Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2009

Aprili: Utasoma vitabu vingapi?

Mkesha wa kuukaribisha mwezi mpya ndio huu. Kesho tutauanza mwezi mpya kwa siku iitwayo 'ya wajinga'. Masuala ya kuangazia kidogo: Ni kwa kiasi gani umepoteza muda mwingi pasi na sababu ya msingi? Soga. Stori zisizojenga. Kuwakatisha tamaa watu. Mabishano. Na kadhalika. Na kadhalika. Umesafiri kilomita ngapi mwezi huu? Hebu fikiria, kama ungeamua kuzitumia kilomita hizo kusoma, ungesoma vitabu vingapi? Kwa mwezi Machi, umeweza kusoma vitabu vingapi? Ni fedha kiasi gani umetumia kununua vitabu? Utasema hela hazitoshi. Hivi unajua ni shi'ngapi umeteketeza kwa kukwangulia vocha mwezi huu? Umekwangua vocha kusaidia kusambaza 'text messages' za mizaha! Umeona ulivyo na fedha? Haya. Hima na tuanze kuzitumia hizo hizo vitabuni mwezi huu! Na tusome. Mwezi Aprili uwe ni wa kusoma.

Wasomi wanakimbia fani, ama wanakimbizwa?

Inasemekana wasomi wanakimbilia siasa. Wanaowaunga mkono wanasema serikali haijali utaalam wao. Inawakejeli kwa malipo kiduchu. Wao, kwa kuona kuwa siasa zinalipa, wanaamua kuzitelekeza fani zao wanakimbilia majimboni kwa lengo la kupata maslahi manono. Inasemwa pia kuwa siasa nayo inawahitaji wataalam kama Maprofesa, Madaktari wa Falsafa na watu kama hao. Kwamba ubobevu wao unatoa mchango mzuri likija suala la maamuzi. Je, ni kweli wanasaidia katika maamuzi? Je, si kweli kwamba kila aina ya ufisadi tunaousikia leo umefanyika mikononi mwa wasomi? Wamesaidia nini? Wanaowapinga, wanasema kuwa elimu yao ilipaswa kujikita katika kuileta jamii maendeleo kupitia fani walizobobea bila kujali serikali inawajali ama la. Kwamba wangejikita vema katika fani zao, ni lazima wangeyapata mafanikio hayo wanayoyafuata katika siasa. Wanasema, kuna ulazima gani wa kila mtu kukimbilia siasa ili kufanikiwa? Je, siasa ndio kila kitu? Je, kukimbilia siasa si dalili ya ufinyu wa elimu yetu? Wanashin

Tunawezaje kutunza muda katika mazingira haya?

Unaamka asubuhi na mapema. Unagusa tepu ya maji uoge, lahaula, yamekatika. Unaokoteza matone machache, unafanikiwa 'kupiga paspoti' kuondoa harufu ya kikwapa. Chai. Umeme haupo. Luku imekata. Hivyo umepanga kwenda benki kisha intaneti, halafu ununue luku, na kupita pita panapowezekana siku hiyo. Shughuli ya kwanza, benki. Kwenda ilipo benki ni shughuli inayohitaji uvumilivu. Unamaliza masaa mawili njiani. Foleni ndefu. Hatimaye unafika benki. Kwenye mashine ya kuchukulia fedha, foleni ndefu. Unangoja kwa karibu saa moja ili kuifikia. Bahati mbaya, unapokaribia unasikia malalamiko, mashine 'imezira' kazi. Hujui ufanyeje. Unaenda kujaribu kwingine, unafanikiwa baada ya kama saa moja. Ishakuwa saa saba, hujatia chochote kinywani. Unaamua kwenda kula. Hotelini wanasema chakula ulichoomba bado kiko jikoni bado, wameamua kutumia mkaa umeme (wa dharura) umekatika. Kwa vile ilivyo joto, unaamua kukingoja badala ya kuungulia juani. Unamalizia saa kamili ukiwa pale. Ba

Uwongo unalipa sio?

Kwa jinsi ambavyo kujielewa ni kazi nzito, waungwana tuko tayari tuambiwe uwongo tufurahi, turidhike. Kuliko tunaambiwe ukweli unaouma, uwezao kutubadilisha. Kwa maana nyingine tunafanya bidii kusikia tunachotaka kusikia.

Maneno ya kuepa unapozungumza

Unaweza kuwa unaamini huna dharau. Lakini watu ndivyo wanavyokuona. Yaani vile ujichukuliavyo, sivyo wanavyokuchukulia wenzio. Hali hii inaweza kuchangiwa kwa kiasi kikubwa na maneno unayotumia katika kuwasiliana na watu. Maneno, hata yale madogo madogo, yana nguvu kuliko tunavyoweza kufikiri. Hebu tuangalie mifano michache kuonyesha athari za maneno mawili, 'najua' na 'lakini'. 1. Najua: Unapomjibu mtu anayekuambia jambo kwa neno 'najua', unatoa picha kwamba wewe ni 'machinoo'. Hata kama ulishakijua kinachosemwa, si uungwana kusema '...hiyo nlishajua mbona...?' au '...ah, nshafikiri kabla...'. Sema '...nafurahi kusikia hivyo..' 'Najua' inaleta picha kwamba unajidai kuwa na taarifa nyingi, mjuaji, usiyekubali kujifunza kwa wenzako, unawadharau wenzako na sifa nyingine mbaya mbaya. 2. Lakini: Inakuwa pale unapoanza na kila namna ya sifa nzuri, halafu unaishia na 'lakini' kuonyesha upungufu uliouona

Methali! Methali!

Wahenga walilonga: " La kuvunda..."

Ukiingalia vizuri picha hii unaona nini?

Picha

Wacha CNN watudhalilishe...!

Sijui kwako. Huenda hili halikusumbui na pengine kinachonishangaza mimi hakina uzito stahiki kwako. Lakini binafsi huwa najisikia fedheha Afrika inapotangwa vibaya na vyombo vya magharibi vikiongozwa na CNN. Pamoja na kulaani ushabiki mbaya unaofanywa na vyombo hivyo, bado kuna kila dalili kwamba huenda tunavyotangazwa ndivyo tulivyo. Hebu tuone mifano michache. Inakuwaje anapopita mzungu, watoto mtaa mzima wanachokikumbuka cha kwanza ni '...mzshungu naomba hela...'? Tumewaleaje wanetu? Kwamba ipo ngozi yenye kumaanisha hela kuliko nyingine? Na hii si kwa watoto tu, hata watu wazima wenye elimu kubwa, wanapokutana na rafiki wa kizungu, kwao hiyo ni fursa muhimu ya kutengeneza fedha. Rafiki mzungu ni 'dili' uswahilini na ukionekana una ukiongozana naye watu wanakuona 'umeula'. Nenda Moshi na Arusha uone waswahili tunavyojidhalilisha. Jamaa wanawalazimisha wazungu kununua kitu wasichokitaka kwa kiingereza cha kuunga-unga na kamba. Mzungu wa watu ataghasiw

Jumuiya yetu isife bila taarifa...

Picha
(picha kutoka Mawazoni bila ruhusa) Ningependa kumwomba mheshimiwa Katibu Mtendaji wa JUMUWATA ruhusa ya kuuliza swali hili. Tumefikia wapi na ile Jumuiya ya Wanablogu Tanzania? Mnaonaje tukifanya mjadala wa wazi kuhusu 'ufufuaji' wa jumuiya yetu? Jamani yasijeyakawa yale ya mwaka elfu tisa mia sabini na saba.

Usiyetaka kukosea...

KUNA watu huamini kabisa kukosea kwao hakupo. Kukosea ni kudhalilika. Wanasahau kukosea ni sehemu ya kupatia. Na kupatia hakuwezi kuwepo bila kukosea. Wanasahau 'wasiokosea' ni wale wasiofanya lolote jipya. Waoga wa kujaribu. Waoga wa kukoselewa. Ndio maana kwao, kuomba msamaha ni sehemu ya adhabu dhalili. Je, ni haki kuwalaumu 'wakosefu'?

Kutoka kwa Da'Subi, unaelewa picha hii ilivyo?

Picha
Ukiiangalia kwa makini picha hii, utaamua mwenyewe ikiwa hawa jamaa wanajenga darini ama sakafuni? HIyo ngazi iliyowekwa ina kazi gani? Huu ni mfano mzuri wa jinsi akili zetu zinavyofanya kazi. Unakifikiri kinatokana na ulichokiingiza ubongoni mwako kabla.

Ukiona watu wazima wanaumbuana hadharani...

Ukiona watu wazima wa nyumba moja Wanaodai kwao umoja ndio sera Hadharani wanaonyana na kuumbuana Nini maana yake? Ndani ku shwari?

Unaona nini kwenye picha hii?

Picha
Ukitazama picha hii kwa makini, unaweza kubaini utata fulani wa kimaamuzi. Ukiitazama kwa haraka haraka, huwezi kuuona utata huo na hivyo huwezi kukubaliana na mtazamaji mwingine atakayedai kuuona utata usiouona wewe. Sasa itazame kwa makini kadiri unavyoweza halafu ujiridhishe kwamba unachokiona ndicho kinachopaswa kuonwa. Heri ya mwezi mpya.