Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2017

Mbinu za Kuchagua Kazi Itakayokupa Utoshelevu

Picha
Maamuzi ya kazi gani ufanye ni moja wapo ya mambo ya msingi yanayoathiri maisha ya mtu. Kazi iwe ya kujiajiri au kuajiriwa ndiyo maisha yako. Muda unaoutumia ukiwa kazini unaweza kuwa mwingi kuliko muda unaoutumia ukiwa kwingineko. Maana yake ni kwamba unapofikiri kazi ipi uifanye kimsingi unafanya maamuzi yatakayoathiri mfumo mzima wa maisha yako.

Mbinu za Kujenga Ujuzi wa Mwanafunzi

Picha
PICHA: Shutterstock Nakumbuka siku ya kwanza kusikia neno ‘cell’ nikiwa kidato cha kwanza haikuwa kazi rahisi kupata picha kamili. Mwalimu wetu aliandika ubaoni, ‘ cell is a basic unit of life .’ Niliduwaa. Sikujua anamaanisha nini zaidi ya kutazama kamusi kujua maana ya maneno aliyoyatumia. Mwalimu alirudia maneno hayo hayo kuweka msisitizo, na kisha akatafsiri kwa Kiswahili. Alisema, ‘maana yake ni hivi kuna kitu kidogo kisichoonekana kwa macho kwenye miili yetu kinachofanya tuishi. Mmeelewa?’  Kwa kweli hatukuwa na namna nyingine zaidi ya ‘kuelewa’ na tukaitikia, ‘ndiyo!’

Vyuo Vikuu Vinawajibika Kukuza Ujuzi wa Wahitimu Wake

Picha
Kukosekana kwa ujuzi unaohitajika katika soko la ajira ni moja wapo ya sababu kubwa zinazochangia ukosefu wa ajira unaoendelea kuwa tatizo hapa nchini. Akizungumza katika uzinduzi wa mafunzo ya uanangezi mjini Dodoma wiki iliyopita, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema waajiri wengi wamekuwa wakilalamika kuwa vijana wengi wanaoingia kwenye soko la ajira wanakosa ujuzi unaohitajika katika kazi.

Mwalimu Anavyoweza Kukuza Uelewa wa Mwanafunzi

Picha
PICHA: Sunday Adelaja Dhima kuu ya elimu iliyo bora ni kuzalisha raia wenye sifa ya udadisi. Hawa ni raia wanaofikiri kwa makini, wanaohoji mazoea, wasioridhishwa na majibu yaliyozoeleka na wenye ari ya kutafuta majibu ya changamoto zinazoikabili jamii yao. Hatua ya kwanza ya mwanafunzi kuwa mdadisi ni kuelewa kile alichojifunza. Mwanafunzi asiyeelewa maudhui ya somo, hawezi kuwa na fursa ya kufanya udadisi.

Sababu za Watu Kufanya Uchaguzi Mbaya wa Kazi

Picha
Uchaguzi wa kazi ni maamuzi anayoyafanya mtu kuanzia pale anapopata wazo la kazi anayotaka kuifanya mpaka anapostaafu. Haya ni maamuzi anayoyafanya mtu kutimiza ndoto zake kimaisha tangu anapokuwa masomoni; anapoomba kazi kwa mara ya kwanza na kuipata; anapobadilisha kazi na hata pale anapofikia umri wa kustaafu kazi.

Tumia Mbinu Hizi Kuelewa Unachokisoma -3

Picha
PICHA: thesouthern.com Siku moja nikiwa kwenye maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wanafunzi wa shahada za awali waliingia kufanya mtihani wa muhula wa mwisho wa masomo. Wakati wanaingia, mmoja wao alijigamba kwamba hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kukanyaga maktaba tangu amejiunga na chuo hicho miaka mitatu iliyopita. Nilishangaa inawezekanaje mwanafunzi wa chuo kikuu kujisifia jambo la fedheha kama hilo.

Namna ya Kutambua Kazi ya Wito Wako

Picha
Kuna mawazo yanapandikizwa kwenye fahamu za vijana kuwa mafanikio hayaji bila mtu kufanya aina fulani ya kazi. Wahubiri wa mawazo haya wanapima tija na heshima ya kazi kwa mizani ya kipato. Mtazamo huu,   kwa kiasi kikubwa, unachochewa na mfumo wa kibepari unaotukuza faida anayopata mtu binafsi dhidi ya manufaa mapana ya jamii. Katika mfumo huu, mtu anaweza kufanya kazi yoyote almuradi inamnufaisha yeye binafsi.

Tumia Mbinu Hizi Kuelewa Unachokisoma -2

Picha
PICHA: Shutterstock Katika makala yaliyopita tuliona mbinu tatu unazoweza kuzitumia kuelewa mambo unayojifunza. Kwanza, ni ‘njaa’ inayokusukuma kuelewa. Unapokuwa na ari ya kuelewa jambo, mara nyingi, utahamasika kulielewa bila kutumia nguvu nyingi. Pili, tuliona ni muhimu kutengeneza picha kubwa ya jambo unalojifunza kabla hujaanza kujifunza undani wa mambo madogo madogo ndani ya picha hiyo. Kwa mfano, unaposoma aina za vyakula, lazima kwanza uelewe vyakula. Uelewa wa jumla wa vyakula utakurahisishia kazi ya kuchanganua aina zake kwa sababu tayari unayo rejea utakayoitumia kuelewa zaidi. Mbinu ya tatu ni kukihusisha kitu unachokisoma na mambo unayoyafahamu tayari. Unaposoma aina za vyakula, kwa mfano, lazima uwe unafikiria vyakula mbalimbali unavyovifahamu katika mazingira yako. Unapojaribu kuhusianisha kile unachokisoma na maisha yako ya kila siku, unaurahisishia ubongo wako kazi ya kupokea kuliko kuingiza kitu kipya kisichohusiana kwa vyovyote vile na kile