Malezi yanapokuwa ‘rasha rasha’ tuilaumu teknonojia?

PICHA: businessday.ng Kama ambavyo imeanza kuwa vigumu wengi wetu kumaliza siku bila usaidizi wa zana za teknolojia, ndivyo malezi nayo yanavyoanza kuchukua uelekeo wa kuhitaji usaidizi wa teknolojia. Saa nyingine mzazi usingependa watoto waangalie katuni muda mrefu. Lakini unafanyaje sasa kama wewe mwenyewe hata unapokuwepo nyumbani huna mengi ya kufanya na watoto? Ombwe, kwa kawaida, huwa ni muhimu lizibwe. Lakini pamoja na kusaidia kujaza ombwe la sisi wazazi kutokuwepo kwenye maisha ya watoto, bado teknolojia inayo mengi yenye manufaa. Kubwa zaidi ni kuwachangamsha watoto kiakili. Nitumie mfano wa mwanangu. Hajakamilisha miaka mitatu. Ukikaa naye anayo mengi ya kukusimulia. Uwezo tu wa kusimulia jambo na likaeleweka katika umri wa miaka miwili sikuuona kwa dada yake waliozidiana karibu muongo mzima. Ingawa bado ni mapema mno kumpeleka darasani, anatambua herufi na tarakimu zote, ana uelewa wa awali wa kuhesabu, anafahamu majina ya rangi nyingi, anawafahamu majina na tabia ...