Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2005

Naanza kublogu dini, imani, sayansi na kadhalika

Katika blogu hii natarajia kuwa naendesha mijadala kadha wa kadha. Moja, dini na imani kwa lengo la kuangalia undani wa imani zetu. Je, inawezekana kuishi bila dini? Je, kuna dini ya kweli? Je, Yesu ni Mungu? Mtume Muhammad aliuanzisha Uislam? Na maswali mengine mengi. Pili, nitapitia mara kwa mara masuala ya saikolojia na falsafa nikiamini kwamba ili tuishi vizuri na nafsi zetu lazima tujitambue. Tuzifahamu nafsi zetu na kisha tuwatambue wengine. Tatu, nitarajibu kujipenyeza kwenye mijadala ya sayansi. Ningependa kuona namna sayansi inavyohusiana au kugombana na imani.. Yapo maswali lukuki. Je, sayansi inaweza kufanya kazi bila kuwepo imani? Na je imani bila sayansi, inafaa kwa lolote? Vipi sayansi na dini vinavyoweza kufanya kazi pamoja na kadhalika na kadhalika. Changamoto kubwa, sina kompyuta wala mtandao. Tutafika tu