Kitabu Kipya cha Malezi na Makuzi



Malezi ya sasa yamekumbwa na changamoto nyingi na kusababisha watu kushindwa kuwasaidia watoto na vijana wao ili kufanikiwa. Mmomonyoko wa maadili umekuwa chanzo kikubwa cha matatizo yanayomkumba kijana na jamii kwa ujumla. Matatizo hayo ni kama vile ukosefu wa ajira, kushindwa kufikia ndoto za maisha, migogoro katika familia, pamoja na watu kushindwa kuwa na utulivu na amani.

Kwa bahati mbaya, masuala haya hayajapewa nafasi katika mijadala yetu. Na hata pale yanapojadiliwa, uchambuzi wake umekuwa wa kijuu juu usiojaribu kutazama kiini cha matatizo. Kadhalika, pamekuwa na uhaba wa maandishi yanayoweza kuchochea mijadala inayolenga kutafuta ufumbuzi wa masuala haya mazito.

Mwalimu Joseph Chikaka ameandika kitabu kinachoitwa “Watoto na Ndoto za Maisha.” Katika kitabu hiki, mwandishi anachambua kwa kina malezi na makuzi ya mtoto yanayosababisha tupate vijana, familia zilizo imara, na hatimaye, taifa lenye furaha. Anakupa mbinu na ushauri wa kimalezi na kimakuzi zitazokuwezesha kupata jamii bora yenye usawazo kiroho, kiakili (kimtazamo), kimwili (afya) na kijamii (mahusiano).

Pia, kitabu hiki kinatoa mbinu na ushauri wa masuala ya msingi ya mzazi, mlezi na mwalimu ya kuzingatia; ili kumsaidia mtoto, kijana na mtu yeyote kuweza kutimiza ndoto zake. Jinsi gani mtu anaweza kutimiza ndoto zake kupitia watu wengine, jinsi gani anadumu ama kupotea kwa njia ya kuelekea katika ndoto.

Mwandishi anachambua kwa kina, jinsi ambavyo watoto huzaliwa na kukua kwenye familia nyingi wakiwa na ndoto nyingi katika maisha yao ya baadae. Ndoto hizo huweza kutimizwa au kushindwa kutokana na jinsi gani wazazi, walezi na serikali zinaweza kusaidia. Aghalabu, wanakuwa na ndoto za kuwa wahandisi, wasanii, walimu, kasisi/ mchungaji, wanasiasa, madaktari, wakulima wa kisasa au kuwa fundi sanifu.

Kwa bahati mbaya, ndoto hizi hazitimii watu wanapofikia umri wa ujana na utu uzima. Sababu kubwa ni changamoto za maisha na ukosefu wa malezi na makuzi bora; ambazo mwandishi ametoa suluhu yake kwa kina.
Vile vile, amethibitisha kwamba, mafanikio ya mtu hayaji kwa bahati mbaya, bali huandaliwa; na mafanikio ya kijana wa leo ni matokeo ya malezi na makuzi ya utotoni.

Mwandishi ni mwalimu mwandamizi katika shule ya Awali na Msingi ya Ignatius, Dodoma. Pia, amefundisha shule mbalimbali hapa nchini. Ni mbobezi katika uandishi wa vitabu, makala, ujasiriamali, unasihi na saikolojia. Pia, ni mtaalamu wa kuendesha mafunzo, semina, kongamano na matamasha ya kitaaluma, michezo na stadi za maisha.


Kitabu hiki kinapatikana kwenye duka la vitabu lililo karibu nawe kwa bei nafuu ya Tsh 15,000. Pia, unaweza kupiga simu namba 0755 423 258, 0658 423 258 kwa mawasiliano zaidi.

Maoni

Zilisomwa zaidi wiki hii...

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Maana ya Saikolojia na Nafasi Yake Katika Jamii -1

Haiba ni nini?

Pay $900? I quit blogging

Heri ya mwezi mpya!