Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Elimu

Unayafahamu Anayopitia Mwanao na Hakuambii?

Picha
Kama sehemu ya wajibu wangu wa kitaaluma, huwa ninaandaa, kuendesha na kutathmini mafunzo ya ulinzi wa mtoto kwa walimu, wanafunzi na wazazi kwenye shule mbalimbali nchini. Nimeendesha mafunzo hayo kwa shule nyingi hususani za binafsi na zile zinazoendeshwa na mashirika binafsi na kidini.     Hivi karibuni nilipata bahati hiyo kwenye shule moja kubwa inayoendeshwa na shirika moja la kitawa. Imani tuliyonayo wazazi wengi kwa shule hizi ni mfumo madhubuti wa malezi unaowahakikishia watoto usalama wao. Ingawa ni kweli matarajio ya wazazi wengi ni ufaulu mzuri, hili la malezi yenye kumjenga mtoto kimaadili ni kubwa zaidi.   Siku hiyo, Ijumaa, kabla ya kuzungumza na wazazi Jumamosi yake, nilipata wasaa wa kusema na watoto wa kidato cha kwanza na cha pili. Madhumuni ya kuanza na watoto ni kupata uzoefu halisi ninaoweza kuutumia kama rejea kwenye mazungumzo na wazazi. Nafahamu sisi wazazi huwa hatupokei jambo kirahisi hasa linapoonekana halina uhalisia. Ninapokuwa na mifano hali...

ChatGPT Inapoaminika Kuliko Mzazi

Picha
Jioni moja wiki iliyopita nilikuwa Instabul. Huu ni mgahawa mmoja maarufu jijini Dar es salaam. Hapa nafanya nazungumza na Damari, mwanafunzi wa shahada katika taasisi moja ya elimu ya juu jijini Dar es salaam. Sikumwuuliza umri lakini nakadiria ana miaka 21. Kikao chetu kimezaliwa na kipindi nilichokuwa nimekifanya asubuhi hiyo kwenye kituo kimoja cha televisheni.   Tulizungumza kwa kirefu suala alilokuwa nalo na tufikia muafaka. Kisha nilimwuuliza swali ambalo huwa nawauliza ‘wadogo’ zake ninapokuwa naendesha mafunzo ya malezi shuleni.  "Nani ni rafiki yako wa karibu?" Nalenga kujua anamwamini nani.  Hakufikiri mara mbili akanijibu, "ChatGPT!” Sikuzuia mshangao. Jambo hili, kwa hakika, lilinisumbua. Sikuwahi kufikiri ChatGPT ingewahi kuwa rafiki wa mtu. Kama huifahamu, ChatGPT ni programu tumizi inayotumia teknolojia ya akili mnemba. Imentegenezwa kuwezesha mazungumzo yanayolingana na unachoulizia.    “Umesema ChatGPT ndio rafiki yako?” “Ndio. Rafiki ninayemwa...

Unalea watoto au unafuga watoto?

Picha
Kila siku saa 12 jioni, Mah’mood mwenye miaka 12 hutoka shule anakosoma moja kwa moja kwenda nyumbani. Mah’mood  anawajua wazazi. Hawawezi kuthubutu kumruhusu kuchelewa nyumbani hata dakika tano. Jaribio lolote la kuchelewa litakaribisha matusi, ukali, na ikibidi kiboko bila maelezo yoyote.  Mah’mood anatamani kuwa mchezaji hodari wa mpira. Ndoto hii imekatishwa baba yake alimwambia, “Hutakula mpira, soma uwe mwanasheria. Hutaki acha shule. Kila Mah’mood anapouliza swali, jibu huwa ni kama limerekodiwa mahali, “nyamaza, wewe ni mtoto.” Kadiri miaka inavyoenda, Mah’mood alizidi kuwa mnyonge na kujiamini kwake. Ukiongea na Mah’mood unaweza kuhisi ni jasiri. Lakini ukisikiliza vizuri unagundua ana unyonge unaoua utu wake, ndoto zake, na uhuru wa kuwa yeye. Je, haya ni malezi au ufugaji? Je, Mah’mood analelewa au anaishi na wazazi wake kama mfugo? Jamii zetu zinaamini mno katika utii na nidhamu. Tunafikiri bila nidhamu iliyopindukia, utii usiohoji basi mtoto hawezi kufanikiwa...