Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2013

Unaionaje Dublin kupitia jicho langu?

Picha
Leo nimepata bahati ya kutembea kidogo katika jiji la Dublin. Gari linalotumika kumwezesha mgeni kusafisha macho. Picha: @bwaya         Majengo ya zamani yanayovutia. Picha: @bwaya Mitaa yenye majengo yanayoitwa ya 'King George' wa Uingereza. Ireland ilikuwa koloni kwa miaka mingi. Picha: @bwaya Mto katikati ya Dublin. Picha: @bwaya Mavazi ya wa-Irish Picha: @bwaya Magogoni ya Ireland. Picha: @bwaya

Kupanda na kushuka kwa dini nchini Ireland

Picha
Nimebahatika kutembelea Chuo Kikuu cha Taifa Maynooth, Dublin Ireland. Ni chuo cha zamani sana tangu enzi hizo kikiwaandaa makasisi, kikiitwa St Patrick College. Maynooth University, Ireland. Picha: Jielewe Jambo la ajabu, nimeona picha zinazoeleza idadi ya wanafunzi waliokuwa wanajiunga kuchukua masomo hayo ya Upadre kila mwaka. Idadi inaonekana kupungua kila mwaka, mpaka walipoamua kukigeuza kuwa Chuo Kikuu kifundishe mambo mengine. Madhari ya Maynooth, Dublin. Picha: Jielewe Kwa ujumla, msisimko wa dini haupo nchini humu. Makanisa mengi ya Kikatoliki yamefungwa au kugeuzwa matumizi kusaidia shughuli nyingine. Kanisa maarufu nikiwa jengo la makumbusho. Picha: Jielewe 'Nikiwa hapa, ndiyo kwanza kashfa za makasisi kudhalilisha watoto zinapamba moto. Mambo yamebadilika. Sanamu ya Papa John Paul II alipotembelea hapa. Picha: Jielewe Dublin, mji mkuu wa Ireland ndiko yaliko makazi ya makampuni makubwa ya teknolojia. Ndiko waliko Yahoo! Na makampuni meng

Guiness: Alama ya Taifa la Ireland

Picha
Kiwanda kinacholinda heshima ya walevi, Dublin, Ireland. Picha: Jielewe Katika bidhaa wanayojivunia wa-Irish, ni pombe maarufu ya Guiness. Ukikatiza mitaa saa za usiku baada ya kazi, wanywaji (najua ni kosa kubwa kuwaita walevi) hawanywi pombe nyinine zaidi ya Guiness. Kila baa ni Guiness. Nawambia mwenyeji wangu sinywi pombe, wananishangaa. 'Utarudije kwenu hujanywa Guiness?' Alama ya Guiness ni nembo ya Taifa. Pombe ni urithi wa taifa. Picha: Jielewe Kitu kingine ambacho nimekigundua, kumbe ile nembo ya Guiness unayoiona, ndiyo nembo ya Taifa. Kwa maana nyingine, wakati sisi urithi wetu ni Ngorongoro na mbuga za wanyama, hawa jamaa, urithi wao ni pombe. Pombe ni urithi wa taifa. Natania. Mtaani kweli imepangwa. Hongereni. Nimekumbuka kwetu. Sisi ni wazalishaji wakubwa wa bangi na mirungi tena kwa wingi sana ingawa kwa siri. Wa-Irish ni wazalishaji wakubwa wa Pombe. Sote letu moja. Unalijua?

Nilipozungumza na blogu ya Maneno Matamu: “Kiswahili ni alama ya Uafrika wangu.”

Picha
Yafuatayo ni mahojiano yangu na blogu ya Maneno Matamu kuhusu, pamoja na mambo mengine, suala la lugha za Kiafrika na nafasi ya blogu katika kukuza lugha hizo katika enzi hizi. Ulianza kuandika blogu mwaka 2005. Uliamuaje kushiriki katika mtandao wa Internet namna hii? Nakumbuka nikiwa mwanafunzi nilikuwa mfuatialiaji mzuri wa makala za mwandishi maarufu,   Ndesanjo Macha   (ambaye sasa ni Mhariri wa Global Voices eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara). Yeye ni mwanablogu wa kwanza wa Kiswahili. Na kwa kweli niilivutiwa sana na aina yake ya uandishi, mijadala aliyokuwa akiiendesha kwenye blogu yake pamoja na matumizi mazuri ya lugha. Kwa hiyo hamasa ya kublogu ilitokana na  blogu yake . Blogu kwangu niliiona kama fursa nzuri na rahisi ya kujadili masuala ninayoyaelewa vizuri ya kiutambuzi na sayansi. Mule niliona ingekuwa rahisi kupata jukwaa la kubadilishana mawazo na watu bila kikwazo chochote na pia pasipo kulazimika kuonana nao. Si tu ninaelimisha kama ninavyofikiri, lak