Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2006

Afrika: Bara linalokimbiwa na Waafrika wenyewe

Katika kujadili matatizo ya bara letu, watu wengi tumekuwa tukiwalaumu wazungu eti kwa kupora mali zetu. Nimesoma vitabu vingi vilivyoandikwa kuhusu Afrika. Nilichokiona katika maandishi ya wengi, ni malalamiko. Tunawalaumu wazungu. Hatusemi chochote kuhusu namna tulivyouchangia umasikini wetu wenyewe. Na inakuwa kama vile ukijaribu kuzungumzia upande wa pili, basi wewe si muungwana. Watu wanakutizama kwa jicho la marienge. Maandishi haya yanakusudia kugeuza kibao cha lawama. Bonyeza hapa kuendelea.

Raha ya kublogu ni uhuru wenyewe

Kwa mara ya kwanza nilisikia neno blogu kwa rafiki yangu aliyekuwa akijitolea kufundisha (volunteer) katika shule moja hapa nchini. Alinionyesha blogu yake na kwa kweli kama zilivyo za wazungu wengi, haikuwa na jambo la maana zaidi ya masimulizi ya hadithi zisizo na mashikio. Nikafungua na yangu, ikifuata nyayo hizo hizo za porojo nyepesi nyepesi. Haikuwahi kuingia kichwani kwangu kwamba inawezekana mtu kuisoma. Nilikuwa na sababu nyingi. Kwanza, rafiki zangu wengi hawakuwa wamehamasika na matumizi ya teknolojia ya habari. Aidha, wachache walioipenda hawakuvutiwa na mambo ya habari habari, wao waliziita za kizee. Nakumbuka tukitoka tuisheni za Makongo, tungeweza kupitia kwenye vioski vya mtandao (cafee) pale Mwenge kuchungulia hili na lile. Wakati mimi nikihangaika kusoma “templates” za blogu, wenzangu walikuwa, na mpaka leo, wanapenda kuangalia mambo flani ya ngono na udaku. Lakini pili sikuwa na wazo kwamba blogu yaweza kuwa uwanja mpana wa kukutana na falsafa mbali mbali. Nilijua

Duniani hakuna mwadilifu, wote tunahangaika

Maadili, mfumo wa kubaini jema na baya, hatuzaliwi nayo. Tunazaliwa tunayakuta yapo, yameanzishwa na wengine kwa makusudi yao ili kukidhi haja ya wakati husika. Hata waanzilishi wenyewe wa hayo yanayoitwa maadili yetu, tunakuwa hatuwajui ni akina nani na walitumia vigezo gani kutoka wapi ili kutuundia hayo yanayoitwa maadili. Hapa ninajaribu kuonyesha kuwa kila mmoja anaweza kuwa na mfumo wake binafsi wa maadili. Endelea hapa .