Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2007

Unahusianaje na nafsi yako?

Huwa unajisikiaje ukijitazama kwenye kioo? Unaridhika na sura unayoiona? Vipi ukiangalia picha zako za hivi karibuni? Unaridhika na ulivyo? Umbo lako? Mtindo wa nywele zako? Rangi ya ngozi yako? Unajionaje? Watu wengi tunapata shida sana kujikubali. Hatujipendi. Kila tunapojitazama, tunaona kasoro. Wachache wetu huziona kasoro hizo kama vitu vidogo visivyotupa tabu sana. Mtu aweza kujiangalia kwenye kioo, akaona kasoro ndogo, lakini akajipa moyo: "Ngoja nichane, nitapendeza". " Ngoja niende saluni, nikabadili mtindo". Akaziona kasoro na zisimsumbue. Lakini wengi wetu huvunjika moyo kwa kudhani/amini kuwa kasoro hizo hazirekebishiki. Pengine rangi ya ngozi si nyeupe vya kutosha. Ama umbo letu halivutii, na mambo kama hayo. Kuvunjika moyo kwa namna hiyo, husababisha kujengeka kwa hisia hasi kuhusu nafsi ya mtu mwenyewe. Jambo moja kabla hatujaendelea: Mahusiano mema na nafsi zetu hutokana na vile tujichukuliavyo. Mahusiano mabaya na nafsi zetu husababisha kujidh

Sherehe bila mwenye sherehe, inawezekanaje?

Picha
Umewahi kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa mtu fulani bila ridhaa yake? Au unaigeuza kabisa inakuwa sio kumsherehekea yeye, ila kufanya utakayo, kwa mwamvuli wa kumsherehekea yeye! Kama ingekuwa ni wewe ndiye mwenye sherehe, ungejisikiaje? Watu wala, wanywa, hata kadi ya mwaliko hawakupi. Na bado wanadai wanakumbuka kuzaliwa kwako. Kweli? Hivi ingekuwa wewe ungejisikiaje?

Tofautisha dini yako na utamaduni wa "wenye dini"

Wakati umefika wa kuchukua juhudi binafsi za kutenganisha dini na utamaduni wetu kama vitu viwili tofauti. Tuweze kupambanua mambo ambayo ni ya kidini na yale ya utamaduni wa nje, ambayo kwa kujua ama kutokujua tunadhani kwa kuyafanya maana yake tunashika dini. Kuvaa kanzu na baibui si utamaduni wetu. Kuitwa Mathayo hakuhalalishi ukristo wako. Kukaa chini katika ibada, wakati kuna uwezekano wa kupata viti, ni kujaribu kuwaiga wenye dini na mazingira yao. Na bahati mbaya twayafanya hayo tukiamini kuwa tunashika dini kumbe ni ulevi tu wa utamaduni wa watu fulani fulani. Tujielewe.

Tusitegemee uzalendo kwa elimu hii

Kati ya mambo ambayo wana wa Kitanzania wanayakosa katika vyumba vyao madarasa, ni elimu ya kujielewa. Elimu ya kuwafanya waelewe nafsi zao wenyewe. Elimu ya kuwapandikizia falsafa za taifa lao wenyewe. Elimu ya kuwakomboa kimtazamo, wajue umuhimu wa utamaduni wao. Elimu ya kuwafanya waelewe wajibu wao katika kuufufua utamaduni huo ndani yao wenyewe na katika watu wao. Wenye kufundisha, hawajui nchi inayofalsafa gani. Nchi yenyewe haieleweki inayo falsafa ipi. Mitaala nayo haifahamiki imetayarishwa kwa shinikizo la nani na nani atapanda dau lini kuibadilisha. Na matokeo yake ni kwamba kila kijana "huhitimu" na falsafa yake anayoijua yeye na huelekea anakokujua mwenyewe. Kila jambo linakuwa shaghalabagala! Ndani ya mfumo kama huu, haitokaa iwezekane kuwa na Tanzania yenye dira inayoeleweka. Haitokaa itokee kuwa na Tanzania iliyojipembua kwa utamaduni wake. Haitokaa itokee tuwe na Tanzania yenye wazalendo waliotayari kuitetea raslimali za nchi yao kwa dhati ya mioyo. Haitokaa i

Je, umewahi kuiadhibu nafsi yako mwenyewe?

Wajibu ni nini? Haki ni nini? Je, waweza kudai haki fulani fulani kutoka katika nafsi yako mwenyewe? Je, waweza kujiadhibu wewe mwenyewe kwa kutokutimiza wajibu fulani? Je, ni sahihi kudai haki (zako) kutoka kwa wengine, wakati (wewe mwenyewe) hujitendei haki? Tujielewe.

Unapojielewa nini huwa kimetokea?

Kujielewa. Tunasisitiza sana kujielewa. Lakini je, kujielewa maana yake nini? Unapoelewa jambo nini hasa huwa kimetokea katika ufahamu wako? Je, kuna tofauti gani iliyopo unapolinganisha kabla hujaelewa na baada ya kuelewa jambo? Je, twaweza kuelewa na/au kujua kila kitu? Je, upo ukomo (limit) wa uelewa?

Ukweli ni lazima uwe uhalisi?

Uhalisi (reality) ni nini , na unatofautianaje na ukweli (truth)? Je, uhalisi lazima uwe ukweli? Je, kila ukweli ni halisi? Je, utajuaje kuwa unachojua ni uhalisi usio ukweli ama ukweli usio uhalisi?

Akili hutengenezwa!

Huwezi kufikiri jambo ambalo halipo ubongoni. Haiwezekani. Kufikiria ni kupekua mafaili. Kama mafaili yenyewe hayapo, huna cha kutafuta. Ubongo wa mtoto ni kama ofisi mpya ambayo mamlaka ya kuifanya upendavyo yako mikononi mwako. Unaingiza fanicha uzipendazo, kwa kadiri ya mahitaji ya Ofisi yako hiyo. Unapanga makarabrasha yako kwa utaratibu uupendao mwenyewe. Sababu wewe ndio ofisi. Na unapohitaji sasa kuyatumia makrabrasha hayo, uchaguzi wako utakuwa “katika” yale yale uliyoyihifadhi awali. Pamoja na mapungufu ya mfano huu, bado unaweza kutumika kuelezea hali halisi. Huwezi kutafuta kitu ambacho ni wazi hukukiweka. Au labda tuseme, ubongo wa binadamu ni sawa kompyuta tupu isiyoweza kufanya chochote mpaka mmiliki apandishe (install) programu azipendazo mwenyewe. Na uchaguzi wa kipi akifanyie kazi kwenye kompyuta yake unategemea na yaliyomo. Watafiti wengi wanakubaliana kuwa kila mtoto huzaliwa na ubongo safi. Wenye uwezo safi. Wenye nguvu (potential) ya kuwa chochote. Pamoja na tofaut

Mkono wa Mama

Picha
Enzi za ujana wangu, mwanzoni mwa miaka ya elfu mbili, nikiwa mwanafunzi wa "shule za manerumango" nilipoukamata mkono wa mama Migiro mbele ya Pro.Mmuya. Nilikuwa nimeshinda shindano la nsha. Hapa nakabidhiwa "karatasi" la ushahidi kama ilivyo kawaida ya waswahili, kwamba kila kitu lazima kifuatane na cheti. Nimeiweka picha hii kukukumbuka siku nilipozaliwa. Sina hakika kama ndiyo yenyewe, manake naonekana mzee mzee.

Hivi mtoto huwaza kama mtu mzima?

Picha
Kama umewahi kujiuliza swali kama hilo, tafadhali karibu tuchangie mawazo. Mtoto huwaza nini? Mtoto hufikiri nini na kwa upana gani? Katika mambo yanayofurahisha sana katika akili ya binadamu, ni vile ubongo wake unavyoweza kutengeneza mtandao wa kuhusianisha "tukio" moja na lingine, na hivyo kuleta mtiririko wa matukio unaoweza kujulikana kama mawazo. Unapowaza maana yake ni kwamba ubongo wako unao uwezo wa kuunganisha vipande vingi vya matukio (schema) kwa kadiri yanavyohusiana, na hivyo kuleta mtiririko fulani, unaleta mlolongo wa uhusiano wa aina fulani. Inakuwa kama ile mikanda ya sinema yenye picha nyingi zisizotembea zenye mtitiriko wa matendo yanayokaribiana ambayo huunganishwa na kuleta mtiririko unaotembea. Mawazo hapa yakimaanisha mtiririko wa vipande vya habari katika ubongo wa binadamu. Ikiwa ubongo utashindwa kufanya hivyo, kwa maana ya kukosekana kwa mwendelezo wa vipande hivyo, kamwe mwenye ubongo huo hawezi kuwaza jambo. Sababu ni kwamba kati ya kipande kimoj

UKIMWI una tiba kumbe?

Picha
Sikuandika siku kadhaa zilizopita, kipingamizi kikiwa ni uvamizi wa kirusi. Nafurahi kwamba "tabibu" alipatikana, na tiba sahihi ilifanyika, UKIMWI ukasalimu amri. Shukrani za pekee zimwendee Bwana Minja, msomaji wa blogu (yeye anadai inatosha kuzisoma) na fundi mwanafunzi katika sayansi ya kompyuta. Kwa hakika tunawahitaji sana watu kama hawa katika jamii zetu, watusaidie "kugawana" umasikini wetu. Minja. Minja kaozea katika teknolojia. Minja. Minja na spana. Minja. Ukienda kwa Minja hutathubutu kuongea siasa. Si tu kwamba hatakusiliza, lakini pia mazingira hayatakuruhusu. Bush kafanyeje, wala hajui na hataki kujua. Ongea teknolojia. Ndugu yangu utakoma. Huo ndio mgawanyo wa kazi unaotutofautisha wenyewe kwa wenyewe. Ndugu Minja nakushukuru sana. Nitajaribu kuchukua hatua za dharura, tatizo lisijirudie. Wanasema tubadili tabia ili kuepuka gonjwa lile. Basi huenda tabia yangu ya kunyonya blogu mtandaoni na kuzihamishia kwenye kimeo changu inaniponza. Muhimu, niwe

Hitilafu ndogo

Kutokana na sababu ambazo ni za wazi, ili kublogu huwa natumia tarakilishi-paja kuandikia na kisha kuja mtandaoni kupesti maandiko yangu. Kufanya hivyo hunipunguzia gharama za muda wa kukaa mtandaoni ambao kwa nchi tajiri kama yetu, unagharimu sana. Kwa bahati mbaya sana, tarakilishi hiyo imepata UKIMWI siku kadhaa zilizopita! Kuna kirusi kaivamia na ananizuia kufanya chochote. Jitihada za kumtafuta daktari wake zinaendelea.

Kuwa halisi, ufe halisi

Kila binadamu anazaliwa halisi/origino. Uwezo halisi. Akili halisi. Mtazamo halisi. Maono halisi. Sura halisi. Machache kwa kutaja. Uhalisi huu una maana ya kuwa na uwezo wa kipekee katika uasili wake ili kutimiza jukumu halisi na la kipekee katika jamii. Bahati mbaya idadi kubwa ya wanadamu hawa waliozaliwa origino, wanakufa wakiwa "fotokopi" za watu fulani. Wanaiga kila kitu. Mtizamo bandia. Fikra bandia. Akili bandia. Uwezo bandia. Sura bandia. kazi bandia. Na kadhalika. Bandia hapa ina maana ya kuwa ama kujaribu kuwa mtu mwingine tofauti na yule halisi aliyezaliwa akiwa wewe. Bandia ina maana ya kutafuta kufanya jambo lisilo lako. Kuiga. Kupoteza muda kufanya kitu ambacho si halisi yako. Vipi, u halisi wewe? Au umekuwa fotokopi ndugu yangu? Rudi kwenye mstari utafute uhalisi wako. Hapo utakuwa umejielewa.

Tubadilishe mfumo wa kufikiri

Hivi ingekuwaje kama tungeweza kuutumia ubongo wetu walau kwa asilimia chache za uwezo wake halisi? Hivi ingekuwaje kama kila Mtanzania angeamua kuacha uvivu na kuzifanyia kazi baadhi tu ya seli mabilioni zinazounda ubongo wake? Tungebaki hapa tulipo? Nina mashaka iwapo kila raia wa nchi hii anajisumbua kujua matumizi sahihi ya ufahamu wake. Kila raia naamini anayo akili nzuri ambayo kama ikitumiwa kwa kiwango kizuri lazima isababishe mabadiliko ya aina fulani. Na tunapozungumzia akili nzuri, haturejei kwa wale wachache waliobahatika kuyakanyaga madarasa. Kama hivyo ndivyo, kwa nini tunaendelea kurudi nyuma kwa kasi mpya? Kwa nini tuna mazoea mabovu ya kulalamikia mambo ambayo wakati mwingine ni sisi wenyewe tumeyasababisha? Hivi kweli tunatumia akili zetu ipasavyo? Sababu imekuwa kawaida kusikia malalamiko. Watu tunajua kulalamika. Na kulalamika maana yake ni jitihada za kukwepa majukumu kwa kuwatupia wengine mzigo ambao kimsingi ni wa kwako. Kulalamika ni kule kushindwa kukubali ud

Acha woga, zaa mawazo

Leo naamkia uzazi. Uzazi wa mawazo. Mawazo. Mawazo. Upo umuhimu mkubwa sana wa sisi kama binadamu kujielewa. Kujielewa kutatusaidia kutatua matatizo yetu mengi. Matatizo ya kiutamaduni. Kisiasa. Kijamii. Na kadhalika. Kulielewa ni muhimu sana. Kujielewa ninakokuzungumza hapa ni kule kufahamu kuwa ndani mwako yapo mawazo ambayo usipoyagundua yatakufa na wewe. Wewe unayo mawazo muhimu sana kwa ajili ya maendeleo ya watu wanaokuzunguka. Bahati mbaya ni kwamba mawazo hayo yanakusubiri wewe uache woga. Useme. Ueleweke unawaza nini. Mengi ya matatizo yetu hayako huko tunakodhani. Si unajua mara zote huwa hatupendi kuwajikia matatizo? Chanzo cha matatizo yetu kiko katika fahamu zetu wenyewe. Lakini ajabu ni kwamba watu wengi tunajua sana kuzungumzia udhaifu wa wengine. Tunajua kuchambua hoja za wengine. Tunajua kupuuza vya wengine. Tunajua kulalamika. Kusononeka. Lakini kumbe kufanya hivyo hakuwezi kuleta mabadiliko ya kweli. Hivi sasa wananchi wanalalama. Serikali imefanya hiki. Serikali. Se

Ni kujielewa si kujitambua tena

Haya. Nilipotea. Kwa vigezo vyenu nakubali. Sasa nimerudi. Kurudi kwangu kumekuwa kwa jina jipya. Blogu hii tuliita Jitambue lakini baada ya kupitia pitia kumbukumbu, tukafahamu kuwa ipo blogu ambayo inaitwa kwa jina hilo ingawa imekuwa mapumzikoni tangu elfu mbili na tano. Hatujui itarejea lini ila tunaamini itarejea. Sasa ili kumrudisha ukumbuni mwenye blogu hiyo, tumeona ni vyema sisi wa hapa tujitambulishe kwa jina jingine ambalo maana yake inabaki kuwa ni ile ile. Mengi ya maudhui yetu yatakuwa yamejikita katika kujielewa. Tutajaribu kuzungumza kwa muhtasari sana habari ya sisi kama binadamu kujielewa wenyewe kazi ambayo ni muhimu sana. Watu wengi wamekuwa na kazi ya kuelewa mambo mengine, wakati wao wenyewe hawajijui. Tunadhani kwamba kuyaelewa mambo mengi bila kujielewa mwenyewe ni hasara na kujilisha upepo. Unapotembelea blogu hii, usitazamie kusoma siasa. Kwa sababu siasa haikusaidii kujielewa. Tazamia kusoma maswali yanayoweza kukufanya uongeze tafakari kukuhusu wewe mwenyewe

Nini maana ya muda?

Kuna rafiki yangu mmoja kanitumia ujumbe mrefu wa barua pepe akinipa vidonge vyangu kwa kuitelekeza blogu hii kwa muda mrefu. Yeye hana blogu, ila ni mfuatiliaji wa wenye blogu akifatilia yupi yuko wapi ana ansema nini. Basi, kupata ujumbe ule kunanikumbusha nadharia ya muda (kosmolojia): Muda ni nini hasa? Unaposema muda unaenda, unamaanisha nini hasa? Ili kujibu vidonge vya huyo rafiki yangu huyo hebu tuone muda maana yake nini. Muda unatokana na mabadiliko. Huwezi kuhesabu muda kama hauna mabadiliko. Dunia inahesabu masaa kwa sababu kuna mabadiliko. Inakuwa mchana inakuwa usiku. Inakuwa kiangazi inakuwa masika. Mabadiliko. Yasingekuwapo mabadiliko hayo pasingekuwapo na kitu kinachoitwa muda. Aidha, muda unatofautiana kati ya desturi na desturi, mtu na mtu, kazi na kazi na kadhalika. Kwa mfano, kwa mtu alikufa kwake muda ni sifuri kwa sababu mwili wake hauna mabadiko ya aina yoyote kwa vigezo vya kiumbe hai. Na pia katika jamii ambamo mabadiliko ni ya haraka, kwao muda unakuwa mdogo.

Wewe ni nani?

"Wewe ni nani?" Uliza swali hili kwa kila unayekutana naye na sikiliza majibu yao: "Mimi ni Idi" "Mimi ni Mashaka" Tena kwa kujiamini kabisa. "Mimi ni Masumbuko" Huku akikushangaa kwa kumuuliza swali la kitoto. Ukionesha kutokuridhika na majibu hayo mepesi, ukaongeza swali jingine, sana sana utaonekana mtu wa ajabu unayeuliza kitu kinachoeleweka. Utaonekana huna kazi. "Unaulizaje swali kama hilo? Ina maana unataka kunifanya mimi sijijui?" Lakini ukweli ni kwamba pasipo kujibu swali hilo, kila unachokifanya kitakuwa ni kupotea njia. Sababu wewe ulikuwa wewe kabla hujapewa hilo jina ulilonalo. Yaani wewe ulikuwa wewe kabla hujaambiwa ni wewe. Jitahidi usipotee njia. Anza leo. Jijibu swali hilo. Nakutakia siku njema ambayo inaweza kuwa mwanzo wa kujua wewe ni nani hasa wakati unazaliwa.

Jua furaha yako iko wapi, itafute

Tofauti ya binadamu na viumbe wenzake wote, iko katika ufahamu. Binadamu anaweza kutumia ubongo wake vizuri zaidi na hivyo kujitofautisha na "wanyama" wenzake wasiojua wanakotoka na wanakoelekea. Anao uwezo wa kujua anataka nini na afanyaje kukibapata. Wenzake wote, pamoja na Sokwe mwenye Di Eni Ei zinazokaribia kufanana na zake, na hata wengine tukadhani wanachangia babu wa babu, hawana kingine wanachokitafuta zaidi ya uzazi. Wao, kuzaa kunamaana ya kufikia kiwango cha juu cha mafanikio katika kipindi cha maisha yao. Wakishazaa basi, hata wakifa, kwao kifo hicho hakitahesabika kuwa cha hasara. Nini kusudi la binadamu kuzaliwa? Je, binadamu huyu anatafuta kitu gani katika kipindi cha maisha yake ambacho akikipata hicho basi anaridhika? Anataka nini ambacho akiisha kukipata basi, kwake hayo ndiyo mafanikio katika kilele chake? Je, ni kuzaa kama ilivyo kwa ndugu zetu wanyama? Je, ni kuwa na mke mrembo kuliko wote (kama kweli yupo)? Ni kuwa bilionea nambari moja Bongo yote? Ama

Self-Esteem: Ni muhimu kwa mwanao

Ninaanza na kukupa hitimisho: Mzazi anayo nafasi muhimu sana ya kumfanya mwanae ajenge fikra-chanya kuhusu maisha yake mwenyewe zitakazomfanya ajiamini. Na mzazi huyohuyo asipokuwa mwangalifu, anaweza kumsababishia mwanae fikra-hasi na hivyo kumfanya ajione duni. Kujenga fikra chanya kwa mwanao si kazi rahisi sana. Ni kazi ngumu inayodai muda wa kutosha wa mahusiano ya karibu kati ya mzazi na mwanae. Kazi hii haifanywi na wazazi wengi ambao huzaa pasipo kuhesabu gharama za uzazi husika. Hii ni kwa sababu kitendo kinachosababisha uzazi huwa hakihesabiki kama kazi. Kitendo hicho hufanyika katika mazingira ya starehe ya tamaa ya mwili kiasi kwamba wapenzi wengi huwa hawafikiri zaidi ya tamaa hiyo. Kwa maana nyingine, inaweza kukubalika nikisema kuzaa si kazi. Ndio maana hata wahenga walilonga: Kuzaa si kazi, kazi ni kulea. Kila mmoja wetu anaweza kuzaa akipenda. Ndio maana unawafahamu wasichana wadogo walioshika mimba bila kupenda. Hii ina maana kwamba kila binadamu asiye na hitilafu ya

Vipi kuhusu mahausigeli?

Hapa nchini, hivi sasa karibu kila nyumba inamiliki mtumishi wa ndani anayejulikana kama hausigeli. Mahausigeli wamekuwa fasheni manyumbani mwetu. Bila hausigeli inaonekana kama vile haijatulia. Mwidimi Ndosi anawaona watumishi hawa kama watumwa. Mahausigeli wengi ni wasichana waliokata tamaa ya maisha. Ni mabinti walioonja machungu ya makali ya maisha vijijini kwao na hivyo kuuzwa utumwani na wazazi wao wenyewe. Wengine ni wasichana walioikosa shule, japo waliipenda shule. Kisa? Kuna wanaume wakora waliutumia umasikini wa wazazi wao kuwadanganya na kulazimisha mahusiano nao, mahusiano ambayo huhitimika ghalfa pale inapoonekana kwamba yametengenza kiumbe tumboni mwa binti. Matokeo yake, binti ndiye hufukuzwa nyumbani eti kwa kosa la kuiaibisha familia. Shule inakuwa ndio basi. Mwenye mimba anakana mashitaka ya kuhusika na kiumbe hicho. Nyumbani inakuwa polisi. Binti anakosa kimbilio kati ya watu wake mwenyewe isipokuwa kupotelea mjini. Matukio kama haya ya kinyama ndiyo hasa yamesabab

Tabia zetu zimekosewa

Juma lililopita tulijaribu kuona athari za malezi katika ujenzi wa tabia zetu. Tuliona namna ambavyo matendo yanayofanywa na wazazi wetu kwa kujua kwao ama kutokujua kwao, yanatusababisha tuwe hivi tulivyo. Tukasema kuwa tulivyo, ni matokeo ya walivyo/walivyokuwa wazazi wazazi wetu. Leo ningependa tuangalie ukweli mmoja kuwa asilimia kubwa ya watu unaowaona barabarani, unaofanya nao kazi, unaosoma nao na pengine wewe mwenyewe, wamekosewa. Kukosewa ninakokuzungumzia hapa ni katika ujenzi wa tabia ama haiba yetu. Sina neno zuri kushika nafasi ya “Personality”. (Pengine Mwalimu wangu Makene atanisaidia) Kila binadamu anayo haiba/tabia yake—yaani namna anavyofikiri, anavyojisikia, anavyofanya mambo yake, anavyovaa, anavyoonekana na vilevile anavyohusiana na watu wanaomzunguka. Makosa ya tabia zetu yanahusisha matendo ambayo yanakinzana na iliyokawaida ya utamaduni wetu na matarajio ya wanaotuzunguka. Hata hivyo si kila afanye kivyume na matarajio ya watu ana kilema cha tabia. Na wala ha

Kwa nini uko hivyo ulivyo?

Bila shaka umewahi kuonana na watu wenye aibu. Huenda na wewe unalo tatizo hilo la aibu. Au unamfahamu binadamu mwenye tatizo la mkono wa birika. Ama watu wenye mtazamo hasi tu katika kila kitu. Wenye kuwaza ubaya tu kwa watu wengine. Au pia inawezekana umewahi kuwaona watu wenye kupenda ngono utafikiri chakula na chai ya asubuhi. Na vijitabia vingi vingi hivi ambavyo hutokea hatuvipendi ila tunavyo. Ningependa tujadili chanzo cha tabia hizi na namna ya kuachana nazo. Ninajaribu kurahisisha maelezo ya kisaikolojia katika lugha nyepesi ili kuona namna ya kushughulikia matatizo-nafsi kwa namna rahisi zaidi. Ukweli ni kwamba kila mtu ni mwana-saikolojia. Hata kama wapo wanadhani kujua saikolojia ni mpaka ukasugue dawati darasani kwa miaka kadhaa lakini bado ukweli uko pale pale kwamba wewe ni mwana-saikolojia. Labda utadhani natania. Hebu fikiria, ni mara ngapi umeweza kubaini kuwa mtu fulani hana furaha ama ana huzuni ama amekasirika na kadhalika? Umejuaje? Unapoweza kujifunza kinachoen

Shinto: Dini iliyoanzia Japani na kuishia Japani.

Nchi zilipokea dini zilizokuwa zimeanzishwa katika nchi nyingine. Inaaminika kuwa dini hizi zilipokelewa bila tafakuri ama kwa sababu ya kupumbazwa na ubunifu ulikuwa ukitumiwa na waenezaji wa dini hizo. Katika Japani, hali ni tofauti kidogo. Wajapani walianzisha na kuamua kuienzi dini yao maarufu ya Shinto ambayo yaweza kuchukuliwa - hasa na watu waliathirika na umagharibi- kuwa ni kishenzi. Maana kwa watu hawa dini ya kweli ni ile yenyeuhusiano wa jinsi yoyote na wale jamaa wanaopambana na ugaidi. Shinto ni dini iliyoanzishwa Japani na inaonekana kushindwa kuvuka mipaka ya Japani. Lakini inayo umaarufu wake nchini humo. Bonyeza hapa kusoma zaidi kuhusu dini hii yenye waumini wasiozidi milioni 4 duniani. Nitapandisha maelezo mafupi kuhusu Urastafariani hivi karibuni.