Jana nilikuwa nikitazama kipindi cha kiislamu kwenye televisheni ya Chaneli 10. Suala la mali katika ndoa za dini hiyo lilikuwa likijadiliwa. Kwamba Kiislam, mali katika ndoa si suala la wanandoa kwa pamoja. Kwamba mali anazoingia nazo mwanandoa kwenye ndoa, zinabaki kuwa zake mwenyewe. Na wakiachana, kila mmoja anaondoka na alichokuja nacho. Hata ndani ya ndoa, mali zinapatikana 'separately' kwa maana ya kwamba kila anachopata mwanandoa hicho ni haki yake yeye mwenyewe. Wakitengana, kila mtu anaondoka na vyake. Katika kufakari hayo, nilijaribu kumfikiria mwanamke na nafasi yake katika ndoa. Nikamwona kama kiumbe anayenyanyaswa na dini. Kwa nini? Wanaume wengi hutafuta mali kwanza ndio waoe, na hata wanapooa, huwaoa wanawake watakaowategemea wao. Katika hali hii nini salama ya mwanamke katika dini inayoruhusu talaka? Hizi si dalili za wazi za ukandamizaji wa jinsia ya kike?
kaka Bwaya, hapa kazi hipo.Darasa kali, kazi kwelikweli
JibuFutaUkweli ndiyo huo,jamii imetufundisha kuukubali uongo ili tujisikie nafuu.
JibuFutaKaka bwaya kuna kitu ninajiuliza ni kwanini tulipokuwa wadogo tuliambiwa kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto ni kukosa adabu?Wanablog naomba msaada wenu?
Kweli kabisa,Ndg Bwaya.Ndio maana baadhi ya watawala wanachotaraji katika hotuba zao ni makofi,vigeregere,shwangwe,vifijo,nderemo,makofi,nk...akizomewa,basi hapo hapakaliki.
JibuFutaTatizo kubwa ni kwamba tukiambiwa ukweli huwa tunakasirika na kuwa wakali, lakini pamoja na hayo mi bado napenda kuambiwa ukweli ila tu uwe kwenye soft language kidogo
JibuFutaYule bwana aliyewahi kusema kuwa dunia hii ina umbo la bapa kama meza alionekana mkweli, lakini yule aliyesema kuwa dunia ina umbo la duara aliswekwa lupango kwa na mfalme kwa kusema uongo.
JibuFutakaka Bwaya leo hii ukisema kuwa njia hii ya kuchagua viongozi wetu kwa kutumia nadharia ya Wagiriki wenyewe wanaita Demokrasia haitufai bali turejee kwenye zile njia zetu za asili za kuwapata viongozi walizotumia mababu zetu utaonekana mwehu na juha.
Habari za hapa Kaka Bwaya.
JibuFutaNimepita hapa kibarazani kwako kujitambulisha kuwa nimefungua kijibaraza changu kitakachokuwa kikijihusisha zaidi na masuala ya vijana.
Nimekuwa nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu, na sasa nimeamua na mimi nijitose uwanjani ili kuongeza mchango katika kuielimisha jamii.
Niko ntayari kuelimishwa na kukosolewa pale nitakapoonekana natoka nje ya mstari.
Natarajia ushirikiano wako.
Digna
Bennet na Digna karibuni sana. Nafurahi kuwapokea kama wadau muhimu wa kibaraza hiki.
JibuFuta