Kizazi chetu kinakabiliwa na magonjwa mengi yasiyoonekana. Tunaumwa, na wakati mwingine taabani, lakini hatujui kuwa tunaumwa. Tunatembea, tunakutana na watu, tunapiga picha zenye nyuso zilizochangamka, tunaonekana kufurahia maisha lakini tunateseka na mahangaiko mengi tusiyoweza kuyasema. Tazama kiwango chetu cha ukatili. Haiwezi kuwa kawaida, kwa mfano, kuona mwenzako anaumizwa na wala hujali. Unamuumiza mtu na bado unashangaa kwa nini analalamika. Unamtesa mwenzako kihisia na bado unamdhihaki anapougulia maumivu. Unajiuliza, tumefikaje mahali mwanadamu unaweza kumtesa mwenzako, ukamsababishia maumivu na hujisikii kujutia. Mbaya, wakati mwingine, kiwango hiki cha ukatili kinakuwa kama nyenzo ya kupata tunachokitaka. Tunataka madaraka, tunataka umaarufu, mali na kila kinachotufanya kujione tunnawazidi wengine. Tunakuwa waraibu wa ukatili dhidi ya binadamu wenzetu na hatujisikii kujutia. Tazama kiwango chetu cha ubinafsi. Kwa nini tumepoteza uwezo wa kuafikiria hisia...
kaka Bwaya, hapa kazi hipo.Darasa kali, kazi kwelikweli
JibuFutaUkweli ndiyo huo,jamii imetufundisha kuukubali uongo ili tujisikie nafuu.
JibuFutaKaka bwaya kuna kitu ninajiuliza ni kwanini tulipokuwa wadogo tuliambiwa kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto ni kukosa adabu?Wanablog naomba msaada wenu?
Kweli kabisa,Ndg Bwaya.Ndio maana baadhi ya watawala wanachotaraji katika hotuba zao ni makofi,vigeregere,shwangwe,vifijo,nderemo,makofi,nk...akizomewa,basi hapo hapakaliki.
JibuFutaTatizo kubwa ni kwamba tukiambiwa ukweli huwa tunakasirika na kuwa wakali, lakini pamoja na hayo mi bado napenda kuambiwa ukweli ila tu uwe kwenye soft language kidogo
JibuFutaYule bwana aliyewahi kusema kuwa dunia hii ina umbo la bapa kama meza alionekana mkweli, lakini yule aliyesema kuwa dunia ina umbo la duara aliswekwa lupango kwa na mfalme kwa kusema uongo.
JibuFutakaka Bwaya leo hii ukisema kuwa njia hii ya kuchagua viongozi wetu kwa kutumia nadharia ya Wagiriki wenyewe wanaita Demokrasia haitufai bali turejee kwenye zile njia zetu za asili za kuwapata viongozi walizotumia mababu zetu utaonekana mwehu na juha.
Habari za hapa Kaka Bwaya.
JibuFutaNimepita hapa kibarazani kwako kujitambulisha kuwa nimefungua kijibaraza changu kitakachokuwa kikijihusisha zaidi na masuala ya vijana.
Nimekuwa nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu, na sasa nimeamua na mimi nijitose uwanjani ili kuongeza mchango katika kuielimisha jamii.
Niko ntayari kuelimishwa na kukosolewa pale nitakapoonekana natoka nje ya mstari.
Natarajia ushirikiano wako.
Digna
Bennet na Digna karibuni sana. Nafurahi kuwapokea kama wadau muhimu wa kibaraza hiki.
JibuFuta