Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Uandishi wa Kiraia

Pay $900? I quit blogging

Picha
Global Voices Citizen Media Summit in Cebu, The Philippines in 2015. Photo Courtesy of Global Voices I started my blog in 2005. I was among very few Tanzanians who were inspired by Ndesanjo Macha to start blogging.  For those of you who do not know, the history of Tanzanian blogosphere recognizes the contribution of this great man. His influential  weekly column in a local newspaper invited many of us to his blog. In fact he was the first Tanzanian to blog in Kiswahili . That was in 2004. I had the privilege of meeting him in Nairobi, Kenya in 2012 and in Cebu, The Philippines in 2015. We were both attending Global Voices Citizen Media Summits. For me, blogging was fun. I never thought that blogs could actually threaten politicians. That was until 2010 when I had an opportunity to attend the Global Voices Citizen Media Summit   in Santiago de Chile. I was shocked to hear friends talking about restriction of fr...

Uamuzi wa Kuachana na Blogu

Picha
Mkutano wa Global Voices, mtandao wa wanablogu, uliofanyika Cebu, Ufilipino, 2015 PICHA: Global Voices Nilianza kublogu katikati ya mwaka 2005. Wakati huo ilikuwa nadra kusikia mtu anaongelea blogu.  Ndesanjo Macha ndiye hasa aliyenifanya nikavutiwa kuanza kublogu. Wakati huo alikuwa mwandishi wa safu ya Gumzo la Wiki iliyochapishwa na gazeti la Mwananchi kila Jumapili. Historia ya blogu hapa nchini haikamiliki bila kumtaja Ndesanjo Macha. Kimsingi, Ndesanjo ndiye mwanablogu wa kwanza kublogu kwa Kiswahili. Huo ulikuwa mwaka 2004. Nilipata bahati ya kukutana naye mara mbili kwenye mikutano ya waandishi wa kiraia kupitia mtandao wa wanablogu uitwao Global Voices. Mara ya kwanza ilikuwa jijini Nairobi, 2012 . Mara ya pili ikatokea jijini Cebu,Ufilipino, 2015 . Nakumbuka mwaka 2010 nikiwa nahudhuria mkutano wa wanablogu uliofanyika  Santiago de Chile , nilistushwa na masimulizi ya baadhi ya washiriki waliokuwa wakiongelea 'kuminywa kwa uhuru wa kujieleza kwenye...

Nilichojifunza Katika Miaka 10 ya Kublogu

Picha
Kwa mara ya kwanza nililisikia neno blogu mwaka 2004. Wakati huo nilikuwa msomaji wa dhati wa safu ya ‘Gumzo la Wiki’ iliyokuwa ikiandikwa na Ndesanjo Macha katika gazeti la Mwananchi. Kwa kufuatilia anuani iliyokuwa ikihitimisha safu hiyo, niligundua kuwa sikuhitaji kusubiri   Jumapili kuweza kulisoma ‘Gumzo’. Anuani hiyo ilikuwa ni ya blogu ya kwanza ya Kiswahili ikiitwa Jikomboe .

Tabora wamemsamehe Lowassa, au ni dalili za kukubalika kwa UKAWA?

Picha
Matokeo ya utafiti mdogo uliofanywa na mwandishi wa makala haya katika mitaa ya mji wa Tabora jioni ya leo, umeonesha kwamba kuna ushindani mkali kati ya Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Ufisadi wa Richmond, Edward Lowassa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Dk Wilbroad Slaa, kama uchaguzi mkuu ungefanyika kati ya saa 10 – 12:30 jioni hii. Matokeo hayo yanaonesha kwamba Lowassa ana asilimia 28 na Dk Wilbroad Slaa angepata asilimia 22.

Watoto Waliokosa Masomo Nchini Libya Wafundishwa kwa Njia ya Skype

Picha
Hali tete ya kiusalama nchini Libya imewafanya watoto washindwe kwenda shule tangu mwezi Oktoba. Kwa kuwa watoto hawawezi tena kuhudhuria masomo katika shule zao, El-Zahawi aliwaza ni kwa nini asisogeze madarasa karibu na huko walipo? Na hapa ndipo Shule ya Skype ya Benghazi ilipozaliwa rasmi.

CCM ni maarufu Kigoma kwa 40.2%, ikifuatiwa na CHADEMA kwa 27.2%

Picha
Utafiti huru uliofanywa na mwandishi wa makala haya, umeonesha kwamba mgombea yeyote wa nafasi ya Urais wa Chama cha Mapinduzi angeweza kuchaguliwa na wapiga kura wa Manispaa ya Ujiji/Kigoma kwa asilimia 40.2% ikiwa uchaguzi mkuu ungefanyika kati ya saa 11 mpaka saa 1 na nusu jioni ya leo.

Wafilipino Wauliza ‘Rais Yuko Wapi?’ Wakati wa Majanga ya Kitaifa?

Picha
  "TWITI TENA kama unadhani PNoy alipaswa kuhudhuria mapokezi ya heshima badala ya tukio la Kiwanda cha Magari. #NasaanAngPangulo" alitwiti @BobOngWords. Alama habari #NasaanAngPangulo, yenye maana 'Rais yuko wapi' katika lugha ya Kitagalog, ilikuwa mada maarufu zaidi kwenye mtandao wa Twita duniani wakati Wafilipino walipokuwa wakionesha hasira zao kwa Rais Noynoy Aquino kufuatia  kukosekana kwake  kwenye mapokezi ya heshima ya miili ya polisi waliouawa wakiwa kwenye operesheni maalum.

Mwaka unakatika....Tumesonga mbele ama nyuma???

Picha
Nashukuru kwa blogs na tovuti mpya ambazo zinachipuka na kuendeleza nia njema ya kuigusa jamii. Ningependa tuanze kwa kujiuliza, 'Je! Tunasonga mbele ama nyuma katika harakati zetu?' ...kwa ujumla, haijalishi ni sababu gani ilikufanya u-blog, mwisho wa safari sote tunajikuta na zao moja ama "mlaji" mmoja ambaye ni JAMII.

Mwaliko wa Mkutano wa Global Voices, Dar es Salaam, Novemba 1, 2014

Tunayo furaha kubwa kutangaza mkutano wa Global Voices unaotarajiwa kufanyika Dar es Salaam, Tanzania siku ya Jumapili, Novemba 2, 2014 kuanzia saa 6 mchana hadi saa 10 adhuhuri. Mkutano huo utafanyika kwenye Kituo cha Teknolojia na Mambo ya Jamii, KINU , washirika wa Global Voices Swahili hapa nchini.

Tunapambana na UKIMWI kwa kupambana na utu wa watu wanaoishi na VVU?

Picha
Hivi majuzi nilipata fursa ya kushiriki mradi unaojaribu kudhibiti maambukizi ya virusi vinavyosababisha UKIMWI kwa kuwasaidia watu wanaoishi na virusi hivyo kukabiliana na hali hiyo ambayo kwa hakika hugeuza kabisa maisha yao. Fursa hii adhimu ilinifungua macho kuona kile ambacho sikuwahi kukiona kwa muda mrefu. Nisingependa kutoa takwimu za tafiti za majumuisho zinazojaribu kuonesha hali ikoje kwa ujumla bali takwimu za hali halisi niliyoiona kwa macho yangu.

Siku ya Blogu Oktoba 16: Shiriki Kujadili Dhana ya Kutokuwepo kwa Usawa

Picha
Tangu 2007, Siku ya Wajibu wa Blogu Duniani imekuwa ikitumika kuwaweka pamoja wanablogu kutoka duniani kote ili kujadili mada muhimu zinazokuwa zimewekwa mezani. Siku hiyo, wanablogu kwa pamoja, huwa utaratibu wa kuvamia anga la blogu kwa kuchapisha maelfu ya posti kuhusu masuala ya maji, mabadiliko ya tabia nchi, umasikini, chakula na nguvu ya pamoja. Kwa mara nyingine mwaka huu, Global Voices Online inayo fahari kuwa mshirika rasmi wa siku hiyo.

Rais mteule atumia mitandao ya kijamii kuwaomba raia kumchagulia Baraza la Mawaziri

KATIKA kuthibitisha kwamba kasi ya matumizi ya mitandao ya kijamii ni kubwa, hivi majuzi, Rais mpya wa Indonesia Mhe Joko Widodo (maarufu kama Jokowi) amewaomba watumiaji wa mtandao wa Facebook kumsaidia kuteua baraza lake la mawaziri kwa kupendekeza majina ya watu wanaoweza kushika wadhifa wa kuwa Mawaziri. Hatua hiyo, ni mwendelezo wa kile anachokiita mwenyewe 'kuongeza  kwa ari ya kujitolea' miongoni mwa raia wa nchi hiyo, baada ya watu wengi kujitolea kumsaidia katika harakati zake za kuingia ikulu. Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Jokowo ametoa orodha ya nafasi 34 za Uwaziri , zenye majina matatu yanayopendekezwa kwa kila nafasi, huku kukiwa na nafasi ya nne wazi kwa wananchi kupendekeza wanayemtaka. Widodo anataapishwa ifikapo Oktoba 20, 2014 kuwa Rais. Joko Widodo (53) Gavana wa zamani wa Jakarta, amechaguliwa kuwa Rais wa Indonesia baada ya kumbwaga mpinzani wake Prabowo Subianto kwa asilimia 53 ya kura milioni 130 zilizopigwa tarahe 9 Julai, 2014. Kama ilivyo ...

Blogu inavyosaidia kujiona unavyokua na kubadilika

Nilianza kublogu mwaka 2005. Takribani miaka tisa. Wakati huo nilikuwa kinda. Kijana mdogo. Blogu kwangu ilikuwa kama sehemu ya kusema ninayofikiri bila kuhofu. Nimekuwa na utaratibu wa kurudia niliyowahi kuyaandika enzi hizo. Wakati mwingine ninacheka. Ninaweza kuona namna mtazamo wangu ulivyokuwa ukibadilika hatua kwa hatua hasa katika masuala ya dini na imani. Watu hutarajia mwandishi asibadilike. Maana kwao, mwandishi ni mlishaji. Hajifunzi. Mimi si mwandishi. Ni mwanablogu. Tofauti ya mwandishi na mwanablogu ni kwamba, wa pili anaingiliana sana na hao anaowaandikia. Anajifunza. Anabadilika. Mtazamo unabadilika. Wa kwanza sina hakika na yote hayo. Kwa hiyo, ninafurahia kubadilika. Zamani nilikuwa mbishi. Niliona raha kusumbuana na wabishi wenzangu. Siku hizi sibishani sana. Ninasikiliza zaidi. Zamani nilikuwa mwongeaji. Siku hizi nimekuwa na aibu. Nina haya. Yote hayo ni mabadiliko. Yawe chanya ama hasi. Lakini bado ni mabadiliko. Kufikia miaka ya 2010 hapa kumefumuka mitan...

Kurudi Bloguni

Habari za miaka wapenzi wana-blogu. Tafadhali karibuni sana kwenye blogu yetu iliyokuwa mapumzikoni kwa takribani miaka miwili. Sababu za kupotea zilikuwa za kijamii na nje kabisa ya udhibiti wa kawaida. Sasa tunaweza kuahidi kuwa blogu yetu imerejea rasmi kwa nguvu mpya na mtazamo mpya tangu dakika hii. Na masuala ya kijamii yanayohusiana na mahusiano yetu na nafsi zatu pamoja na mahusiano yetu na wanaotuzunguka, tabia zetu, mitazamo yetu, na kadhalika, yataendelea kupewa kipaumbele kwa sura mpya zaidi. Karibuni sana.

Nilipozungumza na blogu ya Maneno Matamu: “Kiswahili ni alama ya Uafrika wangu.”

Picha
Yafuatayo ni mahojiano yangu na blogu ya Maneno Matamu kuhusu, pamoja na mambo mengine, suala la lugha za Kiafrika na nafasi ya blogu katika kukuza lugha hizo katika enzi hizi. Ulianza kuandika blogu mwaka 2005. Uliamuaje kushiriki katika mtandao wa Internet namna hii? Nakumbuka nikiwa mwanafunzi nilikuwa mfuatialiaji mzuri wa makala za mwandishi maarufu,   Ndesanjo Macha   (ambaye sasa ni Mhariri wa Global Voices eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara). Yeye ni mwanablogu wa kwanza wa Kiswahili. Na kwa kweli niilivutiwa sana na aina yake ya uandishi, mijadala aliyokuwa akiiendesha kwenye blogu yake pamoja na matumizi mazuri ya lugha. Kwa hiyo hamasa ya kublogu ilitokana na  blogu yake . Blogu kwangu niliiona kama fursa nzuri na rahisi ya kujadili masuala ninayoyaelewa vizuri ya kiutambuzi na sayansi. Mule niliona ingekuwa rahisi kupata jukwaa la kubadilishana mawazo na watu bila kikwazo chochote na pia p...

Nilipokutana na Mshairi Serina wa Upande Mwingine

Picha
Katika mkutano wa wanablogu na waandishi wa habari za kiraia uliofanyika Nairobi, Kenya, nimebahatika kukutana na mwanablogu niliyekuwa na hamu sana ya kuonana naye. Naye si mwingine bali, dada Serina Kalande, anayetuandikia kwenye blogu ya Upande mwingine . Na Serina Kalande, wa Upande mwingine. Picha: Deogratias simba Ni dada mkarimu, mpole, mwanana na mwema sana kuzungumza naye. Serina, asante kwa baraka ya kukuona.

Mgomo wa Mabasi ya Abiria Mjini Moshi

Picha
 Wakazi wa Manispaa ya Moshi na vitongoji vyake leo wameonja adha ya kukosa usafiri kufuatia mgomo wa mabasi  yanayotoa huduma ya usafiri mjini hapa, maarufu kama daladala.  Kituo kikuu cha Mabasi mjini Moshi kama inavyoonekana dakika chache zilizopita  Mgomo huo umetokea kama hatua za waendeshaji wa huduma hiyo kupinga kupanda kwa kiwango cha ushuru kilichotangazwa na Halmashauri ya Manispaa hiyo. Vibao vipo, magari hayaonekani  Kwa  mujibu wa tangazo la Halmashauri hiyo inayoongozwa na CHADEMA, ushuru huo umepanda kwa asilimia 50 kutoka Tsh. 1000 zilizokuwa zikilipwa awali mpaka Tsh 1500 zinazotakiwa kuanza kulipwa mara moja. Kituo kikiwa tupu, huku Polisi wa 'kutuliza' ghasia wakiwa kazini Tayari Katibu wa CHADEMA mkoani Kilimanjaro, Bw. Lema, kupitia Radio za FM mjini hapa ametoa tamko la kupinga vikali ongezeko hilo, akiliita kuwa 'hujuma' inayofanywa na baadhi ya watendaji wa Halmashauri hiyo inayoongozwa ...

Blogging Revolution: Shubiri kwa wajiitao serikali

Picha
Kitabu kizuri kinachoangazia mabadiliko ya kijamii na kisiasa yaliyoletwa na matumizi ya zana za uandishi wa kiraia hususani blogu.  Kinatazama namna blogu zilivyochangia Mapinduzi yanayoendelea katika nchi za kiarabu –maarufu kama Arab Spring – na jinsi ambavyo blogu hizi zinaanza kuwatia hofu watu wanaojiita serikali.

Wanablogu wanasemaje kuhusu utaratibu wa "Kutuzwa"?

Picha
Tangazo lilianzia hapa kwamba kuna mwuungwana -japo hakuwa anafahamika jina lake wala mahali aliko- kapata wazo la kutunuku kazi za wanablogu. Huenda hili bado halijulikani kwa wanablogu wengi kama ilivyokuwa kwangu kabla ya kusoma posti ya mwanablogu matata, Bw. Mubelwa Bandio juma lililopita. Blogu ya mwandaaji wa Tuzo hizo inajinadi kwa maneno haya: "...Our wish is to help bloggers to success, beat the odd and push past their limitation. We believe bloggers can play an important role keeping their places, villages, towns, cities or countries visible. Tanzanian Blog Awards is another opportunity to showcase your blog to the world and get some free traffic and subscribers..." Pamoja na kupongeza wazo hilo (la kuandaa tuzo kwa wanablogu), Mubelwa Bandio alionyesha wasiwasi wake ikiwa zoezi hilo litafanyika katika mazingira ambamo masuala ya msingi kuhusu blogu hayajafanyiwa kazi. Kwamba blogu zinaeleweka vyema kwa wadau (wateuzi na wateuliwa), hilo lilimtia mashak...

Wakubwa wetu huko Ufaransa

Picha
Picha hii imechukuliwa kwenye ukumbi wa mijadala wa Jamii Forums ikiwaonyesha watawala wetu walipohudhuria mkutano huko Ufaransa.