Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Matangazo

Pay $900? I quit blogging

Picha
Global Voices Citizen Media Summit in Cebu, The Philippines in 2015. Photo Courtesy of Global Voices I started my blog in 2005. I was among very few Tanzanians who were inspired by Ndesanjo Macha to start blogging.  For those of you who do not know, the history of Tanzanian blogosphere recognizes the contribution of this great man. His influential  weekly column in a local newspaper invited many of us to his blog. In fact he was the first Tanzanian to blog in Kiswahili . That was in 2004. I had the privilege of meeting him in Nairobi, Kenya in 2012 and in Cebu, The Philippines in 2015. We were both attending Global Voices Citizen Media Summits. For me, blogging was fun. I never thought that blogs could actually threaten politicians. That was until 2010 when I had an opportunity to attend the Global Voices Citizen Media Summit   in Santiago de Chile. I was shocked to hear friends talking about restriction of fr...

Uamuzi wa Kuachana na Blogu

Picha
Mkutano wa Global Voices, mtandao wa wanablogu, uliofanyika Cebu, Ufilipino, 2015 PICHA: Global Voices Nilianza kublogu katikati ya mwaka 2005. Wakati huo ilikuwa nadra kusikia mtu anaongelea blogu.  Ndesanjo Macha ndiye hasa aliyenifanya nikavutiwa kuanza kublogu. Wakati huo alikuwa mwandishi wa safu ya Gumzo la Wiki iliyochapishwa na gazeti la Mwananchi kila Jumapili. Historia ya blogu hapa nchini haikamiliki bila kumtaja Ndesanjo Macha. Kimsingi, Ndesanjo ndiye mwanablogu wa kwanza kublogu kwa Kiswahili. Huo ulikuwa mwaka 2004. Nilipata bahati ya kukutana naye mara mbili kwenye mikutano ya waandishi wa kiraia kupitia mtandao wa wanablogu uitwao Global Voices. Mara ya kwanza ilikuwa jijini Nairobi, 2012 . Mara ya pili ikatokea jijini Cebu,Ufilipino, 2015 . Nakumbuka mwaka 2010 nikiwa nahudhuria mkutano wa wanablogu uliofanyika  Santiago de Chile , nilistushwa na masimulizi ya baadhi ya washiriki waliokuwa wakiongelea 'kuminywa kwa uhuru wa kujieleza kwenye...

Vitabu Nilivyosoma kwa Mwaka 2017!

Picha

Mwaliko wa Mkutano wa Global Voices, Dar es Salaam, Novemba 1, 2014

Tunayo furaha kubwa kutangaza mkutano wa Global Voices unaotarajiwa kufanyika Dar es Salaam, Tanzania siku ya Jumapili, Novemba 2, 2014 kuanzia saa 6 mchana hadi saa 10 adhuhuri. Mkutano huo utafanyika kwenye Kituo cha Teknolojia na Mambo ya Jamii, KINU , washirika wa Global Voices Swahili hapa nchini.

Tunapambana na UKIMWI kwa kupambana na utu wa watu wanaoishi na VVU?

Picha
Hivi majuzi nilipata fursa ya kushiriki mradi unaojaribu kudhibiti maambukizi ya virusi vinavyosababisha UKIMWI kwa kuwasaidia watu wanaoishi na virusi hivyo kukabiliana na hali hiyo ambayo kwa hakika hugeuza kabisa maisha yao. Fursa hii adhimu ilinifungua macho kuona kile ambacho sikuwahi kukiona kwa muda mrefu. Nisingependa kutoa takwimu za tafiti za majumuisho zinazojaribu kuonesha hali ikoje kwa ujumla bali takwimu za hali halisi niliyoiona kwa macho yangu.

Siku ya Blogu Oktoba 16: Shiriki Kujadili Dhana ya Kutokuwepo kwa Usawa

Picha
Tangu 2007, Siku ya Wajibu wa Blogu Duniani imekuwa ikitumika kuwaweka pamoja wanablogu kutoka duniani kote ili kujadili mada muhimu zinazokuwa zimewekwa mezani. Siku hiyo, wanablogu kwa pamoja, huwa utaratibu wa kuvamia anga la blogu kwa kuchapisha maelfu ya posti kuhusu masuala ya maji, mabadiliko ya tabia nchi, umasikini, chakula na nguvu ya pamoja. Kwa mara nyingine mwaka huu, Global Voices Online inayo fahari kuwa mshirika rasmi wa siku hiyo.

Tembelea Website mpya

Pole na shuguli za kutupasha habari mbali mbali zinazotokea ndani na nje ya Tanzania. Naomba nafasi katika blog yako ili niwajulishe ndugu zangu watanzania kwamba nimetengeneza website www.rusumo.com ambapo wataweza kusikiliza nyimbo mbali mbali za Tanzania kama vile taarab,segere,dance,bongo flava,gospel na nyimbo za kigeni kama vile raggae,za kihindi,pop na nyengine nyingi tu. Pia kuna dictionary ya kisasa kabisa ambayo ina lugha zote za Ulaya na baadhi ya lugha za Asia,katika dictionary hii baada ya kupata tafsiri ya neno pia unaweza kuona picha za neno hilo kwa kubofya upande wa pili wa Ukurasa. Kadhalika wadau wataweza kuona hali ya hewa na wakati wa sehem mbali mbali za dunia. Karibuni sana wadau, ni mimi MSAFIRI ISMAIL RUSUMO. www.rusumo.com

Da' Subi kahamia makazi mapya

Naomba nafasi katika blogu yako kuwataarifu wasomaji kuwa tovuti ya mpya ya wavuti.com imechukua nafasi ya iliyokuwa nukta77.com na nukta77.blogspot.comNaomba yeyote aliyekuwa ameweka linki ya nukta77 aihariri na kuweka wavuti.com Karibuni sana kutembelea kwa taarifa za nafasi za masomo na kazi kwa burudani na bila kusahau habari na porojo!Asanteni.wavuti.com ************ Kuanzia sasa pata habari zote kwa kubonyeza hapa . Na kama utapenda kufanya kama nilivyofanya mimi, unaweza kujiandikisha uwe unatumiwa habari kila anapoziweka pale.

Tovuti bure...wahi!

Nimepata ujumbe kutoka wataalamu hawa wa kutengeneza tovuti. Hivi ndivyo wanavyosema: " Pole na kazi ya kuelimisha na kuburudisha jamii yetu. Tumekuja na huduma mpya ya BURE kwa watanzania tu tunaomba uwafahamishe. Kuzingatia umuhimu wa kuwa na tovuti, na ya kwamba ni gharama sana hapa TZ kupata tovuti, na tena watu wanafanya biashara rasmi kwa barua pepe za bure kama yahuu na giimeili, hii yote inaonesha ukosefu au gharama kubwa ya kupata tovuti. Sisi tumedhamiria kubadili uelekeo mzima wa upepo, na tumepata wasamaria wema na sasa rasmi tumefanikiwa kuleta ufumbuzi na neema kwa waTZ kwa suala la tovuti na anuani rasmi za barua pepe. Na sasa kwa awamu ya kwanza kwa kuanzia tu, WATU 100 WATATENGENEZEWA TOVUTI BURE. Watu 100 kwa maana ya mtu binafsi, kampuni, biashara, shirika, asasi zisizochukua faida (NGO), kikundi, duka, mjasiriamali, saluni, shule ama Saccos n.k. BASI KILA ALIYEDHAMIRIA KUWA NA WEBSITE/TOVUTI ajiunge na utaratibu huu wetu atengenezewe TOVUTI MOJA...

Kumradhi wadau...

Sitakuwepo kwa siku mbili tatu sita kumi hivi, kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu. Nimefanya hivi nikiamini si vibaya kupeana taarifa. Mpaka hapo nitakaporejea, Amani kwenu nyote!

Mkaribishe mwanablogu mpya wa dini/imani

Picha
Naomba kufahamisha blogu mpya yenye kugusa zaidi maisha na mienendo ya watu. Baadhi ya watu watakuwa wamemsoma Mhandisi na Mwelimishaji ndugu Sabato E. Tarimo katika gazeti la MsemaKweli kwenye makala zake mbalimbali. Sasa amejikita katika ulimwengu wa blogu ili kuwafikia wengi zaidi hasa wale wanaoishi nje ya Tanzania. Bonyeza hapa kumsoma.

Michael Jackson na athari za malezi

Si muda mrefu nilikuwa nikitazama ibada ya maziko ya Michael Jackson. Kwa wengi, Michael ni alama ya watu wasiojikubali. Wengi wanamlaumu kwa uamuzi wake wa kujifanyia marekebisho sura yake. Wengine wakamwita 'Wacko' yaani chizi. Kama umefuatilia historia ya uhusiano wake na wazazi wake utabashiri nini kilikuwa chanzo cha yote hayo. Uhusiano wake na baba yake haukuwa mzuri. Mzee si tu kwamba alikuwa mkali sana, lakini pia alikejeli maumbile ya mwanae huyo. Nadhani yapo zaidi ya haya yasiyosemwa wazi. Maana fikiria hata wosia aliouacha Michael umeonya kuwa wazazi wake wasihusishwe na mirathi. Hata katika maziko, wazazi hawakuongea! Inasemwa, wakati Michael anaanza kujikwatua, mzee alimwonya sana pasipo mafanikio. Kisiki kwa wazazi wengi: Wanadhani kumwonya mtoto msiyehusiana nae kwa karibu, mtoto aliyekufuta akini mwake, kunasaidia...! Mzazi usifanye kosa la Mzee Joseph Jackson.

Nenda hapa upate mwangaza...

Kissima ni mwanablogu mgeni. Ameanza kublogu mwaka huu. Nafurahi kwamba amekuwa mchangiaji mzuri katika blogu mbalimbali. Na inafurfahisha kwamba baadhi ya wanablogu wamekuwa mstari wa mbele kuchangia mijadala motomoto anayoianzisha bloguni kwake. Tafadhali bonyeza hapa kumtembelea, ukikumbuka kuchangia maoni katika mijadala yenye mwangaza.

Kaluse mwanablogu wa utambuzi

Je, unaujua utambuzi? Kama sivyo, basi ujio wa huyu mwanablogu mpya utakupa majibu. Bonyeza hapa umsome . Anazungumzia mambo yanayohusu nafsi zetu. Saikolojia. Binafsi nimependezwa na ujio wa mwanablogu huyu. Naamini utapenda kumsoma na kujadiliana na wasomaji wengine humo.

Fahamishwa na nifahamishe.com

Kuna tovuti mpya inatangazwa. Nimeipitia. Ina kiingereza na kiswahili. Kwa mujibu wa waendeshaji wake, tovuti hiyo imebeba mambo mengi ya kukuhabarisha ndugu msomaji. Wanayataja: "Habari mbali mbali za Tanzania na za kimataifa, Habari katika picha na video, Live radio, Online Game, Habari za burudani na wasanii wa bong, Utaweza kusikiliza nifahamishe nonstop bolingo na lingala mix, Kuuza kwa kuweka tangazo lako bure au kununua nyumba, magari, vitu vya electronics na kadhalika, Kushare picha na watanzania duniani na kadhalika". Gonga hapa kuwatembelea ujionee mwenyewe.

Mtembelee mwanablogu mpya Kristine Missanga

Karibu umtembelee mwanablogu mwenzetu, ambaye bila shaka anayo mengi mapya. Falsafa. Mtizamo mpya. Maswali. Lengo lake kama anavyosema mwenyewe ni kutujengea utamaduni wa kujiuliza. Blogu yake inaitwa Jiulize. Unaweza kumtembelea kwa kubofya hapa kumsalimia.

Changamoto za kublogu zinaendelea

Kwa siku kadhaa pamekuwapo tatizo la wavu wa mtandao hapa nilipo. Hivyo nilishindwa kuweka chochote hapa. Nadhani hali ni shwari, nitaweka chochote kuanzia sasa. Karibuni tuendelee.