Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2010

Tumefinyangwa kuwa wakimbizi wa kudumu

KADIRI siku zinavyosonga mbele, ndivyo waswahili tunavyozidi kuwa watu tusiojitambua. Namaanisha kutokujifahamu sisi ni akina nani na tunatofautianaje na wasio watu wengine waliobaki katika uso wa dunia. Tunashindwa kuyaelewa mazingira yetu na thamani ya ustaarabu wetu ambao (huenda) ni ushenzi kwa wengine. Badala yake tunageuza ushenzi wao kuwa ndio ustaarabu rasmi wa jamii yetu. Tunashindwa kujua mwelekeo wetu kama watu wenye ustaarabu wao ambao ndio unaoleta maana ya maisha yenye alama ya Utanzania. Matokeo ya haya matatu ni kurudi nyuma katikati ya hayo yanayoonekana kuwa ni maendeleo. Hapo ndipo tunapogeuka kuwa mazuzu wenye vitu ambavyo babu zetu hawakuwavyo lakini bado tukiishi hovyo kuliko hata walivyoishi wao. Kwa maana nyingine, tunakuwa watu wenye “zaidi” kwa habari ya vitu, lakini wenye “ukosefu” kwa habari ya thamani ya kweli ya utu wetu. Swali tunalojiuliza hapa ni iwapo ni busara kung’ang’ania kuyatafuta maendeleo (kwa maana ya vitu na huduma) pasipo kwanza kuubaini

Sisi ni nchi ya kaulimbiu?

Nimekuwa nikijiuliza: Hivi raia wa Tanzania tunatambulishwa kwa kitu gani hasa? Tuna mawazo gani ambayo tunaweza kusema, haya ndiyo mwelekeo wa Watanzania? Ni masuala yepi ambayo nje ya vyama vya siasa yanaongoza mwelekeo wa taifa letu? Maslahi ya taifa (ambayo si lazima yafananane nay a chama kimoja kimoja) ni yepi? Je, tunawafundisha nini wanafunzi wetu ambacho kinawafanya wajitambue kama Watanzania? Utamaduni wetu kama raia wa Tanzania ni upi? Tunajipambanuaje kama wananchi mahsusi wa Tanzania katikati ya bara zima la Afrika? Hivi falsafa hasa ya taifa letu ni ipi? Je, ni kasi zaidi na ari zaidi? Je, tumekuwa nchi ya "miaka mitano mitano"? Kwamba baada ya uchaguzi, viongozi wanajiandaa kwa uchaguzi ujao? Tumekuwa nchi ya kauli mbiu? Nchi yetu inaongozwa kwa mwelekeo upi? Ni nini ambacho kiongozi yeyote akishika mamlaka ndicho atakachopaswa kutusaidia tukifikie? Hakuna kitu kibaya sana kama kuishi bila dira. Hakuna ugonjwa mbaya sana kama ule wa kutokujua unakokwend

Kwa nini watu hatutulii kwenye fani tulizonazo?

Kwa nini watu wengi hutumia sehemu kubwa ya maisha yao kumangamanga huku na huko, wakibadili kazi na shughuli kutoka ofisi moja kwenda nyingine? Inakuwaje kijana aliyesoma kuwa mtaalamu wa kilimo, hataki kabisa kufanya kazi ya kilimo aliyoisomea na badala yake anatafuta kazi itakayompeleka mbali zaidi na kilimo? Kwa nini mwalimu haridhiki na chaguo lake la awali la kutokotosha fikra za wanafunzi, na badala yake anatumia sehemu kubwa ya maisha yake kutafuta namna ya kuchomoka afanye kazi zisizohusiana na ualimu? Tunatafsiri vipi kitendo cha daktari aliyesomea utabibu kwa miaka isiyopungua mitano, katika mazingira magumu ambayo hatma yake yanamfanya awatumikie wananchi wenzake kwa kuokoa maisha yao, anaachane na utabibu ili kuwa mwanasiasa wa majukwaani? Ninachojiuliza ni hiki: Kwa nini hatutulii kwenye taaluma zetu? Kwa nini hatuzitumii taaluma tulizonazo ambazo zimetupotezea miaka kibao kuzipata? Je, ni aina ya elimu tunayopata? Je, tafsiri ya mafanikio tuliyokuzwa nayo tangu t

Kanisa Katoliki na ushirikina...

Nasikitika kwamba sijawa na muda wa kutulia kuendelea na mijadala ya imani ambayo nimekuwa niiendesha huko nyuma. Mijadala hiyo imenipa uzoefu mpya ambao mwanzoni sikuwa nao. Mijadala hiyo imenifanya nishangae inakuwaje watu wenye imani ama dini kumtukana mtu anayejaribu kuhoji masuala yaliyo ndani ya dini yake. Mtu akikuonyesha upungufu wako kwa hoja, si ni bora kumshukuru? Pengine ndiyo hulka ya dini: Waamini hujadili kwa kuongozwa na ushabiki na hisia zaidi na sio hoja. Katika blogu ya Strictly Gospel ambayo ni blogu maalumu kwa mijadala ya Kikristo, nimekutana na mjadala ambao pamoja na kuwa bado haujapata wachangiaji wa kutosha, nadhani utakuwa mjadala moto moto huko mbeleni. Mjadala wenyewe unahusu uchawi wa kanisa Katoliki. Hebu bonyeza hapa kushiriki mjadala huo . Muhimu sana kushiriki kwenye mijadala. Na unaposhiriki kubali kujifunza. Ujue tumedanganywa vingi. Tumezungukwa na uongo. Katika familia zetu. Katika shule zetu. Katika siasa zetu. Dini. Na kadhalika. Na katika