Malezi yanavyochochea ubabe katika jamii
Natamani tutafakari jambo hili kwa kina. Nyumbani tumemzoesha mtoto fujo —fimbo, makofi, matusi na aina nyingine za ubabe. Sisi wazazi tunaamini hatuwezi kulinda mamlaka yetu bila kumsababishia mtoto maumivu iwe kwenye mwili wake au hisia zake. Ukiangalia yanayoendelea nyumbani hakuna mazungumzo yenye upendo na mtoto. Tunaamini amani na utulivu kwenye ngazi ya familia ni pale tunapokuwa na watoto wasiofikiri, wasiouliza, wasiothubutu kutofautiana na wazazi ambao ndio mamlaka katika familia. Shuleni mtoto anakutana na mwalimu anayeamini njia pekee na ya uhakika kulinda heshima na mamlaka yake darasani ni vitisho, fimbo na kila aina ya ubabe kwa mwanafunzi. Ukiangalia mbinu za ufundishaji wake huoni wapi anaamini katika ushirikishwaji wa mwanafunzi. Tangu asubuhi mpaka jioni zoezi linalotawala ni wanafunzi kupokea maelekezo na kuyakariri. Mwalimu anaamini nidhamu ni pale amani na utulivu vinapotawala darasani. Hii, huenda ndio sababu shule zinahangaika na wapiga...
Naona chombo cha kuweka vumbi za sigara na mtu maisha yamemshinda
JibuFutabwaya amini usiamini hakuna kitu chochote ambacho kinaweza kufupisha maisha ya bin adamu na hakuna kitu chochote ambacho kinaweza kurefusha maisha ya bin adamu hata kama ni hizo arv wanazotudanganya nazo.
JibuFutakila mmoja wetu awe na starehe anayoipenda.kama mimi natumia sigara,pombe na kufanya zinaa ni maisha yangu kwani hapa sitokuwa nafupisha maisha.
amani kaka.
Sio sigara tu kaka Bwaya, hata vyakula tulavyo hufupisha maisha.
JibuFutawewe kama huvuti sigara halafu unakula hovyo unaweza kutangulia kufa ukamuacha mvuta fegi anatesa duniani.
Hebumuangalie mzee Fedel Castro wa Cuba.
mzee anakula SIGA ila mbaya lakini anaendelea kupeta na maisha, hana wasiwasi.
Du picha nzuri ukicheki vizuri sigara inakuwa mwili wa marehemu umelazwa sakafuni.
JibuFutakwaani nani kasema kufa ni kubaya? mnaogopa au kuchukia kufa? kama ni kweli basi mnajichukia wenyewe
JibuFutaKamala kumbe ile elimu ya milo uliyokuwa unatupa ni ili kuharakisha kifo eh?
JibuFutandio
JibuFutaBasi ungefafanua ili wasomaji wako waamue kabla ya kuutumia ushauri wako. Baadhi yetu tulifikiri tofauti. Kwamba elimu ya kula ingesaidia kurefusha maisha.
JibuFutaMimi huwa nafurahi sana napokutana na comments nyingi za Kalama, unakuta ni fupi ila ujumbe ni mzito mno.Nakuaminia brother.
JibuFutaHiyo picha kusema kweli inaonesha kama mtu flani....da kweli hiyo taswira Bwaya.
Thanks Bwaya kwa pic hiyo
MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
Nani asiejua kama sigara ni mbaya na inauua pole pole lakini waswahili wanalonga kua kufa kufaana, yetu macho tu.
JibuFuta