Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Mahusiano na Ndoa

Mahusiano yenye ‘utulivu’ bila amani

Picha
Chanzo: stock.adobe.com Hivi umewahi kutaka kumwambia mtu jambo unaloona ni muhimu lakini ukakosa namna nzuri ya kumwambia?Unatamani ujumbe ufike lakini maneno sahihi ya kuubeba huna. Unafanyaje? Wengine huamua kuacha. Kuliko kumwuumiza mwenzako, huona bora mtu uugulie maumivu ndani kwa ndani. Mwingine hajali. Huamua bora ‘kutema nyongo’ hivyo hivyo bila kujali maumivu yatakayoyasababishwa na ujumbe. Wanachosahau, matokeo yanayotokana na k u jiumiza kwa kuuzuia ujumbe yanaweza kuwa sawa na madhara ya kuuachia ujumbe kiholela bila kujali maumivu ya atakayeupokea.   Mawasiliano ni sayansi yenye nafasi nyeti katika mahusiano. Ukikosea kanuni, mawasiliano yana nguvu ya kuleta uharibifu mkubwa unaoweza kugharimu afya ya mahusiano. M awasiliano ni sanaa pia.   Namna unavyosema jambo ni muhimu wakati mwingine kuliko hata ujumbe wenyewe. Ukishindwa kuchagua maneno sahihi na mazingira sahihi ya kusema jambo unaweza kufubaza uzito wa ujumbe wako. Thamani ya unachokisema inabebwa pia...

Jinsi ya kumlinda mtoto na tofauti zenu

Picha
Simulizi la Renee limenikutanisha na wadau wa ushunuzi mjini Moshi. Tunapata kahawa jioni baada ya shughuli za siku. Hatujaonana muda. Tunasalimiana na kisha mada inageuka ghafla. Rebert anarejea mfano wa Renee, “Suala la mgogoro wa wazazi kumuathiri mtoto hilo halina mjadala.” Robert ‘anavuta’ kahawa kidogo kama mtu anayesikilizia ladha ya kinywaji cha moto sana na kisha anaendelea.   “Ukimsoma huyu dada ni dhahiri migogoro ya kifamilia ilikuwa na nguvu ya kuchora mwelekeo wa maisha yake ya kimahusiano.” Robert anasita. Wajumbe wamepotelea kwenye vioo vya simu zao. Kajihisi anaongea mwenyewe. Natingisha kichwa kumwitikia.   “Inasikitisha sana namna maamuzi yetu kama wazazi yanavyoweza kumnyanyasa mtoto kwa kiasi kile. Sitamani niwe mzazi nitakayemfanya mtoto awe na kazi kubwa ya kurekebisha tabia alizojifunza kwangu,” anajitahidi kujieleza Robert lakini kakatishwa tamaa. Wanaume hawamsikilizi wanacheka na simu zao. Hata mimi pia ninahisi huenda ninamsikiliza mwenyewe...

Unataka Kumjua Rafiki Atakayekusaliti? Soma hapa

Picha
PICHA: Recycle Coach Katika nyakati kama hizi za Pasaka, mara nyingi, tunasikia marehemu Yuda Iskariote akijadiliwa kama jitu ovu lisilo na maadili lililokuwa tayari kumsaliti Bwana wetu Yesu Kristo. Binafsi naamini, pamoja na ubaya wake, usaliti wa Yuda ulikuwa muhimu katika kuwezesha mpango wa Mungu kwa wokovu wetu. Wakati mwingine Mungu hutumia mabaya kuwezesha mazuri. Hata hivyo, kwa maoni yangu, Yuda hakuwa na nia mbaya kivile. Kwanza, alikaa na Yesu kwa muda wa kutosha na hivyo alifahamu Yesu hakuwa mtu wa hivi hivi anayeweza kuchezewa kienyeji. Yesu alifanya miujiza mingi na Yuda alishuhudia. Yesu alitembea juu ya maji. Yesu alifufua wafu. Si mara moja. Tena kuna wakati Yesu alimfufua mtu aliyekuwa kazikwa siku tatu. Unamkumbuka Lazaro. Aidha, kuna nyakati washikadini na wanafiki walitaka kumshughulikia Yesu, wakashindwa kwa sababu Yesu aliwaponyoka. Yuda aliyafahamu yote haya. Kama baadhi yetu tunavyofanya leo, Yuda aliutazama uwezo huu wa Yesu k...

Tunatofautiana sana...

Picha
PICHA: Verastic Mwanamke, kwa asili yake, anajisikia vizuri kusema matatizo yake kwa mtu wake wa karibu anayemwamini –kama, mathalani, mume wake. Ile tu kujua kuna mwanaume yuko tayari kusikia yanayousibu moyo wake kunamfanya ajisikie salama.

Kwa Nini Wanawake Wenye Mafanikio Wanaogopwa?

Picha
UPO ukweli kuwa wanaume wengi wanawaogopa wanawake wenye mafanikio. Hawa ni wanawake wenye kiwango kikubwa cha elimu, fedha, umaarufu au hata madaraka katika jamii. Hoja ya wanaume wenye mawazo haya ni ugumu wa kuwaongoza wanawake wanaowazidi kama alivyonieleza Godfrey, mwalimu wa sekondari jijini Arusha:

Ukitaka Mwenzako Akuamini, Jifunze Kutanguliza Mahitaji Yake

Picha
PICHA: Merriam-Webster WIKI iliyopita nilitoa mifano michache ya namna ubinafsi unavyoweza kuwa na manufaa katika kutusaidia kupambana na hatari zinazotishia usalama wetu –kimwili na kisaikolojia. Nilisema ubinafsi pamoja na ukakasi wake unalenga kutusukuma kupata mahitaji yetu ya msingi. Jambo hili liliwahi kuelezwa na Abraham Maslow.

Mambo ya Kutafakari Unapoanzisha Uhusiano wa Kimapenzi Kazini

Picha
PICHA: Shalinii Choudhary   Sehemu kubwa ya maisha yako kama mfanyakazi unaitumia kwenye eneo la kazi. Ingawa inategemea na aina ya kazi unayoifanya, ni wazi muda mrefu kwa siku unaoutumia kutekeleza majukumu yako unakuweka karibu zaidi na wafanyakazi wenzako kuliko hata familia na marafiki. Mazingira haya ya ukaribu wa kikazi, wakati mwingine, yanatengeneza uwezekano wa uhusiano wa kimapenzi baina ya wafanyakazi.

Ukitaka Kuaminiwa Jenga Mazingira ya Kuaminika

Picha
PICHA:  PsyBlog “Nina mke asiyeniamini kabisa,” aliniambia bwana mmoja hivi majuzi. “Hana imani kabisa na mimi.  Juzi kati hapa nimemkuta anachunguza simu yangu. Tuligombana sana.” Nilimwuliza kwa nini anafikiri mke wake hamwamini. “Basi tu ndivyo alivyo. Hata ufanyaje hana imani.”

Hakuna Ulazima wa Kushinda Kila Majadiliano

Picha
PICHA: Elly Prior Chukulia mnajadiliana jambo na rafiki yako. Inaweza ikawa ni mtandaoni, nyumbani, ofisini au mahali kwingineko. Katika mazungumzo yenu unabaini hamuelewani. Kile unachoona ni sahihi, sivyo anavyoona mwenzako. Kila mmoja wenu anajaribu kutetea upande wake kuliko anavyoelewa mtazamo wa mwenzake. Unadhani kipi ni sahihi kufanya katika mazingira hayo? Je, ni busara kuendelea kuthibitisha ulivyo sahihi hata kama ni dhahiri mwenzako hayuko tayari kukuelewa? Unajisikiaje mwenzako akikuonesha haukuwa sahihi? Mara nyingi tunafikiri kushindwa na kutokuwa sahihi ni udhaifu. Tunapambana na wasiotuelewa kwa mabishano na majibizana kwa lengo tu la kuonesha tulivyo kwenye upande sahihi. Unazungumza ili kushinda? Nakumbuka siku moja nilishiriki mjadala mmoja kwenye mitandao ya kijamii. Katika mjadala huo, kulikuwepo na pande mbili zinazotofautiana kimtazamo. Kadri mjadala ulivyoendelea, niligundua hapakuwa na jitihada za pande mbili hizo kuelewana. Kila upande...

Mafanikio Hayamfanyi Mwanamke Anayejitambua Kuacha Wajibu Wake

Picha
PICHA: RealClearPolitics USAWA wa kijinsia katika dunia ya leo si suala linalohitaji mjadala. Tunakubaliana kimsingi kuwa hakuna jinsia bora kuliko nyingine na pia hakuna jinsia inayohitaji kulipa gharama ya kulinda hadhi ya jinsia nyingine. Mwanamke, anayo haki ya kupata elimu kulingana na uwezo wake, kufanya kazi anayoiweza, kumiliki na hata kurithi mali sawa na mwanaume.

Mwanaume Anayejitambua Hatishwi na Mafanikio ya Mwanamke

Picha
PICHA: Ayo Martins Upo ukweli usiosemwa wazi kuwa wanaume wengi wanawaogopa wanawake wenye mafanikio. Wanawake waliosoma, wenye mali na fedha, wenye madaraka makubwa katika jamii, wanakuwa na mtihani mkubwa kuanzisha na kudumisha uhusiano na wanaume.

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke -2

Picha
Katika makala iliyopita , tuliona kuwa mwanamke anahitaji kujua anavyopendwa na mwenzi wake kwa maneno na vitendo. Kadhalika, tuliona mwanamke anatamani kuwa na uhakika wa nafasi ya kwanza kwa mwenzi wake. Hatamani kuona akishindana kwa umuhimu na chochote kile kinachoweza kuchukua nafasi yake kwa mwenzi wake.

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Picha
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.

Miaka miwili ya Kuwa 'Mama' Ina Mafunzo Makubwa Kwangu...

Picha
Nilipoamua kuchukua uamuzi wa kubadilishana majukumu na mke wangu sikujua ni kwa jinsi gani uamuzi huo ungenibadilisha mimi na kunipa mtazamo mpya kabisa katika maisha. Baada ya kuzaliwa Baraka siku kama ya leo mwaka 2012 tuliamua kubadilishana majukumu ya familia; mimi nibaki na kuangalia watoto na kutunza nyumba na mahitaji yake yote na mke wangu aendelee kufanya kazi na kusaidia wakati wowote anaoweza.

Unaanzisha mahusiano ya ndoa/mapenzi?

Picha
MAZUNGUMZO mengi yanayohusu maandalizi ya ndoa hujikita katika kufanikisha tukio la siku ya harusi. Na wakati mwingine wanaojiandaa kwa ndoa huandaliwa siku chache sana kabla ya tukio hilo. Kwa ujumla, suala la ndoa limerahisishwa kiasi cha kuonekana kuwa yeyote anaweza kukabiliana nalo kwa uzoefu pasipo maandalizi ya kutosha. Hata hivyo, pamoja na wepesi wa maandalizi halisi, na msisitizo uliowekwa na jamii katika 'siku ya harusi', ndoa nyingi huishia kwenye migogoro mingi muda mfupi baada ya tukio la harusi.

Kuogopwa kwa wanawake wenye mafanikio na dhana ya kichwa cha familia

Picha
NILIPATA fursa ya kushiriki mjadala mmoja kwenye mtandao wa Facebook leo mchana. Mjadala wenyewe ulianzishwa na Samuel Sasali , ambaye kwa maoni yangu ana uwezo mkubwa wa kuchokoza mada zinazohusu maisha yetu ya kila siku. Hoja iliyokuwa mezani ililetwa kwa njia ya mchoro unaoonesha changamoto anazokabiliana nazo mwanamke anapofanikiwa kielimu. Kwamba kadri mwanamke anavyokwea ngazi ya mafanikio ya kielimu, ndivyo wanaume wanavyozidi kumkimbia.

Muhtasari na Hitimisho, 'Kanuni zinazoongoza mahusiano na migogoro ya wanandoa'

Picha
TANGU tulipoanza mfululizo wa makala za mahusiano , jambo kubwa nililojaribu kulionesha ni nafasi ya mahitaji ya hisia katika kuimarisha au kuvuruga mahusiano. Na msingi wa haya yote ni kusema kwamba mahusiano hayana miujiza. Mahusiano yanaongozwa na kanuni za kawaida sana ambazo ukifanikiwa kuzitambua na kuzitumia utapunguza kama sio kuondoa matatizo mengi. Kwa mhutasari, ningependa tuyapitie mambo makuu yaliyojitokeza katika mjadala wetu kwa kuyaweka katika makala moja inayojitegemea.

Umuhimu wa kutofautiana ili kujenga mahusiano imara

Picha
Kwa wale wafuatiliaji wenzangu wa tamthlia isiyopendwa na wengi, Isidingo the Need, mtakuwa mmeona mgogoro wa kimahusiano kati ya Rajesh Kumar na mkewe Priya. Wawili hawa wamejaliwa mtoto mmoja wa kike, Hiranya, ambaye si mtoto wa kuzaa wa Rajesh. Sasa ikafika mahali mwanaume huyu akatamani kuwa na mtoto ‘wa kumzaa mwenyewe’. Priya hayuko tayari kupata mtoto mwingine. Anadhani   kilicho muhimu kwa sasa ni kumlea mtoto wao na sio kuongeza majukumu ya malezi.

"Ningerudia ujana tena, kipaumbele changu kingekuwa familia!"

Picha
Re-living my life ? " anauliza halafu anajijibu mwenyewe, "Ningebadili mtazamo wa tafsiri ya mafanikio. Mafanikio yangemaanisha ubora wa mahusiano yangu na familia yangu. Hivyo, ningewajibika zaidi kujenga na kuilea familia yangu kwa karibu. Ningetumia muda mwingi na wanangu na mke wangu. Ningepunguza ukali usio  na sababu kwa mke wangu na wanangu. Ningewafanya wanangu wajisikie kuwa na baba anayewaelewa na anayejua mahitaji yao. Ningepatikana zaidi. Ningemfanya mke wangu ajione ni kipaumbele cha maisha yangu.

Chimbuko la wivu na athari zake katika mahusiano

Picha
Umewahi kuhisi unaachwa na mtu unayetarajia kumwoa au kuolewa nae? Umewahi kutamani kuwa na 'access' na simu au barua pepe ya mwenzi wako ili angalau ujisikie kutulia moyoni? Umewahi kujisikia vibaya mwenzi wako akizungumza na mtu mwingine hata kama hukuwa na ujasiri wa kumwambia? Umewahi kumchukia mtu na hata kupambana nae kwa siri au wazi sababu tu umehisi anahatarisha uhusiano wako? Kama lolote kati ya hilo linaelezea hali yako, basi makala haya yanakuhusu.