Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2008

Mwaka wa malengo mahususi ndio huu

Mwaka unaishia leo. Watu wengi watakwambia jitathmini. Kuona wapi ulikosea. Wapi ulilikoroga. Wapi ulifanya vizuri na mambo kama hayo. Binafsi sioni sababu yoyote ya kufanya hivyo. Sioni sababu ya kufanya hicho kinachoitwa tathmini ya mwaka. Sababu ni kwamba hata kama ungegundua wapi ulikoharibu, huna unachoweza kufanya zaidi za kujiumiza moyo. Utaumia moyo, na historia itabaki pale pale. Maana historia ilikwisha kuandikwa. Kama ulishindwa mwaka huu, hesabu ni upepo umepita. Hata kama ungegundua wapi ulifanya vizuri, ukweli ni kwamba hayo wameshapita. Yaache yaende. Hakuna haja ya kulewa sifa zisizoweza kukusaidia leo. Siafa za jana zinabaki kuwa za jana. Huna sababu ya kuangalia nyuma. Historia haiwezi kukusaidia. Una sababu ya kuiacha ipite vile ilivyokuwa. Nionavyo mimi, huu ni wakati wa kutazama mbele. Kuwa na malengo. Usipojua unakokwenda, utaishia kokote. Wafanyakazi waangalie namna watakavoboresha utendaji wao wa kazi. Wanafunzi wajiangalie watakavyoweza kusoma kwa bidii.

Shule za "yeboyebo" na Mimba za utotoni

Ni ajabu na kweli. Baada ya kubaini kuwa karibu vijana wengi wanaotumia internet hapa Singida, lengo lao ni kujiridhisha na picha za ngono, kumbe lipo tatizo jingine. Mimba za utotoni. Sijafikia kuhalalisha uhusiano uliopo kati ya uangaliaji wa picha za ngono na hili la mimba. Lakini kwa mbali naanza kuhisi. Kwa sababu nimegundua pia kuwa mitaa mingi imesheheni sehemu za kuonyeshea filamu za "kikubwa" ambapo ndiko zilipo prepo za wanafunzi wengi wa shule za yeboyebo (kata). Ukweli ni kwamba siku hizi kila mwanafunzi "anafaulu" kuingia sekondari. Maana tumetoka nyakati zile za kufaulu na bado ukakosa nafasi, mpaka nyakati hizi ambapo unafeli na bado unaambiwa umefaulu. Pamoja na neema ya kufaulu, karibu kila familia ninayoitembelea hapa Singida inauguza maumivu ya binti kuzaa kabla ya wakati. Mabinti wa shule za msingi na sekondari wanapachikwa mimba (Mara nyingine na waalimu wao ambao wengi ni wale wa voda fasta). Wale walioshindwa kuendelea na masomo wanazalia

Nitautambuaje udhaifu nilionao?

Hivi karibuni tulijadili kwa ufupi kuhusu dhana ya ukosoaji na kusifiwa . Ninafurahi kuona namna watu wanavyotoa maoni mazuri tofauti tofauti ambayo ukiyasoma yanakupa uelewa mkubwa zaidi. Kwa hakika, maana hasa ya blogu ni majadiliano. Ule mtindo kongwe wa mwandishi kuandika kwa fikra kwamba anachokifikiria ndicho sahihi na kinachopaswa kumezwa na wasomaji, hapa si mahala pake. Blogu inatuweka karibu waandikaji na waandikiwa (ambao kimsingi inakuwa kama hawapo maana wote wanajadili kilicho mezani). Kwa hiyo, blogu ni majadiliano ndio maana binafsi sipendi kuandika kwa mtindo wa hitimisho. Hata kama mjadala utakaojitokeza unaweza usifikie hitimisho, bado huamini kuwa huko mbeleni, hitimisho husika laweza kufikiwa na wasomaji. Katika mada hiyo, kuna msomaji mmoja alinipigia tukajadili kwa muda mrefu. Ninawapongeza wasomaji wanaopenda kuendeleza mijadala tunayoianzisha katika blogu zetu hata kwa njia ya simu. Basi. Kilichojitokeza katika majadiliano hayo, ni namna tunavyoweza kuubain

Gwamaka: Kile tusichofundishwa madarasani

Leo nilipata fursa ya kupata chakula cha mchana na rafiki yangu Gwamaka. Gwamaka ni kijana mwenye changamoto nyingi. Ukiongea naye hukosi jipya. Ni mwanaharakati, mwanafalsafa mwenye kichwa kinachofikiri. Ni msomaji mzuri wa vitabu. Na unaweza kubashiri inakuwaje ukikutana na msomaji wa vitabu kama Gwamaka. Ni lazima nikiri kuwa vitabu vingi nilivyosoma, yeye ndiye alinishawishi. Hivi sasa kaniambia anasoma kitabu kiitwacho: Why we need you rich . Ameniahidi kuwa kina mambo mazuri katika eneo la fedha. Japo sijawa msomaji mzuri wa vitabu vya "fedha" nimeshawishika kukitafuta. Kwa hiyo unaweza kuona kwa nini tukio la kukutana naye huwa na umuhimu wa aina yake kwangu. Basi. Gwamaka alipomaliza 'shule' aliamua kujikita katika shughuli binafsi. Hataki kuajiriwa. Aliwahi kuajiriwa miezi michache akaona sio. Hivi sasa yuko kwenye mchakato wa kutengeneza ofisi yake mwenyewe pale Mwenge, barabara ya Sam Nujoma. Mambo ya ujasiria mali. Kupata, kadiri ya unavyowekeza. Anayo

Mkaribishe Koero

Naam. Idadi ya wanablogu inaongezeka. Na kila mwanablogu anakuja na mtazamao mpya. Hebu mtembelee Koero uone. Kama utakavyoona, ujio wa watu kama hawa ni wa muhimu sana. Karibu sana Koero tujadiliane.

Rariki yangu Rama muuza magazeti

Kazi ya kwanza niliyoifanya baada ya kufika Singida ni kulazimisha matangazo ya blogu zetu. nimekuwa nikibadili 'settings' kwenye kila kompyuta niliyoitumia kwa kubadili 'home page' iliyopo kuwa blogu moja wapo kati ya nyingi tulizonazo watanzania. Nimebadili badili baadhi ya kopyuta na mpaka sasa kuna kama blogu kumi hivi kama home page. Kwahiyo, kama inavyotarajiwa, kila mtumiaji wa kompyuta husika anapojaribu kuingia mtandaoni, atasalimiwa na blogu ya kiswahili. Hiyo nadhani inaongeza wigo wa blogu zetu. Nilifanya hivyo pia kwa baadhi ya miji niliyopita mwaka huu. Nadhani inasaidia kuzitangaza blogu. Ukweli ni kwamba bado matumizi ya mtandao yamekuwa zaidi katika kuandikiana barua pepe na mambo yetu yaleee niliyoyasimulia juzi. Hata ivyo naamini mabadiliko hata kama yanaonekana kwenda taratibu, bado yanakuja. Ni wajibu wetu kuyachochea. Leo nimekuja kwenye cafe nyingine. Hii kidogo iko wazi sio kama ile iliyokuwa imefunikwa gubi gubi. Kuna jamaa hapa tumekaa ka

Singida: Here I come

Niko Singida. Baada ya kufika niliona ingefaa kupata huduma ya intaneti cafe. La haula! Nakutana na picha za ngono. Nahisi jamaa aliyekuwa akitumia kompyuta hii ndio kazi kubwa iliyomleta hapa. Uzuri, kama kweli ni uzuri, kompyuta za hapa zimewekewa uzio. Privacy. Unafanya kile unapenda bila hofu ya kuichunguliwa. Waswahili ukiwapa uhuru, ndo umeharibu kabisa. Jamaa aliyeondoka hapa ni mtu na heshima zake. Tai. Suti na vitu kama hivyo. Mtu na ofisi yake bila shaka. Sitaki kuamini kwamba ndicho alichokuwa anakifanya hapa. Ni lini net zitatumika kwa mambo ya maana, hilo ndilo twapaswa kujiuliza. Vijana wanajazana net siku hizi. Usifikiri (wengi wao) wanafanya vya maana. Ngono ndugu msomaji. Hivi hata nilitaka kuandika nini hata nimeshahau. Kwa nini ngono? Labda anajifunza lakini. Tuchukulie anajifunza. Sasa kujifunza kupi kwa picha za mnato wajameni? Mjadala hapa. Au tuwashauri wenye net waondoe uhuru? No. Hilo sio jibu. Siku hizi kuna simu. Watu "wanafaidi" mambo haya waki

Yupi wa maana kwako: Akukosoaye ama akusifiaye?

Ipo haja kubwa ya sisi kama binadamu kuufahamu udhaifu wetu. Ni kazi ngumu ambayo watu wengi hatuipendi. Huenda ni kwa sababu ni kazi isiyoonekana kuwa na tija ya haraka haraka. Na pengine sitakosea nikisema ni zoezi linalojeruhi mtazamo wetu hasa ikiwa hatujielewi. Mtu asiyejielewa ni rahisi kuumia akiambiwa alikokosea. Hufarijika sana akisifiwa kizembe. Kwa nini iko hivi, hapo ndiko twapaswa kuanzia: Je, sifa zamsaidiaje asiyejielewa? Najua Mtambuzi ameandika mara nyingi kutusihi kuhusu kutokuutazama upande wa pili. Nakubaliana naye. Kwamba wengi wetu, hutumia muda mwingi sana kuutazama upande wa udhaifu/mapungufu waliyonayo watu wengine. Tunakuwa mafundi wa kuchambua madhaifu ya wengine. Kila kitu kinatazamwa kwa nia ya kugundua tatizo la wengine. Iwe katika haiba (personality), kazi, mafanikio nk. Ndio maana hata tunaposikia mwenzetu kaharibu mahala, twathubutu kufurahia (hata kama ni kimoyomoyo). Kutokuungalia upande wa pili, vile vile ni aina fulani ya faraja. Ni juhudi za

Usawa wa viumbe mbele za Mungu uko wapi?

TURUDI kwenye ule mjadala wetu wa suala la Mungu ambalo bado ninalitafutia wakati mzuri zaidi. Kuna changamoto ndogo nadhani itastahili kutazamwa. Nayo inahusu usawa wa viumbe mbele za Mungu wao. Tunaamini kwamba Mungu alituumba sisi wanadamu pamoja na viumbe wengine mfano mimea pamoja na aina nyingine za wanyama. Na inavyoonekana, mbingu iko kwa ajili ya sisi wanadamu zaidi. Sasa hoja ni kwamba nafasi ya hawa viumbe wengine iko wapi katika ufalme wa mungu? Kwa sababu hatuelezwi wazi kuwa viumbe wengine watafaidikaje na umilele tunaoutarajia (sisi wanadamu) ambao tu viumbe kama wao. Jibu la haraka haraka ambalo mtu anaweza kulitoa kama majibu ni kwamba viumbe wengine hawana upeo/utashi wa kutambua. Lakini jibu hili nadhani haliwezi kuwa sahihi. Kwa sababu hebu tuchukulie mfano ng'ombe anapopelekwa machinjioni. Anapofikishwa pale, kiumbe huyu huonekana kupatwa na mfadhaiko mkubwa kiasi cha kuweza hata kubomoa uzio ushahidi kwamba anajua kinachoendelea. Kwamba kuna kundi la viumb

Unafiki na kutokujiamini kwetu

Unafiki ni hali ya kukuficha kwa makusudi kile kilichomo mawazoni/moyoni kwa lengo la kumwonyesha mtazamaji kuwa anachokiona ndicho, wakati ukweli wa mambo ni kwamba anachokiona ni tofauti sana na uhalisia. Unafiki ni kama kuvaa gamba lisilo lako. Kubadili rangi ya mwonekano wako. Kuwa "artificial". Unafiki ni kinyume cha uhalisi. Kwamba naweza kuigiza mwonekano fulani ambao kimsingi si wangu katika hali halisi. Naweza kumtabasamulia mtu, wakati ukweli wa mambo ni kwamba ndani yangu nasikia kinyaa. Naweza tembelewa na mtu, rafiki yangu mathalani, na ukweli ni kwamba nina kazi nyingi za kufanya lakini kwa kutaka kumridhisha rafiki yangu huyo, basi namwonyesha kufurahia ujio wake ingawa moyoni (ukweli wenyewe) ni kwamba namwona kama mpotezaji mkubwa wa muda wangu.Simwambii jinsi alivyoharibu ratiba yangu. Ila usoni anaona ninavyofurahia kuja kwake kiasi kwamba anaendelea kubaki. Na hata anapoaga, naweza kumwomba aendee kubaki, kumbe moyoni nikimsema kwa kukosa kwake busara.

Kwa nini watu huongopa?

Kusema uongo ni kutokusema ukweli. Kupindisha uhalisia wa mambo, basi. Kwa namna moja ama nyingine, sisi kama binadamu tumewahi kuongopa. Tumewahi kuwaongopea marafiki. Wazazi. Waalimu wetu. Wakubwa zetu. Na watu wengine wanaotuzunguka. Na pengine tumewahi hata kujiongopea nafsi zatu wenyewe kwa namna moja ama nyingine. Na uongo huwa na sababu bila shaka. Haiwezekani kusema uongo bila sababu. Kwa sababu kwa hakika kila mtu hupenda kusema ukweli. Sasa ni kwa nini watu hudanganya hapo ndiko lilipo swali langu. Katika kulijibu swali hili, msomaji anaweza kurudi nyuma kadiri awezavyo, kukumbuka matukio yote ya uongo aliyowahi kukumbana nayo, halafu achunguze, ni kwa sababu gani alisema uongo? Alipenda kudanganya ama alilazimika? Kipi hasa kilisababisha aseme aindishe ukweli wa mambo? Je, uongo huo ulimpa faida ya nafsi ama hasara? Lakini pia kuna jambo la kukumbuka. Wapo watu ni waongo wazuri kiasi kwamba hawawezi tena kujua kuwa wao ni waongo (unakuwa mwongo mpaka unauona uongo kama

Mawazo yako ndiyo nguvu uliyonayo

Upo uhusiano mkubwa sana baina ya namna unavyofikiri, na jinsi unavyoishi. Kushindwa kwako, hakutegemeani na nguvu yoyote ulivyonayo isipokuwa ufahamu wako. Kuanguka kwako hakutegemei maadui wengi ulionao, isipokuwa aina ya mtazamo ulionao. Kurudi nyuma kwako hakutegemei historia yoyote uliyowahi kuwa nayo, isipokuwa namna unavyoendekeza mawazo yako ya kushindwa. Naelewa kwamba panahitaji mjadala wa kina kuhusu kipi kinachomtawala mwenzie: mawazo yetu ndiyo yanayotuongoza ama ni sisi ndio tunayaongoza mawazo. Hapo inapidi tushukie penye uelewa na namna mawazo yetu yanavyojengeka vichwani mwetu. Kwa haraka haraka, nadhani, twawaza vile tulivyoviingiza ubongoni iwe kwa hiari yetu wenyewe ama pasipo hiari hiyo. Kwa maneno mengine sisi ndio watawala wa mawazo yetu. Hiyo ni kusema kwamba unavyojiona, ndivyo ulivyo. Ukijidharau, hakuna mtu atakuja kukufanyia kazi ya kukuonyesha thamani uliyonayo. Ukianza leo kujiona masikini, ni wazi kuwa akili yako itakubaliana nawe na kusema kweli, u

Uhuru huu ni kwa ajili ya nani?

Ninaomba msamaha kama hutanielewa. Ila ninadhani jambo hili ni muhimu ukalitafakari kwa kina wakati ukisherehekea “uhuru” wa nchi yako iliyo masikini kuliko zote kusini mwa jangwa la Sahara. Hivi kweli nchi yetu ina haki ya kusherehekea hicho kilichopewa jina la “uhuru”? Uhuru maana yake ni nini? Ni kwa kiasi gani twaweza kujikagua kuona ikiwa tu huru kweli? Kama uhuru una maana ya mambo kuwa hivi yalivyo, vipi utumwa? Ni kwa kiasi gani uchumi wa nchi hii unathibitisha kuwa kweli tu “huru”? Ni kwa kiasi gani utamaduni wetu unathibitisha hicho kinachoitwa “uhuru”? Ni kwa kiasi gani? Ni kwa vipi tunaweza kujiridhisha kwamba elimu yetu inakubaliana na kelele zetu za “uhuru”? Hivi mababu zetu walipokuwa wakiusaka uhuru lengo hasa lilikuwa nini? Leo hii tunasoma Vyuo Vikuu kwa vitisho kutoka kwa wenzetu wanaofafana na sisi. Haturuhusiwi kufikiri. Elimu yenyewe imekaa mkao wa kitumwa. Tunafundishwa akademia ituondoayo katika wigo wa kuyaelewa matatizo yetu ya kila siku. Inatuondoa k

Mpendao simu oneni

Picha

Kwa wageni: Ujumbe wa Mwenyekiti wetu

Waraka wa mwenyekiti wa Jumuiya ya wanablogu Tanzania (JUMUWATA) kwa wanablogu wote: "Wapendwa katika jina la Watanzania. Amani iwe juu yenu. Natumai wote muwazima. Hii ni kuwataarifu rasmi kuwa, baada ya kimya cha muda mrefu sana, mahangaiko ya hapa na pale na mambo mengine, hatimaye ndugu, kijana, mpiganaji, muungwana na mpigikaji mwenzenu nimerejea ulingoni. Najua kuna ambao walikuwa wangali wakinisaka katika www.msangimdogo.blogspot.com na najua kuwa kuna wale ambao watakuwa huenda ni wapya kabisa katika taarifa hizi.la nyote kwa ujumla, napenda kuwataarifu rasmi kwa, maskani yangu kwa sasa ni hapa . Kuna kitabu cha wageni pale, makala zangu zilizotangulia ambazo zilitoka katika sehemu mbalimbali nilizozurura nakadhalika. Ila hatimaye, nimeamua kutulia hapo. Nawakaribisheni sanjari na kuwaomba mwafikishie ujumbe huu Blogaz wenzenu ambao mnawafahamu, pamoja na kutiwekea taarifa hizi katika blogi zenu kwa wale watakaoweza. Mwisho kabisa, naomba wale ambao viungo vyao (link

Dialectic thinking: Ukweli ni kinyume chake

Dialectic thinking ni nini kwa Kiswahili? Sijui. Ninahitaji msaada wa dharura wa BAKITA. Lakini wakati tunangoja fasiri fasaha, hebu, walau kwa sasa, tukubaliane kuwa dialetic thinking ni aina ya tafakuri inanyosisitiza katika migongano ya hoja. Migongano ya hoja, maana yake, ni kukubali kuhitalafiana kama namna njema ya ufikwaji wa hitimisho sahihi. Hebu na tuiangalie falsafa hii kwa mifano rahisi. Ukweli unatokana na tofauti. –tofauti hapa ikimaanisha opposite. Labda tuseme kinyume. Ukweli unatokana na kinyume cha ukweli huo. Kwamba vinyume (opposites) kwa asili hutegemeana. Hebu angalia: Unawezaje kulielewa giza kama huwezi kuuelewa mwanga? Huwezi kujua kwamba unapenda kama hujawahi kuchukia. Huwezi kuielewa furaha kama hujui huzuni ikoje. Utajiri hauna maana bila umasikini? Huwezi kuwa mwerevu kama hakuna wajinga wanaokuzunguka. Uhai hauwezekani ikiwa atakuwepo mwanamke bila mwanamme. Mifano ni mingi na hata wewe ndugu msomaji unaweza kukubalina nami kwamba vitu vyote tunavyo

Matokeo ya utafiti wa Mwaipopo

Mwaipopo, mwanablogu wa Sauti ya baragumu ameonyesha mfano wa namna wanablogu tunavyoweza kuyachunguza mambo na kisha kupata michango yenye uzito unaovutia. Mfano huu ni wa kuigwa na kila mpenda mijadala. Nataraji kwamba wasomaji watakumbuka lile swali la lugha nililokuwa nimeliuliza kuonyesha ugumu uliopo katika kulitafsiri kwenda kwenye kiingereza ambacho hakitapoteza maana. Tulipata majibu mengi. Ndipo Mwaipopo kwa msukumo wa kupenda utafiti, akafanya uchunguzi na haya ndiyo majibu yake: " Jamani sikuishia hapo. Nilikuwa nafanya kautafiti kadogo ili nije tena...Swali hili liliponitoa jasho nikaona nimuulize rafiki yangu mzungu. Nae kaiona shida. Bahati njema anajuajua kidogo Kiswahili cha kuendea kariakoo. Kama mjuavyo mimi ni linguist. Niliwahi kusoma translation course. Hili ni tatizo miongoni mwa matatizo ya fasili - maneno ama miundo yenye kuegemea katika utamaduni wa lugha husika. hata hivyo panapo nia ya kutafsiri lazima njia itafutwe. hasa ni kwa nia ya kujif

Elimu tu inatosha kupambana na UKIMWI?

Kuna jambo la msingi la kutazama taratibu kuhusu kampeni kabambe za kupambana na UKIMWI. Kampeni hizi zinalenga kuelimisha watu kuhusu namna ya kupambana na janga hili ambalo nina hakika linamtisha kila adhaniwaye kuwa na akili timamu. Na kwa kiasi fulani elimu hii imesambaa. Watu wanayo elimu hii. Kuhusu elimu tumefanikiwa. Makofi tafadhali. We tazama barabara. Kuta. Miti. Redio. Luninga. Kila eneo mabango ya kuelimisha kupitia ujumbe wa aina tofauti tofauti. Ajabu yenyewe ni kwamba kasi ya kuenea kwa UKIMWI inazidi kasi ya kusambaza ujumbe. Na inasikitisha kwamba hata hao wanaoitwa waelimishaji, nao wanashindwa kuitumia vyema elimu hiyo kijikinga na UKIMWI. Narudia. Waelimishaji wenyewe, hawajaweza kuitumia elimu hiyo nzuri wanayoigawa kwa wanajamii. UKIMWI unawaanza wenyewe. Kwamba watu wanaojua kusoma wanapita kwenye barabara zenye mabango yenye kuonya kuhusu tabia ya ngono na kuhimiza matumizi ya kondomu, wanapanga mikakati kwenye baa yenye mango hayo hayo, wanaingia kutenda

Kwa mabingwa wa Tafsiri fasaha

Kwa wanaopenda kiingereza.Tafadhali naomba tafsiri ya maneno haya kwa kiingereza ambacho hakitabadili maana iliyopo katika kiswahili hiki: "MAMA, HIVI MIMI NI MWANAO WA NGAPI KUZALIWA?" Ukipata tushirikishane.

Unadhani macho yako yanaaminika?

Picha
Nianze kwa kuomba msamaha. Sijakuwepo mtandaoni kwa siku kadhaa. Nikuombeni kutokukata tamaa ya matembezi kibarazani hapa. Leo ningependa tuangalie suala moja. Kwamba mara nyingi tunavyoyaona mambo sivyo yalivyo. Milango ya fahamu zetu haiaminiki. Hebu tazama picha hii hapa chini. Angalia kwa makini kiboksi A na kiboksi B uone unavyodanganywa na macho. Angalia viboksi hivi. Hakuna rangi yoyote kati ya kiboksi kimoja na kingine, japo macho yako yanakuambia kuna rangi ya kijivu. Bonyeza na hapa uone picha hii . Unajifunza nini? Ukweli na uhalisia ni vitu viwili tofauti.

Long live JUMUWATA

Picha
Leo ni siku ya kuadhimisha maendeleo ya blogu Tanzania. Maadhimisho haya yalianza rasmi mwaka juzi, kwa makubaliano ya wanablogu wenyewe walipokutana kwa mkutano mkuu wa kwanza wa mtandaoni. Soma blogu hii hapa kwa maelezo zaidi. Kusema kweli tuna kila sababu ya kufurahia kuanzishwa kwa jumuiya hii muhimu ya kutuunganisha. Siku hii haikupaswa kabisa kuwa hivi ilivyo leo. Kwamba kila mmoja anasherehekea kivyake vyake si jambo la kujivunia sana. Kwa wanablogu wapya, ni vyema kufahamu kuwa tunayo jumuiya yetu yenye viongozi waliochaguliwa kwa kura. Angalia majina yao hapa . Napenda kumpongeza sana Kitururu kwa kazi kubwa aliyoifanya akishirikiana na wenzake. Najua anayo majukumu mengi ya kufanya. Lakini bado hajasita kujitolea kwa faida ya wote. Yupo Da Mija mwamke wa shoka ambaye juhudi zake za kujitolea zimeipeleka mbele jumuiya yetu. Ndesanjo mzee wa kujikomboa. Majukumu nayo bila shaka yamembana. Historia inamkumbuka. Mwenyekiti wetu blogu yake haipatikani. Sijui kilichotoke

Mchango wa msomaji

Jana kuna mchango wa mawazo niliupata kutoka kwa msomaji Prosper Mwakitalima. Huyu ni mwanafalsafa na rafiki yangu wa siku nyingi. Mjadala wetu ulikuwa katika hoja ya nguvu kuu iliyozungumziwa na Kamala. Anasema: "...Kwamba tunapofikia kuamini kuwa ipo nguvu kuu kwa sababu ya kushindwa kuamini kuwa viumbe vyote na asili yake visingeweza kujiratibu vyenyewe, na hapo hapo tukakubali kuwa nguvu hiyo haina chanzo, na mwisho wake hauelezeki, tunashindwa vipi kuamini kuwa hata viumbe navyo vimekuwapo vyenyewe bila nguvu fulani kuu zaidi? Kwa sababu kama tunaamini kuwa hiyo nguvu haina chanzo, kwa nini tushindwe kukubaliana kuwa hata viumbe navyo vyaweza kuwapo bila chanzo?..." Hiyo ni changamoto nyingine inayohitaji majibu. Najua anachokoza mawazo kwa lengo la kutufikirisha zaidi. Nimetangulia kukujulisheni kuwa yeye ni mwanafalsafa mwenye dini.

Zimebaki siku tano...

Tarehe kumi na nane mwezi huu ni siku ya maadhimisho ya wanablogu. Tukumbushane kushiriki. Mambo kama haya yasionekane madogo kihivyo. Yanatunganisha. Tujiandae.

Kaluse mwanablogu wa utambuzi

Je, unaujua utambuzi? Kama sivyo, basi ujio wa huyu mwanablogu mpya utakupa majibu. Bonyeza hapa umsome . Anazungumzia mambo yanayohusu nafsi zetu. Saikolojia. Binafsi nimependezwa na ujio wa mwanablogu huyu. Naamini utapenda kumsoma na kujadiliana na wasomaji wengine humo.

Hakuna kujifunza bila kutofautiana kimawazo

Ni Jumapili nyingine njema. Hatuna budi kukumbushana kwamba siku ndo zinaenda hivyo. Siku ya tisa leo. Zinaenda. Bado siku chache tuelekee kwenye mwezi wa lala salama. Mwezi wenye sherehe nyingi kuliko utekelezaji wa mipango ya wanajamii. Siku zinakatika. Kwangu Jumapili ni siku ya kupumzika kwa asilimia mia moja. Sababu ni kwamba katika siku sita za juma huwa ninabanwa kisawasawa na dunia. Kwa hiyo Jumapili kwangu ni siku ya kujisomea ninavyovitaka. Kulala. Stori. Kula. Alimuradi tu kufurahia mwisho wa juma. Nimekuwa nikitafakari michango kadhaa ya wachangiaji wa blogu hii hasa kwenye makala za uwapo wa Mungu. Najua kila mtu anao mtazamo wake. Japo najua watu wengi hawajajaliwa kuweka wazi mawazo yao hasa inapokuja suala lenye utata kama hili. Nawashukuru waliomajasiri kujaribu kuchokoza mawazo ya wengine. Kuchokoza mawazo si kazi rahisi. Nilikuwa napitia pitia niliyopata kuyaandika. Basi nikapata makala hii niliyoiandika miaka miwili iliyopita. Ilihusu biblia na imani zetu. Hiy

Kutoka maktaba: Laana? Ama?

Haya nikurudishe nyuma kidogo. Twende kwenye kumbukumbu zetu. Soma makala hii: Hivi waafrika ni kweli tumelaaniwa? Kumbuka sikuwa nimehitimisha. Nilikuwa katika tafakari tu. Usinielewe vibaya kama baadhi ya watu wengine walivyofikiri. Soma katikati ya mistari.

Tofauti ya Magharibi na Kusini

Natafakari tofauti hasa iliyopo kati ya mataifa ya magharibi na kusini. Wakati Zimbabwe kura zinapigwa na mwezi unakatika ndo matokeo yafahamike...wakati Kenya inachukua majuma kadhaa...wakati Bongo unaelewa mwenyewe...Marikani imechukua masaa kadhaa matokeo yamejulikana. Na si tu masaa hayo, lakini mshindwa anatoa kauli ya moja kwa moja kwamba aliyeshinda kashinda. Anampongeza. Mimi sielewi. Hivi tofauti hii inatokana na nini? Umasikini? Uroho? Ujambazi? Ama ni ujinga flani mukichwa? Sielewi. Hivi sisi ndugu zangu tumepungukiwa nini hasa? Mwenyezi Mungu alitunyima nini sisi wanadamu wa dunia ya sita? Kuna haja ya kujielewa. Ipo haja hiyo.

Je, kuna Mungu? - Mchango wa Nuru Shabani

Kuna wachangiaji wananiandikia kwa barua pepe. Sijui ni kwa nini wanataka tujadiliane sirini. Nadhani tukijadili waziwazi inapendeza zaidi kwa faida ya wasomaji wengine. Hapa ninao mchango wa Nuru Shabani kupitia kisanduku cha maoni. Kwa kuheshimu mchango wa msomaji huyu, naomba niupandishe hapa uusome. "...Ningependa kuungana na Kamala kuwa hakuna kitu kinachoitwa Mungu,kama wengi tulivyoambiwa. Zamani kabla hawajaja wakoloni(wazungu na waarabu) hakukuwa na kitu kinachoitwa Mungu,wao waliamini ktk Nguvu kuu.Ndiyo maana utakuta wengine waliamini ktk miti wengine katika majabali,na kikubwa ndugu zangu ieleweke wengi wa watu wa zamani waliamini zaidi katika kanuni za kimaumbile ndiyo ilikuwa msingi wao. Kwa mtazamo wangu wengi hatumwelewi mungu sana tunachofanya ni kujenga hofu kwa Mungu,linapokuja suala la kutaka kumjua huyo mungu kwa undani utaambiwa unakufuru,sasa mi huwa ninajiuliza iweje utake kujua asili za aliyetuumba uambiwe unakufuru? Haingii akilini umuulize mzazi w

Je, kuna Mungu? - Mchango wa Kamala

Haya. Nashukuru kwa michango ya wasomaji kuhusu hoja ya uwapo wa Mungu. Ufuatao ni mchango wa Kamala mwanablogu machachari anayepatikana hapa . Yeye anasema: " Kwa vyovyote kuna nguvu inayoendesha haya mambo, kuna nguvu ambayo ni ya ajabu katika hufanyaji kazi wake. nguvu hii wakristo huuita Mungu na waislamu huiita Allah, kila mtu hujiona yuko sahihi lakini wanasayansi ndio basi kwani wao huiita Nguvu tu kama ilivyo. siku zote wanasayansi hukataa kuwepo kwa mtu anayeitwa Mungu lakini hukubali kuwepo kwa nguvu na wanasema kuwa nguvu haiwezi kubadirishwa wala kuharibiwa na wala kupindishwa! uwepo wa nguvu unaonekana tu wenyewe, biblia inasema tumeumbwa kwa mfano wa Mungu kwa hiyo basi na sisi ni nguvu au Roho kama ilivyo hiyo Mungu. sisi kama binadamu mawazo yetu, maneno (kauli) yetu, yananguvu kuliko tunavyofikiri na hubadirisha na kutupangia maisha yetu. kwamfano, Tanzania sio nchi masikini na wala watanzania sio masikini bali ni nguvu ya Hoja ya watu fulani na sisi kuipo

Je, kuna mungu?

Hakuna mjadala kwamba kila jamii inaamini katika Mungu. Hata kama tafsiri hasa ya mungu huyo hutofautiana kutoka jamii moja hadi nyingine, lakini ukweli unabaki kuwa kila jamii inaamini katika mungu. Ningependa tujipe nafasi ya kujadili dhana ya Mungu katika jamii kwa mtazamo usio wa kigomvi wala kulazimishia majibu kwa kutumia imani tulizonazo. Najua dini zetu zilituzuia kujiuliza maswali ya msingi kama haya. Zinatulazimisha kuamini hata kama hatuelewi. Na tunapojaribu kufanya hivyo, tunaambiwa, tunakufuru. Siamini kuwa kujadili jambo kwa nia ya kulielewa ni kukufuru. Tunaishi katika kizazi kinachotaka ushahidi zaidi kuliko imani. Kwa hiyo hapa ninayo maswali ya kuuliza: 1. Je, Mungu yupo? 2. Na kama yupo, nini kinatufanya tuamini hivyo? 3. Je, ni kweli kwamba sayansi inamkana mungu? Nadhani kujielewa ni pamoja na kupata majibu ya maswali haya kwa ufasaha.

Fahamishwa na nifahamishe.com

Kuna tovuti mpya inatangazwa. Nimeipitia. Ina kiingereza na kiswahili. Kwa mujibu wa waendeshaji wake, tovuti hiyo imebeba mambo mengi ya kukuhabarisha ndugu msomaji. Wanayataja: "Habari mbali mbali za Tanzania na za kimataifa, Habari katika picha na video, Live radio, Online Game, Habari za burudani na wasanii wa bong, Utaweza kusikiliza nifahamishe nonstop bolingo na lingala mix, Kuuza kwa kuweka tangazo lako bure au kununua nyumba, magari, vitu vya electronics na kadhalika, Kushare picha na watanzania duniani na kadhalika". Gonga hapa kuwatembelea ujionee mwenyewe.

Kamwe usikate tamaa

Haya tena. Siku zinakimbia kama nini vile. Ni juzi tu mwezi umeanza. Leo eti masaa machache yajayo mwezi unakatika hivi hivi. Mwaka ndio usiseme. Mwezi wa kumi na moja huu. Bado mwezi tu na mwaka ukatikie mbali. Sijui kinachosababisha siku kukimbia namna hii. Muda ni mfupi kuliko matarajio. Mambo mengi kuliko dakika zilizopo. Kazi kweli kweli. Binafsi mwezi huu umepita vizuri pamoja na changamoto za hapa na pale. Nafurahi nimeweza kuzitazama changamoto hizo kwa jicho la kujisahihisha. Nawe ndugu msomaji bila shaka mwezi umekuendea vyema. Hata kama inawezekana umekumbana na changamoto mbili tatu hakuna haja ya kukata tamaa. Usikate tamaa. Kuna mtu aliwahi kuniambia picha nzuri kusafishwa kwenye chumba cha giza. Giza ni muhimu ili kusafisha picha. Maana yake yake unapojikuta kwenye hali inayofanana na giza vile, kwa maana ya changamoto, kukatishwa tamaa, chukulia hiyo kama mchakato wa kukutengenezea picha nzuri mbeleni. Usikate tamaa. Pigana kiume. Songa mbele. Anza mwezi wa kumi

Haiba ni nini?

Sipendi kutumia kiingereza kwa sababu kwanza ninadhani kiswahili kinanitosha kabisa kuelezea kile ninachotaka kusema. Hata hivyo najua pia matumizi ya kiswahili chetu hayajawa katika kiwango kile kilichokusudiwa. Kuna maneno mengi yasiyoeleweka vizuri katika kiswahili cha kitabuni. Moja wapo ya maneno hayo ni hili ninalolitumia leo hii. Haiba. Pengine niweke msisitizo kwa faida ya wale wasiolifahamu neno hili vizuri. Personality. Wengine wanasema maana ya hichi kinachoitwa personality ni utu kwa kiswahili. Ni bahati mbaya kwamba niliyakimbia masomo ya lugha siku nyingi. Ila nimejiridhisha kwamba haiba ndiyo tafsiri muafaka kabisa. Haiba ni nini? Watu wengine watafikiria tunazungumzia mwonekano wa mtu kimavazi. Lakini haiba ni neno pana zaidi ya mwonekano wa mtu kwa nje. Haiba ni jumla ya tabia za mtu zinazotokana na kile anachofikiri, anachopenda, anavyojichukulia yeye mwenyewe, anavyowachukulia watu wengine na kadhalika. Haya yote hujenga mwonekano wa mtu unaopimika (tabia) kama vi

Nadharia ya kuwaelewa wenzio

Bila shaka umeshawahi kugombana. Kupishana na mtu. Kushindwa kuelewana na mwenzako. Kupishana maana yake ni wawili ninyi kushindwa kuelewa kila mmoja wenu anataka nini. Pengine tuanzie hapo. Kuwaelewa wengine. Je, tunaweza kuwaelewa watu wengine? Na tutajuaje kuwa tunawaelewa? Kuelewa mawazo ya mtu, imani yake, matakwa, nia na kadhalika ni jambo la muhimu. Na pengine si tu kuelewa mtu mwingine anawaza vipi, bali vilevile kutumia uelewa huo ili kutafsiri ya kile kinachosemwa na kufanywa na mtu mwingine. Pengine tunaweza kukubaliana kwamba ni kushindwa kuwaelewa wengine ni upungufu mkubwa katika masha ya kimahusiano. Upungufu wa kuwaelewa wengine kujionyesha katika dalili zifuatazo: o Kutokuguswa na hisia za watu wengine. o Kutokuweza kuzingatia wanachojua wengine o Kutokuweza kusuluhisha mambo kwa kuitazama nia ya mtu mwingine wakati alipokosea o Kushindwa kuelewa ikiwa anayekusikiliza anavutiwa na unachosema ama unaongea tu kwa sababu una mdomo o Kushindwa kubashiri maana il

Teknolojia ya simu kwa maendeleo ama kuongeza upuuzi?

Siku hizi kila mtu ana simu ya mkononi. Na kama huna simu unaonekana kama mshamba flani hivi. Kijana gani huna simu? Na si tu kuwa na simu bali ughali wa simu yenyewe. Tunaambiwa asilimia karibu 35% ya watanzania wanamiliki simu za kiganjani. Pengine hayo ni maendeleo. Chukulia Tanzania ambayo ni nchi fukara kuliko hata zile zinazoitwa za ulimwengu wa tatu eti nayo katika hili la simu za mkononi unaambiwa ni kati ya nchi wateja wazuri wa teknolojia hii. Hapo unaona uhusiano wa simu hizi na akili za kimaskini. Sasa tuachane na hayo. Tuje katika matumizi yenyewe ya hizi simu. Kusema kweli wengi wa watumiaji simu hizi, wanazitumia katika mambo ambayo kuainisha faida zake hasa si kazi rahisi. Simu ni mapenzi. Simu ni ngono. Simu ni kuongea upuuzi tu kwa mamia ya dakika. Na ni ajabu sana kwamba waathirika wakuu ni wanafunzi wa vyuo vikuu. Wasomi. Kama vile intaneti zinavyotumika kwa mambo ya kipuuzi na wasomi hawa, ndivyo simu nazo zinavyoendeleza kasumba ile ile: Matumizi wa teknoloj

Kwa nini tunatafuta kasoro zaidi? Mchango wa Nuru Shabani

Tuliwahi kuzungumzia tabia ya kuwaza kupenda kutafuta kasoro. Ilijitokeza michango kadhaa. Hapa ningependa kukuletea mchango mmojawapo uliojaribu kueleza sababu za watu kuwa na tabia hiyo. Namshukuru msomaji Nuru Shabani asiyeishia kusoma na kuondoka. Yeye kuacha maoni yenye lengo la kupanua mjadala zaidi. Anasema: "Watu wengi tumelelewa katika kuutafuta udhaifu au makosa ya mtu na ndiyo tunachokina zaidi kuliko uimara wake. Hiyo siyo asili ya mwanadamu ila ni malezi ambayo tumefundishwa na wazazi nyumbani,walimu mashuleni na jamii iliyotuzunguka. Vitabu vya dini vinatuambia tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, sasa Mungu huyo ambaye ametuumba mbona haangalii kasoro zetu?? "Hii inaonesha kuwa tabia ya kukosoa ni ya kufundishwa na wanadamu wenzetu tena wale wasiojiamini na wenye kutazama mambo kwa upande mbaya. " Kutizama mambo kwa mkabala hasi ni jambo ambalo tumekuwa tukifundishwa kila siku na watu ambao kwa namna moja au nyingine tumepita katika mikono yao kimalezi,n

Je kuna uhusiano kati ya kutembea kwa mtu na tabia yake?

Nuru shabani ni mchangiaji mzuri katika kibaraza hiki. Michango ya msomaji huyu ama kwa hakika kuleta mawazo mapya na yenye faida. Asante sana Nuru Shabani. Kuna swali ameliuliza na nadhani kwa sababu blogu hii ni uwanja wa kujadili mambo yanayohusiana na tabia zetu, swali hili lipo mahali pake. Nimeona ipo haja ya kuliweza wazi kwa ajili ya tafakari za wasomaji wengine wanaopenda mijadala ya aina hii. Yeye anauliza: " Je, kuna uhusiano kati ya kutembea kwa mtu na tabia yake?" Karibuni kwa michango ya maandishi kupitia kisanduku cha maoni kwa faida ya wasomaji wengine. Je, anavyotembea mtu, kunaweza kutafsiri anavyowaza/tabia yake? Asante Nuru Shabani kwa usomaji wenye faida.

Je, hatuwezi kuishi bila ngono?

Siku hizi ni kawaida watu kukutana kimwili  bila ndoa. Ndio maana neno tendo la ndoa halitumiki. Ni ngono. Na hata hivyo inaonekana pia chaweza kufanyika bila mapenzi, kwa hiyo wakabatilisha kukiita kufanya mapenzi. Hiyo ndiyo hali halisi. Mjadala wenyewe ulikuwa katika kuhoji ikiwa kijana wa kisasa anaweza kufikisha miaka zaidi ya ishirini na tano bila kuonja ngono(na kijana mwenyewe asiwe mgonjwa, kwa maana ya hitilafu katika mfumo wake wa uzazi) Je, anaweza kuahirisha kuanza ngono hata kama mwili wake unamshawishi kufanya hivyo? Maana inasemekana kwa mujibu wa wadau hawa, katika siku za leo, ngono haikwepeki! Wewe unasemaje? Ngono ni kama chakula? Kwamba usipoipata utaumwa? Na je, haiwezekani kuwa na mahusiano ya karibu (mno)lakini 'no' ngono? Na kwamba huu mtindo wa kuanza ngono mapema kwa vijana wengi unasababishwa na nini? Ni mwili tu ama ni tatizo la kisaikolojia zaidi? Kwamba ni kujilemaza fulani hivi kuwa aah kila mmoja anafanya bwana? Jielewe

Siri ya mwandiko wako (2)

Kama tunavyoweza kumwelewa mtu kwa maneno anayoongea, pia twaweza kumwelewa kwa kuuangalia mwandiko wake. Unapoandika kwenye karatasi, ukweli ni kwamba unatupa dodoso kuhusu tabia zako. Hebu na tuangalie mifano michache ya aina za miandiko na tabia zinazojidhihirisha kupitia miandiko yenyewe: 1. Mwandiko wa kukandamiza: Maana yake akiandika nundu nundu za herufi zinaonekana upande wa pili wa karatasi. Ni dalili ya fikira chanya, kujiamini (hata kunakozidi mipaka) jeuri saa nyingine, majigambo. 2. Kuandika juu juu kwa kuparua: Kutokujiamini, na tabia ya kufikiria mambo kinyume. Yaani kufikiria ubaya, udhaifu wa jambo zaidi. 3. Mwandiko unaolalia kulia: Mwandishi anafikiria anakoenda zaidi, anafikiria mbele. Mara nyingi hana muda wa kutafakari makosa yaliyowahi kumtokea kwenye maisha yake. 4. Mwandiko unaolalia kushoto: Hufikiria jana na yaliyopita. Hujilaumu kwa makosa aliyowahi kuyafanya. 5. Mwandiko unaoongozeka ukubwa kadiri unavyoandika: Mwandikaji ni mbunifu, mkali, huju

Siri ya mwandiko wako

Hivi umewahi kujiuliza kwa nini mwandiko wako unatofautiana na miandiko ya watu wengine? Hivi unajua kwamba mwandiko unaweza kutupa habari za kutosha kuhusu tabia yako, mwenendo wako, kiasi cha akili ulichonacho na kadhalika? Kuna siri gani katika miandiko yetu? Subiri kidogo nakuja...

Jinsi ya kumsikiliza mwenzio

Tulikwisha kuangalia kwa utangulizi umuhimu wa kusikiliza. Kwamba watu tunaozungumza nao wanaweza kuwa hawajui yale tunayoyajua ama hata kwa kiwango chetu. Lakini je, tunajua kila kitu? Jibu ni wazi kwamba si kweli. Wapo watu wengi wanaojua kuliko sisi katika maeneo kadha wa kadha. Watu hao hawana alama usoni inayowaonyesha weledi wao. Bahati mbaya ni kwamba wajuao huonekana kama vile hawajui. Kwa hivyo, kwa sababu hiyo ya kutoweza kumtambua ajuaye kwa kumwangalia tu, basi hiyo iwe ni sababu tosha ya kukushawishi kuwasikiliza watu wanaokuzunguka. Tufanyeje kusikiliza kwa makini? Tutumie mbinu gani? Hapa tutataja kadhaa, ambazo hata hivyo si msahafu. Tuzijadili kuona kama zaweza kufaa kutufanya kuwa wasikilizaji wazuri zaidi. Mawasiliano ya kweli baina ya watu wawili yana hatua tatu: 1. Kusikiliza: Maana yake kufanya jitihada za dhati kujaribu kusikiliza kile hasa kinachosemwa na mwenzio. 2. Kuelewa: baada ya kufanya jitihada za kusikiliza kinachosemwa, sasa unajitahidi kupat

Jifunze kusikiliza kuliko kusema

Kusema ni rahisi kuliko kusikiliza. Kumsikiliza mtu ni kazi ngumu. Hasa kama anayezungumza anaonesha kuwa na mawazo unayodhani yanatofautiana na mawazo yako ama pengine yanapingana kwa kiasi kikubwa na mawazo yako. Kazi inakuwa kubwa kweli kweli hasa inapoonekana kama vile mzungumzaji ana uelewa mdogo kuliko wako. Yaani anapozungumza unahisi kama unaelewa anakokwenda, anachotaka kusema, anawaza nini na kwa nini anataka kusema hivyo anavyovisema. Unaelewa na unashindwa kujizua kuonyesha hisia hizo na hivyo unathubutu kuingilia sentensi zake. Kumsikiliza mwenzio na kusoma mawazo ya mwenzio si kazi rahisi. Ni kazi ngumu kweli kweli. Ni bahati mbaya sana kwamba wengi wetu tunapenda kusema. Tunapenda kusikilizwa. Tunapenda watu wengine wasikilize zaidi mawazo yetu kuliko sisi tunavyowasilikiza wao. Pengine ni kwa sababu ya ile hulka kwamba "Ninajua..." Hatuwezi kuukana umuhimu wa sisi kujitahidi kujifunza kwa bidii kuwasikiliza wenzetu. Sababu ni kwamba vile tunavyovijua n

Kwa nini miungu ni mingi kiasi hiki?

Hakuna jamii ambayo haijawahi kuwa na wazo la uwapo wa nguvu iliyo juu ya asili ya ulimwengu. Nguvu hii imeitwa majina mengi lakini lililo maarufu ni mungu. Wengi wetu, hata kama hatuna ushahidi wa kujitosheleza, bado hatusiti kabisa kuamini kuwa mungu yupo. Ukiangalia vyema utaona namna ambavyo dunia inayo miungu kwa maelfu, na kila mungu ana sifa zake tofauti na miungu wengine. India kwa mfano, tunaambiwa kuwa idadi ya miungu inaweza kuzidi hata idadi ya waumini wenyewe! Na ni makosa kudhani kwamba wingi wa miungu hiyo ni majina tofauti tofauti kwa mungu huyo huyo. Sababu ni kwamba hata mahitaji yao yanatofautiana. Kanuni wanazotoa ili tuwafikie zinatofautiana. Tabia zao zinatofautiana. Kwa hiyo, ni wazi kuwa miungu wako wengi. Sasa kwa nini dunia inayo miungu mingi hilo ndilo swali ninalotaka kukuachia leo. Inakuwaje kila jamii inavutiwa na wazo kuwa yupo mungu hata kama haonekani? Wapo wanaoamua mpaka kutengeneza sanamu kuhusianisha kile wanachokiamini na kitu kinachoonekana.

Kulikoni JUMUWATA?

Picha
WENGI wetu tunakumbuka namna ambavyo vuguvugu hili la blogu lilikuja kwa kasi kama miaka mitatu hivi iliyopita. Na Ndesanjo Macha akiwa mhamasishaji mkuu katika ukuzi wa Teknolojia ya blogu katika kiswahili kwa kujitolea. Kampeni zake zilitufikia wengi wetu kupitia ukurasa wake wa gumzo la wiki katika gazeti la mwananchi . Nina hakika kwamba kazi hiyo hakuifanya kwa malipo. Alijitolea muda wake na matunda yake yalikuwa wazi. Bila yeye, bila shaka blogu maarufu kama Michuzi , Bongo celebrity , Kijiji cha Mjengwa , Haki Ngowi , Now and then na nyinginezo nyingi bila shaka zisingekuwepo. Narudia neno bila shaka. Historia ya Blogu Tanzania haiwezi kukamika bila kumtaja yeye. Basi. Kasi ya blogu iliendelea kukua kwa kasi mno kiasi cha kufikia kuundwa kwa Jumuiya ua Wanablogu Tanzania. Wakachaguliwa viongozi tarehe 29 Juni 2007. Tukafurahi. Hata hivyo, lazima tuwe wazi kwamba kasi ya ukuaji wa blogu imeendelea kuwa ndogo kwa karibu mwaka sasa. Jeff Msangi aliwahi kuzungumzia suala h

Hivi watoto 'wa mitaani' wakikua huenda wapi?

Mimi sikuwahi kujiuliza swali hili. Baada ya kuisoma makala ya Ayoub Ryoba katika Gazeti la kila wiki la Raia Mwema nilifikiri mara mbili mbili: Hivi kweli hawa watoto tuliowabandika majina mengi ya fedheha kama eti watoto wa mitaani huenda wapi wakikua? Hapo tu. Hawa watoto ambao wengi wetu hatuna habari nao, si wanakua? Je, wakikua 'wanaishiaga' wapi? Ni watoto waliokata tamaa. Hawana amani. Wanaiona jamii kama inayowaonea. Wana kisasi. Je, wanapokuwa huishia kuwa akina nani? Hii ni changamoto ya aina yake. Namshukuru mwandishi huyu kwa kutukumbusha eneo hili kwa uzito unaostahili. Fikiria watu kama wabwia unga. Majambazi sugu. Makahaba na kadhalika. Uone mzunguko wa aibu tunaoujenga katika jamii. Kama unadhani kuwa matatizo yao hayakuhusu, tafakari kwa bidii. Tunaweza kupunguza tatizo hili la kuwa na watoto wengi wa aina hii, amabo wakiisha kukua wanaturudia kwa mlango wa nyuma kwa kuacha tabia ya hovyo ya kupenda kuzaa bila kuhesabu gharama.

Kura nipige mimi, kula wale wenyewe?

Niko saluni jioni Jumamosi. Kuna vijana wanne. Umri wao wote ni kati ya miaka 20-30. Kinyozi: (Huku akininyoa baada ya kimya kifupi)…Ee bwana watu wengine noma. Mie: Imekuwaje? Kinyozi: Hapa watu karibu wapigane kisa Simba (timu ya mpira wa miguu) kafungwa mbili na Azam kitimu kidogo... Mie: Kwani tatizo ni nini? Kinyozi: Tatizo ni kwamba wanaopigana hata kadi za uanachama hawana. Mie: Labda ushabiki si unajua tena…au wewe hushabikii mpira? Kinyozi: Mi hata sifuatilii sana mambo ya kijinga haya. Mi nafuatilia mambo yangu bwana. Mie: Kwa hiyo mpira hufuatilii kabisa? Kinyozi: Hata mara moja bosi wangu. Upuuzi mtupu. (Akalalamikia uongozi mbaya wa timu zetu kwa zaidi ya dakika tano kisha…) Mi labda timu za Ulaya. Napenda Aseno. (Akatumia dakika kadhaa kuifagilia) Mie: Una kadi ya Aseno? Kinyozi: (Akicheka) Sina ila sipigani wakifungwa Mie: Sasa hapa home unafuatilia nini? Kinyozi: Bongo nifuatilie nini hapa pamechoka hivi… kwanza ningekuwa na uwezo ningezamia

Mtembelee mwanablogu mpya Kristine Missanga

Karibu umtembelee mwanablogu mwenzetu, ambaye bila shaka anayo mengi mapya. Falsafa. Mtizamo mpya. Maswali. Lengo lake kama anavyosema mwenyewe ni kutujengea utamaduni wa kujiuliza. Blogu yake inaitwa Jiulize. Unaweza kumtembelea kwa kubofya hapa kumsalimia.

Maisha hayawezekani bila wanasiasa?

Kama kuna 'kazi' ambazo zinanitatanisha ni zile zenye uhusiano wa moja kwa moja na kile kinachoitwa siasa. Kazi hizi zimepata umaarufu sana katika nchi za dunia ya tano ikiwamo Tanzania. Kuna wanaoamini kuwa siasa ni porojo. Siasa ni usanii. Siasa ni uchezewaji wa wazi wa akili za watawaliwa. Udanganyifu. Utapeli wa wazi. Siasa. Sina hakika kama ninakubaliana na mawazo haya. Bado natafakari. Kwamba siasa ina uhusiano na maendeleo yetu (hasa sisi wa dunia ya tano) hilo ni jambo la kufikirisha. Siku hizi siasa imekuwa kama muziki wa Bongo Flava. Kila mtu anataka kujihusisha nayo. Wataalamu wa fani mbambali wenye ujuzi adhimu, wanazitosa ofisi zao na kukimbilia siasa. Tunawafahamu walimu wa Vyuo Vikuu ambao hata hawana haiba ya siasa, bado walidiriki kuzitosa ofisi zao. Kisa? Ulaji. Samahani siasa. Na idaidi yao haihesabiki. Mtu unajiuliza mwananchi aliyesomeshwa kwa fedha ya walipa kodi fukara, na akawa mathalani daktari bingwa, ama mtaalam wa uchumi kwa mfano, anaachana

Furaha ni uamuzi wako mwenyewe, amua

KILA mtu angependa kuwa mwenye furaha. Wapo wanaamini kuwa lengo la maisha ya mwanadamu hapa duniani ni kuitafuta furaha. Kwamba purukushani zote hizi katika maisha zina lengo la kuisaka furaha. Fikiria vitu kama pesa, elimu, ndoa nzuri, familia, umaarufu na kila kilichojema ambacho mwanadamu hukitafuta kwa bidii lengo ni kuitafuta furaha. Vitu kama dini kimsingi lengo ni hilo hilo -furaha. Kwamba dini inakuwa ni kimbilio rahisi katika kuyasahau matatizo tunayokumbana nayo hapa duniani kwa mawazo kwamba tuendako ni bora kuliko hapa. Matokeo yake tunakuwa na matumaini zaidi. Tunakuwa wenye furaha. Lakini ni bahati mbaya sana kwamba watu wengi hatuna furaha. Tunatafuta elimu tukidhani tunaweza kupata furaha lakini si hivyo inavyokuwa.(Inasemekana kwa kadiri unavyokuwa na elimu ndivyo unavyozidi kuziona kasoro katika maisha yanayokuzunguka na hivyo kukupungizia furaha) Tunatafuta pesa, kwa matumaini hayo hayo, lakini hata tunapokuwa nazo bado hazitupi furaha. Tunapata mahusiano tuna

Kukosoa, kutafuta makosa, si tabia njema

Siamini kwamba ukosoaji ni asili ya mwanadamu. Kufikiria kinyume (negative). Kwamba watu wote wanakosea isipokuwa wewe. Kwamba watu wote wamepotea isipokuwa wewe. Kwamba watu wote wanahitaji msaada isipokuwa wewe. Kufikiria ubaya zaidi wa jambo kuliko uzuri wake. Kufikiria udhaifu kuliko ubora wake. Kufikiria uharibifu zaidi kuliko uboreshaji. Kwamba unaweza kusoma kitabu cha mwandishi fulani, si kwa sababu unataka kujifunza, bali kupekua wapi kakosea. Kwamba unaweza kuzungumza habari za mtu, si kwa nia ya kujenga, bali kwa nia ya kumtafutia makosa yake. Kwamba watu wanaweza kukwambia jambo zuri na la manufaa, lakini wewe ukalichukulia kwa mtazamo hasi. Ukakosoa. Kwa nini iwe rahisi zaidi kufikiria udhaifu/ubaya wa mtu/suala kuliko kufikiria uzuri wake? Hivi mwanadamu anavutiwa na nini kutafuta kasoro? Je, kutafuta/kupekua kasoro ni asili ya mwanadamu ama ni tabia inayojiotea kulingana na mazingira ya mhusika?

Kwenda mbele kunahitaji kugeuka nyuma?

Ningependa leo tuone ikiwa inatulazimu kuikumbuka jana ili kuweza kuendea kesho. Maana yapo mawazo kwamba ili tuweze kwenda mbele kwa ufanisi, ni vyema kugeuka nyuma kutathmini tulikotoka. Kwamba ni kwa kutumia historia twaweza kubashiri mwelekeo wetu. Tunaambiwa historia hutuelimisha kuhusu mwenendo wetu na namna mwenendo huo ulivyoweza kutufikisha hapa tulipo. Ni kwa kutumia historia hiyo, inasemwa, twaweza kupata maarifa yatakayotusaidia kujikosoa ama kujizatiti kwa faida ya kesho na kuendelea. Wenye mtazamo huu, wanaamini katika nguvu ya historia katika maisha ya mwanadamu. Kwamba maisha yajayo, hayana miujiza. Ni mwendelezo wa mambo yale yale kwa namna isiyotofautiana sana na haya tunayoyajua. Kwamba maisha yatarajiwayo ni kama mwendelezo wa tamthilia ndefu yenye vipande vingi. Vipande hivi vinategemeana. Tukio la kipande kimoja cha tamthlia, hutupa bashiri ya simulizi za vipande vinavyofuata –pamoja na kwamba badiliko dogo laweza kutokea. Katika kujaribu kutanabaisha hiki

Je,nini hasa kinachoongoza mwenendo na tabia yako?

Umewahi kufikiri ni kitu gani hasa kinachoyaongoza maisha yako na namna unavyotekeleza matakwa yako? Kitu gani hasa ambacho ndicho unachoweza kukitaja kwa hakika kwamba ndicho kinachokuongoza. Je, ni mafundisho ya dini yako? Je, ni mtizamo wa watu wanaokuzunguka pamoja na utamaduni wao? Je, ni mambo unayojifunza kwa kuyasoma ama kutazama? Je, ni mtizamo wako/falsafa binafsi? Au ni kitu usichokijua? Nauliza tu. Jielewe.

Kitabu kipya, nimekipata Book Point Arusha jana

Picha
Kitabu kizuri kimeandikwa na Marshall Goldsmith. Kitafute ukisome, kitakufaa.

Kwanini watu huwasema vibaya wenzao?

Binadamu wengi hatupendi tusemwe vibaya. Tunajisikia kuvunjika moyo tunapohisi kuwa yupo mwenzetu anaona fahari kuyasema mapungufu yetu bila staha. Kama wewe si mmoja wapo samahani. Wenzako ndivyo walivyo. Sababu ni kwamba binadamu tunapenda kuonekana wa thamani hata kama mara nyingine thamani hiyo tunayoidai hatunayo. Tunalo hitaji la kuona kuwa wengine wanatuheshimu, kututhamini na kuwa na maoni chanya kutuhusu. Kinachotofautiana, ni kiwango. Hebu fikiria. Mfanyakazi mwenzako anakujia na kuuponda utendaji wako wa kazi uso bin uso. Bila adabu. Bila staha. Ama mwenzi wako anakukosoa mbele za watu kuhusu mambo ambayo yanawahusu ninyi wawili. Ama mkuu wako wa kazi anapokuhamakia kikaoni. Ama rafiki yako anakusemea mbovu mtaani. Kwa wengi wetu, japo katika viwango tofauti, itauma. Sasa ni hivi: Hivyo unavyojisikia ndivyo binadamu wengine wanavyojisikia ukiwaponda. Ni ajabu na kweli. Sisi hawahawa, tunaodai heshima kwa nguvu, ndio hao hao tunaoona raha kuwashushia wenzetu thama

"True confension', mhalifu anapokiri kosa

Picha
Jana nilipita hapa nikakumbuka enzi hizo. Sikumbuki ni idadi gani ya vitabu "nilivichomoa" humu. Enzi hizo nilikuwa mteja wa kudumu humu. Nilikesha ndani ya jengo hili wakati huo wenzangu wakifanya mambo mengine mitaani.

Hasira ina maana gani kwetu?

Hasira si kitu kigeni. Kama hujawahi kuwa na hasira maishani mwako, basi bila shaka mwenzetu unacho kitu fulani ambacho binadamu wenzako wote hawanacho (kasoro?). Hasira ni jambo la kawaida kututokea sisi kama binadamu. Waweza kusababishiwa hasira na watu wengine, vitu ama wewe mwenyewe ukajikasirisha. Bila kujali chanzo chake, ukichunguza vyema utaona ya kwamba karibu mazingira yote yaliwahi kukusababishia hasira yanafanana –fanana kimsingi. Yaani kila jambo fulani akilini mwako lilipoguswa, uliwaka moto kwa hasira. Ulifura. Sasa ningependa tujiulize: Hasira hasa ni nini na ina maana gani kwetu? Inahusianaje na namna tunavyojifikiria? Pengine sijielezi ninavyotaka. Hebu tujaribu hivi: Je, kuna tofauti gani ya kujifikiria wewe mwenyewe kama wewe kabla na wakati wa hasira? Je, kuna tofauti gani ya kuwafikiria wengine (wanaotusababishia hasira) kabla na wakati wa hasira? Je, kwa nini kuna watu hasira huyeyuka kirahisi ilhali wengine hasira ikiacha makovu ya kudumu? Hasira ni kipimo