Naam. Idadi ya wanablogu inaongezeka. Na kila mwanablogu anakuja na mtazamao mpya. Hebu mtembelee Koero uone. Kama utakavyoona, ujio wa watu kama hawa ni wa muhimu sana. Karibu sana Koero tujadiliane.
Labda naweza kuwa nakosea, lakini nadhani ile dhana kuwa hatupendi kufikiria inaanza kuondoka polepole. Labda sasa ni kwamba hatupendi kuchangia fikra zetu lakini nalo litaondoka. Ule mtazamo wa kila mwenye blog aje na picha sasa unaanza kupoteza ukweli na sasa watu wanaanza kufikirisha wasomaji zaidi. Lakini pia twahitaji taswira kwa hiyo wenye kufikirisha kama Koero karibuni saaana na wenye taswira pia mwakaribishwa maana mwatusaidia "kusindikiza" tafakuri zetu. Karibu Koero na wenye nia ya hivyo
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.
Umewahi kujiuliza kwa nini, wakati mwingine, mtu mwenye akili nzuri, mwenye weledi na uelewa mpana wa mambo, hujikuta na majanga mengi linapokuja suala la namna anavyoishi na watu? Shida ni nini? Iweje mtu aelewe mambo mengine vizuri lakini asindwe mambo madogo kama kuwa msikivu, mvumilivu wa mawazo tofauti, mwenye subira hali inayoweza kumuingiza kwenye magomvi na watu? Kinyume na tunavyoamini wengi wetu, hisia hubeba maamuzi yetu mengi na ukitazama matatizo yetu mengi ya kitabia unaweza kuona mchango mkubwa wa kushindwa kuzielewa na kuzimudu hisia zetu. Ingawa tunazipuuza, ukweli ni kwamba ukishashindwa kuzishughulikia hisia zako, uwezekano wa kukabiliana na matatizo mengi ya kimtazamo, kimaamuzi na kitabia unakuwa mkubwa. Hapa ninakuletea, japo kwa mukhtasari, elimu ya hisia, UmahiriHisia (UH) — emotional intelligence — ambao kimsingi ni uwezo kuelewa namna hisia zetu zinavyofanya kazi, kuzitambua kadri zinavyoitokeza, kuelewa nini kinazichochea, kuzirekeb...
YAMEKUWEPO madai kwamba Uislam ulianza tangu kuumbwa kwa dunia. Na wapo watu wanaotuaminisha hayo. Ukweli ni kwamba Uislam ulianzishwa na Nabii Muhammad mwaka 622 BK huko Arabia. Kabla yake, dini zilizokuwepo zilikuwa ni Uyuda ambayo ni dini rasmi ya Wayahudi (Judaism) na Ukristo ambayo ni dini ya mataifa wasio Wayahudi ulioanza miaka kadhaa baada ya Yesu kuwa ameondoka mwaka 33BK. Yesu mwenyewe hakuanzisha Ukristo. Alisali katika misikiti ya Wayahudi. Masinagogi. Maelezo haya yana msingi wa kistoria na sio propaganda za kidini. Ndio ni propaganda kwa sababu dini zote zimekuwa na tabia ya kuonyesha kwamba zenyewe ndizo za kweli kuliko dini nyinginezo hata ikibidi kwa kuichezea historia. Na ni bahati mbaya kwamba Dini zimekuwa na tabia ya kufanana ya kuzima uwezo wa waumini wake kuhoji lolote kwa kuwajengea hofu ya kujitafutia laana. Qur’an inatupa maelezo yanayokinzana kuhusu lini hasa Uislamu ulianza. Baadhi ya mistari katika kitabu hicho zinadai kwamba ‘nabii’ Muhammad ndiye ...
Sipendi kutumia kiingereza kwa sababu kwanza ninadhani kiswahili kinanitosha kabisa kuelezea kile ninachotaka kusema. Hata hivyo najua pia matumizi ya kiswahili chetu hayajawa katika kiwango kile kilichokusudiwa. Kuna maneno mengi yasiyoeleweka vizuri katika kiswahili cha kitabuni. Moja wapo ya maneno hayo ni hili ninalolitumia leo hii. Haiba. Pengine niweke msisitizo kwa faida ya wale wasiolifahamu neno hili vizuri. Personality. Wengine wanasema maana ya hichi kinachoitwa personality ni utu kwa kiswahili. Ni bahati mbaya kwamba niliyakimbia masomo ya lugha siku nyingi. Ila nimejiridhisha kwamba haiba ndiyo tafsiri muafaka kabisa. Haiba ni nini? Watu wengine watafikiria tunazungumzia mwonekano wa mtu kimavazi. Lakini haiba ni neno pana zaidi ya mwonekano wa mtu kwa nje. Haiba ni jumla ya tabia za mtu zinazotokana na kile anachofikiri, anachopenda, anavyojichukulia yeye mwenyewe, anavyowachukulia watu wengine na kadhalika. Haya yote hujenga mwonekano wa mtu unaopimika (tabia) kama vi...
Tunaendelea na elimu ya hisia. Katika makala yaliyopita , tumejifuza msamiati wa hisia. Mbali na kutofautisha mihemuko na hisia, tumedadisi namna hisia, katika ujumla wake, zinavyobeba ujumbe. Kila hisia huja na ujumbe fulani. Umahirihisia ukuwezesha kutafakari ujumbe unaobebwa na hisia zako. Katika makala haya, ningependa tutafakari kwa pamoja namna ya kuzikebu na kuzimudu hisia zetu. Nianze na swali. Unakumbuka mazingira umewahi kujikuta ukifanya maamuzi mabaya kwa sababu hujipa muda wa kupooza hisia zako? Unakumbuka kusema jambo ukiwa na hasira, kwa mfano, halafu baadae ukajutia? Unamwandikia mpenzi wako maneno makali shauri ya hisia za wivu lakini baadae ukishapoa unagundua hukuwa na sababu ya kusema ulichokisema? Napenda nukuu moja ya mama anayeitwa Maya Angelou, “Watu wanaweza kusahau ulichokifanya. Watu wanaweza kusahau ulichokisema. Lakini watu hawawezi kusahau ulivyowafanya wakajisikia .” Unaweza kuona uzito wa hisia katika kumbuk...
Tunamalizia safari yetu ya kujifunza umahirihisia. Tumeangazia maeneo makubwa manne. Kwanza, uelewa wa hisia na sababu zake. Pili, tulitazama namna ya kurekebu hisia zetu . Kisha tukatazama namna tunavyoweza kujenga motisha na hamasa ya kufikia malengo yetu . Kisha tukaangalia namna umahirihisia unavyotuwezesha kuwasiliana na watu pasipokuzalisha migogoro isiyo na sababu. Maeneo haya manne ya umahirihisia, yanatafsirika katika mahusiano yetu na watu —namna tunavyowachukulia wasioamini tunachokiamini, namna tunavyowajibu wasiofikiri kile tunachokifikiri, namna tunavyotatua migogoro na maamuzi tunayochukua pale tunapojisikia kuonewa. Msingi wa mahusiano yenye tija na watu ni uwezo wako wa kujitambua, kutambua namna hisia na tabia zako zinavyoathiri wengine, namna unavyomudu hisia zako lakini pia kiwango chako cha upendo kwa watu. Mtu mwenye #UmahiriHisia hagombani kirahisi. Ukigombana naye anajua namna ya kujinasua na kukuachia ugomvi wako...
Katika utangulizi wetu , nilieleza maana ya umahirihisia na nyanja zake tano. Nilieleza kuwa, ingawa umahirihisia una nyanja hizo tano, ukiyatazama vyema mawanda yake, unaona kuna maeneo makubwa mawili. Eneo la kwanza, ni utambuzi kwa maana ya kuelewa hisia zako, kuzifuatilia na kuzirekebu kwa maana ya kujifunza namna ya kuzimudu zisikuingize kwenye matatizo. Eneo la pili linategemea eneo la kwanza, kwa maana ya uwezo wa kutumia utambuzi huo wa hisia kuelewa namna ya kuelewa, kutambua na kuheshimu hisia za wengine kwa minajili ya kuboresha mahusiano yako na watu. Katika sehemu hii ya pili, ninajielekeza kueleza kwa ufupi jinsi gani umahirihisia unaweza kukuzaidia kuzielewa na kuzirekebu hisia zako. Umewahi kukutana na mtu mwenye uwezo mzuri wa kusoma ujumbe unaobebwa na uso wa mtu? Ukitabasamu, mwingine anaishia kwenye uso huo wenye tabasamu lakini yeye ana uwezo wa kujua kuwa pamoja na tabasamu lako, kuna kitu hakiko sawa. Unashangaa pamoja na k...
Haswa! Koero kaja kakamilika. Tunakukaribisha kwa mikono yote. Kazi yako ni nzuri sana.
JibuFutaLabda naweza kuwa nakosea, lakini nadhani ile dhana kuwa hatupendi kufikiria inaanza kuondoka polepole. Labda sasa ni kwamba hatupendi kuchangia fikra zetu lakini nalo litaondoka. Ule mtazamo wa kila mwenye blog aje na picha sasa unaanza kupoteza ukweli na sasa watu wanaanza kufikirisha wasomaji zaidi. Lakini pia twahitaji taswira kwa hiyo wenye kufikirisha kama Koero karibuni saaana na wenye taswira pia mwakaribishwa maana mwatusaidia "kusindikiza" tafakuri zetu.
JibuFutaKaribu Koero na wenye nia ya hivyo
waama kweli kabisa
JibuFuta