Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2010

Familia ya Lowassa yachunguzwa Ughaibuni

Picha
MTOTO wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa anayeitwa Frederick Lowassa anachunguzwa na Kitengo Maalumu cha Polisi wa Kimataifa wa Uingereza wanaofuatilia utata wa uhamishaji fedha kutoka Tanzania, Raia Mwema limedokezwa. Kwa habari zaidi bonyeza hapa .

Pendekezo la kitabu

Picha
Kama unataka kujielewa, kitafute hiki.

Wasemavyo wanablogu kuhusu Uchaguzi Mkuu

Ifikapo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania zaidi ya milioni 19.6 watafanya uamuzi muhimu kuhusu hatma ya nchi yao. Watafanya hivyo kupitia uchaguzi mkuu wa nne chini ya mfumo wa vyama vingi. Wakati zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi huo, ulimwengu wa blogu wa Tanzania nao unafuatilia kwa karibu yale yanayotokea katika kampeni za vyama mbalimbali. Hapa Deogratias Simba wa Global Voices on line anatukusanyia habari kutoka kwa wanablogu. Bonyeza hapa kusoma makala nzima. Ukitaka kwa kiingereza bonyeza hapa . Unaweza pia kusoma makala nyingine kupitia ukurasa huu wa kiswahili wa Global Voices.

Mnalipwa kwa kushabikia upuuzi?

TULIWAHI kujadili wakati fulani tafsiri hasa ya msomi na usomi. Mimi bado ninaamini nchi yetu ina uhaba mkubwa wa watu wenye hadhi hiyo nyeti. Wengi wetu ni wasomaji kwa maana ya kuwa na uwezo kujua vitabu vimeandikwa nini na kwa kweli ninaamini ‘wasomi’ tulioanao hawatusaidii. Tunafahamu kabisa kwamba uchakachuaji/kughushi ni sehemu muhimu ya mfumo wa elimu yetu. Ndivyo tulivyojengwa. Ndio maana hata sikushangazwa na tafiti za hivi karibuni zilizokuwa na nia ya kubashiri nani na/au chama gani kinakubalika zaidi. Wewe fikiria kama, na si mara moja, mwanafunzi anaweza kabisa kuandaa ripoti ya kisayansi mezani (bila hata kutafuta data maabara) na ikatua mikononi mwa mwalimu wake naye aipitishe; ni nini cha ajabu kwenye tafiti hizi? Umekuwepo mjadala wa kuhoji uhalali wa kuwatumia sampuli ya watu 2000 ili kujua maoni ya watu milioni arobaini. Watu wanadai how comes? Pengine ni vyema kukumbushana kuwa ni kweli inawezekana kabisa maoni ya watu elfu mbili yakajirudia rudia ama kujenga p

Tunapenda ushirikina kuliko vitabu - Prof. Mbele

Picha
"...Umaafuru wa kitabu hiki (Rich Dad Poor Dad) nilianza kuusikia huku Marekani, miaka michache iliyopita. Ni kati ya vitabu vingi ambayo vinasomwa na hao wenzetu, wakati jamii yetu ya Tanzania inaendelea kuzama katika giza au tunangojea kiongozi wa nchi au serikali ituletee maendeleo, na tukijitahidi sana, tunatumia ushirikina. Tuko tayari kulipa laki nyingi kwenye mambo ya ushirikina, eti tupate mafanikio, badala ya kununua vitabu na kuvisoma. Sasa basi, pamoja na vibuyu vyetu, wenzetu wa-Kenya, ambao wamezingatia elimu tangu zamani, wanaingia nchini mwetu na kujichukulia ajira au kuanzisha miradi. Sisi bado tunahangaika na vibuyu badala ya vitabu. Tutakoma, maana wahenga walisema kuwa asiyefunzwa na mamake hufunzwa na ulimwengu. Na bora iwe hivyo, labda hatimaye tutapata akili. Uzembe ulivyokithiri miongoni mwa wa-Tanzania, utawasikia wakilalamika mbona kitabu hiki hakijaandikwa kwa ki-Swahili? Wakishauliza hivi, wanaamini wametoa hoja nzito, badala ya kutambua kuwa wana

Pendekezo la kitabu: Rich Dad Poor Day

Picha
Kama hujawahi kukisoma hiki, kuna mengi unayakosa. Harakisha kukitafuta! Nakisoma kwa mara ya tatu sasa, sijakichoka!

Ujumbe wa Juma: Wapiga kura waumbueni REDET

"...Wapiga kura wasianze kukata tamaa kuwa CCM wataiba kura. Of course wataiba lakini ili 'kura zitoshe' watalazimika kufanya wizi wa 'mchana mweupe' (day light robbery) jambo ambalo sio rahisi sana,japo linawezekana.Wanaweza tu kuchakachua matokeo kama,kwa mfano Dokta Slaa akipata asilimia 51 na Kikwete asilimia 49.Hapo watarejea uchakachuaji kama ule wa Zanzibar.Lakini kama ni tofauti ya double digits,wanaweza kupatwa na kigugumizi katika kufanikisha ujambazi huo. Ni muhimu kutovunjwa moyo na hujuma hizi.Yatupasa kufahamu kuwa Kikwete na CCM yake ni kama mgonjwa mahututi ambaye yuko tayari hata kuning'inia kwenye uzi ili asalimike.Tutashuhudia vituko zaidi ya huo uchakachuaji wa REDET..." Kwa makala nzima bonyeza hapa . Asante sana Ndugu Evarist Chahali wa kulikoni Ughaibuni .

Ujumbe wa wiki hii

Picha
NAANDIKA makala hii kwa moyo wa upendo, mtu unayempenda ni lazima umwambie ukweli. Ukimficha ukweli unakuwa humpendi; ni kweli ukweli unauma na mara nyingi hatupendi kabisa kusikia ukweli; hata hivyo hakuna wa kutengua kwamba msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Kwa vile Mungu hatukutani naye uso kwa uso, bali tunakutana naye kupitia kwa binadamu wenzetu; ni haki kusema kwamba msema kweli ni mpenzi wa watu? Naandika kutoa ushauri na hasa maoni yangu ambayo ni ya nia njema kwa taifa letu la Tanzania. (Picha ya Kijiji cha Mjengwa) Hii ni aina ya barua ya wazi kwa wale wanaotamani kuendelea kutawala wakati miaka ya kustaafu inakaribia. Labda kuna haja ya kuongeza miaka hii ya kustaafu. Miaka sitini ya sasa watu wanakuwa bado wana nguvu na kutaka kuendelea kutumika au kula “utamu” wa uongozi. Kwa vile sasa hivi umri huu haujasogezwa mbele, kuna haja kuwakumbusha ndugu zetu ambao bado wana “Ambition” ya kutaka kuendelea na mbio hizi za hata kukalia viti muhimu kama urais na uspika, kwa

Ndivyo walivyoboresha Elimu?

CCM inajigamba sana kwamba imepanua elimu katika nchi yetu. Katika ilani yake ya uchaguzi, CCM inatuambia kwamba shule za Sekondari zimeongezeka kutoka 1745 mwaka 2005 mpaka shule zipatazo 4102 mwaka jana. Kwamba wanafunzi wanaosoma sekondari katika nchi yetu, wameongezeka kutoka 401,598 mwaka 2005 kufikia 1,401,559 hivi sasa! Kwa mtu anayehesabu mafanikio kwa kuangalia vitu na idadi, haya yanaweza kuonekana kuwa ni mafanikio makubwa sana kuwahi kufikiwa katika nchi yetu. Lakini tukitazama aina ya hao wanaoitwa wanafunzi wanaodaiwa kuwa mashuleni kwa wingi, utashangaa! Katika wanafunzi hao ni asilimia 17.8 tu ndio hufaulu kwa daraja la I. II na III. Umati mwingine unaobaki (yaani asilimia 82.2) wanaishia kupata daraja sifuri na lile la IV. Kwa maana nyingine, kwa kila wanafunzi 10 wanaofanya mtihani wa Taifa, ni wanafunzi wawili tu hupata angalau daraja la III. Hiyo ni elimu ya Sekondari hata baada ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari. Ukija kwenye elimu ya msingi ambayo n

Kuvunjika kwa koleo...

Picha
Hivi kama watu mnapendwa na wananchi, mabango haya yote ya kazi gani? Kama kweli ninyi ni chaguo la wananchi, inakuwaje mnatumia mapesa mengi hivi kuwashawishi wananchi hao hao? (picha kutoka Kijiji cha Mjengwa)

Cheka na utafakari kwa bidii!

Hii ni kauli mbiu ya mdau mmoja kwenye jukwaa la majadiliano pale Jamiiforums . Yeye anasema: Usifanye kosa kuchagua RAIS MGONJWA tukaingia hasara ya kurudia uchaguzi! Nimecheka kwa sababu nilihitaji kucheka asubuhi hii. Ila nimeikopi nikitafakari. Jumamosi njema wadau!

Ethics na somo la maisha yetu

Nimefuatilia kidogo mfululizo wa tamthilia ya 24. Kuna mhusika mkuu anayeitwa Jack Bauwer. Huyu kwake kilicho muhimu ni matokeo ya kile anachokifuatilia. Na katika kuthamini matokeo, huyu bwana hujikuta matatani sana. Kwake mbinu si jambo la maana sana hata ziwe haramu lakini mwisho (matokeo) ndicho kilicho muhimu. Na kweli huzitumia mno hadi kumfikisha kwenye matokeo aliyoyataka ambayo ndiyo yanayokuwa jawabu kwa wote. Kwamba haramu imekuwa halali kwa sababu tu mwisho umekuwa mtamu. Jack ananifanya nitafakari maisha yetu vile yanavyoelekea kubadilika ghafla. Kwamba kwa nini tunachoanza kukijali kama taifa ni mwisho (matokeo) bila kujali mbinu? Kwa nini tumeanza kuwa watu wa kutizama matokeo kwa mbinu zozote? Why? Je, ninapopata mafanikio makubwa kimaisha kwa gharama ya uhalifu wa kimaadili kwa jamii, nami tuseme nitakuwa nimefanikiwa? Vipi ninaposhinda uchaguzi kwa matumizi wa zile zinazoitwa siku hizi "siasa za maji taka" yaani kuwachafua washindani wangu ili nifaniki

Kujifunza katika upana wake!

Nimesoma majadiliano kati ya Mubelwa Bandio na msomaji wake. Nimejifunza maana ya kujifunza. Labda na wewe utajifunza. Tafadhali bonyeza hapa kusoma mazungumzo hayo niliyoyapenda sana huenda ukajifunza kujifunza. Asante Mubelwa kwa changamoto hiyo.

Tumefinyangwa kuwa wakimbizi wa kudumu

KADIRI siku zinavyosonga mbele, ndivyo waswahili tunavyozidi kuwa watu tusiojitambua. Namaanisha kutokujifahamu sisi ni akina nani na tunatofautianaje na wasio watu wengine waliobaki katika uso wa dunia. Tunashindwa kuyaelewa mazingira yetu na thamani ya ustaarabu wetu ambao (huenda) ni ushenzi kwa wengine. Badala yake tunageuza ushenzi wao kuwa ndio ustaarabu rasmi wa jamii yetu. Tunashindwa kujua mwelekeo wetu kama watu wenye ustaarabu wao ambao ndio unaoleta maana ya maisha yenye alama ya Utanzania. Matokeo ya haya matatu ni kurudi nyuma katikati ya hayo yanayoonekana kuwa ni maendeleo. Hapo ndipo tunapogeuka kuwa mazuzu wenye vitu ambavyo babu zetu hawakuwavyo lakini bado tukiishi hovyo kuliko hata walivyoishi wao. Kwa maana nyingine, tunakuwa watu wenye “zaidi” kwa habari ya vitu, lakini wenye “ukosefu” kwa habari ya thamani ya kweli ya utu wetu. Swali tunalojiuliza hapa ni iwapo ni busara kung’ang’ania kuyatafuta maendeleo (kwa maana ya vitu na huduma) pasipo kwanza kuubaini

Sisi ni nchi ya kaulimbiu?

Nimekuwa nikijiuliza: Hivi raia wa Tanzania tunatambulishwa kwa kitu gani hasa? Tuna mawazo gani ambayo tunaweza kusema, haya ndiyo mwelekeo wa Watanzania? Ni masuala yepi ambayo nje ya vyama vya siasa yanaongoza mwelekeo wa taifa letu? Maslahi ya taifa (ambayo si lazima yafananane nay a chama kimoja kimoja) ni yepi? Je, tunawafundisha nini wanafunzi wetu ambacho kinawafanya wajitambue kama Watanzania? Utamaduni wetu kama raia wa Tanzania ni upi? Tunajipambanuaje kama wananchi mahsusi wa Tanzania katikati ya bara zima la Afrika? Hivi falsafa hasa ya taifa letu ni ipi? Je, ni kasi zaidi na ari zaidi? Je, tumekuwa nchi ya "miaka mitano mitano"? Kwamba baada ya uchaguzi, viongozi wanajiandaa kwa uchaguzi ujao? Tumekuwa nchi ya kauli mbiu? Nchi yetu inaongozwa kwa mwelekeo upi? Ni nini ambacho kiongozi yeyote akishika mamlaka ndicho atakachopaswa kutusaidia tukifikie? Hakuna kitu kibaya sana kama kuishi bila dira. Hakuna ugonjwa mbaya sana kama ule wa kutokujua unakokwend

Kwa nini watu hatutulii kwenye fani tulizonazo?

Kwa nini watu wengi hutumia sehemu kubwa ya maisha yao kumangamanga huku na huko, wakibadili kazi na shughuli kutoka ofisi moja kwenda nyingine? Inakuwaje kijana aliyesoma kuwa mtaalamu wa kilimo, hataki kabisa kufanya kazi ya kilimo aliyoisomea na badala yake anatafuta kazi itakayompeleka mbali zaidi na kilimo? Kwa nini mwalimu haridhiki na chaguo lake la awali la kutokotosha fikra za wanafunzi, na badala yake anatumia sehemu kubwa ya maisha yake kutafuta namna ya kuchomoka afanye kazi zisizohusiana na ualimu? Tunatafsiri vipi kitendo cha daktari aliyesomea utabibu kwa miaka isiyopungua mitano, katika mazingira magumu ambayo hatma yake yanamfanya awatumikie wananchi wenzake kwa kuokoa maisha yao, anaachane na utabibu ili kuwa mwanasiasa wa majukwaani? Ninachojiuliza ni hiki: Kwa nini hatutulii kwenye taaluma zetu? Kwa nini hatuzitumii taaluma tulizonazo ambazo zimetupotezea miaka kibao kuzipata? Je, ni aina ya elimu tunayopata? Je, tafsiri ya mafanikio tuliyokuzwa nayo tangu t

Kanisa Katoliki na ushirikina...

Nasikitika kwamba sijawa na muda wa kutulia kuendelea na mijadala ya imani ambayo nimekuwa niiendesha huko nyuma. Mijadala hiyo imenipa uzoefu mpya ambao mwanzoni sikuwa nao. Mijadala hiyo imenifanya nishangae inakuwaje watu wenye imani ama dini kumtukana mtu anayejaribu kuhoji masuala yaliyo ndani ya dini yake. Mtu akikuonyesha upungufu wako kwa hoja, si ni bora kumshukuru? Pengine ndiyo hulka ya dini: Waamini hujadili kwa kuongozwa na ushabiki na hisia zaidi na sio hoja. Katika blogu ya Strictly Gospel ambayo ni blogu maalumu kwa mijadala ya Kikristo, nimekutana na mjadala ambao pamoja na kuwa bado haujapata wachangiaji wa kutosha, nadhani utakuwa mjadala moto moto huko mbeleni. Mjadala wenyewe unahusu uchawi wa kanisa Katoliki. Hebu bonyeza hapa kushiriki mjadala huo . Muhimu sana kushiriki kwenye mijadala. Na unaposhiriki kubali kujifunza. Ujue tumedanganywa vingi. Tumezungukwa na uongo. Katika familia zetu. Katika shule zetu. Katika siasa zetu. Dini. Na kadhalika. Na katika

Strictly gospel na mijadala ya kiimani

Nimekuwa mfuatiliaji wa karibu wa blogu maarufu ya Strictly Gospel . Tofauti na blogu nyinginezo, wachangiaji wengi wa blogu hii nawafahamu kwa sura ingawa mmiliki wake sijawahi kuonana naye. Japo mara nyingine nashindwa kushiriki mijadala hiyo ya kiimani moja kwa moja kama ambavyo huwa nashindwa kublogu humu ndani, ni karibu kila siku lazima napita pale kuona namna mijadala ya kiimani inavyokwenda. Hapa nimeupata huu hapa mmoja. Bonyeza hapa kuusoma na bila shaka utajifunza mengi. Unayo maoni yoyote? Tembelea blogu nzima hapa .

Bongo inaumwa kisichoonekana (2)

TUMEKWISHA kuona namna nchi yetu inavyopiga hatua kubwa za kimaendeleo. Na sina shaka kwamba msomaji atakuwa amebaini kwamba hizo zinazoonekana kuwa hatua za kimaendeleo zina walakini. Aidha, tulikuwa tumeishia katika kuyatazama hayo yanayoitwa maendeleo katika sekta ya elimu yanavyolisaidia taifa. Muunganiko wa muhimu ukawa ni kwa vipi rasilimali watu ambayo taifa halikuwa nayo miaka iliyopita, inatusaidia katika kusukuma “maendeleo” mbele? Hapa tungependa kudodosa namna ambavyo ukuaji wa taaluma katika maeneo mbalimbali unavyosukuma mbele maendeleo yetu ili kujaribu kuona ulikolalia ugonjwa wa taifa. ******************************************************* Tumekuwa tukifundisha wanasheria kwa miongo kadhaa sasa. Hawatoshi, lakini wapo na wnafanya kazi zao katika maeneo mbalimbali nchini. Je, watu hawa wametusaidiaje kuondokana na unyanyasaji wa kisheria tunaoupata katika jamii zetu? Taaluma ya sheria imegeuka kuwa mashindano ya kupangilia hoja ili kushinda kesi zisizo na tija.

Bongo inaumwa kisichoonekana

Ni wazi kuwa nchi ya Bongo ya miaka kadhaa iliyopita, si hii ya leo. Mambo mengi ya msingi yanabadilika na kwa kweli yanabadilika kwa kasi kubwa. Hata hivyo, ningependa kuonyesha kwamba tatizo tunalokabiliana nalo katika nchi yetu limejificha katikati ya haya tunayoyaona kama maendeleo. Tatizo hilo haliwezi kutatuliwa kwa kusogeza zaidi maendeleo kwa wananchi wala wala kwa kuanua demokrasia zaidi wala kukusanya kodi zaidi wala kwa kuongeza wasomi zaidi. Tatizo hilo linaweza kutatuliwa kwa kupembua upotofu wa aina ya maendeleo yetu tunayoonekana kuyataka zaidi na tukiyapata tunayatangaza kupitiliza. Tutazame maendeleo katika sekta ya mawasiliano. Nchi hii haijawahi kushuhudia maendeleo yaliyofikiwa hii leo katika teknolojia ya mawasiliano. Tuko juu katika nyaja ya mawasiliano baada ya kuwa tumefungua milango yote miaka ya tisini. Yapo makampuni kibao yenye wateja wanaokaribia milioni ishirini kati ya raia milioni arobaini. Na wote hao wanapigiana simu na kuandikiana ujumbe mfupi wa m

Kwa nini wewe tena Oktoba hii?

Picha
Unatusumbua! Kadiri siku zinavyosonga wajikomba sa-na Salaamu mpaka unaboa! Eti ‘mmeamkaje wapenzi wangu niwapendao…’ Fataki mkubwa wewe! Ulikuwa wapi siku zote? Kisa cha kumsalimia mtu barabarani? Umejua maana yetu eh? Hivi hukutujua siku za nyuma? Unadhani tumesahau… Sikia, Tunakumbuka nyodo zako mara chache ulizokuja Tunakumbuka kauli zako za maudhi Eti sie wako tu iwe isiwe Tukupe tusikupe haikusumbui Ukasema hata ukiwa kule sie wa hapa ni wako Sasa babu sikiliza Mwaka huu ni wa hapa hapa Wote ‘twajua huna uumini wowote Unatafutaga nini kipindi hiki? Ni hivi hivi tu waja majisidi? Wenzio ‘twaswali weye unadipu Kisa? Eti ule mpango wa mlo huko nje Unachekesha… Yaani mie mwenye njaa nikulishe wewe unayebeua! Yaani unitumie fasta, kama kondomu sina maana tena? Umesahau ulivyotufanyia siku zile? Tumekupa ukala ukaondoka? Shukrani yako sitasahau: vumbi la fo wili mjini Kama hunijui vile… Nashangaa umenirudia

‘Vijana waache kutumiwa’

Picha
JINA LA KAMALA si geni kwa wanablogu wengi. Yeye ni mwendeshaji wa blogu maarufu inayojadili (pamoja na mambo mengine) masuala ya kiutambuzi. Bonyeza hapa kuitembelea . Ndugu Kamala anajulikana pia kwa namna yake ya utoaji maoni huru katika blogu anazozitembelea ambayo hufikirisha na mara nyingine kuibua mijadala zaidi. Blogu hii ilipata fursa ya kuzungumza naye siku chache zilizopita kuhusu falsafa zake, blogu, dini, siasa na mambo yake binafsi. Karibu kujua zaidi kuhusu mwanablogu huyu anayeblogu kutokea kanda ya ziwa. ________________________________________ Ndugu Kamala, nashukuru kwa kukubali kutumia muda wako ili tuweze kujadiliana masuala mawili matatu. Labda tuanze na falsafa yako binafsi. Unaamini nini katika maisha ambacho ndicho kinachobeba utambulisho wako kama Kamala? Naamini katika utu, ubinadamu, upendo na umoja. Napenda kuelewa vitu na kudadisi na ndio maana natumia majina ya kihaya tu ninayoelewa maana yake na kwa nini yawepo… napenda kuacha maisha yaende na kuf

Mazungumzo na Kamala Luta

Siku chache zilizopita nilipata bahati ya kufanya mazungumzo mafupi na Bw. Kamala Luta, mwanablogu machachari ambaye si mara moja amewahi kuibua mijadala mizito kupitia maoni yake huru ama makala kwenye blogu yake. Kaa mkao wa kula. Nitayachapisha mazungumzo yake mapema sana namalizia kuweka koma, nukta na funga semi.

Msaada wa msamiati...

Baada ya kimya cha ukumbi huu kwa muda mrefu na mwendo wa 'kuibuka na kuzama' kwa sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu, sasa nimerejea rasmi. Tutaendelea kujadili, kuhoji, kuelimishana na hata kupotoshana inapotulazimu. Kumbuka huwezi kuelimika pasipo kupotosha mtazamo ulionao. Sasa nitangulie kuwaomba misamiati ya maneno haya kwa kiswahili fasaha: ethics, ethos, morality na morals. Nayafahamu maneno haya vizuri lakini sina maneno husika kwa kiswahili fasaha. Sipendi ule mtindo wa kutumia sentensi nzima kuelezea neno moja. Naomba mnisaidie kuongeza msamiati. Nitafurahi kupata majibu hayo hata kwa barua pepe kwa watakaopenda kutumia njia hiyo. Natanguliza shukrani za dhati!

Vitabu Uarabuni

Picha
Saa nyingine si vibaya kupitia maeneo haya. Ingawa kuna gharama zake. /> Kwa tusiopenda kazi, ikawa rahisi sana kuona kitabu cha aina hii: Lakini pia si vibaya saa nyingine kujua imani za watu zinavyosemwa na wasio ndani: Hata hivyo, hiyo ikatosha kuwa ni zawadi ya Uarabuni.

Mhe. Zitto ni mwanablogu

Picha
Pamoja na kutumia nyenzo za uandishi wa kiraia kama twitter, facebook na majamvi ya kijamii kama Jamiiforums nk, Mhe. Zitto Kabwe ni mwanablogu. Na blogu yake imesheheni elimu na maarifa ambayo tunayahitaji kwenye majikwaa haya ya kiraia. Ameitambulisha blogu yake siku chache zilizopita (tarehe 25 Mei) kwa maneno machache yafuatayo: "Ndugu msomaji, nimekuwa na blogu hapo kabla lakini sikuweza kuifanyi kazi kama invyostahili. Nimeamua kuanzisha blogu hii mpya ili liwe jukwaa la kujadiliana jinsi ya kuimarisha demokrasia nchini kwetu Tanzania, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Karibu kwa maoni, ushauri na hata makatazo!" Bonyeza hapa kumsoma , halafu uone namna mwanasiasa huyu kijana alivyotofauti na wanasiasa wazee wasiojua kingine zaidi ya redio na magazeti ya kila wiki. Hawajui kwamba zama hizo zilishapita na hazitarudi tena. Karibu sana Mhe. Zitto.

Ni usalama wa Taifa au ni ubaguzi wa rangi?

Picha
Tuko ndani ya uwanja wa ndege wa Sao Paulo, Brazil. Ni usiku, tunangoja usafiri wa kwenda Dubai, kama lisaa limoja lijalo. Nimekamata kitabu changu nasoma. Ni kitabu cha rafiki yangu kanigawia nionje yaliyomo. Yeye naye kakaa zake kimya anasoma kitabu changu pia. Saa nyingine tunafunika vitabu, tunazungumza mawili matatu, tunaendelea kupekua pekua. Ni katika kuongoja tu usafiri. Faizul, Deo, Bijoy, na mimi jijini Sao Paulo. Picha: Dr Awab Mara wanatufuata watu wawili waliovaa kiraia. Mmoja kajazia, kajichora tatuu mkononi, kavaa viatu vinavyompyaya. Mtu wa mazoezi. Mwingine mdogo dogo tu, ila shida yake hasemi kiingereza. Kwa hiyo ni "mpole fulani hivi". Baunsa anatuonesha kitambulisho chake. Ni askari wa Kibrazil. "Ninaomba kuona hati yako ya kusafiria tafadhali?"askari bonge ananiambia, mwenzie akimsaidia kwa macho. Nilisita kidogo, nikijiuliza inakuwaje aje kwangu wakati nilikuwa na wasafiri wengine. Ndicho nilichomwuliza. Baada ya kudai kuwa anafanya

Blogu zakutanisha wanablogu...!

Picha
(picha mali ya Mtanga wa Mwananchi mimi) Habari za kukutana kwa wenzetu watano nilizipokea kwa furaha kubwa. Hii kwa hakika ni hatua kubwa na ya kupigiwa mfano. Bila shaka, kama wanavyofikiri wanablogu wengine, huu utakuwa mwanzo mzuri kwa wengine wetu tukukutana mmoja mmoja na hatimaye wote kwa wakati mmoja kama walivyofanya wenzetu hawa. Hongereni sana Mwananchi mimi , Hadubini , Mtambuzi , Lundunyasa na Chacha Wambura kwa kutuonyesha njia. Wapo watu wanadhani matumizi ya majina bandia yanawasaidia. Niliona mjadala fulani kwenye mtandao wa Jamii forums ambao kwa kweli ni vigumu wanachama wake kukutana kama walivyofanya wenzetu. Bonyeza hapa uone na utafakari. Tuachane na hao wasitaka kufahamika. Turudi kwa wenzetu waliweza kuutumia mtandao mpaka wakaweza kukutana siku ile. Hivi ndivyo Ndugu Fadhy anavyosimulia tukio hili: "Muda huu hapa hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam. Tunamshukuru sana Mungu kwani leo tumeweza kukutana tena bloggers kama unavyotuona

Ya Santiago na nguvu za Kiraia

Mkutano uliokusanya wanablogu, wanahabari, wanaharakati na wanateknolojia watokao katika nchi mbalimbali umemalizika. Siku mbili za mwanzo zilihudhuriwa na watu wa kada mbalimbali kutoka hapa Chile na sehemu nyinginezo ikiwa ni pamoja na Kampuni za google, Yahoo, You tube na wengineo. Kilichokuwa muhimu sana katika siku hizo mbili za mwanzo, ni kutizama mifano ya namna uandishi wa kiraia (mablogu, twita, facebook, simu nk) ulivyoweza kushika kasi katika nchi mbalimbali zinazoendelea. Unaweza kusoma muhtasari hapa kuona namna blogu zinavyoleta mageuzi nchini Madagaska kupitia jumuiya ya wanablogu iitwayo Foko . Nilizungumza na Lova Rakotomalala juzi na nilishangazwa na jinsi jamaa wanavyoweza kufanya mambo makubwa katika mazingira magumu yanayofanana na yetu. Madagaska wamekuwa mfano mzuri wa nguvu ya uandishi wa kiraia. Siku zile mbili za mkutano zilitupa ushahidi wa wazi wazi wa namna uandishi wa kiraia unavyopamba moto katika nchi zinazoendelea. Bofya hapa uone mifano mic

Mkutano wa wanablogu Santiago

Picha
Nimepata fursa ya kukuhudhuria mkutano wa wanablogu wa jumuiya ya Global Voices unaofanyika kwenye Ukumbi wa Maktaba ya Taifa, Santiago Chile. Moja ya vivutio vya mkutano huo ni kukutana na mwanablogu wa kitanzania aishiye Australia Bw. Joe Nambiza Tungaraza na Njeri Wangari mwanablogu wa mashairi wa Kenya .

Ubabe wa dini wa kuhodhi maarifa isiyonayo

Dini kama msamiati, inaeleweka. Lakini tafsiri rasmi naweza kusema ni vigumu kuipata maana inategemeana mara nyingi na matakwa, maoni, makusudi ya huyo anayetafuta maana. Wapo wanaotafsiri dini kwa kuhusisha na dhana ya Mungu kama msingi mkuu wa dini. Wengine wanatafsiri dini kwa kuihusisha na masuala ya ‘kiroho’ yaani spirituality, hisia na imani. Wengine wanaposikia dini mawazo yao yanakimbilia kwenye ‘vyama vya ushabiki wa kiroho’ yaani makanisa, misikiti, mahekalu na vitu kama hivyo. Inachekesha kwamba neno tunalolitumia mara zote, eti linatusumbua kulitafsiri. Sababu ni kwamba tafsiri sahihi yapaswa kuwa ile itakayotuwezesha kuzikusanya ‘dini’ mbalimbali kwa pamoja. Mkusanyiko huu hauwezi kufanywa kwa matumizi ya tafsiri ya dini fulani tu. Kwa maana hiyo, tunaweza kuzikusanya dini zote kwa kusema kwamba ni jumla ya imani zinazohusiana na vile tusivyoviona kwa macho, zinazojaribu kuleta majibu juu ya mikanganyiko ya maisha ili kuleta namna fulani ya matumaini ama ridhiko la