Imani, Mitazamo na Tabia │ Malezi na Makuzi │ Mahusiano na Ndoa │ Kazi na Ajira │ Elimu na Tafiti
Mkaribishe Koero
Pata kiungo
Facebook
Twitter
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
Naam. Idadi ya wanablogu inaongezeka. Na kila mwanablogu anakuja na mtazamao mpya. Hebu mtembelee Koero uone. Kama utakavyoona, ujio wa watu kama hawa ni wa muhimu sana. Karibu sana Koero tujadiliane.
Labda naweza kuwa nakosea, lakini nadhani ile dhana kuwa hatupendi kufikiria inaanza kuondoka polepole. Labda sasa ni kwamba hatupendi kuchangia fikra zetu lakini nalo litaondoka. Ule mtazamo wa kila mwenye blog aje na picha sasa unaanza kupoteza ukweli na sasa watu wanaanza kufikirisha wasomaji zaidi. Lakini pia twahitaji taswira kwa hiyo wenye kufikirisha kama Koero karibuni saaana na wenye taswira pia mwakaribishwa maana mwatusaidia "kusindikiza" tafakuri zetu. Karibu Koero na wenye nia ya hivyo
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.
SAIKOLOJIA, neno lililotoholewa kutoka neno la kiingereza psychology, si elimu inayoeleweka sana katika jamii yetu. Asili ya 'psychology' ni neno 'psyche' lenye maana ya nafsi. Katika makala haya, tunasaili kwa ufupi maana ya saikolojia kama taaluma na kuonesha nafasi ya taaluma hiyo ngeni katika jamii yetu katika kutatua matatizo ya kijamii na hivyo kuharakisha juhudi za watu kujiletea maendeleo yetu.
Kama tulivyoona katika makala yajuma lililopita , usaili ni hatua ya mwisho kuelekea kupata kazi. Sehemu kubwa ya usaili ni maswali na majibu yanayolenga kupima uwezo wako wa kukabiliana na changamoto halisi za kazi. Ingawa yapo maswali yanayoweza kukupa wasiwasi wa nia ya mwuulizaji, fahamu kuwa hakuna swali linaulizwa kwa nia mbaya au kwa bahati mbaya. Kila swali linaloulizwa linalenga kutafuta uthibitisho kuwa wewe ni mtu sahihi kwa kazi unayoomba.
Katika makala haya, tunatazama kwa ufupi makuzi ya mtoto mwenye umri wa siku moja mpaka miezi 36. Tutaangalia mambo ya msingi yanayonesha ukuaji wa mtoto unavyoendelea katika maeneo makubwa manne; 1) ukuaji wa kimwili 2) kiakili 3) kimahusino na watu wengine na mwisho 4) kihisia. Kwa kawaida maeneo haya manne yanategemeana ili kumwezesha mtoto kukua kwa ujumla. Kwa mfano ili mtoto akue kimwili, anahitaji ukuaji wa akili ipasavyo ambayo nayo itaathiri namna anavyomudu hisia zake na hivyo kuhusiana na watu wengine. Kwa hiyo ni sawa tukisema hakuna ukuaji wa eneo moja usiotegemea eneo jingine.
Barua ya kuomba kazi ni waraka ambao mara nyingi husomwa kabla ya waraka mwingine wowote unaoambatanishwa katika kuomba kazi. Ni vyema barua ya kuomba kazi ikaandaliwa kwa umakini, na kujaribu kugusa kwa ufupi mambo yaliyoonekana kwenye wasifu binafsi kumvutia mwajiri mtarajiwa.
Global Voices Citizen Media Summit in Cebu, The Philippines in 2015. Photo Courtesy of Global Voices I started my blog in 2005. I was among very few Tanzanians who were inspired by Ndesanjo Macha to start blogging. For those of you who do not know, the history of Tanzanian blogosphere recognizes the contribution of this great man. His influential weekly column in a local newspaper invited many of us to his blog. In fact he was the first Tanzanian to blog in Kiswahili . That was in 2004. I had the privilege of meeting him in Nairobi, Kenya in 2012 and in Cebu, The Philippines in 2015. We were both attending Global Voices Citizen Media Summits. For me, blogging was fun. I never thought that blogs could actually threaten politicians. That was until 2010 when I had an opportunity to attend the Global Voices Citizen Media Summit in Santiago de Chile. I was shocked to hear friends talking about restriction of freedom of speec
Kwa sasa sipatikaniki vya kutosha kwa sababu ambayo nitaieleza hapa chini kwa maneno matano. Kwa wale wanaopenda chemsha bongo mnaweza kujaribu na kisha kuweka majibu kwenye kisanduku cha maoni ama kuniandikia kupitia sanduku la barua pepe: Meelekezo: Hizi ni herufi zilizofichwa (codes) ambazo ili kukupa ujumbe, inakubidi kugundua kanuni iliyotumika kuziandika ili kupata maneno matano ya kiswahili fasaha. OJUBLVXB OB OJUIBOJ KVNB MJKBMP! Chemsha ubongo kidogo ndugu msomaji.
Haswa! Koero kaja kakamilika. Tunakukaribisha kwa mikono yote. Kazi yako ni nzuri sana.
JibuFutaLabda naweza kuwa nakosea, lakini nadhani ile dhana kuwa hatupendi kufikiria inaanza kuondoka polepole. Labda sasa ni kwamba hatupendi kuchangia fikra zetu lakini nalo litaondoka. Ule mtazamo wa kila mwenye blog aje na picha sasa unaanza kupoteza ukweli na sasa watu wanaanza kufikirisha wasomaji zaidi. Lakini pia twahitaji taswira kwa hiyo wenye kufikirisha kama Koero karibuni saaana na wenye taswira pia mwakaribishwa maana mwatusaidia "kusindikiza" tafakuri zetu.
JibuFutaKaribu Koero na wenye nia ya hivyo
waama kweli kabisa
JibuFuta