Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2010

Ndivyo walivyoboresha Elimu?

CCM inajigamba sana kwamba imepanua elimu katika nchi yetu. Katika ilani yake ya uchaguzi, CCM inatuambia kwamba shule za Sekondari zimeongezeka kutoka 1745 mwaka 2005 mpaka shule zipatazo 4102 mwaka jana. Kwamba wanafunzi wanaosoma sekondari katika nchi yetu, wameongezeka kutoka 401,598 mwaka 2005 kufikia 1,401,559 hivi sasa! Kwa mtu anayehesabu mafanikio kwa kuangalia vitu na idadi, haya yanaweza kuonekana kuwa ni mafanikio makubwa sana kuwahi kufikiwa katika nchi yetu. Lakini tukitazama aina ya hao wanaoitwa wanafunzi wanaodaiwa kuwa mashuleni kwa wingi, utashangaa! Katika wanafunzi hao ni asilimia 17.8 tu ndio hufaulu kwa daraja la I. II na III. Umati mwingine unaobaki (yaani asilimia 82.2) wanaishia kupata daraja sifuri na lile la IV. Kwa maana nyingine, kwa kila wanafunzi 10 wanaofanya mtihani wa Taifa, ni wanafunzi wawili tu hupata angalau daraja la III. Hiyo ni elimu ya Sekondari hata baada ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari. Ukija kwenye elimu ya msingi ambayo n

Kuvunjika kwa koleo...

Picha
Hivi kama watu mnapendwa na wananchi, mabango haya yote ya kazi gani? Kama kweli ninyi ni chaguo la wananchi, inakuwaje mnatumia mapesa mengi hivi kuwashawishi wananchi hao hao? (picha kutoka Kijiji cha Mjengwa)

Cheka na utafakari kwa bidii!

Hii ni kauli mbiu ya mdau mmoja kwenye jukwaa la majadiliano pale Jamiiforums . Yeye anasema: Usifanye kosa kuchagua RAIS MGONJWA tukaingia hasara ya kurudia uchaguzi! Nimecheka kwa sababu nilihitaji kucheka asubuhi hii. Ila nimeikopi nikitafakari. Jumamosi njema wadau!

Ethics na somo la maisha yetu

Nimefuatilia kidogo mfululizo wa tamthilia ya 24. Kuna mhusika mkuu anayeitwa Jack Bauwer. Huyu kwake kilicho muhimu ni matokeo ya kile anachokifuatilia. Na katika kuthamini matokeo, huyu bwana hujikuta matatani sana. Kwake mbinu si jambo la maana sana hata ziwe haramu lakini mwisho (matokeo) ndicho kilicho muhimu. Na kweli huzitumia mno hadi kumfikisha kwenye matokeo aliyoyataka ambayo ndiyo yanayokuwa jawabu kwa wote. Kwamba haramu imekuwa halali kwa sababu tu mwisho umekuwa mtamu. Jack ananifanya nitafakari maisha yetu vile yanavyoelekea kubadilika ghafla. Kwamba kwa nini tunachoanza kukijali kama taifa ni mwisho (matokeo) bila kujali mbinu? Kwa nini tumeanza kuwa watu wa kutizama matokeo kwa mbinu zozote? Why? Je, ninapopata mafanikio makubwa kimaisha kwa gharama ya uhalifu wa kimaadili kwa jamii, nami tuseme nitakuwa nimefanikiwa? Vipi ninaposhinda uchaguzi kwa matumizi wa zile zinazoitwa siku hizi "siasa za maji taka" yaani kuwachafua washindani wangu ili nifaniki

Kujifunza katika upana wake!

Nimesoma majadiliano kati ya Mubelwa Bandio na msomaji wake. Nimejifunza maana ya kujifunza. Labda na wewe utajifunza. Tafadhali bonyeza hapa kusoma mazungumzo hayo niliyoyapenda sana huenda ukajifunza kujifunza. Asante Mubelwa kwa changamoto hiyo.