WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.
Umewahi kujiuliza kwa nini, wakati mwingine, mtu mwenye akili nzuri, mwenye weledi na uelewa mpana wa mambo, hujikuta na majanga mengi linapokuja suala la namna anavyoishi na watu? Shida ni nini? Iweje mtu aelewe mambo mengine vizuri lakini asindwe mambo madogo kama kuwa msikivu, mvumilivu wa mawazo tofauti, mwenye subira hali inayoweza kumuingiza kwenye magomvi na watu? Wengine tunafikiri tuna misimamo mikali, tumenyoooka na hatujali kutofautiana na nani lakini ukitazama vizuri hiyo inayoitwa misimamo mikali ni changamoto za kihisia, uwezo mdogo wa kuelewa mitazamo ya wengine, na saa nyingine ni kiburi tu kuwa tunajua kuliko wengine, hawana wanachoweza kutuambia na kadhalika. Kinyume na tunavyoamini wengi wetu, hisia hubeba maamuzi yetu mengi na ukitazama matatizo yetu mengi ya kitabia unaweza kuona mchango mkubwa wa kushindwa kuzielewa na kuzimudu hisia zetu. Ingawa tunazipuuza, ukweli ni kwamba ukishashindwa kuzishughulikia hisia zako, uwezekano wa kukabiliana na matatizo...
Kizazi chetu kinakabiliwa na magonjwa mengi yasiyoonekana. Tunaumwa, na wakati mwingine taabani, lakini hatujui kuwa tunaumwa. Tunatembea, tunakutana na watu, tunapiga picha zenye nyuso zilizochangamka, tunaonekana kufurahia maisha lakini tunateseka na mahangaiko mengi tusiyoweza kuyasema. Tazama kiwango chetu cha ukatili. Haiwezi kuwa kawaida, kwa mfano, kuona mwenzako anaumizwa na wala hujali. Unamuumiza mtu na bado unashangaa kwa nini analalamika. Unamtesa mwenzako kihisia na bado unamdhihaki anapougulia maumivu. Unajiuliza, tumefikaje mahali mwanadamu unaweza kumtesa mwenzako, ukamsababishia maumivu na hujisikii kujutia. Mbaya, wakati mwingine, kiwango hiki cha ukatili kinakuwa kama nyenzo ya kupata tunachokitaka. Tunataka madaraka, tunataka umaarufu, mali na kila kinachotufanya kujione tunnawazidi wengine. Tunakuwa waraibu wa ukatili dhidi ya binadamu wenzetu na hatujisikii kujutia. Tazama kiwango chetu cha ubinafsi. Kwa nini tumepoteza uwezo wa kuafikiria hisia...
Katika utangulizi wetu , nilieleza maana ya umahirihisia na nyanja zake tano. Nilieleza kuwa, ingawa umahirihisia una nyanja hizo tano, ukiyatazama vyema mawanda yake, unaona kuna maeneo makubwa mawili. Eneo la kwanza, ni utambuzi kwa maana ya kuelewa hisia zako, kuzifuatilia na kuzirekebu kwa maana ya kujifunza namna ya kuzimudu zisikuingize kwenye matatizo. Eneo la pili linategemea eneo la kwanza, kwa maana ya uwezo wa kutumia utambuzi huo wa hisia kuelewa namna ya kuelewa, kutambua na kuheshimu hisia za wengine kwa minajili ya kuboresha mahusiano yako na watu. Katika sehemu hii ya pili, ninajielekeza kueleza kwa ufupi jinsi gani umahirihisia unaweza kukuzaidia kuzielewa na kuzirekebu hisia zako. Umewahi kukutana na mtu mwenye uwezo mzuri wa kusoma ujumbe unaobebwa na uso wa mtu? Ukitabasamu, mwingine anaishia kwenye uso huo wenye tabasamu lakini yeye ana uwezo wa kujua kuwa pamoja na tabasamu lako, kuna kitu hakiko sawa. Unashangaa pamoja na k...
Tunamalizia safari yetu ya kujifunza umahirihisia. Tumeangazia maeneo makubwa manne. Kwanza, uelewa wa hisia na sababu zake. Pili, tulitazama namna ya kurekebu hisia zetu . Kisha tukatazama namna tunavyoweza kujenga motisha na hamasa ya kufikia malengo yetu . Kisha tukaangalia namna umahirihisia unavyotuwezesha kuwasiliana na watu pasipokuzalisha migogoro isiyo na sababu. Maeneo haya manne ya umahirihisia, yanatafsirika katika mahusiano yetu na watu —namna tunavyowachukulia wasioamini tunachokiamini, namna tunavyowajibu wasiofikiri kile tunachokifikiri, namna tunavyotatua migogoro na maamuzi tunayochukua pale tunapojisikia kuonewa. Msingi wa mahusiano yenye tija na watu ni uwezo wako wa kujitambua, kutambua namna hisia na tabia zako zinavyoathiri wengine, namna unavyomudu hisia zako lakini pia kiwango chako cha upendo kwa watu. Mtu mwenye #UmahiriHisia hagombani kirahisi. Ukigombana naye anajua namna ya kujinasua na kukuachia ugomvi wako...
Tunaendelea na elimu ya hisia. Katika makala yaliyopita , tumejifuza msamiati wa hisia. Mbali na kutofautisha mihemuko na hisia, tumedadisi namna hisia, katika ujumla wake, zinavyobeba ujumbe. Kila hisia huja na ujumbe fulani. Umahirihisia ukuwezesha kutafakari ujumbe unaobebwa na hisia zako. Katika makala haya, ningependa tutafakari kwa pamoja namna ya kuzikebu na kuzimudu hisia zetu. Nianze na swali. Unakumbuka mazingira umewahi kujikuta ukifanya maamuzi mabaya kwa sababu hujipa muda wa kupooza hisia zako? Unakumbuka kusema jambo ukiwa na hasira, kwa mfano, halafu baadae ukajutia? Unamwandikia mpenzi wako maneno makali shauri ya hisia za wivu lakini baadae ukishapoa unagundua hukuwa na sababu ya kusema ulichokisema? Napenda nukuu moja ya mama anayeitwa Maya Angelou, “Watu wanaweza kusahau ulichokifanya. Watu wanaweza kusahau ulichokisema. Lakini watu hawawezi kusahau ulivyowafanya wakajisikia .” Unaweza kuona uzito wa hisia katika kumbuk...
Kuna kukosa ari ya kaza. Msimamizi wako asipokufuatilia na kuweka utaratibu wa kukudhibiti ufanye unachopaswa kufanya, hakuna unachoweza kuonesha kama matokeo. Huna msukumo wowote wa kujituma na wala hujisikii hatia. Hali kama hii inaweza kusabishwa na mengi. Kuna suala la mazingira magumu ya kazi. Hupati vitendea kazi unavyohitaji ili kufanya kazi yako vizuri. Kuna suala la uongozi usiojali hisia zako. Unalalamika na hakuna anayeonekana kusikia. Kuna mengi yanayoweza kukufikisha mahali ukapoteza motisha ya kazi. Wengi wanaposikia motisha wanawaza matokeo mazuri unayopata aghalau kutoka kwa mtu kama kichocheo cha kufanya kazi. “Hapa hatupewi motisha yoyote.” “Tunafanya kazi na hakuna motisha.” “Toeni motisha muone nitakavyofanya kazi.” Tunapozungumzia motisha hatuzungumzii kutambuliwa kwa kazi unayofanya, kuonekana, kusifiwa, kupandishwa cheo wala kupewa kitu kama bakhshishi ya bidii yako ya kazi. Motisha ni ile sababu inayoamsha ari ya ...
waswahili walinena, "Ukiona kobe kainama ujue anatunga sheria"
JibuFutaMchoko wa Dowans.....
JibuFutaMoja ya Mtazamo:
JibuFutaWamevaa suti nzuri kweli !:-(
Duuh, heri mimisijasema...!
JibuFutaHivi Waziri Mzima unapolala kwenye mkutano (ambao nauli na per Di Em inalipwa kwa kodi za wananchi) pembeni kabisa mwa bosi wako maana yake nini?
JibuFutaNaunga mkono usemi wa Mwaipopo.
JibuFutaakitoka hapo anasaini mkataba......yaliyomo sasa utajiju
JibuFuta