Naam. Idadi ya wanablogu inaongezeka. Na kila mwanablogu anakuja na mtazamao mpya. Hebu mtembelee Koero uone. Kama utakavyoona, ujio wa watu kama hawa ni wa muhimu sana. Karibu sana Koero tujadiliane.
Labda naweza kuwa nakosea, lakini nadhani ile dhana kuwa hatupendi kufikiria inaanza kuondoka polepole. Labda sasa ni kwamba hatupendi kuchangia fikra zetu lakini nalo litaondoka. Ule mtazamo wa kila mwenye blog aje na picha sasa unaanza kupoteza ukweli na sasa watu wanaanza kufikirisha wasomaji zaidi. Lakini pia twahitaji taswira kwa hiyo wenye kufikirisha kama Koero karibuni saaana na wenye taswira pia mwakaribishwa maana mwatusaidia "kusindikiza" tafakuri zetu. Karibu Koero na wenye nia ya hivyo
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.
SAIKOLOJIA, neno lililotoholewa kutoka neno la kiingereza psychology, si elimu inayoeleweka sana katika jamii yetu. Asili ya 'psychology' ni neno 'psyche' lenye maana ya nafsi. Katika makala haya, tunasaili kwa ufupi maana ya saikolojia kama taaluma na kuonesha nafasi ya taaluma hiyo ngeni katika jamii yetu katika kutatua matatizo ya kijamii na hivyo kuharakisha juhudi za watu kujiletea maendeleo yetu.
Sipendi kutumia kiingereza kwa sababu kwanza ninadhani kiswahili kinanitosha kabisa kuelezea kile ninachotaka kusema. Hata hivyo najua pia matumizi ya kiswahili chetu hayajawa katika kiwango kile kilichokusudiwa. Kuna maneno mengi yasiyoeleweka vizuri katika kiswahili cha kitabuni. Moja wapo ya maneno hayo ni hili ninalolitumia leo hii. Haiba. Pengine niweke msisitizo kwa faida ya wale wasiolifahamu neno hili vizuri. Personality. Wengine wanasema maana ya hichi kinachoitwa personality ni utu kwa kiswahili. Ni bahati mbaya kwamba niliyakimbia masomo ya lugha siku nyingi. Ila nimejiridhisha kwamba haiba ndiyo tafsiri muafaka kabisa. Haiba ni nini? Watu wengine watafikiria tunazungumzia mwonekano wa mtu kimavazi. Lakini haiba ni neno pana zaidi ya mwonekano wa mtu kwa nje. Haiba ni jumla ya tabia za mtu zinazotokana na kile anachofikiri, anachopenda, anavyojichukulia yeye mwenyewe, anavyowachukulia watu wengine na kadhalika. Haya yote hujenga mwonekano wa mtu unaopimika (tabia) kama vi...
YAMEKUWEPO madai kwamba Uislam ulianza tangu kuumbwa kwa dunia. Na wapo watu wanaotuaminisha hayo. Ukweli ni kwamba Uislam ulianzishwa na Nabii Muhammad mwaka 622 BK huko Arabia. Kabla yake, dini zilizokuwepo zilikuwa ni Uyuda ambayo ni dini rasmi ya Wayahudi (Judaism) na Ukristo ambayo ni dini ya mataifa wasio Wayahudi ulioanza miaka kadhaa baada ya Yesu kuwa ameondoka mwaka 33BK. Yesu mwenyewe hakuanzisha Ukristo. Alisali katika misikiti ya Wayahudi. Masinagogi. Maelezo haya yana msingi wa kistoria na sio propaganda za kidini. Ndio ni propaganda kwa sababu dini zote zimekuwa na tabia ya kuonyesha kwamba zenyewe ndizo za kweli kuliko dini nyinginezo hata ikibidi kwa kuichezea historia. Na ni bahati mbaya kwamba Dini zimekuwa na tabia ya kufanana ya kuzima uwezo wa waumini wake kuhoji lolote kwa kuwajengea hofu ya kujitafutia laana. Qur’an inatupa maelezo yanayokinzana kuhusu lini hasa Uislamu ulianza. Baadhi ya mistari katika kitabu hicho zinadai kwamba ‘nabii’ Muhammad ndiye ...
Kama tulivyoona katika makala yajuma lililopita , usaili ni hatua ya mwisho kuelekea kupata kazi. Sehemu kubwa ya usaili ni maswali na majibu yanayolenga kupima uwezo wako wa kukabiliana na changamoto halisi za kazi. Ingawa yapo maswali yanayoweza kukupa wasiwasi wa nia ya mwuulizaji, fahamu kuwa hakuna swali linaulizwa kwa nia mbaya au kwa bahati mbaya. Kila swali linaloulizwa linalenga kutafuta uthibitisho kuwa wewe ni mtu sahihi kwa kazi unayoomba.
Global Voices Citizen Media Summit in Cebu, The Philippines in 2015. Photo Courtesy of Global Voices I started my blog in 2005. I was among very few Tanzanians who were inspired by Ndesanjo Macha to start blogging. For those of you who do not know, the history of Tanzanian blogosphere recognizes the contribution of this great man. His influential weekly column in a local newspaper invited many of us to his blog. In fact he was the first Tanzanian to blog in Kiswahili . That was in 2004. I had the privilege of meeting him in Nairobi, Kenya in 2012 and in Cebu, The Philippines in 2015. We were both attending Global Voices Citizen Media Summits. For me, blogging was fun. I never thought that blogs could actually threaten politicians. That was until 2010 when I had an opportunity to attend the Global Voices Citizen Media Summit in Santiago de Chile. I was shocked to hear friends talking about restriction of fr...
"Wewe ni nani?" Uliza swali hili kwa kila unayekutana naye na sikiliza majibu yao: "Mimi ni Idi" "Mimi ni Mashaka" Tena kwa kujiamini kabisa. "Mimi ni Masumbuko" Huku akikushangaa kwa kumuuliza swali la kitoto. Ukionesha kutokuridhika na majibu hayo mepesi, ukaongeza swali jingine, sana sana utaonekana mtu wa ajabu unayeuliza kitu kinachoeleweka. Utaonekana huna kazi. "Unaulizaje swali kama hilo? Ina maana unataka kunifanya mimi sijijui?" Lakini ukweli ni kwamba pasipo kujibu swali hilo, kila unachokifanya kitakuwa ni kupotea njia. Sababu wewe ulikuwa wewe kabla hujapewa hilo jina ulilonalo. Yaani wewe ulikuwa wewe kabla hujaambiwa ni wewe. Jitahidi usipotee njia. Anza leo. Jijibu swali hilo. Nakutakia siku njema ambayo inaweza kuwa mwanzo wa kujua wewe ni nani hasa wakati unazaliwa.
Haswa! Koero kaja kakamilika. Tunakukaribisha kwa mikono yote. Kazi yako ni nzuri sana.
JibuFutaLabda naweza kuwa nakosea, lakini nadhani ile dhana kuwa hatupendi kufikiria inaanza kuondoka polepole. Labda sasa ni kwamba hatupendi kuchangia fikra zetu lakini nalo litaondoka. Ule mtazamo wa kila mwenye blog aje na picha sasa unaanza kupoteza ukweli na sasa watu wanaanza kufikirisha wasomaji zaidi. Lakini pia twahitaji taswira kwa hiyo wenye kufikirisha kama Koero karibuni saaana na wenye taswira pia mwakaribishwa maana mwatusaidia "kusindikiza" tafakuri zetu.
JibuFutaKaribu Koero na wenye nia ya hivyo
waama kweli kabisa
JibuFuta