Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2014

Tabia za Mtoto wa Miaka 0 – 3 Kimahusiano na Kihisia

Katika makala yaliyopita , tuliangalia matukio muhimu ya kimakuzi katika maeneo mawili makubwa ya ukuaji wa mtoto nayo ni 1) kimwili na 2) kiakili. Katika sehemu hii ya pili, tunasaili ukuaji wa kimahusiano na kihisia ili kutazama yabia zinazojitokeza pasipo kuathiriwa na malezi na haiba ya wazazi. Kwa lugha nyingine, haya ni matarajio ya mtoto yanayoendana na umri wake bila kuingiliwa na matarajio na yanayofanywa na mzazi kwake.

Ukuaji wa Kiakili na Kimwili kwa Mtoto wa Miaka 0 – 3

Picha
Katika makala haya, tunatazama kwa ufupi makuzi ya mtoto mwenye umri wa siku moja mpaka miezi 36. Tutaangalia mambo ya msingi yanayonesha ukuaji wa mtoto unavyoendelea katika maeneo makubwa manne; 1) ukuaji wa kimwili 2)  kiakili 3)  kimahusino na watu wengine na mwisho 4) kihisia. Kwa kawaida maeneo haya manne yanategemeana ili kumwezesha mtoto kukua kwa ujumla. Kwa mfano ili mtoto akue kimwili, anahitaji ukuaji wa akili ipasavyo ambayo nayo itaathiri namna anavyomudu hisia zake na hivyo kuhusiana na watu wengine. Kwa hiyo ni sawa tukisema hakuna ukuaji wa eneo moja usiotegemea eneo jingine.

Uhusiano wa haiba ya mzazi na malezi ya watoto – 2

Picha
Wakati tunajiandaa kuangalia kwa kina malezi ya watoto wenye umri wa miaka 0 – 3 kama tulivyoahidi , na kuona namna watoto hawa wanavyoweza kuathiriwa na malezi wanayoyapata, ni vizuri tutazame japo kwa ufupi haiba kuu nne za wazazi zinazoweza kuathiri sana malezi ya watoto.

Miaka miwili ya Kuwa 'Mama' Ina Mafunzo Makubwa Kwangu...

Picha
Nilipoamua kuchukua uamuzi wa kubadilishana majukumu na mke wangu sikujua ni kwa jinsi gani uamuzi huo ungenibadilisha mimi na kunipa mtazamo mpya kabisa katika maisha. Baada ya kuzaliwa Baraka siku kama ya leo mwaka 2012 tuliamua kubadilishana majukumu ya familia; mimi nibaki na kuangalia watoto na kutunza nyumba na mahitaji yake yote na mke wangu aendelee kufanya kazi na kusaidia wakati wowote anaoweza.

Mwaka unakatika....Tumesonga mbele ama nyuma???

Picha
Nashukuru kwa blogs na tovuti mpya ambazo zinachipuka na kuendeleza nia njema ya kuigusa jamii. Ningependa tuanze kwa kujiuliza, 'Je! Tunasonga mbele ama nyuma katika harakati zetu?' ...kwa ujumla, haijalishi ni sababu gani ilikufanya u-blog, mwisho wa safari sote tunajikuta na zao moja ama "mlaji" mmoja ambaye ni JAMII.

Uhusiano wa haiba ya mzazi na malezi ya watoto – 1

Picha
Katika mfululizo huu tunatarajia kujadili mahitaji ya kimahusiano ya mtoto mwenye umri usiozidi miaka 20 kwa vipengele kadhaa. Katika kufanya hivyo, tunajikita kwenye uhusiano wa moja kwa moja ulipo kati ya haiba ya wazazi na namna haiba hiyo inavyoweza kuathiri vile tunavyolea watoto wetu. Tutaona namna malezi hayo yanavyoathiri tabia na mwenendo wa watoto tangu wanavyozaliwa mpaka wanapofikia umri wa kujitegemea. Tutaonesha kwamba kwa kiasi kikubwa tabia tunazoziona kwetu si za kuzaliwa na wala hazitokei kwa bahati mbaya. Ni matokeo ya haiba na mahusiano yenu na wazazi waliotulea.

Mtoto ni nani?

Picha
Sheria na mikataba mbalimbali inayozungumzia huduma na haki za mtoto, inamtambulisha mtoto kama mtu yeyote mwenye umri wa miaka chini ya 18. Hata hivyo, kutumia umri kama msingi wa tafsiri ya utoto hakuwezi kutusaidia kujua kwa nini mtu mwenye umri huo aitwe mtoto. Katika makala haya, ningependa tumtazame mtoto kwa kuangalia mitazamo tofauti katika jitihada za kumtofautisha mtoto na mtu ‘mzima’ bila kutumia idadi ya miaka kama msingi mkuu.

‘Hakuna uhusiano wa elimu ya mzazi na ubora wa malezi’ –watafiti

Picha
IMEJENGEKA dhana kwamba kiwango kikubwa cha elimu anachokuwa nacho mzazi kinaamaanisha ubora na ufanisi wa malezi. Katika nchi za ki-Magharibi kwa mfano, ubora wa malezi kwa maana ya uelewa wa mahitaji ya kisaikolojia ya mtoto umekuwa ukihusishwa na elimu ya wazazi inayokwenda sambamba na uwajibikaji wa kimalezi. Hali inaonekana kuwa tofauti katika nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara. 

Kwa nini ni rahisi kumsifia mtu akifa kuliko akiwa hai?

Picha
Hatupendi kuwasifu wengine wala kusikia wakisifiwa na wengine, lakini ni wepesi sana kumsifia marehemu. Na ni nadra kusikia tabia ya marehemu ikikosolewa. Hata waliokuwa hawamsifii akiwa hai, huomba fursa ya kuusemea vizuri wasifu wa mpendwa aliyetutoka. Mtu fulani maarufu akifa, kwa mfano, watu ambao hata siku moja hawakuwahi kumsema marehemu enzi za uhai wake, ndio huanza kushindana kutundika picha zake zikiambatana na maneno ya ‘apumzike kwa amani’. Sasa swali, kwa nini ni vyepesi kumsifia marehemu asiyesikia kuliko kumsifia binadamu anayesikia?

Unaanzisha mahusiano ya ndoa/mapenzi?

Picha
MAZUNGUMZO mengi yanayohusu maandalizi ya ndoa hujikita katika kufanikisha tukio la siku ya harusi. Na wakati mwingine wanaojiandaa kwa ndoa huandaliwa siku chache sana kabla ya tukio hilo. Kwa ujumla, suala la ndoa limerahisishwa kiasi cha kuonekana kuwa yeyote anaweza kukabiliana nalo kwa uzoefu pasipo maandalizi ya kutosha. Hata hivyo, pamoja na wepesi wa maandalizi halisi, na msisitizo uliowekwa na jamii katika 'siku ya harusi', ndoa nyingi huishia kwenye migogoro mingi muda mfupi baada ya tukio la harusi.

Malezi yanayofanya mtoto amsikilize na kumwamini mzazi

Picha
TAFITI zinaonesha kwamba watoto wengi   ni 'mayatima' wenye wazazi tunaoishi lakini hatupo kwenye maisha yao. Wazazi tupo lakini hatuna muda wa kujua hisia zao, fadhaa zao, maoni yao, hofu zao na hata matumaini yao. Aidha, tafiti hizo hizo zinasema wazazi wengi tunatumia muda mwingi na watoto wetu ama kuwaonya, kuwakosoa ama kuwapa hotuba/maagizo ya ‘fanya hivi, acha hiki’ kuliko tunavyowasaidia kujenga mahusiano ya moja kwa moja kati yetu na watoto.

Kuogopwa kwa wanawake wenye mafanikio na dhana ya kichwa cha familia

Picha
NILIPATA fursa ya kushiriki mjadala mmoja kwenye mtandao wa Facebook leo mchana. Mjadala wenyewe ulianzishwa na Samuel Sasali , ambaye kwa maoni yangu ana uwezo mkubwa wa kuchokoza mada zinazohusu maisha yetu ya kila siku. Hoja iliyokuwa mezani ililetwa kwa njia ya mchoro unaoonesha changamoto anazokabiliana nazo mwanamke anapofanikiwa kielimu. Kwamba kadri mwanamke anavyokwea ngazi ya mafanikio ya kielimu, ndivyo wanaume wanavyozidi kumkimbia.

Muhtasari na Hitimisho, 'Kanuni zinazoongoza mahusiano na migogoro ya wanandoa'

Picha
TANGU tulipoanza mfululizo wa makala za mahusiano , jambo kubwa nililojaribu kulionesha ni nafasi ya mahitaji ya hisia katika kuimarisha au kuvuruga mahusiano. Na msingi wa haya yote ni kusema kwamba mahusiano hayana miujiza. Mahusiano yanaongozwa na kanuni za kawaida sana ambazo ukifanikiwa kuzitambua na kuzitumia utapunguza kama sio kuondoa matatizo mengi. Kwa mhutasari, ningependa tuyapitie mambo makuu yaliyojitokeza katika mjadala wetu kwa kuyaweka katika makala moja inayojitegemea.

Umuhimu wa kutofautiana ili kujenga mahusiano imara

Picha
Kwa wale wafuatiliaji wenzangu wa tamthlia isiyopendwa na wengi, Isidingo the Need, mtakuwa mmeona mgogoro wa kimahusiano kati ya Rajesh Kumar na mkewe Priya. Wawili hawa wamejaliwa mtoto mmoja wa kike, Hiranya, ambaye si mtoto wa kuzaa wa Rajesh. Sasa ikafika mahali mwanaume huyu akatamani kuwa na mtoto ‘wa kumzaa mwenyewe’. Priya hayuko tayari kupata mtoto mwingine. Anadhani   kilicho muhimu kwa sasa ni kumlea mtoto wao na sio kuongeza majukumu ya malezi.

Mwaliko wa Mkutano wa Global Voices, Dar es Salaam, Novemba 1, 2014

Tunayo furaha kubwa kutangaza mkutano wa Global Voices unaotarajiwa kufanyika Dar es Salaam, Tanzania siku ya Jumapili, Novemba 2, 2014 kuanzia saa 6 mchana hadi saa 10 adhuhuri. Mkutano huo utafanyika kwenye Kituo cha Teknolojia na Mambo ya Jamii, KINU , washirika wa Global Voices Swahili hapa nchini.

"Ningerudia ujana tena, kipaumbele changu kingekuwa familia!"

Picha
Re-living my life ? " anauliza halafu anajijibu mwenyewe, "Ningebadili mtazamo wa tafsiri ya mafanikio. Mafanikio yangemaanisha ubora wa mahusiano yangu na familia yangu. Hivyo, ningewajibika zaidi kujenga na kuilea familia yangu kwa karibu. Ningetumia muda mwingi na wanangu na mke wangu. Ningepunguza ukali usio  na sababu kwa mke wangu na wanangu. Ningewafanya wanangu wajisikie kuwa na baba anayewaelewa na anayejua mahitaji yao. Ningepatikana zaidi. Ningemfanya mke wangu ajione ni kipaumbele cha maisha yangu.

Tunapambana na UKIMWI kwa kupambana na utu wa watu wanaoishi na VVU?

Picha
Hivi majuzi nilipata fursa ya kushiriki mradi unaojaribu kudhibiti maambukizi ya virusi vinavyosababisha UKIMWI kwa kuwasaidia watu wanaoishi na virusi hivyo kukabiliana na hali hiyo ambayo kwa hakika hugeuza kabisa maisha yao. Fursa hii adhimu ilinifungua macho kuona kile ambacho sikuwahi kukiona kwa muda mrefu. Nisingependa kutoa takwimu za tafiti za majumuisho zinazojaribu kuonesha hali ikoje kwa ujumla bali takwimu za hali halisi niliyoiona kwa macho yangu.

Siku ya Blogu Oktoba 16: Shiriki Kujadili Dhana ya Kutokuwepo kwa Usawa

Picha
Tangu 2007, Siku ya Wajibu wa Blogu Duniani imekuwa ikitumika kuwaweka pamoja wanablogu kutoka duniani kote ili kujadili mada muhimu zinazokuwa zimewekwa mezani. Siku hiyo, wanablogu kwa pamoja, huwa utaratibu wa kuvamia anga la blogu kwa kuchapisha maelfu ya posti kuhusu masuala ya maji, mabadiliko ya tabia nchi, umasikini, chakula na nguvu ya pamoja. Kwa mara nyingine mwaka huu, Global Voices Online inayo fahari kuwa mshirika rasmi wa siku hiyo.

Chimbuko la wivu na athari zake katika mahusiano

Picha
Umewahi kuhisi unaachwa na mtu unayetarajia kumwoa au kuolewa nae? Umewahi kutamani kuwa na 'access' na simu au barua pepe ya mwenzi wako ili angalau ujisikie kutulia moyoni? Umewahi kujisikia vibaya mwenzi wako akizungumza na mtu mwingine hata kama hukuwa na ujasiri wa kumwambia? Umewahi kumchukia mtu na hata kupambana nae kwa siri au wazi sababu tu umehisi anahatarisha uhusiano wako? Kama lolote kati ya hilo linaelezea hali yako, basi makala haya yanakuhusu.

'Usawa wa kijinsia' unavyoweza kuharibu mahusiano

Picha
Wanawake wanatafuta haki ya kuwa sawa na wanaume. Na wamefanikiwa. Katika makala haya tunajaribu kuonesha hatari ya wanawake kudhani wanaweza kuwa sawa kijinsia na wanaume na bado waweze kuwa na mahusiano imara na wanaume. Ni salama zaidi kwa wanawake kuelewa kwamba usawa wa kijinsia haumaanishi kufanana kwa wanaume na wanawake. Ingawa ni kweli tunapigania usawa wa fursa, bado twapaswa kutambua haitawezekana wanaume wakageuka kuwa wanawake na wanawake kadhalika wakageuka kuwa wanaume.

Iweje waliotulia hawaolewi, aolewe huyu asiyetulia?

Picha
Si mara zote uhusiano wa ndoa ni matokeo ya upendo kama inavyotarajiwa. Yapo mahusiano mengi tu ya ndoa ambayo kimsingi ni arrangements za watu kujipatia mahitaji mengine kabisa yasiyohusiana na mapenzi. Katika makala haya, tunajaribu kuonesha kwamba si kila mwanamke aliyeolewa maana yake ni kuwa anafaa na kadhalika, si kila asiyeolewa maana yake ni kuwa hafai.

Msomaji anauliza, 'Nilipenda pesa zake, naweza sasa kumpenda mwenyewe?'

Picha
Wapo watu hujikuta wameingia kwenye mahusiano na watu wasiowapenda kwa sababu kadha wa kadha. Katika makala haya, tunajaribu kuonesha kwamba kisaikolojia, upo uwezekano mkubwa wa watu hao kuingia kwenye mapenzi ya dhati na wenzi hao ikiwa mambo kadhaa yatafanyika. Ni mambo gani hayo?

Mahusiano ya kimapenzi yanavyoweza kuanzishwa bila kutarajiwa

Picha
Unaweza kushangaa lakini ndio ukweli wenyewe kwamba upo uwezekano mkubwa kabisa wa kuanzisha na kuendeleza mahusiano na mtu yeyote bila kujali mwonekano wake, tabia yake na imani yake. Katika makala haya tunaeleza kanuni za kimaumbile zinazoongoza mahusiano ya watu wawili ambao mara nyingi watu hao hukutana kwa njia ya nasibu.

Waajiri wanajifunza nini kupitia Mradi wa ILO unaotambua na kukuza ujuzi usio rasmi?

Picha
Shirika la Kazi Duniani hapa nchini, ILO, kwa ushirikiano na wadau wengine wa kazi na ajira hapa nchini wameanzisha mafunzo ya aina yake yanayolenga kutambua na kukuza ujuzi usiorasmi hivyo kuchangia kutatua changamoto hiyo. Kupitia mafunzo maalum yanayoitwa uanagenzi (apprenticeship), ambayo kwa sehemu kubwa hutolewa mahali pa kazi, mwajiriwa mwenye ujuzi usiotambuliwa rasmi anawekewa mazingira rafiki yanayowezesha ujuzi wake kutambuliwa rasmi na inapobidi, kuwezeshwa kupata mafunzo yanayoimarisha ujuzi alionao ili kufanya kazi zenye staha na kwa ufanisi wakati huo huo akiendelea na kazi.

Makundi Makuu Matano ya Waislamu

Mchekeshaji mwenye asili ya Pakistani, Sami Shah, anachambua makundi makuu matano ya wa-Islam.  Pengine hujawahi kuyasikia kama mimi na ungependa kujua umeangukia kundi lipi. Bonyeza hapa kusoma makala hiyo , ambayo kimsingi imekusudiwa kukufanya ucheke na kufurahi wakati huo huo, ukitafakari kwa kina kile hasa kinachokuchekesha.

Dhana ya 'mapenzi' kwa mtazamo wa kisaikolojia

Picha
Makala haya yanasaili namna mtazamo wa awali wa watu wanaoamua kuingia katika uhusiano wa kimapenzi unavyoweza kuathiri kwa kiasi kikubwa namna wawili hao watakavyohusiana. Na tunaonesha namna kiwango cha mapenzi kati yao kinatengemea masuala matatu makuu; Ukaribu wa kihisia, tamaa ya mwili na maamuzi yao.

Mambo Yanayoweza Kumvutia Mwanamume kwa Mwenzi Wake -2

Picha
Tuliona katika makala yaliyopita kuwa mwanaume anahitaji sana kutambuliwa uwezo wake. Huna sababu ya kumwambia mwanaume unampenda. Lugha ya upendo anayoielewa zaidi ni kusifiwa uwezo wake. Sambamba na hili la kwanza, tuliona mwanaume anayo njaa ya heshima. Heshima ni kumtii na kumstahi hata pale anapokuwa mkosaji kwa lugha, maneno na tabia. 

Mambo Yanayoweza Kumvutia Mwanamume kwa Mwenzi Wake -1

Picha
Swali hili huulizwa na karibu wanawake wote wanaotamani kuwa na uhusiano wa kudumu na wanaume. Kwamba mambo yepi hasa yanayoweza kumvutia mwanaume pale anapoanzisha uhusiano na mwanamke. Ingawa zipo tofauti ndogo ndogo miongoni mwa wanaume, kwa ujumla, uchambuzi wa tafiti mbalimbali za mahusiano unabainisha mambo kadhaa yanayowaunganisha wanaume wengi kimahitaji. Tuyatazame katika mfululizo wa makala hizi.

Kushinda Vikwazo vya Jitihada za Kumpa Mwenzi Anachostahili

Picha
KUYAELEWA mahitaji ya kihisia ya mwanamke ni suala moja, lakini kuuishi uelewa huo ni jambo jingine kabisa. Yapo mambo mengi tunayoyafahamu na tunajua kuyaelewa lakini hatuyaishi. Tujua kwa kina lakini hakuna tunalolitenda. Matokeo yake tunatenda tusiyoyajua na tunayoyajua hayatusaidii kubadili maisha yetu. Katika makala haya, ningependa kusimulia changamoto nilizokumbana nazo katika kupambana na utamaduni niliokulia wa kupuuza mahitaji ya msingi ya mwanamke.

Kama mwanaume, uko tayari kulipa gharama za mahusiano bora?

Picha
UNAPOWASIKILIZA wanaume wengi wakizungumzia kile wanachodhani wao kinawagusa wanawake kwenye mahusiano, utashangaa orodha ya vitu hutawala mazungumzo. Kwa mwanaume wa kawaida, mwanamke anahitaji vitu ili akupende. Utasikia, "Ah, mwanamke pesa. Ukiwa na hela zako bwana, basi." Imani ni kwamba wanawake wanahitaji sana vitu na hivyo ndivyo vinavyowavuta na kuwabakiza kwenye mahusiano. Pamoja na ukweli fulani kwamba vitu navyo vina nafasi yake kwenye mahusiano, hasa kwenye kizazi hiki cha sasa kinachotanguliza thamani ya fedha kuliko kitu kingine chochote, bado huwezi kuthamanisha moyo wa mwanamke na fedha, ingawa ni kweli anazihitaji. Kudhani kwamba baada ya kuhakikisha mwanamke amepata kila anachokihitaji kwa maana ya vitu, basi unaweza kuendelea na shughuli nyingine kwa kuamini umemaliza kazi, ni kutokuelewa mahitaji halisi ya kihisia ya mwanamke. Najua wapo wanawake wasiohitaji kingine chochote kwa mwanaume zaidi ya fedha na vitu. Mahitaji ya kihisia tunayoyaz

Msingi wa mahusiano si matarajio bali kutambua na 'kushibisha' mahitaji ya kihisia ya mwenzi wako

Picha
NI VIGUMU kwa kijana aliye kwenye kilele cha msisimko wa mapenzi hii leo kudhania bashasha hiyo inaweza kabisa kugeuka kuwa hasira, uchungu, na kushuhudia ile shauku ya kuongea, kusikiliza, kutaniana na mpenzi wake huweza kupotea so naturally kwa jinsi hiyo hiyo mapenzi yalivyoanza. Aliyewahi kusema upo mstari mwembamba mno unaotenga mapenzi na chuki, alilitambua hili. Kwa jinsi msisimko wa mwanzo wa kimapenzi unavyokuwa-ga mkubwa, huwa haingii akili kwa kijana anaposikia kwamba wapo wanandoa huweza kuchelewa kurudi nyumbani katika jitihada za kujaribu kuyakimbia matatizo na wenzi wao. Kijana anashindwa kuelewa inakuwaje watu wawili wanaopendana kwa dhati, wanaweza kufikia mahali pa kutamani kuzungumzia matatizo yao kwa uwazi, lakini wasiweze, wakatamani kuwa karibu kihisia, wasiweze. Haya yote pamoja na kuwa mabaya kuyasikia, huweza kumpata mtu yeyote, tena mwenye mapenzi mazito, hatua kwa hatua. Mahusiano ni suala zito lakini linalowezekana Tunapoyasema haya, hatukusudii kum

Namna mahitaji ya kihisia ya wenzi yanavyosababisha misuguano ya kimahusiano na ndoa

Picha
PAMOJA na dini nyingi kubwa kupiga marufuku talaka kwa waumini wake, takwimu rasmi za Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) zinaonyesha kwamba talaka nchini zimeongezeka kwa asilimia 49 katika kipindi cha mwaka 2007 hadi 2009. Kwa upande wa Zanzibar pekee, tunaambiwa, asilimia 95 ya migogoro 1,753 ya ndoa iliyosajiliwa kwenye Mahakama ya Kadhi nchini humo iliishia kwa talaka. Hali inatisha, au sio? Katika hali halisi, shauri ya utamaduni wa kuyaonea aibu masuala ya kuachana, hali inaweza kuwa mbaya zaidi. Watu wengi wanaweza kuwa wanaugulia maumivu ya ndoa na kuamua ama kufa na tai shingoni, au kutafuta 'michepuko' ya hapa na pale katika jitihada za kupunguza maumivu. Katika nchi za Ulaya, ambako kidogo kuna uhuru wa mtu kufanya atakalo ikiwa ni pamoja na kuomba talaka, hali ni tete zaidi. Kwa mfano, tunaambiwa, wakati idadi ya ndoa zinazofungwa mwaka 2010 ilipungua kwa asilimia 39 barani humo, talaka zimeongozeka kwa asimilia 200 katika kipindi cha mwaka 1979 mpa

Mambo ya Kufanya Unapotafuta Kazi

Picha
INGAWA inafahamika kuwa wapo wahitimu, tena wengi tu, ambao hufanya maamuzi ya kutumia ujuzi na maarifa waliyoyapata darasani kujiajiri wenyewe, kwa maana ya kubadilisha maarifa na ujuzi walionao kuwa bidhaa pasipo kumtegemea mtu aitwaye mwajiri, bado tunajua kuwa wahitimu wengi, kadhalika, huchagua kutafuta ajira. Kwao, huona ni rahisi kujipatia kipato cha kuendesha maisha yao kwa njia hiyo. Makala haya yanasaili mambo yanayoweza kumsaidia mhitimu anayetafuta ajira kupata taarifa zinazohusiana na namna bora ya kuwasiliana na mwajiri kwa matumaini ya kupata ajira anayoitegemea.

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -2

Tuliona katika makala iliyopita  maana ya saikolojia na kuhitimisha kwamba kinachotazamwa zaidi katika saikolojia ni tabia. Kwa hakika matatizo mengi yanayoikabili jamii yetu chanzo chake ni tabia. Tabia ndio chanzo cha matendo tunayoyaona kama kukosekana kwa uaminifu, ubadhilifu wa mali za umma, ufisadi, migogoro ya ndoa, misuguano ya kijamii, chuki, upendo, ugaidi, unyanyapaa, ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa kidini, changamoto za kimalezi na kadhalika. Yote haya yanaweza kuchambuliwa na kupatiwa majibu yake kwa kutumia sayansi ya tabia (saikolojia). Katika makala haya nitatoa mifano mifano kadhaa kuonesha namna sayansi ya tabia, inavyoweza kutumika kutatua matatizo yanayoikabili jamii.

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -1

Picha
SAIKOLOJIA, neno lililotoholewa kutoka neno la kiingereza psychology, si elimu inayoeleweka sana katika jamii yetu. Asili ya 'psychology' ni neno 'psyche' lenye maana ya nafsi. Katika makala haya, tunasaili kwa ufupi maana ya saikolojia kama taaluma na kuonesha nafasi ya taaluma hiyo ngeni katika jamii yetu katika kutatua matatizo ya kijamii na hivyo kuharakisha juhudi za watu kujiletea maendeleo yetu.

Mambo Muhimu ya Kuzingatia Unapoondika Barua ya Kuomba Kazi

Picha
Barua ya kuomba kazi ni waraka ambao mara nyingi husomwa kabla ya waraka mwingine wowote unaoambatanishwa katika kuomba kazi. Ni vyema barua ya kuomba kazi ikaandaliwa kwa umakini, na kujaribu kugusa kwa ufupi mambo yaliyoonekana kwenye wasifu binafsi kumvutia mwajiri mtarajiwa.

Wajibu wa pamoja wa mwajiriwa na mwajiri katika kuziba pengo la ujuzi unaotakiwa kazini

Picha
Katika makala yaliyopita tulisaili kwa uchache kile hasa ambacho waajiri wengi wanahitaji kukiona kwa watu waombao ajira. Kwa kifupi tuliona kwamba pamoja na uwezo wa kutumia nadharia za darasani katika mazingira ya kazi, waajiri wanatafuta kuona ujuzi tuliouita 'rahisi', au kwa kiingereza soft skills. Huu ni ujuzi usiosomewa lakini ndio huwa mithili ya mafuta yalainishayo ngozi iliyofubaa, kwa maana ya kuongeza ufanisi wa ujuzi rasmi wa kazi. Kama tulivyoona, kutokuoana (mismatch) kwa mahitaji ya mwajiri na sifa za mtafuta kazi ni moja wapo ya changamoto kubwa katika ulimwengu wa sasa wa ajira. Kwamba wapo watu wengi wenye kutafuta ajira kwa kuamini kuwa wanazo sifa za kuajiriwa, lakini waajiri wanaotazamiwa kuwapokea watu hao wakiwatilia shaka kuwa hawana uwezo wa kujaza nafasi walizonazo. Ni tatizo la elimu au mtazamo ? Wapo wanaoamini kwamba tatizo ni elimu. Kwamba tunawajaza wanafunzi maarifa ya kinadharia ambayo kwa hali halisi hayahitajiki kwenye soko la ajira.

Waajiri Wanatarajia Nini kwa Waombaji wa Kazi?

Taarifa ya Utafiti wa Ajira na Kipato ya mwaka 2012 , iliyotolewa na Idara ya Takwimu ya Taifa mwezi Julai 2013, inaonyesha kwamba nchi yetu ina waajiriwa rasmi 1,550,018.  Kati yao, asilimia 64.2 wameajiriwa katika sekta binafsi na waliobaki (asilimia 35.8) wameajiriwa katika sekta ya umma. Aidha, taarifa inasema ni asilimia 24.8 pekee ya wafanyakazi hawa, wanapata kipato cha kuanzia Tsh 500,001 kwa mwezi [vipato vya wafanyakazi wengi (asilimia 54.4) ni chini ya Tsh 300,000 kwa mwezi.] Nafasi za kazi zisizojazwa Takwimu za taarifa hiyo zinathibitisha kwamba moja wapo ya changamoto zinazokabili soko la ajira hapa nchini, ni kukosekana kwa waajiriwa wanaokidhi matarajio ya ajira. Kwa mfano, wakati kwa mwaka 2011/12 zilikuwepo nafasi za kazi 126,073 nchini kote, ni wafanyakazi wapya 74,474 tu waliweza kuingia kwenye soko la ajira kwa kipindi hicho. Kadhalika, takwimu hizo hizo zinaonyesha kuwa nafasi za kazi zipatazo 45,388 hazikuweza kujazwa katika kipindi hicho. Pa

[VIDEO]: Mazungumzo na Liberatus Mwang'ombe na Solomon Chris baada ya Uchaguzi DMV

Picha
Mubelwa Bandio kati akiwa na aliyekuwa mgombea wa nafasi za Mwenyekiti wa Jumuiya DMV Liberatus Mwang'ombe (L) na mgombea nafasi ya Katibu Msaidizi Solomon Chris (R0 wakati wa mahojiano Agosti 9, 2014, Jumuiya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia nchini Marekani ilifanya uchaguzi wake mkuu. Matokeo yake yamekuwa yakipingwa na waliokuwa wagombea wa uchaguzi huo kutokana na sababu mbalimbali. Wamaketi na Vijimambo Blog na Kwanza Production kueleza sababu hasa za kupinga matokeo hayo siku ya Jumatano ya Agosti 13, 2014. Karibu uungane nasi kusikia wanachopinga

Nilichojifunza katika maonyesho ya tatu ya wanasayansi chipukizi wiki hii

Picha
MAONYESHO ya wanasayansi chipukizi yaliyoandaliwa na T aasisi ya Young Scientists Tanzania yamefikia hatma yake wiki hii. Maonyesho haya ya siku mbili, yaliyofanyika kati ya tarehe 13 na 14 Agosti katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es salaam, yameacha mafunzo makubwa kadhaa. Kwanza, yameweza kufanya ieleweke vizuri zaidi kwamba wanafunzi wanayo hamasa kubwa ya kufanya sayansi ikiwa watawezeshwa, kinyume kabisa na madai ya mara kwa mara kwamba sayansi haipendwi na wala haifanyiki mashuleni. Washindi wa kwanza wakikabidhiwa zawadi na Dk Bilal. Picha: @bwaya Katika muda wa siku mbili hizi, nimeshuhudia namna bongo za wanafunzi wa shule za sekondari, tena nyingi zikiwa zile za kata, zinavyochemka katika kujaribu kutatua changamoto zinazowakabili. Inasisimua kuwaona wanafunzi wakijaribu kutafuta mbinu za kupambana na vyanzo vya magonjwa, uharibifu wa mazingira na kutatua changamoto zinazowakabili watu wetu katika kujiletea maelendeleo kwa ujumla. Hilo limekuwa wazi kupitia maonyes

Wanafunzi waonyesha namna teknolojia rahisi inavyoweza kurahisisha upigaji kura bila kufika kituoni

Picha
NIMEFIKA hapa Diamond Jubilee kama mwananchi anayetamani kujionea hamasa waliyonayo wanasayansi chipukizi kuonyesha kazi zao nzuri. Ni maonyesho ya tatu ya Sayansi katika ukumbi wa Diamond Jubilee ambayo hatimaye hapo kesho yatawaibua wanafunzi wawili kama washindi wa tatu wa shindano la wanasayansi chipukizi hapa nchini linaloandaliwa na Young Scientists Tanzania. Baadhi ya washiriki kwenye ufunguzi wa maonyesho leo. Picha: @bwaya Kwa hakika hamasa ni kubwa. Wanafunzi wamejawa na msisimko wa aina yake kuonyesha matokeo ya tafiti zao walizozifanya tangu mwanzoni mwa mwaka huu. Wamejawa na matumaini, hasa kwa sababu ya maneno ya ufunguzi yaliyosemwa na Mkurugenzi wa YST, Dk Kamugisha wakati akiwakaribisha asubuhi ya leo. "Tulipata maombi ya kushiriki kutoka shule zaidi ya 200...lakini ni maombi 100 pekee yalifanikiwa kupenya katika mchujo. Mpaka hapo ninyi ni washindi. Kilicho muhimu zaidi, ni kwamba pamoja na kwamba kazi zenu zitapitiwa na watu wanaoelewa vyema zaidi maene

Young Scientists Tanzania: Kujenga utamaduni wa kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu kisayansi

Picha
YAMEKUWEPO madai ya siku nyingi kwamba elimu yetu haijaweza bado kutufundisha kufikiri sawa sawa. Kwamba tunafundishwa kukariri, kukumbuka na kurudia rudia yale yale tunayofunindishwa madarasani. Hatufundishwi zaidi ya nadharia za mambo yanayojulikana tayari. Hatufundishwi kuyatazama mambo kwa macho ya kutafuta kujua yasiyojulikana. Matokeo yake, tunaambiwa, hata wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu, wamekuwa wakipata taabu kujifunza namna sahihi ya kufanya tafiti kama sehemu ya Shahada zao. Nini sababu ya hali hii? Mwonekano nje ya ukumbi wa Diamond Jubilee jioni hii. Picha: @bwaya Wengine wanasema, hatujaweka msisitizo kwenye sayansi, kwa maana ya kutafiti. Kutafuta majibu ya matatizo yetu kwa njia za kisayansi. Inasemwa, hali iko hivi kwa sababu shule zetu hazijawezeshwa. Resources. Siku zote wimbo umekuwa ni ule ule kwamba "Serikali, serikali, serikali", "Shule zetu hazina maabara...wala vifaa",  "Kukosekana kwa maabara, maana yake ni kupungua kwa