Hivi kama watu mnapendwa na wananchi, mabango haya yote ya kazi gani? Kama kweli ninyi ni chaguo la wananchi, inakuwaje mnatumia mapesa mengi hivi kuwashawishi wananchi hao hao?
i dont think km ugonjwa ndio sela.huyo mtu kaishiwa sela ndio maana kasema hivyo isijekuwa ukienda kumpima yeye ataoneka mgonjwa kuliko huyo anayemsema.
Mimi natafakali sana, hivi kama mimi nimefanya kazi ipasavyo kwa kutimiza ahadi zangu, kuna haja gani la kutumia nguvu na ahadi mpya nyingi huku mabango makubwa yakiuuza sura!!! Wewe tulia tumia nguvu kidogo kwa kuwa umelitumikia taifa kwa miaka mitano kwa mafanikio.
Padre Karugendo ameandika haya (kwenye Tanzania Daima) kumhusu huyo jamaa kwenye hilo bango
Naandika kutoa ushauri na hasa maoni yangu ambayo ni ya nia njema kwa taifa letu la Tanzania.
Hii ni aina ya barua ya wazi kwa wale wanaotamani kuendelea kutawala wakati miaka ya kustaafu inakaribia. Labda kuna haja ya kuongeza miaka hii ya kustaafu. Miaka sitini ya sasa watu wanakuwa bado wana nguvu na kutaka kuendelea kutumika au kula “utamu” wa uongozi.
Hakuna haja ya kusubiri kuzomewa na kugomewa hadi kufikia hatua ya kukulazimisha kujitoa. Hakuna haja ya kusubiri kufanyiwa maandamano na vikao vya kukujadili kama unafaa au hapana. Ni kweli kwamba Watanzania ni wasahaulifu; wengine hawakumbuki yaliyotendeka jana.
Lakini si kweli kwamba wote ni wasahaulifu; wachache hao wanatosha kuchochea moto kiasi cha kukufanya kujuta ni kwa nini hukujikalia kimya na kufanya mambo yako.
Vidonda bado ni vibichi, hata watoto wadogo bado wanaimba Richmond na wengine kwenda mbali na kuibatiza Rich Monduli. Atakaye kuambia hili limesahaulika, atakuwa hakupendi.
Kwa vile umekubalika kwa mzee wa kimila, tosheka! Washauri na kuwaelekeza ndugu zako huko na kuingia kwenye mtandao wa wazee mashuhuri ndani ya taifa letu.
Nakubali kabisa kwamba tulifurahi pamoja, tukadhalilishwa, tukaonewa na kusikitika pamoja, sasa tusonge mbele: Ushindi ni wetu! Sina matatizo na hili. Na kama ushindi wenyewe unalenga kumhudumia Mtanzania na kumsaidia kupiga hatua kuelekea maendeleo;
Kama hautakuwa ushindi wa kujilipiza kisasi, kuchota rasilimali kiasi cha kutosha na kuwatajirisha marafiki, ndugu na jamaa. Labda mimi ningesema hivi: Tulifurahi pamoja, tukadhalilishwa, tukaonewa na kusikitika pamoja, sasa tupumzike!
Tusifikiri kwamba bila sisi hakuna kitakachofanyika. Tutoke kwenye ndoto na malengo haya ya kutaka kufika tulikolenga miaka mingi bila ya mafanikio. Sote tuna malengo, lakini si yote yanafanikiwa.
Hata hivyo tunamshukuru Mungu, na kutosheka pale tulipo! Hata wale waliostaafu na kupumzika wana mchango mkubwa katika kuliendesha taifa letu la Tanzania. Si lazima mtu uwe rais, waziri, waziri mkuu au spika wa Bunge, ndio utoe mchango wa maana.
Binafsi ningeifanya kauli mbiu hii mpya iwe hivi:Tulifurahi pamoja, tulisikitika pamoja na sasa tusonge mbele hadi ushindi, na kuishi ya maisha ya hekima, busara na ushauri zaidi ya kuwa kauli mbiu ya siasa za kiwendawazimu.
Siasa zisizo soma alama za nyakati na kukubali mabadiliko yaliyosukwa na Vision, historia na bidii ya kufanya mabadiliko hayo; siasa za ili liende, heshima na utukufu na kuendelea kuutukuza umasikini kana kwamba sisi tuliumbwa tumelaaniwa.
Kaulimbiu mpya inahitaji watu wapya, mazingira mapya na ‘vision' mpya inayochimbuka ndani ya historia ya Taifa letu; historia inayokusuta pale unapotaka kujichanganya kuendeleza ndoto zako zisizo tekelezeka.
Lakini pia ni muhimu kwamba wale unaotaka au kutamani kuwaongoza wakukubali na kukupenda vinginevyo, itakutesa wewe na kuwatesa wale unaotamani kuwaongoza.
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.
Umewahi kujiuliza kwa nini, wakati mwingine, mtu mwenye akili nzuri, mwenye weledi na uelewa mpana wa mambo, hujikuta na majanga mengi linapokuja suala la namna anavyoishi na watu? Shida ni nini? Iweje mtu aelewe mambo mengine vizuri lakini asindwe mambo madogo kama kuwa msikivu, mvumilivu wa mawazo tofauti, mwenye subira hali inayoweza kumuingiza kwenye magomvi na watu? Kinyume na tunavyoamini wengi wetu, hisia hubeba maamuzi yetu mengi na ukitazama matatizo yetu mengi ya kitabia unaweza kuona mchango mkubwa wa kushindwa kuzielewa na kuzimudu hisia zetu. Ingawa tunazipuuza, ukweli ni kwamba ukishashindwa kuzishughulikia hisia zako, uwezekano wa kukabiliana na matatizo mengi ya kimtazamo, kimaamuzi na kitabia unakuwa mkubwa. Hapa ninakuletea, japo kwa mukhtasari, elimu ya hisia, UmahiriHisia (UH) — emotional intelligence — ambao kimsingi ni uwezo kuelewa namna hisia zetu zinavyofanya kazi, kuzitambua kadri zinavyoitokeza, kuelewa nini kinazichochea, kuzirekeb...
Katika utangulizi wetu , nilieleza maana ya umahirihisia na nyanja zake tano. Nilieleza kuwa, ingawa umahirihisia una nyanja hizo tano, ukiyatazama vyema mawanda yake, unaona kuna maeneo makubwa mawili. Eneo la kwanza, ni utambuzi kwa maana ya kuelewa hisia zako, kuzifuatilia na kuzirekebu kwa maana ya kujifunza namna ya kuzimudu zisikuingize kwenye matatizo. Eneo la pili linategemea eneo la kwanza, kwa maana ya uwezo wa kutumia utambuzi huo wa hisia kuelewa namna ya kuelewa, kutambua na kuheshimu hisia za wengine kwa minajili ya kuboresha mahusiano yako na watu. Katika sehemu hii ya pili, ninajielekeza kueleza kwa ufupi jinsi gani umahirihisia unaweza kukuzaidia kuzielewa na kuzirekebu hisia zako. Umewahi kukutana na mtu mwenye uwezo mzuri wa kusoma ujumbe unaobebwa na uso wa mtu? Ukitabasamu, mwingine anaishia kwenye uso huo wenye tabasamu lakini yeye ana uwezo wa kujua kuwa pamoja na tabasamu lako, kuna kitu hakiko sawa. Unashangaa pamoja na k...
Tunaendelea na elimu ya hisia. Katika makala yaliyopita , tumejifuza msamiati wa hisia. Mbali na kutofautisha mihemuko na hisia, tumedadisi namna hisia, katika ujumla wake, zinavyobeba ujumbe. Kila hisia huja na ujumbe fulani. Umahirihisia ukuwezesha kutafakari ujumbe unaobebwa na hisia zako. Katika makala haya, ningependa tutafakari kwa pamoja namna ya kuzikebu na kuzimudu hisia zetu. Nianze na swali. Unakumbuka mazingira umewahi kujikuta ukifanya maamuzi mabaya kwa sababu hujipa muda wa kupooza hisia zako? Unakumbuka kusema jambo ukiwa na hasira, kwa mfano, halafu baadae ukajutia? Unamwandikia mpenzi wako maneno makali shauri ya hisia za wivu lakini baadae ukishapoa unagundua hukuwa na sababu ya kusema ulichokisema? Napenda nukuu moja ya mama anayeitwa Maya Angelou, “Watu wanaweza kusahau ulichokifanya. Watu wanaweza kusahau ulichokisema. Lakini watu hawawezi kusahau ulivyowafanya wakajisikia .” Unaweza kuona uzito wa hisia katika kumbuk...
Tunamalizia safari yetu ya kujifunza umahirihisia. Tumeangazia maeneo makubwa manne. Kwanza, uelewa wa hisia na sababu zake. Pili, tulitazama namna ya kurekebu hisia zetu . Kisha tukatazama namna tunavyoweza kujenga motisha na hamasa ya kufikia malengo yetu . Kisha tukaangalia namna umahirihisia unavyotuwezesha kuwasiliana na watu pasipokuzalisha migogoro isiyo na sababu. Maeneo haya manne ya umahirihisia, yanatafsirika katika mahusiano yetu na watu —namna tunavyowachukulia wasioamini tunachokiamini, namna tunavyowajibu wasiofikiri kile tunachokifikiri, namna tunavyotatua migogoro na maamuzi tunayochukua pale tunapojisikia kuonewa. Msingi wa mahusiano yenye tija na watu ni uwezo wako wa kujitambua, kutambua namna hisia na tabia zako zinavyoathiri wengine, namna unavyomudu hisia zako lakini pia kiwango chako cha upendo kwa watu. Mtu mwenye #UmahiriHisia hagombani kirahisi. Ukigombana naye anajua namna ya kujinasua na kukuachia ugomvi wako...
YAMEKUWEPO madai kwamba Uislam ulianza tangu kuumbwa kwa dunia. Na wapo watu wanaotuaminisha hayo. Ukweli ni kwamba Uislam ulianzishwa na Nabii Muhammad mwaka 622 BK huko Arabia. Kabla yake, dini zilizokuwepo zilikuwa ni Uyuda ambayo ni dini rasmi ya Wayahudi (Judaism) na Ukristo ambayo ni dini ya mataifa wasio Wayahudi ulioanza miaka kadhaa baada ya Yesu kuwa ameondoka mwaka 33BK. Yesu mwenyewe hakuanzisha Ukristo. Alisali katika misikiti ya Wayahudi. Masinagogi. Maelezo haya yana msingi wa kistoria na sio propaganda za kidini. Ndio ni propaganda kwa sababu dini zote zimekuwa na tabia ya kuonyesha kwamba zenyewe ndizo za kweli kuliko dini nyinginezo hata ikibidi kwa kuichezea historia. Na ni bahati mbaya kwamba Dini zimekuwa na tabia ya kufanana ya kuzima uwezo wa waumini wake kuhoji lolote kwa kuwajengea hofu ya kujitafutia laana. Qur’an inatupa maelezo yanayokinzana kuhusu lini hasa Uislamu ulianza. Baadhi ya mistari katika kitabu hicho zinadai kwamba ‘nabii’ Muhammad ndiye ...
Kuna kukosa ari ya kaza. Msimamizi wako asipokufuatilia na kuweka utaratibu wa kukudhibiti ufanye unachopaswa kufanya, hakuna unachoweza kuonesha kama matokeo. Huna msukumo wowote wa kujituma na wala hujisikii hatia. Hali kama hii inaweza kusabishwa na mengi. Kuna suala la mazingira magumu ya kazi. Hupati vitendea kazi unavyohitaji ili kufanya kazi yako vizuri. Kuna suala la uongozi usiojali hisia zako. Unalalamika na hakuna anayeonekana kusikia. Kuna mengi yanayoweza kukufikisha mahali ukapoteza motisha ya kazi. Wengi wanaposikia motisha wanawaza matokeo mazuri unayopata aghalau kutoka kwa mtu kama kichocheo cha kufanya kazi. “Hapa hatupewi motisha yoyote.” “Tunafanya kazi na hakuna motisha.” “Toeni motisha muone nitakavyofanya kazi.” Tunapozungumzia motisha hatuzungumzii kutambuliwa kwa kazi unayofanya, kuonekana, kusifiwa, kupandishwa cheo wala kupewa kitu kama bakhshishi ya bidii yako ya kazi. Motisha ni ile sababu inayoamsha ari ya ...
i dont think km ugonjwa ndio sela.huyo mtu kaishiwa sela ndio maana kasema hivyo isijekuwa ukienda kumpima yeye ataoneka mgonjwa kuliko huyo anayemsema.
JibuFutaMimi natafakali sana, hivi kama mimi nimefanya kazi ipasavyo kwa kutimiza ahadi zangu, kuna haja gani la kutumia nguvu na ahadi mpya nyingi huku mabango makubwa yakiuuza sura!!! Wewe tulia tumia nguvu kidogo kwa kuwa umelitumikia taifa kwa miaka mitano kwa mafanikio.
JibuFutaMpondela, hawawezi kutulia wanajua wakitulia imekula kwao.
JibuFutaPadre Karugendo ameandika haya (kwenye Tanzania Daima) kumhusu huyo jamaa kwenye hilo bango
JibuFutaNaandika kutoa ushauri na hasa maoni yangu ambayo ni ya nia njema kwa taifa letu la Tanzania.
Hii ni aina ya barua ya wazi kwa wale wanaotamani kuendelea kutawala wakati miaka ya kustaafu inakaribia. Labda kuna haja ya kuongeza miaka hii ya kustaafu. Miaka sitini ya sasa watu wanakuwa bado wana nguvu na kutaka kuendelea kutumika au kula “utamu” wa uongozi.
Hakuna haja ya kusubiri kuzomewa na kugomewa hadi kufikia hatua ya kukulazimisha kujitoa. Hakuna haja ya kusubiri kufanyiwa maandamano na vikao vya kukujadili kama unafaa au hapana. Ni kweli kwamba Watanzania ni wasahaulifu; wengine hawakumbuki yaliyotendeka jana.
Lakini si kweli kwamba wote ni wasahaulifu; wachache hao wanatosha kuchochea moto kiasi cha kukufanya kujuta ni kwa nini hukujikalia kimya na kufanya mambo yako.
Vidonda bado ni vibichi, hata watoto wadogo bado wanaimba Richmond na wengine kwenda mbali na kuibatiza Rich Monduli. Atakaye kuambia hili limesahaulika, atakuwa hakupendi.
Kwa vile umekubalika kwa mzee wa kimila, tosheka! Washauri na kuwaelekeza ndugu zako huko na kuingia kwenye mtandao wa wazee mashuhuri ndani ya taifa letu.
Nakubali kabisa kwamba tulifurahi pamoja, tukadhalilishwa, tukaonewa na kusikitika pamoja, sasa tusonge mbele: Ushindi ni wetu! Sina matatizo na hili. Na kama ushindi wenyewe unalenga kumhudumia Mtanzania na kumsaidia kupiga hatua kuelekea maendeleo;
Kama hautakuwa ushindi wa kujilipiza kisasi, kuchota rasilimali kiasi cha kutosha na kuwatajirisha marafiki, ndugu na jamaa. Labda mimi ningesema hivi: Tulifurahi pamoja, tukadhalilishwa, tukaonewa na kusikitika pamoja, sasa tupumzike!
Tusifikiri kwamba bila sisi hakuna kitakachofanyika. Tutoke kwenye ndoto na malengo haya ya kutaka kufika tulikolenga miaka mingi bila ya mafanikio. Sote tuna malengo, lakini si yote yanafanikiwa.
Hata hivyo tunamshukuru Mungu, na kutosheka pale tulipo! Hata wale waliostaafu na kupumzika wana mchango mkubwa katika kuliendesha taifa letu la Tanzania. Si lazima mtu uwe rais, waziri, waziri mkuu au spika wa Bunge, ndio utoe mchango wa maana.
Binafsi ningeifanya kauli mbiu hii mpya iwe hivi:Tulifurahi pamoja, tulisikitika pamoja na sasa tusonge mbele hadi ushindi, na kuishi ya maisha ya hekima, busara na ushauri zaidi ya kuwa kauli mbiu ya siasa za kiwendawazimu.
Siasa zisizo soma alama za nyakati na kukubali mabadiliko yaliyosukwa na Vision, historia na bidii ya kufanya mabadiliko hayo; siasa za ili liende, heshima na utukufu na kuendelea kuutukuza umasikini kana kwamba sisi tuliumbwa tumelaaniwa.
Kaulimbiu mpya inahitaji watu wapya, mazingira mapya na ‘vision' mpya inayochimbuka ndani ya historia ya Taifa letu; historia inayokusuta pale unapotaka kujichanganya kuendeleza ndoto zako zisizo tekelezeka.
Lakini pia ni muhimu kwamba wale unaotaka au kutamani kuwaongoza wakukubali na kukupenda vinginevyo, itakutesa wewe na kuwatesa wale unaotamani kuwaongoza.