Mwezi wa tano ndio huu. Tarehe mbili leo. Kama ulikuwa hujapanga cha kufanya mwezi huu, ndugu, hujachelewa. ( Si unajua haipendezi kufanya chochote bila kupanga?) Tabia ya kusubiri mwisho wa mwaka ndio tuanze kufikiri kupanga mipango mingi ya mwaka mzima ( ambayo hata hivyo haitekelezeki) si nzuri sana. Nakukumbusha mipango yako ya mwaka huu: Ulipanga kufanya nini mwaka huu? Je, umefikia walau nusu ya mipango yako? Una mikakati gani na mwezi huu wa tano? Nusu ya mwaka ndo inayoyoma! Nakukumbusha kutafakari upya mambo yako mwaka huu, uone wapi umefanikiwa na wapi unahitaji kujipanga vyema zaidi. Nakukumbusha kutafakari changamoto ulizokumbana nazo katika sehemu ya kwanza ya mwaka huu, na ufikiri namna ya kukabiliana nazo vizuri zaidi kwa nusu iliyobaki. Na unapofanya hivyo, usiache kupitia hapa kuanzia juma hili kwa ajili ya vipande vya saikolojia na falsafa za kutafakari pamoja namna ya kujielewa. Niwatakieni wanablogu wote heri ya mwezi mpya wenye mafanikio (pamoja na uki
hapo ipo kazi je kuna usalama kwani naona kama kitanda hapo.
JibuFutahapo ipo kazi je kuna usalama kwani naona kama kitanda hapo.
JibuFutaBwaya,
JibuFutaJe hii imetokea waoi?
Je kulikuwa na maafa?
hebu tujuze basi, mkasa mzima juu ya habari hii.
Kweli kabisa nakubaliana na kaka Shaban hapo kwamba TUJUZE lakini kuna watu kama siyo vijitu havisikii kama siyo hawaelewi labda hawajaelewa. Lakini kweli hii ni hatari
JibuFutaWadau,
JibuFutaAliyekuwa mmiliki wa hayo mabaki ya simu na kitanda kinachoonekana, alikuwa akiongea na simu hali ikiwa imeunganishwa kwenye umeme. Ikalipuka. Akafa.
Tunajifunza nini? Je, tunajua maafa yanayoambatana na matumizi ya simu?
siamini chris kweli tena hii ni kututisha tu
JibuFutaEbwanaee,kwa sasa kompyuta za mapajani,simu vimekuwa ni kama ulevi nchi hizi.Hapa udosini majuzi mzee mmoja kaungua sikio na sehemu ya kichwa upande wa kuume baada ya kulipukiwa na simu.
JibuFutaJamaa wanawalaumu wachina kwa bidha zao kuwa haizna ubora wa kutosha.Ulevi wa hivyo vitu umeanza kuniandama.
Ebwanaee,kwa sasa kompyuta za mapajani,simu vimekuwa ni kama ulevi nchi hizi.Hapa udosini majuzi mzee mmoja kaungua sikio na sehemu ya kichwa upande wa kuume baada ya kulipukiwa na simu.
JibuFutaJamaa wanawalaumu wachina kwa bidha zao kuwa haizna ubora wa kutosha.Ulevi wa hivyo vitu umeanza kuniandama.
Chrissie na Edigio, huu ni upande wa pili wa teknojia. Si utani. Kompyuta zinapofusha. Kompyuta za mapajani zinaharibu mbegu za kiume, simu ndiyo hivyo. Kila kitu kina pande mbili.
JibuFuta