Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Utamaduni

Ukifikiri Upendo ni Vitu Utamkinai Anayekupenda

Picha
Juzi naongea na kijana mmoja, umri nakadiria kavuka miaka thelathini, ananiambia ameanza kuhisi kama vile hakuumbiwa mapenzi. Ukisikia mtu anatoa kauli nzito hivi ujue kuna jambo. Kudodosa, kumbe, kayapambania mapenzi na yamekaribia kumtoa roho. Kila anayempenda kwa dhati anaishia kumwacha hewani.     Haelewi afanye nini.   “Hawa wanawake wanataka nini?” Kaniuliza. Tuliongea mengi. Naomba nikushirikishe, japo kwa muhtasari, maudhui ya mazungumzo yetu.    Picha: Tony Cordoza   |  Getty Images Tumeanza kuwa na kizazi cha vijana werevu, watafutaji, wenye uwezo mkubwa wa kutafuta pesa lakini wenye hisia kificho, wasiojali hisia na wasio na haja ya kina cha mahusiano.  Hiki ni kizazi, aghalabu, kilichozaliwa na kizazi cha wazazi wasomi, wenye maarifa zaidi na pesa zaidi kuliko kizazi kilichopita. Tunatumia muda mwingi kazini, kwenye biashara, na shughuli nyingine za kutafuta vitu. Ukiangalia kwa haraka unaona hiki ni kizazi chenye watu wenye kazi ...

Ukishasahau ulikotoka huwezi kuwa mzazi mzuri

Picha
  Sijui kama umewahi kuwaza kama mimi. Je, mafanikio yetu yanawasaidia watoto kuwa binadamu timamu? Je, uwezo tulionao kiuchumi unawezesha watoto kujifunza tabia zitakazowafanikisha kiuchumi? Kuna namna ninaogopa kuwa huenda tunawanyima watoto wetu fursa ya kujifunza maisha katika uhalisia wake. Nafahamu wapo baadhi ya wazazi wamekulia kwenye familia zinazojiweza kiuchumi. Hata hivyo, hiyo haiondoi ukweli kuwa wengi wetu tumetoka kwenye familia masikini na tumekuwa kizazi cha kwanza kupambana na kuuweza umasikini. Je, tunawaandaa watoto wetu kujikwamua kama tulivyojikwamua sisi?   PICHA: Marlous de Milliano Tunafahamu namna umasikini unavyofedhehesha. Umasikini unafanya maisha yako yasiwe na uchaguzi. Umasikini unakufanya upate kinachopatikana na sio kile unachokihitaji.  Hili, pamoja na ubaya wake, kwa kiasi kikubwa limekuwa kichocheo cha wengi wetu kuwa na hasira kubwa kupambana na umasikini kwa nguvu zote. Bidii ya kazi unayokuwa nayo ni matokeo ya hasira kuwa usi...

Kipimo cha Uadilifu Wetu ni Namna Tunavyopambana na Mimba za Utotoni

Picha
PICHA:  Huffington Post NINGEPENDA kuamini, katika mjadala unaoendelea kuhusu mimba za utotoni, kila mchangiaji bila kujali mapendekezo yake, anatamani kuona tunamaliza tatizo hili. Hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kutetea watoto wa kike kupata ujauzito katika umri mdogo.

Tujitathmini Kabla Hatujamhukumu Mtoto Mjamzito

Picha
PICHA: AboveWhispers Matukio ya watoto wa kike kupata ujauzito yanaongezeka. Kwa mujibu wa Takwimu za Elimu (BEST) wanafunzi 4,718 wa sekondari kwa mwaka 2012 na 3,439 mwaka 2015 walikatishwa masomo yao kwa sababu ya ujauzito. Takwimu kamili hazipatikani lakini kwa elimu ya msingi hali haina tofauti kubwa. Hata hivyo, Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA) linadai kwamba msichana mmoja kati ya sita wenye umri wa miaka 15 mpaka 19 wakiwemo wasiokuwepo shuleni hupata ujauzito kila mwaka hapa nchini. Ni wazi kuwa mimba za utotoni ni tatizo kubwa katika jamii yetu.

Mabadiliko ya Kijamii Yanavyoathiri Malezi -1

Picha
PICHA:  The Conversation TUNAISHI katika nyakati ambazo maarifa kuhusu malezi ya watoto vinapewa umuhimu. Sambamba na ongezeko la mijadala ya malezi katika majukwaa mbalimbali, malezi yamevutia hisia za watafiti wengi kuliko ilivyopata kuwa. Kila siku, kwa mfano, zinachapishwa tafiti nyingi kuchunguza changamoto za malezi ya watoto.

Desturi Zetu Zilivyosaidia Malezi Bora ya Watoto -2

Picha
PICHA: The Community Voice NIMEJARIBU kubainisha baadhi ya desturi zilizosaidia kukuza watoto wanaojitambua. Unaweza kusoma makala ya kwanza hapa . Kwa kuanzia, tuliona namna familia zilivyowajibika kumtunza mama aliyejifungua. Mtoto na mama walipata muda wa kutosha kujenga mahusiano ya karibu.

Desturi Zetu Zilivyosaidia Malezi Bora ya Watoto

Picha
PICHA: Huffington Post WAAFRIKA tumekuwa na utaratibu mzuri wa kuwalea watoto wetu. Mila na desturi za jamii nyingi za ki-Afrika zimeyapa malezi ya watoto uzito unaostahili. Malezi yalichukuliwa kama fursa nyeti waliyonayo wanajamii kurithisha utambulisho wa kabila husika kwa kizazi kinachofuata.

Mwalimu Anavyoweza Kukuza Udadisi kwa Wanafunzi

Picha
PICHA: OBrown & Associates Education Consulting Mara nyingi tumesikia watu wakilaumu mtalaa wetu kwamba unafunga fahamu za wanafunzi wetu. Wenye madai haya wanafikiri bila mtalaa kufanyiwa marekebisho makubwa, haiwezekani elimu yetu ikamnufaisha mwanafunzi. Hata hivyo, tulisema wiki iliyopita, kazi ya mtalaa ni kutoa diraya jumla ya aina ya raia wanaotarajiwa kufundwa kupitia mtalaa husika.

Mwanaume Anayejitambua Hatishwi na Mafanikio ya Mwanamke

Picha
PICHA: Ayo Martins Upo ukweli usiosemwa wazi kuwa wanaume wengi wanawaogopa wanawake wenye mafanikio. Wanawake waliosoma, wenye mali na fedha, wenye madaraka makubwa katika jamii, wanakuwa na mtihani mkubwa kuanzisha na kudumisha uhusiano na wanaume.

Ayafanyayo Mzazi Huamua Atakavyokuwa Mtoto

Picha
PICHA: Pinterest 'Mwanangu ni mtundu haijapata kutokea’ alilalamika msomaji mmoja wa safu hii. Sikuelewa ana maana gani aliposema mwanae ni mtundu. Nikaomba ufafanuzi. ‘Hasikii. Jeuri asikwambie mtu. Usipomfanyia purukushani huwezi kumwambia kitu akasikia.’ Kwa mujibu wa maelezo yake, kuna nyakati hubidi amtishe, amwadhibu vikali na hata kumtukana ikibidi.

Unavyoweza Kumfundisha Mtoto Kuwa Mkweli

Picha
PICHA: Heaths Haven Fikiria uko jikoni ukiandaa chakula cha jioni. Watoto wako wawili wadogo Fred na Joe wanacheza sebuleni. Salome yuko mezani akifanya kazi za shule. Mara unasikia mlio wa kitu kuvunjika sebuleni. Unapatwa na wasiwasi. Unakwenda haraka kujua kilichotokea. Maji yanatiririka sakafuni. Chupa ya chai imedondoka na kupasuka. Unakasirika.

Jifunze Namna Bora ya Kumrudi Mtoto

Picha
PICHA: IT News Africa Tunapojadili mbadala wa adhabu ya bakora tunatambua changamoto kadhaa. Kwanza, ni wazi bakora zimekuwa sehemu ya malezi yetu. Kwa wazazi wengi, unapozungumzia nidhamu ya mtoto, maana yake unazungumzia bakora. Imejengeka imani kwa watu kuwa bakora ndiyo nyenzo kuu inayoweza kumrekebisha mtoto.

Utamaduni wa Demokrasia Uanzie Ngazi ya Familia

Picha
PICHA: Dennis Louis Tumesikia madai kuwa baadhi ya watawala wetu wa ki-Afrika ni madikteta. Watawala hawa wanashutumiwa kupuuza haki ya raia kueleza mawazo yao wazi wazi bila hofu ya ‘kushughulikiwa.’ Inavyoonekana wananchi wana matamanio ya kushiriki moja kwa moja katika shughuli za kudhibiti serikali wanazokuwa wameziweka madarakani. Bahati mbaya watawala wanapopata madaraka huziba masikio yao sambamba na kuhakikisha vivywa vya wananchi haviwezi kusema kinyume na maoni waliyonayo watawala.

Kuyamudu Mafanikio Yako...

Picha
Fikiria umehitimu masomo kwenye chuo maarufu; umepata alama nyingi kwenye mtihani mgumu; umepata kazi yenye heshima; umejenga nyumba nzuri; umenunua gari la ndoto zako; umesafiri kwenda mahali wanakotamani kwenda watu na hawawezi au basi tu umekutana na mtu fulani maarufu. Unajisikiaje kama watu hawatafahamu? Kwa nini watu wakifahamu unajisikia vizuri zaidi?

Unavyoweza Kukuza Tabia Njema kwa Mwanao -4

Picha
Katika makala yaliyopita tumejifunza aina mbili za misukumo ya utovu wa nidhamu. Kwanza, tumeona mtoto huweza hufanya ukorofi kutafuta kusikilizwa. Anaposumbua na hata kudeka bila sababu, mara nyingi, anajaribu kutuambia kuwa hatujampa muda wa kuwa karibu naye. Anafanya hivyo kutafuta usikivu wetu. Pia, tumeona wakati mwingine mtoto husukumwa na hisia za kutaka kulipiza kisasi. Kama ilivyo kwa mtu mzima, mtoto naye anazo hisia. Anaweza kuumizwa na kauli na matendo anayoyatafsiri vibaya. Jitihada za kupunguza maumivu yake huishia kuwaumiza na wengine. Namna gani tunawasaidia watoto kuondoa tafsiri hizi potofu, huamua aina ya tabia watakazojifunza. Katika makala haya tunaangazia malengo mengine mawili yanayotengeneza msukumo wa kukosa nidhamu.

Tunayopaswa Kuyafahamu Kuhusu Shule za Msingi za Bweni

Picha
Katika miaka ya hivi karibuni, shule za msingi za bweni zimekuwa maarufu. Kimsingi, si tu shule za msingi, lakini hata shule za awali za bweni. Hivi sasa, miji karibu yote katika nchi hii inazo shule kadhaa zinazopokea watoto wadogo na kuwasomesha kwa mfumo wa bweni. Takwimu rasmi za hivi karibuni hazipatikani. Lakini kwa mujibu wa Wizara ya Elimu, mwaka 2012 nchi yetu ilikuwa na shule za msingi zipatazo 684 zenye huduma ya bweni. Shule hizi zinafahamika pia kama shule zinazotumia Kiingereza kama lugha rasmi ya kufundishia, yaani English Medium, zikimilikiwa na watu binafsi au taasisi zisizo za umma.

Vitabu 49 Nilivyovisoma Mwaka 2016

Picha
Namshukuru Mungu nimeweza kusoma vitabu 49 kwa mwaka 2016. Nimejifunza mengi. Kusoma ni kama kupata nafasi ya kufanya mazungumzo na watu wa kila namna ya uelewa ambao kwa hali ya kawaida usingeweza kuwasikia vijiweni.  Msisitizo wangu umekuwa kwenye vitabu vinavyochambua tabia katika maeneo mbalimbali ya maisha. Hata hivyo, vipo vichache vya masuala ya imani, falsafa na dini. Sijawa msomaji wa riwaya/novel. Nikutie moyo wewe mwenye ratiba ngumu kwa siku. Unaweza kufanya maamuzi ya kusoma ikiwa utaamua kuweka ratiba yako vizuri. Nijitolee mfano mimi mwenyewe.

Siri za Watu Wanaotekeleza Maazimio ya Mwaka Mpya

Picha
TULIJADILI baadhi ya sababu zinazofanya watu washindwe kutekeleza maazimio wanayoyaweka kila mwaka mpya unapoanza. Tuliona sababu kubwa tatu; kuweka maazimio kwa msisimko tu wa kuingia mwaka mpya usioenda sambamba na tafakari ya kina; kuweka malengo mapana mno yasiyopimika; na pale malengo yanapohusisha mabadiliko ya tabia, kutokujua uliko mzizi wa mabadiliko hayo.

Kwa Nini Maazimio Mengi ya Mwisho wa Mwaka Huwa Hayatekelezeki?

Picha
Kila mwaka mpya unapoanza, ni kawaida kwa watu wengi kuweka maazimio fulani ya kutekeleza. Wapo ambao huazimia kubadili tabia wasizozipenda. Wengine huazimia kuanzisha mwenendo mpya wa maisha wanayoyatamani. Wengine hufikiria kutekeleza malengo fulani ya kijamii na kiuchumi yatakayobadili maisha yao kwa mwaka unaoanza. Ingawa ukweli ni kuwa mwaka unapoanza kinachobadilika huwa ni tarehe tu, watu huwa na imani kuwa wanaingia kwenye zama za maisha mapya. Imani hiyo huambatana na jitihada za kujaribu kubadili maisha yao yaendane na zama hizo mpya. Wanasema, ‘mwaka mpya na mambo mapya!’

Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Anayefanya Vibaya Shuleni

Picha
Si jambo la kufurahisha kwa mzazi unapoona mtoto hajafanya vizuri masomoni. Unapofahamu kuwa maendeleo ya mwanao si kama vile ulivyotarajia, ni rahisi kupatwa na simanzi, wasiwasi na hasira. Ni dhahiri mzazi unatamani mtoto awe na mustakabali mzuri kimaisha. Matumaini hayo yanakufanya uchukulie kushindwa kwake masomo kama kiashiria cha kuharibika kwa maisha yake ya baadae. Hakuna mzazi angependa mtoto awe na maisha yasiyoeleweka.