Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Dini

Unaweza Kumruhusu Mtoto Afuate Dini Apendayo?

Picha
PICHA: Pixabay Ipo nafasi muhimu ya imani/dini katika malezi ya watoto. Imani si tu inamsaidia mtoto kujitambua, lakini pia ina nafasi ya kumtengenezea mtoto sauti kutoka ndani yake inayomsaidia kupambanua lililo jema na baya. Sauti hii inaitwa dhamira. Utakuwa shahidi kuwa kuna mambo wakati mwingine unatamani kuyafanya lakini unajisikia hatia kuyafanya. Unaweza, kwa mfano, kuwa na uhuru wa kutaka kufanya chochote, lakini kuna sauti ndani yako ikakunyima ujasiri wa kukifanya. Hakuna anayekuona, hakuna anayekuhukumu, lakini kuna kengele ndani yako inakwambia kuwa unachotaka kukifanya sio sahihi. Mwanasaikolojia wa kale anayeitwa Sigmund Freud aliita kengele hiyo ‘Superego’ kumaanisha mkusanyiko wa maelekezo tunayoyapata kwa watu wanaotuzunguka. Kwa kawaida, sauti na maelekezo hayo inayoumbika ndani yetu ndiyo inayoamua namna gani tunadhibiti matamanio yetu ya asili kama hasira na tamaa za mwili. Imani, tafiti zinasema, ina kazi kubwa ya kujenga dhamira. Mtu mwenye ...

Makundi Makuu Matano ya Waislamu

Mchekeshaji mwenye asili ya Pakistani, Sami Shah, anachambua makundi makuu matano ya wa-Islam.  Pengine hujawahi kuyasikia kama mimi na ungependa kujua umeangukia kundi lipi. Bonyeza hapa kusoma makala hiyo , ambayo kimsingi imekusudiwa kukufanya ucheke na kufurahi wakati huo huo, ukitafakari kwa kina kile hasa kinachokuchekesha.

Watoto waliolelewa kidini, wamegundulika kushindwa kutofautisha uhalisia na mambo ya kufikirika

Picha
MIAKA miwili iliyopita, 2012, Justin L. Barret alionyesha kwamba binadamu wote huzaliwa na hitaji la asili la imani na kutambua nguvu zisizoonekana na kwamba imani haitokani na jamii kama wanavyodai watu wasio amini uwepo wa Mungu. Kwa Barret, imani za kidini ni sehemu ya 'maumbile' ya asili anayozaliwa nayo mtu. Hoja zake kuu katika kitabu chake ni mbili 1) kwamba watoto wana uwezo wa asili wa kuamini nguvu za kimungu zisizoonekana kwa sababu ya, pamoja na mambo mengine, huamini uwepo wa miungu iwezayo yasiyowezekana kibindamu kabla hata ya kufikia hatua ya kujua kuwa watu wazima wanajua zaidi ya watoto 2) kwamba watoto sio madodoki ya kunyonya utamaduni unaowafanya kuwa waumini wa dini kwa sababu imani, hata hivyo, hutofautiana kati ya mtu na mtu, mahali na mahali na kadhalika. Soma pitio la kitabu Barret kiitwacho Born Believers: the science of children's religious belief. Hata hivyo, utafiti wa hivi karibuni unapingana na hayo aliyoyasema Barret miaka ipatayo miwil...

Ni kweli Israel haikosei kwa Mkristo kama ilivyo Hamas kwa Mwislam?

Picha
JUZI nikiwa katika pita pita zangu katika mitaa ya mjini, nimebahatika kukutana na bango kubwa sana barabarani. Bango lenyewe lilikuwa na ujumbe wa kuhamasisha maandamano ya siku ya Quds kupinga 'Masaibu ya Wapalestina' yatakayofanyika siku ya Ijumaa ya tarehe 25 Julai, 2014. Kwa mujibu wa taarifa hiyo kwa umma, maandamano hayo yataanza saa 3 asubuhi, kuanzia kituo cha Boma, Barabara ya Kawawa, jijini Dar es Salaam. Bango hilo lina picha ya msikiti. Tutakumbuka kwamba Israel imekuwa ikiwashambulia vikali Wapalestina kwa siku za hivi karibuni, hali ambayo kwa kweli inasikitisha. Mamia ya Wapalestina wamepoteza maisha yao wakiwemo watoto. Ni hali ambayo inatia simanzi. Maandamano kadhaa tayari yameshafanyika kuishutumu Israel kwa mashambulio hayo. Israel kwa upande wao, wanadai wanachokifanya ni kulipiza kisasi kwa uchokozi wa Hamas. Siandiki kutafuta kujua nani anafanya vizuri na yupi anakosea katika mgogoro huo wa enzi na enzi. Hayo si ya leo. Bango lililoko maeneo ya ...

Kupanda na kushuka kwa dini nchini Ireland

Picha
Nimebahatika kutembelea Chuo Kikuu cha Taifa Maynooth, Dublin Ireland. Ni chuo cha zamani sana tangu enzi hizo kikiwaandaa makasisi, kikiitwa St Patrick College. Maynooth University, Ireland. Picha: Jielewe Jambo la ajabu, nimeona picha zinazoeleza idadi ya wanafunzi waliokuwa wanajiunga kuchukua masomo hayo ya Upadre kila mwaka. Idadi inaonekana kupungua kila mwaka, mpaka walipoamua kukigeuza kuwa Chuo Kikuu kifundishe mambo mengine. Madhari ya Maynooth, Dublin. Picha: Jielewe Kwa ujumla, msisimko wa dini haupo nchini humu. Makanisa mengi ya Kikatoliki yamefungwa au kugeuzwa matumizi kusaidia shughuli nyingine. Kanisa maarufu nikiwa jengo la makumbusho. Picha: Jielewe 'Nikiwa hapa, ndiyo kwanza kashfa za makasisi kudhalilisha watoto zinapamba moto. Mambo yamebadilika. Sanamu ya Papa John Paul II alipotembelea hapa. Picha: Jielewe Dublin, mji mkuu wa Ireland ndiko yaliko makazi ya makampuni makubwa ya teknolojia. Ndiko waliko Yahoo! Na makampuni meng...

Kanisa Katoliki na ushirikina...

Nasikitika kwamba sijawa na muda wa kutulia kuendelea na mijadala ya imani ambayo nimekuwa niiendesha huko nyuma. Mijadala hiyo imenipa uzoefu mpya ambao mwanzoni sikuwa nao. Mijadala hiyo imenifanya nishangae inakuwaje watu wenye imani ama dini kumtukana mtu anayejaribu kuhoji masuala yaliyo ndani ya dini yake. Mtu akikuonyesha upungufu wako kwa hoja, si ni bora kumshukuru? Pengine ndiyo hulka ya dini: Waamini hujadili kwa kuongozwa na ushabiki na hisia zaidi na sio hoja. Katika blogu ya Strictly Gospel ambayo ni blogu maalumu kwa mijadala ya Kikristo, nimekutana na mjadala ambao pamoja na kuwa bado haujapata wachangiaji wa kutosha, nadhani utakuwa mjadala moto moto huko mbeleni. Mjadala wenyewe unahusu uchawi wa kanisa Katoliki. Hebu bonyeza hapa kushiriki mjadala huo . Muhimu sana kushiriki kwenye mijadala. Na unaposhiriki kubali kujifunza. Ujue tumedanganywa vingi. Tumezungukwa na uongo. Katika familia zetu. Katika shule zetu. Katika siasa zetu. Dini. Na kadhalika. Na katika...

Strictly gospel na mijadala ya kiimani

Nimekuwa mfuatiliaji wa karibu wa blogu maarufu ya Strictly Gospel . Tofauti na blogu nyinginezo, wachangiaji wengi wa blogu hii nawafahamu kwa sura ingawa mmiliki wake sijawahi kuonana naye. Japo mara nyingine nashindwa kushiriki mijadala hiyo ya kiimani moja kwa moja kama ambavyo huwa nashindwa kublogu humu ndani, ni karibu kila siku lazima napita pale kuona namna mijadala ya kiimani inavyokwenda. Hapa nimeupata huu hapa mmoja. Bonyeza hapa kuusoma na bila shaka utajifunza mengi. Unayo maoni yoyote? Tembelea blogu nzima hapa .

Ubabe wa dini wa kuhodhi maarifa isiyonayo

Dini kama msamiati, inaeleweka. Lakini tafsiri rasmi naweza kusema ni vigumu kuipata maana inategemeana mara nyingi na matakwa, maoni, makusudi ya huyo anayetafuta maana. Wapo wanaotafsiri dini kwa kuhusisha na dhana ya Mungu kama msingi mkuu wa dini. Wengine wanatafsiri dini kwa kuihusisha na masuala ya ‘kiroho’ yaani spirituality, hisia na imani. Wengine wanaposikia dini mawazo yao yanakimbilia kwenye ‘vyama vya ushabiki wa kiroho’ yaani makanisa, misikiti, mahekalu na vitu kama hivyo. Inachekesha kwamba neno tunalolitumia mara zote, eti linatusumbua kulitafsiri. Sababu ni kwamba tafsiri sahihi yapaswa kuwa ile itakayotuwezesha kuzikusanya ‘dini’ mbalimbali kwa pamoja. Mkusanyiko huu hauwezi kufanywa kwa matumizi ya tafsiri ya dini fulani tu. Kwa maana hiyo, tunaweza kuzikusanya dini zote kwa kusema kwamba ni jumla ya imani zinazohusiana na vile tusivyoviona kwa macho, zinazojaribu kuleta majibu juu ya mikanganyiko ya maisha ili kuleta namna fulani ya matumaini ama ridhiko la ...

Mjadala wa dini na sayansi unaendelea...

Najaribu kupangilia mambo yangu niweze kujadili masuala ya dini wakati wowote kuanzia sasa. Wadau wa masuala haya ninawakaribisha nyote. Jana nilianza kwa kujiuliza swali kuu: Je, ni dini inaiogopa sayansi ama sayansi ndiyo inayoiogopa dini? Mdau wa mjadala huo, Profesa Matondo alikuwa na mchango huu wa kusisimua: ' ''Hili ni suala zito ambalo limehangaisha mafilosofa kwa muda mrefu sana. Kuna mambo ambayo sayansi haijaweza kuyaeleza. Dini kwa upande wake, kwa vile haihitaji vithibitisho kama vile sayansi, inaweza kujibu kila kitu kwa mwenye imani. Kuna mzozo mkubwa sana unaendelea hapa Marekani kuhusu ufundishaji wa nadharia ya Evolution ya Charles Darwin. Walokole wa hapa Marekani wanataka ama ifutiliwe mbali kufundishwa mashuleni au uumbaji (creationism) wa Mungu pia nao ufundishwe kama nadharia mbadala (alternative theory). Wanasayansi wanabisha kwamba uumbaji hauwezi kuthibitishwa kisayansi kama kweli ulitokea na kwa hivyo hauwezi kufundishwa mashuleni. Sij...

Dini inaiogopa sayansi?

Nilitegemea kwamba dini na sayansi vingeenda pamoja. Kwa sababu nionavyo mimi, upo uhusiano mkubwa kati ya vitu hivyo viwili. Kwanza, vyote vinahusu maisha ya watu japo kwa namna tofauti. Lakini pili si lazima viwili hivyo vitengane ili kujenga heshima yake. Lakini ajabu, karibu mara zote tangu maendeleo ya sayansi maumbile yanaanza inaonekana wazi kuwa dini imekuwa kinyume nayo. Je, ni hali hii ni halisi au ni hisia? Je, ni dini inaiogopa sayansi ama sayansi ndiyo inayoiogopa dini? Nitafafanua nikirudi

Fikiri zaidi ya dini yako

Picha
Kitabu hiki nilikipata miezi michache iliyopita. Nimekisoma kwa muda mrefu na kujipatia mwanga adhimu kuhusu dini aina aina. Hapa nilipiga baadhi ya kurasa zake, kukuonesha wewe unayetamani kujua zaidi ya dini yako. Ujue kuna watu hawafikiri kabisa nje ya kiberiti cha dini zao. Kitabu hiki nilikipewa na mdogo wangu Fortunatus kama mchango wake kwenye mijadala ya dini ambayo kimsingi sikupata muda wa kuiendeleza. Upatikanaji wake sina hakika nao lakini nipatapo fursa nitawamegea kidogo kidogo wasomaji wangu.

Ujuzi wa kanuni za maumbile haumkani Mungu

TUMEKWISHA kuona mifano ya upotoshaji uliofanywa na baadhi ya ‘wanasayansi’ ambao kimsingi walioongozwa na imani kuliko uhalisia. Tukaona kwa ufupi sana nafasi ya sayansi katika kutambua (sio kuvumbua) kanuni za maumbile ambazo kimsingi zilikuwepo kabla ya maarifa haya hayajakuwepo. Hapa tunaendelea pale pale kwa mifano zaidi. **************** Sayansi kwa kuzichunguza kanuni hizo, imeweza kuyabadili maisha ya mwanadamu kwa namna mbalimbali. Kwanza maarifa hayo yameweza kutusaidia kuvumbua nyenzo muhimu zilizotuwezesha kufanya mambo ambayo hapo awali hatukuwa na uwezo nayo. Pamoja na manufaa yote tuliyoyapata kwa maarifa haya ya sayansi, bado yapo maeneo ambayo kusema kweli sayansi imeharibu. Kwanza, kwa matumizi mabaya ya maarifa hayo yamefanya maisha ya viumbe yawe ya wasiwasi zaidi kuliko ilivyowahi kuwa katika kipindi cha nyuma. Kwa mfano, kwa maarifa yaliyopo, zimetengenezwa silaha ambazo kwa kweli kichaa mmoja akipandwa na hasira asubuhi moja na akakosekana wa kumdhiti anawez...

Uhai na mashaka ya chanzo chake

NILIWAHI kujadili kuhusu suala la mkinzano uliopo kati ya sayansi na dini. Sayansi siku hizi haina mvuto kwa vijana wa leo. Unahitaji kuwa mwehu kuijadili. Kimsingi, tangu zamani binadamu amekuwa akijaribu kudadisi asili yake yeye mwenyewe na viumbe wengine. Hilo limekuwa ni mjadala wa binadamu wengi. Kujua hasa ulipotokea uhai na kisa cha kuwa na viumbe wengi kiasi tukionacho leo. Suala hili limejaribu kushughulikiwa kwa njia za kiimani, ambapo wanadamu mwanzoni kabisa waliamini kuwa uhai umeasisiwa na nguvu iliyojuu ya ufahamu unaoelezeka, yaani Mungu. Wafuasi wa imani hii hawahesabiki katika sayari tunayoishi. Ni wengi hata kama si wote katika hawa wanasadiki kiukweli kweli hicho wakiaminicho. Katika hao wachache walishindwa kusaidiki kwa dhati dhana ya uumbaji, jumlisha maendeleo ya ukuaji wa maarifa yenye juhudi za kujua yanayohisiwa kujulikana, wapo binadamu ambao walianza kusita kukubaliana na ‘imani’ hii kwa madai kwamba ‘inalirahisisha mno’ suala gumu kwa maelezo ambayo ...

Dini: Matamanio ya kinadharia

Dini hunadi matamanio na taraji za kinadharia, zisizo halisi. Dini zinatangaza hukumu kwa mambo ya kimaumbile (nature) zikilenga kuwafanya watu kuishi maisha ya kimaigizo, yasiyoyao. Kwa mfano, zipo dini zinalazimisha 'makada' wake wenye damu kama sisi kutokuoa, ama kuolewa. Ilani hii ya useja, hata ikiwa nzuri vipi, inabaki kuwa mapendekezo mazuri yasiyotekelezeka. Huwezi kupambana na maumbile na ukanikiwa. Huwezi kuusukuma mwamba na kweli ukasogea ukiona. Kwa hiyo, matokeo yake unakuta wenye dini wanabaki kuzungumza kitu wasichokifanyia kazi. Hadharani wanazuia watu kuoa, gizani wanayatenda yayo hayo wanayoyazuia. Hadharani wana uwezo usioelezeka, sirini ni dhaifu kama wadhaifu wengine. Nini maana yake? Je, ni kweli dini i zaidi ya uhalisi? Je, miujiza inayonadiwa na dini, ni jambo lililo halisi? Je, dini si jumla ya matamanio hafifu yenye mipaka ya kibinadamu?

Dini na maoni ya wadau

Ninazo nyaraka kadhaa zilizotumwa kwangu na wadau wa ule mjadala wa dini. Zinafikia kumi. Wengine hawachelewi. Wamekuja na tuhuma nzima nzima kwa watu, ama vikundi vya watu. Ninatafakari namna muafaka ya kuwasilisha maoni yao bila upendeleo. Hata hivyo, ningependa kuwashauri wadau wa dini, kuzungumza mambo ambayo wana hakika nayo, yenye hoja, ambayo hataibua ugomvi usio na tija katika kutuelimisha. Kwa wale wasioridhika bila kutukana, ujumbe wangu kwao: Dini isipoweza kukusaidia kuitetea kwa lugha rahisi, hiyo haiwezi kuwa pungufu ya ubatili mtupu.

Soma maoni ya msomaji: Uislamu ulikuwepo tangu mwanzo

Namshukuru msomaji(ambaye hakutaja jina lake) kutupa maoni yake kuhusu hoja ya lini hasa Uislamu ulianza . Ikumbukwe, lengo hasa ni kujadiliana na si mabishano kama baadhi ya wasomaji walivyofikiri (Poleni nyote mliolalamika kwa SMS na e-mail). Hapa ni majibu ya msomaji huyo katika suala hilo: "...Salamu(amani) juu yenu. Naomba watu wafahamu ya kuwa uislamu si dini iliyopewa jina na muasisi fulani na kusema kuwa wafuasi wake waitwe waislamu, la hasha, bali Uislamu jina hili ukilitafsiri kwa lugha ya kiswahili ni amani, kujisalimisha, kunyenyekea ndiyo maana yake. Mtume Muhammad (S.A.W) si muanzilishi wa dini hii, na emeeleza wazi kuwa uislamu upo yaani (kujisalimisha kwa Mungu) toka kuumbwa kwa ulimwengu. Allah aliumba ulimwengu ili vitu vyote vimtii na kujisalimisha kwake, lakini viumbe hawa wawili (majini na watu) walipewa khiari na matamanio, na huo ndiyo mtihani wenyewe tulioumbiwa nao, ambao watu tunaelekezana, kuelimishana, kujadiliana, kuzozana mpaka tunafikia hata ku...

Nini hukifanya kitabu kuwa kitakatifu?

Picha
Niliyapenda maswali ya mwanazuoni Kamala . Sijayajibu, nikisubiri wengine wayajibu kwa haki. Ninaandika kinachotoka moyoni na nimekitafakari muda mrefu. Ninahitaji kuuelewa 'utakatifu' wa vitabu fulani tunavyoviogopa. (picha kwa hisani ya 3.bp.blogspot.com) Vinaongoza 'ushabiki' wetu kidini, na vinafikirika kuwa mamlaka ya ufahamu wetu. Tukiwa wakweli, vitabu hivi viliandikwa na watu. Hata kama wengine walidai kuwa 'mabomba' ya ujumbe kutoka kwa Mungu, lakini walikuwa watu. Tafsiri 'sahihi' ya vitabu hivi inahitaji imani. Akikisoma asiye na imani, anapata ujumbe tofauti na yule mwenye 'imani.' Sentensi zinazoeleweka, zinapindwa-pindwa kukidhi mukhtadha wa kiimani. Ningependa kujua hasa, vipo vitabu vingapi vitakatifu? Utakatifu wa kitabu unatokea wapi na ni nani mwamuzi wa utakatifu huu? Je, kitabu kitakatifu hakiwezi kusomwa bila uumini na kikaeleweka vizuri zaidi? Je, kitabu kitakatifu ni kweli tupu?

Dini ni ajali ya kuzaliwa

Wengi wetu hatukuchagua kufuata dini tulizonazo. Tumejikuta tunarithi dini za wazazi ambazo leo tunatoana nundu kuzitetea. Tumezivaa dini bila maamuzi na tumezishikilia utafikiri tunazijua. Na ajabu tunaamini kuwa dini nyingine zilizobaki kuwa haziko sahihi wakati kama tungezaliwa na wazazi wengine pengine ndizo zingekuwa zetu! Mkristo (ambaye ni mrithi wa dini ya baba yake) anaamini dini zote zilizobaki zimekosea. Mwislam naye (ambaye kajikuta mwislam kwa kuzaliwa) anaamini wote waliobaki ni 'makafri.' Kinachosikitisha ni kwamba tumejengewa uzio wa kutuzuia kujifunza dini za wenzetu. Na tunapojifunza dini hizo, kimsingi hutafuta kasoro na mapungufu yatakayotupa kuridhika kuwa dini zetu ndizo sahihi. Tungelijua kuwa dini ni ajali, basi ikiwa ni lazima, tungezipitia zote ili kuchagua moja au mbili. Vinginevyo tunabaki vipofu jeuri wanaojua kuelezea mkia wakidhani ndiye tembo.

Uislamu ulianza lini?

Picha
YAMEKUWEPO madai kwamba Uislam ulianza tangu kuumbwa kwa dunia. Na wapo watu wanaotuaminisha hayo. Ukweli ni kwamba Uislam ulianzishwa na Nabii Muhammad mwaka 622 BK huko Arabia. Kabla yake, dini zilizokuwepo zilikuwa ni Uyuda ambayo ni dini rasmi ya Wayahudi (Judaism) na Ukristo ambayo ni dini ya mataifa wasio Wayahudi ulioanza miaka kadhaa baada ya Yesu kuwa ameondoka mwaka 33BK. Yesu mwenyewe hakuanzisha Ukristo. Alisali katika misikiti ya Wayahudi. Masinagogi. Maelezo haya yana msingi wa kistoria na sio propaganda za kidini. Ndio ni propaganda kwa sababu dini zote zimekuwa na tabia ya kuonyesha kwamba zenyewe ndizo za kweli kuliko dini nyinginezo hata ikibidi kwa kuichezea historia. Na ni bahati mbaya kwamba Dini zimekuwa na tabia ya kufanana ya kuzima uwezo wa waumini wake kuhoji lolote kwa kuwajengea hofu ya kujitafutia laana. Qur’an inatupa maelezo yanayokinzana kuhusu lini hasa Uislamu ulianza. Baadhi ya mistari katika kitabu hicho zinadai kwamba ‘nabii’ Muhammad ndiye ...

Kulikoni mambo ya dini

Picha
Ule mjadala hatujauhitimisha. Kama unayo maoni unaweza kuyaacha pale. Kwa sasa ningependa kudurusu baadhi ya mambo yaliyojitokeza kwenye mjadala ule ambao ulipata maoni ya wasomaji mbalimbali. Ikumbukwe kwamba blogu zina maana hasa yanapokuwepo maoni ya wanaosoma na sio kuendeleza tu yale ya aliyeandika. Jambo la kwanza lililojitokeza katika majibizano ya wasomaji wawili walioficha majina yao, ni kuhusu historia ya Uislamu. Kwamba mmoja anadhani Uislamu ulianza tangu kuumbwa kwa Dunia, na mwingine anadhani Uislamu haukuwepo hata miaka 2000 iliyopita. Nijuavyo mimi, kabla ya miaka 2000 iliyopita, haukuwepo Ukristo wala Uislamu. Hizi zote ni dini za juzi juzi. Dini iliyokuwepo enzi hizo katika nchi hizo tunazoiita takatifu ilikuwa ni Judaism. Dini isiyo na uhusiano wa moja kwa moja na Uslamu wala Ukristo. Ibrahimu anayetajwa na msomaji mojawapo kuwa na mila ya dini mojawapo, alikuwa na mila na utamaduni wa Kiyahudi mwenye dini ya Uyuda (Judaism). Maana ya historia hii ni ni...