Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2008

Tuiamini sayansi? Au ni ghiliba tu?

MIONGONI mwa maeneo ambavyo sayansi imekuwa ikijihusisha nayo, elimu ya viumbe ni mojawapo. Unapozungumzia viumbe unalazimika kuanzia na uhai wenyewe, Uhai ulitokea wapi? Tunaambiwa baharini mahala ambapo viini urithi viitwavyo DNA vinaaminika kutokea kirahisi rahisi. Bahari nayo ilitokea wapi, tunajibiwa utafiti bado unaendelea, tuvute subira. Dunia yenyewe ilitokea wapi, hapo nako tunaambiwa wanaotaka kufanya Shahada ya uzamifu, wazame. Hapo hatujauliza ulimwengu uliobaki (universe). Jambo moja ni wazi. Kuwa katika sayansi, mambo yanapokuwa magumu, rufaa huwa: TUNGOJE, maarifa hukua taratibu! Lakini ni ukweli kwamba kauli hii ni kichaka kile kile cha kukimbiwa maelezo. Tukiachana na asili ya uhai, sayansi inajaribu “kupendekeza” nadharia ya utokeaji wa idai tofauti tofauti ya viumbe tulivyonavyo leo. Mahala pa kuanzia ni kwamba inavyoonekana viumbe vyote vinavyo asili moja (common ancestry). Asili hiyo ilibadilika na kufanya viumbe kwa wingi tuuonao leo. Msingi hapa ni

Changamoto za kublogu zinaendelea

Kwa siku kadhaa pamekuwapo tatizo la wavu wa mtandao hapa nilipo. Hivyo nilishindwa kuweka chochote hapa. Nadhani hali ni shwari, nitaweka chochote kuanzia sasa. Karibuni tuendelee.

Mpaka upate jibu...!

Picha
Hapa ni leo asubuhi nikiwa katika maabara. Sina hakika kama huu ulikuwa ni uchunguzi unaoitwa wa kisayansi kwa sababu nilikuwa nalazimishwa kutafuta jibu ambalo muuliza swali analitaka. Sayansi ndio ilivyo. Unatafuta kinachojulikana.

Udhaifu wa sayansi (2)

Picha
NIMEKWISHA kueleza kuwa sayansi si njia bora sana ya kuelezea masuala nyeti. Wanaofikiri kwamba sayansi ndiyo hitimisho la ufahamu, ninathubutu kusema kuwa wanakosea sana . Katika kuthibitisha madai haya, naomba kama nilivyoahidi, kukuletea mifano halisi. Tuanze na mwanasayansi maarufu katika elimu ya mada na tabia zake, bwana August Kekule. Huyu bwana (hapa pembeni) aligundua kile kinachoitwa benzene. Benzene ina umbo hili hapa kwa chini kama huwahi kuisikia. Mdude huu ni muhimu sana ( samahani sina Kiswahili chake) katika organic chemistry. Kekule ndiye aliyeugundua mdude huu wa ajabu ambao leo hii umeleta mabadiliko makubwa katika ufahamu wa mambo ya madawa na kadhalika. Itoshe kusema Benzene ni sehemu muhimu ya elimu ya viini mwili. Mvumbuzi wa umbo hili, Bw. Kikule hakuficha ukweli kwamba hilo umbo la benzene alilipata kwenye NJOZI. Huruhusiwi kushangaa. Hakufanya jaribio maabara, hapana, bali aliliota katika ulimwengu wa ndoto! Kuna watu wanadhani nime

Maajabu ya 'uchawi' wa Sayansi: Inawezeshwa na ndoto mara nyingine!

Picha
Nitaandika habari za bwana mmoja anaitwa Friedrich August Kekule yeliota dude hili hapa pembeni, linaitwa benzene. Huyu bwana ailiita benzene ndio ikawa hivi ilivyo mpaka leo. Ngoja nimalizie kakazi fulani kwanza nitakuambia zaidi.