Malezi yanavyochochea ubabe katika jamii
Natamani tutafakari jambo hili kwa kina. Nyumbani tumemzoesha mtoto fujo —fimbo, makofi, matusi na aina nyingine za ubabe. Sisi wazazi tunaamini hatuwezi kulinda mamlaka yetu bila kumsababishia mtoto maumivu iwe kwenye mwili wake au hisia zake. Ukiangalia yanayoendelea nyumbani hakuna mazungumzo yenye upendo na mtoto. Tunaamini amani na utulivu kwenye ngazi ya familia ni pale tunapokuwa na watoto wasiofikiri, wasiouliza, wasiothubutu kutofautiana na wazazi ambao ndio mamlaka katika familia. Shuleni mtoto anakutana na mwalimu anayeamini njia pekee na ya uhakika kulinda heshima na mamlaka yake darasani ni vitisho, fimbo na kila aina ya ubabe kwa mwanafunzi. Ukiangalia mbinu za ufundishaji wake huoni wapi anaamini katika ushirikishwaji wa mwanafunzi. Tangu asubuhi mpaka jioni zoezi linalotawala ni wanafunzi kupokea maelekezo na kuyakariri. Mwalimu anaamini nidhamu ni pale amani na utulivu vinapotawala darasani. Hii, huenda ndio sababu shule zinahangaika na wapiga...
Ntakitafuta hicho Mkuu!
JibuFutaIla MKUU una ukimya fulani siku hizi MKUU!
Just sayin'.....!
Ni kweli mtakatifu Kitururu. Kuna mambo hayajakaa sawa bado.
JibuFutaElimu ya watanzania iliwafanya wananchi wachukie vitabu sababu toka shule za misingi hadi vyuo vikuu vitabu vinaelezea matukio ya ukoloni, historia zisizokuwa na mizizi ya mtu kuwa mbunifu na mfumo mbovu wa hatima ya elimu kuwa mwenye akili ni yule anayefaulu mtihani wa mwisho.
JibuFutaChachu ya kusoma vitabu ijengwe kutoka mashuleni, watu wanaona bora atembee mtaani kuuza mitumba ya CD/DVD apate riziki kuliko kusoma vitabu mwisho wa siku alale njaa.
NAKUKARIBISHA HUKU PIA, http://www.amosmsengi.blogspot.com/
Kaka habari za siku, naona hata namba zako za simu hasa TIGO haipatikani........
JibuFutaKuhusu kitabu, ni kweli kinaonekana ni kizuri, lakini naomba wakati mwingine uwe unatuelekeza vinapopatikana vitabu hivyo..... ni wazo tu mkuu
Pamoja daima
Amos asante sana kwa maoni yako murua. Karibu kwenye uwanja wa kublogu.
JibuFutaKoero, asante kwa wazo zuri.