Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Mikutano

CCM ni maarufu Kigoma kwa 40.2%, ikifuatiwa na CHADEMA kwa 27.2%

Picha
Utafiti huru uliofanywa na mwandishi wa makala haya, umeonesha kwamba mgombea yeyote wa nafasi ya Urais wa Chama cha Mapinduzi angeweza kuchaguliwa na wapiga kura wa Manispaa ya Ujiji/Kigoma kwa asilimia 40.2% ikiwa uchaguzi mkuu ungefanyika kati ya saa 11 mpaka saa 1 na nusu jioni ya leo.

Mwaliko wa Mkutano wa Global Voices, Dar es Salaam, Novemba 1, 2014

Tunayo furaha kubwa kutangaza mkutano wa Global Voices unaotarajiwa kufanyika Dar es Salaam, Tanzania siku ya Jumapili, Novemba 2, 2014 kuanzia saa 6 mchana hadi saa 10 adhuhuri. Mkutano huo utafanyika kwenye Kituo cha Teknolojia na Mambo ya Jamii, KINU , washirika wa Global Voices Swahili hapa nchini.

Siku ya Blogu Oktoba 16: Shiriki Kujadili Dhana ya Kutokuwepo kwa Usawa

Picha
Tangu 2007, Siku ya Wajibu wa Blogu Duniani imekuwa ikitumika kuwaweka pamoja wanablogu kutoka duniani kote ili kujadili mada muhimu zinazokuwa zimewekwa mezani. Siku hiyo, wanablogu kwa pamoja, huwa utaratibu wa kuvamia anga la blogu kwa kuchapisha maelfu ya posti kuhusu masuala ya maji, mabadiliko ya tabia nchi, umasikini, chakula na nguvu ya pamoja. Kwa mara nyingine mwaka huu, Global Voices Online inayo fahari kuwa mshirika rasmi wa siku hiyo.

Nilichojifunza katika maonyesho ya tatu ya wanasayansi chipukizi wiki hii

Picha
MAONYESHO ya wanasayansi chipukizi yaliyoandaliwa na T aasisi ya Young Scientists Tanzania yamefikia hatma yake wiki hii. Maonyesho haya ya siku mbili, yaliyofanyika kati ya tarehe 13 na 14 Agosti katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es salaam, yameacha mafunzo makubwa kadhaa. Kwanza, yameweza kufanya ieleweke vizuri zaidi kwamba wanafunzi wanayo hamasa kubwa ya kufanya sayansi ikiwa watawezeshwa, kinyume kabisa na madai ya mara kwa mara kwamba sayansi haipendwi na wala haifanyiki mashuleni. Washindi wa kwanza wakikabidhiwa zawadi na Dk Bilal. Picha: @bwaya Katika muda wa siku mbili hizi, nimeshuhudia namna bongo za wanafunzi wa shule za sekondari, tena nyingi zikiwa zile za kata, zinavyochemka katika kujaribu kutatua changamoto zinazowakabili. Inasisimua kuwaona wanafunzi wakijaribu kutafuta mbinu za kupambana na vyanzo vya magonjwa, uharibifu wa mazingira na kutatua changamoto zinazowakabili watu wetu katika kujiletea maelendeleo kwa ujumla. Hilo limekuwa wazi kupitia maonyes...

Unaionaje Dublin kupitia jicho langu?

Picha
Leo nimepata bahati ya kutembea kidogo katika jiji la Dublin. Gari linalotumika kumwezesha mgeni kusafisha macho. Picha: @bwaya         Majengo ya zamani yanayovutia. Picha: @bwaya Mitaa yenye majengo yanayoitwa ya 'King George' wa Uingereza. Ireland ilikuwa koloni kwa miaka mingi. Picha: @bwaya Mto katikati ya Dublin. Picha: @bwaya Mavazi ya wa-Irish Picha: @bwaya Magogoni ya Ireland. Picha: @bwaya

Kupanda na kushuka kwa dini nchini Ireland

Picha
Nimebahatika kutembelea Chuo Kikuu cha Taifa Maynooth, Dublin Ireland. Ni chuo cha zamani sana tangu enzi hizo kikiwaandaa makasisi, kikiitwa St Patrick College. Maynooth University, Ireland. Picha: Jielewe Jambo la ajabu, nimeona picha zinazoeleza idadi ya wanafunzi waliokuwa wanajiunga kuchukua masomo hayo ya Upadre kila mwaka. Idadi inaonekana kupungua kila mwaka, mpaka walipoamua kukigeuza kuwa Chuo Kikuu kifundishe mambo mengine. Madhari ya Maynooth, Dublin. Picha: Jielewe Kwa ujumla, msisimko wa dini haupo nchini humu. Makanisa mengi ya Kikatoliki yamefungwa au kugeuzwa matumizi kusaidia shughuli nyingine. Kanisa maarufu nikiwa jengo la makumbusho. Picha: Jielewe 'Nikiwa hapa, ndiyo kwanza kashfa za makasisi kudhalilisha watoto zinapamba moto. Mambo yamebadilika. Sanamu ya Papa John Paul II alipotembelea hapa. Picha: Jielewe Dublin, mji mkuu wa Ireland ndiko yaliko makazi ya makampuni makubwa ya teknolojia. Ndiko waliko Yahoo! Na makampuni meng...

Waholanzi na utamaduni wa baiskeli, sisi tunakimbilia magari binafsi

Picha
 Wakati sisi tunashindana kwenda kazini na magari ya bei mbaya, wenzetu wanakuja kazini na baiskeli. Hapa ni Ede, Uholanzi. Baiskeli ndio usafiri maarufu. Jambo hili si la kawaida. Fikiria, mwanafunzi wa mwaka wa kwanza Chuo Kikuu achilia Profesa wake, apande baiskeli kwenda chuoni. Kwa hakika ni jambo unaloweza kuliewa pale Dar es salaam. Waholanzi wakiwa wamepaki vyombo vyao vya usafiri. Picha:Jielewe Katika mazingira haya ambapo kila mtu anatafsiri maendeleo kwa kuangalia vitu, na katika mazingira ambayo kila mtu yuko tayari kuonekana naye yupo hata ikibidi kwa mkopo, almuradi aendeshe gari, ni vigumu kupata ufumbuzi wa 'kero' ya kudumu ya foleni jijini Dar es Salaam.  Kila mmoja anafikiri kutatua kero hii kwa kuongeza gari barabarani. Foleni itoke wapi kwa mazingira haya? Picha: Jielewe Kituo cha elimu MDF, Ede, Uholanzi. Picha: Jielewe Hebu fikiri kama watu wangeamua kutumia usafiri wa umma, huu huu uliopo, magari mangapi yangeondoka barabarani? Saa ...

Mitaa ya Nairobi, 'Usomini UoN'

Picha
Chuo Kikuu cha Nairobi, kinachosemekana kuwa moja wapo ya vyuo bora Afrika Mitaa ya Chuo Kikuu cha Nairobi Ndani ya Chuo, karibu na duka la vitabu Bustani za wazi katika maeneo ya Chuo Kikuu cha Nairobu Kama ni kweli, sehemu hii haihusiki basi sawa sawa Sijui nielekee wapi, huku au kule? Alama ya utambulisho wa Chuo Kikuu cha Nairobi

Nilipokutana na Mshairi Serina wa Upande Mwingine

Picha
Katika mkutano wa wanablogu na waandishi wa habari za kiraia uliofanyika Nairobi, Kenya, nimebahatika kukutana na mwanablogu niliyekuwa na hamu sana ya kuonana naye. Naye si mwingine bali, dada Serina Kalande, anayetuandikia kwenye blogu ya Upande mwingine . Na Serina Kalande, wa Upande mwingine. Picha: Deogratias simba Ni dada mkarimu, mpole, mwanana na mwema sana kuzungumza naye. Serina, asante kwa baraka ya kukuona.

Ni usalama wa Taifa au ni ubaguzi wa rangi?

Picha
Tuko ndani ya uwanja wa ndege wa Sao Paulo, Brazil. Ni usiku, tunangoja usafiri wa kwenda Dubai, kama lisaa limoja lijalo. Nimekamata kitabu changu nasoma. Ni kitabu cha rafiki yangu kanigawia nionje yaliyomo. Yeye naye kakaa zake kimya anasoma kitabu changu pia. Saa nyingine tunafunika vitabu, tunazungumza mawili matatu, tunaendelea kupekua pekua. Ni katika kuongoja tu usafiri. Faizul, Deo, Bijoy, na mimi jijini Sao Paulo. Picha: Dr Awab Mara wanatufuata watu wawili waliovaa kiraia. Mmoja kajazia, kajichora tatuu mkononi, kavaa viatu vinavyompyaya. Mtu wa mazoezi. Mwingine mdogo dogo tu, ila shida yake hasemi kiingereza. Kwa hiyo ni "mpole fulani hivi". Baunsa anatuonesha kitambulisho chake. Ni askari wa Kibrazil. "Ninaomba kuona hati yako ya kusafiria tafadhali?"askari bonge ananiambia, mwenzie akimsaidia kwa macho. Nilisita kidogo, nikijiuliza inakuwaje aje kwangu wakati nilikuwa na wasafiri wengine. Ndicho nilichomwuliza. Baada ya kudai kuwa anafanya ...

Blogu zakutanisha wanablogu...!

Picha
(picha mali ya Mtanga wa Mwananchi mimi) Habari za kukutana kwa wenzetu watano nilizipokea kwa furaha kubwa. Hii kwa hakika ni hatua kubwa na ya kupigiwa mfano. Bila shaka, kama wanavyofikiri wanablogu wengine, huu utakuwa mwanzo mzuri kwa wengine wetu tukukutana mmoja mmoja na hatimaye wote kwa wakati mmoja kama walivyofanya wenzetu hawa. Hongereni sana Mwananchi mimi , Hadubini , Mtambuzi , Lundunyasa na Chacha Wambura kwa kutuonyesha njia. Wapo watu wanadhani matumizi ya majina bandia yanawasaidia. Niliona mjadala fulani kwenye mtandao wa Jamii forums ambao kwa kweli ni vigumu wanachama wake kukutana kama walivyofanya wenzetu. Bonyeza hapa uone na utafakari. Tuachane na hao wasitaka kufahamika. Turudi kwa wenzetu waliweza kuutumia mtandao mpaka wakaweza kukutana siku ile. Hivi ndivyo Ndugu Fadhy anavyosimulia tukio hili: "Muda huu hapa hoteli ya Movenpick jijini Dar es Salaam. Tunamshukuru sana Mungu kwani leo tumeweza kukutana tena bloggers kama unavyotuona...

Ya Santiago na nguvu za Kiraia

Mkutano uliokusanya wanablogu, wanahabari, wanaharakati na wanateknolojia watokao katika nchi mbalimbali umemalizika. Siku mbili za mwanzo zilihudhuriwa na watu wa kada mbalimbali kutoka hapa Chile na sehemu nyinginezo ikiwa ni pamoja na Kampuni za google, Yahoo, You tube na wengineo. Kilichokuwa muhimu sana katika siku hizo mbili za mwanzo, ni kutizama mifano ya namna uandishi wa kiraia (mablogu, twita, facebook, simu nk) ulivyoweza kushika kasi katika nchi mbalimbali zinazoendelea. Unaweza kusoma muhtasari hapa kuona namna blogu zinavyoleta mageuzi nchini Madagaska kupitia jumuiya ya wanablogu iitwayo Foko . Nilizungumza na Lova Rakotomalala juzi na nilishangazwa na jinsi jamaa wanavyoweza kufanya mambo makubwa katika mazingira magumu yanayofanana na yetu. Madagaska wamekuwa mfano mzuri wa nguvu ya uandishi wa kiraia. Siku zile mbili za mkutano zilitupa ushahidi wa wazi wazi wa namna uandishi wa kiraia unavyopamba moto katika nchi zinazoendelea. Bofya hapa uone mifano mic...

Mkutano wa wanablogu Santiago

Picha
Nimepata fursa ya kukuhudhuria mkutano wa wanablogu wa jumuiya ya Global Voices unaofanyika kwenye Ukumbi wa Maktaba ya Taifa, Santiago Chile. Moja ya vivutio vya mkutano huo ni kukutana na mwanablogu wa kitanzania aishiye Australia Bw. Joe Nambiza Tungaraza na Njeri Wangari mwanablogu wa mashairi wa Kenya .

Tangazo la Mkutano Mkuu wa Uanahabari wa Kiraia wa Global Voices 2010

Picha
Mkutano wa wanablogu wa Global Voices, utafanyika Mjini Santiago mwezi Mei tarehe 6 na 7 mwaka huu. Nimezipata habari hizo kupitia ukurasa wa kiswahili wa mradi wa Lingua Swahili . Nimetamani kama na sisi tungekuwa tunapanga kukutana siku fulani mwaka huu! Inawezekana! Ni muhimu tuanze kufikiri kukutana uso kwa uso hata kama matanga ya ile Jumuiya yetu hajapita bado.

Mkutano wa Copenhagen: Ugaidi wa kimaendeleo

Picha
Hivi sasa dunia yetu inapitia kipindi kigumu kuliko wakati mwingine wowote. Joto limeongezeka sana. Barafu inayeyuka. Kina cha maji kinaongezeka kwa kasi na kwa kweli ndani ya kipindi kifupi, baadhi ya visiwa vitafurikwa na maji kikiwamo kile cha Zanzibar. Majanga haya yote yamesababishwa na akili ya mwanadamu mwenye fikra potofu ya kile kinachoitwa MAENDELEO. Mwanadamu wa sasa (wa kileo) ndiye hasa chanzo cha dhahama yote hii ambayo kwa sasa imefanyiwa Mkutano maalumu kule Copenhagen ambao ninaamini utaishia wale jamaa kupiga picha ya pamoja na kuja na matamko ya kisiasa then maisha yataendelea kama kawaida. Bonyeza hapa kujua kinachoendelea kwenye mkutano huo na tayari mashindano ya matamko yameanza. Ningependa tufanye tathmini ndogo ya namna ambavyo akili ya mwanadamu wa leo anayejiona kuwa kaendelea kuliko wengine wote waliopita. Moja. Mwanadamu wa leo ameshindwa kabisa kutatua tatizo la utumiaji (ukwapuaji) wa vyanzo vya asili. Akikwapua vikaisha, anahamia kwingine. Aki...