Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2006

Tumkaribishe mgeni jamani!

Nadhani zile makala za Ndesanjo zinafanya kazi kubwa kuliko tunavyodhani. Hatimaye Bw. Albert William ambaye alikuwa Afrika ya Kusini wiki jana katika mpango uitwao "Teaching and AIDS Pandemic" , amekata shauri rasmi. Yeye anasema anapendelea kutumia ung'eng'e zaidi. Kong'ori hapa kumtembelea mgeni kama ilivyo ada. Mpango huu unafanyika katika Afrika ukilenga kuvunja kimya na kuangalia upya namna ya kupambana na Janga la UKIMWI kwa kuwatumia waelimishaji katika sekta ya elimu "Teacher Educators". Huyu bwana ana mengi ya kusema kuhusu masuala haya ya UKIMWI.

Elimu yetu haikidhi haja

Elimu tunayoipata darasani imekaa kikoloni sana kiasi kwamba tunafunzwa kuwa watumwa waaminifu zaidi kuliko kujikomboa na wale maadui tunaodai kuwa tunapambana nao. Ujinga, maradhi na umasikini. Tatizo linaanza katika mitaala yenyewe inayosisitiza kujifunza mambo ya watu wengine ambayo hayana uhusiano na maisha yetu ya kawaida baada ya masomo ambayo kimsingi ni ya kijijini. Tunalishwa falsafa za kigeni zaidi kiasi kwamba tunafika mahali tunadharau kila kinachoonekana kuhusiana na ukwetu-kwetu. Kuna ukweli fulani kuwa watu "waliokwea madarasa" hawataki tena kwenda vijijini kutoa mchango wao katika maendeleo. Hiyo ni kusema kwamba elimu hii inaonekana kushawishi waungwana kukimbilia mijini huku wakiwaacha wale waliowapeleka shule wakiendelea kuteketea vijijini kwa matatizo yanayotatulika. Elimu yetu inatusaidia kukariri na kuhamisha mawazo ya watu badala ya tafakuri za kina katika maisha. Ndio maana inakuwa ngumu kwa wengi wetu kuhamishia mawazo ya darasani kuja mtaani. Maana m

Vazi la Taifa: Imeshindikana?

Picha
Yapo mambo mengi ambayo tumekuwa tukiyaimba tangu kupata uhuru lakini mpaka leo inasikitisha kuona kuwa yameshindikana. Tuanadanganyana. Mfano ni hili suala la umasikini wetu. Watawala wamekuja na kuondoka, lakini tatizo liko pale pale. Tunaambiwa kuwa "bado tunaweka misingi ya maendeleo yetu, tufunge mikanda!". Miaka 40 na ushei hakuna lolote! Niliwahi kusoma makala ya Bwenge katika Gazeti la Rai nikachoka kabisa. Kwamba Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikitumia maneno kwa ufundi na ungalifu mkubwa ili kukwepa hoja za wananchi kuhusu mambo ya msingi. Bwenge anatoa mfano wa yale mabango ya Kampeni ya CCM yaliyokuwa na picha ya mgombea wao wa Urais (Sasa Rais) na ile ya Mzee Mkapa. Upande wa Mkapa unakutana na maneno "uchumi unakua, ajira zinaongezeka n.k" Profesa Bwenge anasema CCM hawakutumia "me" (sijui ndio herufi au neno sijui)ili kusema "uchumi umekuwa". Wakiulizwa mbona tunalala njaa, jibu linakuwa rahisi: "Ndio. Lakini tumesema uchumi un