Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2006

Kumwua Muisrael si kuua?

Wengi wetu tunajua zile amri kumi ambazo Musa/Moshe alizipewa na mwenyezi Mungu ili ziwe dira ya maisha ya wana wa Israel wakati na baada ya safari yao ya jangwani. Tunajua kuwa amri hizo zinatuhusu hata sisi wa kizazi hiki tusiokuwa waisraeli. Katika hizo amri ipo inayosema Usiue. Yaani Mungu akizuia binadamu yeyote kumtoa uhai kwa makusudi binadamu mwenzake. Ninaweza kuonekana wa ajabu nikiuliza: Hivi amri hii ilimaanisha usimwue nani? Ni kuua tunakokufahamu ama kuna neno linaloendelea ambalo huenda lilihaririwa na Moshe? Ninasema hivi kwa sababu, baada ya Musa kufia mlimani, na mamlaka ya kuwaongoza wana wa Israeli kushikwa na Yoshua kuna jambo la ajabu lililotokea. Wale jamaa walipokuwa wakiingia kwenye nchi ya ahadi, Kanani, nchi ambayo ilikaliwa na wenyeji wakati wairaeli wakiishi Misri, yalifanyika mauaji makubwa ambayo hayana tofauti na yale ya kimbari. Watu kwa maelfu walipoteza maisha yao. Mauaji haya ninashawishika kuamini kuwa yaliyazidi yale yaliyotokea Rwanda miaka ya t

Ubuddha: Miungu hufa na haistahili sadaka

Tuendelee na vidokezo kuhusu dini zetu tukiangazia dini zinazopatikana katika bara la Asia. Baada ya kuangalia Uhindu, sasa bonyeza hapa kusoma maelezo mafupi kuhusu Ubuddha, dini inayoamini kuwa kuishi ni kuteseka na kwamba ni muhimu kujikomboa kutoka katika mateso ambayo humpata kila binaadamu. Wa-Buddha wanaamini kuwa kuna miungu, lakini wakiamini kuwa miungu hiyo hufa kama viumbe wengine, na kwamba miungu hiyo haihusiki kwa namna yoyote na mambo ya uumbaji wa ulimwengu huu, kwa hivyo haistahili kuombwa wala kupewa sadaka.

Uhindu: Dini inayoamini dini zote ni sahihi!

Kwa muda sasa, pale Jikomboe/dini kulikuwa na mjadala kuhusu tofauti ya Dini na Imani ukiongozwa na mwanablogu Mwidimi Ndosi. Mjadala huo hatukuumaliza ili kuruhusu maoni ya wasomaji wengine. Kama unapenda mijadala hii, nakushauri upite hapa halafu uache maoni yako. Wakati mjadala ukiendelea, na mara nyingine nje ya ukumbi, kuna wapenzi wa mijadala hii wanadai ipo haja ya kupeana habari zaidi kuhusu dini ambazo wengi hawazijui. Sababu ya kufahamika ama kutokufahamika kwa baadhi ya dini inaweza kuambatana na nguvu za kisiasa na kiuchumi za wasambaza dini husika. Na ni kweli kwamba waumini wengi huwa hawajishughulishi na kujua dini nyingine zaidi ya hizo wanazoziamini. Siwezi kudai kuwa ninazijua sawasawa, ila ni kule kupenda kufuatilia hapa na pale na kuzungumza na huyu na yule, basi ninakuwa na japo kiberiti kidogo cha kutafutia wapi pa kuanzia na hapo wengine wanaongoza na matokeo yake tunavunja ile mila ya kutokujifunza mengi. Wapo watu wanaodhani kuwa dini zao ndizo zilizo sawa kuli

Hivi ni laana ama ni mdudu gani?

Niliwahi kumsikia "mwinjilisti" mmoja aliyekuwa akichapa injili mitaa ya Kariakoo. Siku hizi ni jambo la kawaida kukuta watumishi hawa wanaoitwa wa Mungu wakifanya "vitu vyao" hadharani bila kujali haki za wengine. Kelele nyiiiingi kisa wanasema habari za Mungu. Kwa hiyo kimsingi haikunishangaza. Huyu bwana alikuwa "siriaz" kweli na kazi yake kiasi kwamba ungemhurumia kumwona akisema na watu wasiomsikiliza wala kujali anachosema. Jua lilikuwa kali na alikuwa kavaa koti zito. Joto la Dasalama tunalijua. Japo sikumsikiliza, nilihisi kazi yake ilikuwa ni "kuwarejesha kondoo katika zizi la Bwana". "Afrika na watu wake, imelaaniwa!" alipayuka huyu bwana huku akitembea kwa madaha. Akageuka huku na kule, akanyanyua biblia yake kuuuuubwa akaendelea: "Enyi uzao wa Hamu, mmelaaniwa na laana yenu inakaa!". Kwangu mimi maneno haya yalininyong'onyeza mithili ya mtu aliyenyeshewa mvua. "Hivi anajivunia nini kusema maneno haya? Hata