganisha Ladan na Laleh, mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana sehemu ya vichwa vyao. Mapacha hao hata hivyo walifariki dunia wakiwa na umri wa miaka 29 wakati upasuaji huo ukiendelea huko Singapore. Katika kitabu hiki, mwandishi anajaribu kutupatia somo lilitokana na Upasuaji huo. Ladan na Laleh raia wa Iran muda mfupi kabla ya upasuaji huo uliofanyika Julai 2003.

Elimu pasipo maandishi inawezekana?

Picha
Pamoja na ukweli kuwa wengi wetu tunayakwepa maandishi, lakini hiyo haimaanishi kuwa hatuna kiu ya kujifunza. Pichani, wananchi wa mjini Moshi wakionekana kuvutiwa na matumizi ya video katika kuelimika. Picha: Sayuni Philip

What religion really means

Picha
Kimeandika yaliyo kinyume na imani yangu. Nakisoma. Mwandishi Karen Armstrong na kuchapishwa na Vintage 2010. Kinauzwa kwa Tsh 19,500.

Uliwahi kukisoma hiki?

Picha

Padre karugendo na mijadala ya Imani

Picha
Kitabu hiki nilikisoma mara ya kwanza mwaka jana. Yeye mwenyewe alinielekeza mahali pa kukipata baada ya kuwa amesoma mjadala uliomhusu kwenye blogu hii baada ya kusemekana kuwa Padre Karugendo alikuwa "amevuliwa" upadre. Nilijifunza mengi kuhusu dini. Pengine unaweza kujiuliza; Kwa nini aliandika kitabu hiki? Pamoja na kukieleza kisa kizima kilichosababisha yeye "kufutwa" upadre kupitia tangazo la gazetini, Padre Karugendo anasema katika uk. 22: "...lengo zima la kutafakari kwangu na kukushirikisha wewe msomaji, ni kutaka kujenga utamaduni kama ule wa kule zilikotoka dini hizi za kigeni. Utamaduni wa kuamini kitu unachokifahamu vizuri, unachokitafakari, kinachogusa maisha yako ya jana, leo na kesho. Imani inayojenga historia yetu - historia ya Mungu na watu wake wa taifa la Tanzania!" Pamoja na hilo, Padre karugendo anasema kwa sauti kubwa kabisa kwamba, "Si haki Maaskofu kukemea ufisadi ndani ya serikali na kuacha ufisadi unaoendelea ndani y...

Ninachokisoma sasa...

Picha

Pedagogy of the oppressed

Picha
Paulo Freire katika sura ya pili ya kitabu chake "Pedagogy of the Oppressed" anazungumzia dhana inayosisimua anayoiita "the banking concept of education" kama chombo kinachotumika kuwakandamiza wanyonge. Kwamba katika hayo yanayoitwa madarasa, wapo waungwana wanaojichukulia kuwa wanajua, hulipwa kwa kuwajaza wenzao "elimu" ambayo kimsingi ni chombo cha kuwakandamiza raia wanaoonewa. Freire anadhani hii si sawa kwa binadamu mwenzako kujiweka juu sana kiasi cha kuamua usome nini, na uache kipi (bila kujali mahitaji yako halisi). Anatoa mfano pale mwalimu anapoweza hata kupendekeza kwamba kitabu fulani kisomwe kuanzia ukurasa wa 10 hadi wa 15! Na eti anadhani anamsaidia mwanafunzi! Kwa mujibu wa Freire, elimu hii haiwezi kumkomboa mnyonge. Je, elimu yetu ina tofauti? Wanafunzi zaidi ya asilimia 50 "walishindwa" mtihani hivi majuzi, ni kweli walishindwa ama ni namna nyingine ya kuwakandamiza vijana wasio na hatia?

Shule zisizo na elimu zifungwe!?

Picha
Ivan D. Illich ni mwanafalsafa aliyezaliwa mjini Vienna mwaka 1926. Katika kitabu chake cha Deschooling Society, Illich anazishambulia taasisi ziinazohodhi wajibu wa kuelimisha jamii. Anasema; “…kwenda shule (tofauti na kuelimika) imekuwa ndio utaratibu wa maisha…shule zimeshindwa kukutana na mahitaji ya mtu mmoja moja, na mbaya zaidi zinaendeleza uongo ule ule kwamba yale yanayoitwa maendeleo yanayotokana na uzalishaji, utumiaji na faida ndicho kipimo cha ubora wa maisha ya mwanadamu. “…Vyuo Vikuu (shule) vimegeuka viwanda vya kutengeneza vibarua kwa ajili ya matajiri, vikiwapa raia vyeti kwa ajili ya kutoa huduma, wakati huo huo vikionekana kuwanyang’anya leseni wale vinavyowadhania kuwa hawafai (waliofeli).” Tafsiri ni yangu. Illich anatoa mapendekezo ya kukomesha mfumo huu wa baadhi ya watu kujipa wajibu wa kuwaelimisha wengine wakati wao wenyewe hawajielimishi. Haoni haja ya kuwa na majengo yanayoitwa shule ambayo kazi yake inaonekana kuishia kutengeneza watumwa wa soko huria...

Ajuaye kusoma na hasomi ana nafuu?

Je, kuna tofauti kati ya mtu asiyejua kusoma (illiterate) na yule anayejua kusoma (literate) lakini hasomi?