Inasemekana wasomi wanakimbilia siasa. Wanaowaunga mkono wanasema serikali haijali utaalam wao. Inawakejeli kwa malipo kiduchu. Wao, kwa kuona kuwa siasa zinalipa, wanaamua kuzitelekeza fani zao wanakimbilia majimboni kwa lengo la kupata maslahi manono. Inasemwa pia kuwa siasa nayo inawahitaji wataalam kama Maprofesa, Madaktari wa Falsafa na watu kama hao. Kwamba ubobevu wao unatoa mchango mzuri likija suala la maamuzi. Je, ni kweli wanasaidia katika maamuzi? Je, si kweli kwamba kila aina ya ufisadi tunaousikia leo umefanyika mikononi mwa wasomi? Wamesaidia nini? Wanaowapinga, wanasema kuwa elimu yao ilipaswa kujikita katika kuileta jamii maendeleo kupitia fani walizobobea bila kujali serikali inawajali ama la. Kwamba wangejikita vema katika fani zao, ni lazima wangeyapata mafanikio hayo wanayoyafuata katika siasa. Wanasema, kuna ulazima gani wa kila mtu kukimbilia siasa ili kufanikiwa? Je, siasa ndio kila kitu? Je, kukimbilia siasa si dalili ya ufinyu wa elimu yetu? Wanashin...
kaka Bwaya, hapa kazi hipo.Darasa kali, kazi kwelikweli
JibuFutaUkweli ndiyo huo,jamii imetufundisha kuukubali uongo ili tujisikie nafuu.
JibuFutaKaka bwaya kuna kitu ninajiuliza ni kwanini tulipokuwa wadogo tuliambiwa kumpa mtu kitu kwa mkono wa kushoto ni kukosa adabu?Wanablog naomba msaada wenu?
Kweli kabisa,Ndg Bwaya.Ndio maana baadhi ya watawala wanachotaraji katika hotuba zao ni makofi,vigeregere,shwangwe,vifijo,nderemo,makofi,nk...akizomewa,basi hapo hapakaliki.
JibuFutaTatizo kubwa ni kwamba tukiambiwa ukweli huwa tunakasirika na kuwa wakali, lakini pamoja na hayo mi bado napenda kuambiwa ukweli ila tu uwe kwenye soft language kidogo
JibuFutaYule bwana aliyewahi kusema kuwa dunia hii ina umbo la bapa kama meza alionekana mkweli, lakini yule aliyesema kuwa dunia ina umbo la duara aliswekwa lupango kwa na mfalme kwa kusema uongo.
JibuFutakaka Bwaya leo hii ukisema kuwa njia hii ya kuchagua viongozi wetu kwa kutumia nadharia ya Wagiriki wenyewe wanaita Demokrasia haitufai bali turejee kwenye zile njia zetu za asili za kuwapata viongozi walizotumia mababu zetu utaonekana mwehu na juha.
Habari za hapa Kaka Bwaya.
JibuFutaNimepita hapa kibarazani kwako kujitambulisha kuwa nimefungua kijibaraza changu kitakachokuwa kikijihusisha zaidi na masuala ya vijana.
Nimekuwa nimsomaji wa blog yako kwa muda mrefu, na sasa nimeamua na mimi nijitose uwanjani ili kuongeza mchango katika kuielimisha jamii.
Niko ntayari kuelimishwa na kukosolewa pale nitakapoonekana natoka nje ya mstari.
Natarajia ushirikiano wako.
Digna
Bennet na Digna karibuni sana. Nafurahi kuwapokea kama wadau muhimu wa kibaraza hiki.
JibuFuta