Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Utoshelevu Kazini

Je, Kazi yako Inakuza au Inadumaza Wito Wako?

Picha
Inawezekana unafanya kazi ambayo hukuwahi kufikiri kama siku moja ungeifanya. Labda unadhani hukuchagua vizuri kipi cha kufanya, au pengine mazingira yalikulazimisha kushika kilichokuwa kinapatikana. Kwa upande mwingine, inawezekana pamoja na kuipenda kazi yako, unahisi kuna namna fulani ya udumavu. Hupati fursa za kupanda ngazi kiutendaji na umeanza kujihisi unapoteza wito wako. Vyovyote iwavyo, bado kuna tumaini. Unaweza kabisa kufanya kazi unayojua fika haiendani na wewe, lakini hatua kwa hatua, ikakutengenezea jukwaa zuri la kuumba vizuri wito wako. Hapa ninakuletea uzoefu utakaokusaidia kujitathmini na pengine kuchukua hatua muhimu katika kuchochea ule uwezo wa pekee ambao Mungu ameuhifadhi ndani yako. Unafanya kazi yenye staha? Mratibu wa Ukuuzaji wa Ujuzi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) Dar es Salaam, Bw. Albert William Okal anaeleza namna gani mazingira yako ya kazi yanavyoweza kukuza wito wako: “Hakuna kitu kama uchaguzi mbaya wa kazi. Kila kaz...

Mbinu Nne za Kugundua na Kukuza Kazi ya Wito Wako

Picha
Umewahi kujisikia unafanya kazi isiyokupa utoshelevu? Unaweza kuwa na kiwango kikubwa cha elimu, kazi nzuri yenye heshima na mshahara mkubwa lakini unajikuta hufurahii kile unachokifanya. Ingawa moja ya sababu inaweza kuwa uongozi na mazingira mabaya ya kazi, hata hivyo, mara nyingi, tatizo huanzia ndani yetu  –k ufanya kazi isiyoakisi wito wetu. Mifumo ya elimu hulenga kutuandaa kukidhi mahitaji ya nje matarajio ya jamii, soko la ajira na mengine yanayofanana na hayo –matokeo yake mifumo hiyo inatuchonga kuwa watu tusiokidhi miito tuliyozaliwa nazo. Robert Green, mwandishi wa vitabu maarufu vya “Mastery” na “The 48  Laws of Power” anasema elimu ina nafasi kubwa ya kutupoteza. Kadri tunavyoelimishwa na watu waliotuzunguka ndivyo tunavyojikuta “tumekuwa wageni wa nafsi zetu wenyewe.” Maoni ya wazazi, walimu, marafiki, matarajio ya jamii, mara nyingi, yanatupeleka mbali na wito.  Kwa hiyo, badala ya kuheshimu kile ninachokiita wito, tumefungwa...

Tumia Mitandao ya Kijamii Kuboresha Utendaji wa Taasisi, Kampuni Yako

Picha
PICHA: kairalinewsonline.com Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufikia Novemba 2017, Tanzania ilikuwa na jumla ya watumiaji wa mtandao wa intaneti wapatao 22,995,109.   Moja wapo ya kichocheo kikubwa cha matumizi haya makubwa ya mtandao ni ongezeko la watu wanaotumia simu za viganjani zinazowezesha kuunganishwa na mtandao bila kulazimika kuwa na kompyuta zenye gharama kubwa. Hivi sasa, kwa mfano, takribani   line za simu za kiganjani zinazotumika zinafikia 40,080,954. Uzoefu unaonyesha kuwa wengi wa watumiaji wa mtandao wa intaneti wanatumia zaidi mitandao kama vile WhatsApp, Facebook, Twitter, Instagram na YouTube. Nguvu ya mitandao ya kijamii Nguvu ya mitandao ya kijamii, kwa kiasi kikubwa, inategemea tabia ya watumiaji wake. Inakadiriwa kuwa mtumiaji mzuri wa mitandao hii, huchungulia kinachoendelea mtandaoni zaidi ya mara 20 kwa siku. Makampuni makubwa ya habari kama Mwananchi Communications yanaonekana kuelewa fursa hii...

Zijue Ishara Tano Kuwa Mwajiri Amekuchoka

Picha
UMEWAHI kuhisi huhitajiki kazini? Umewahi kuona dalili kwamba pengine ni muda muafaka kwako kuchukua hatua kabla mambo hayajaharibika? Mwandishi Speancer Johnson aliyeandika kitabu maarufu cha ‘ Who Moved My Cheese ” anasema ni muhimu kusoma alama za nyakati katika maeneo ya kazi. Unapofanya kazi bila kuelewa ishara za awali mambo yanapoanza kwenda mrama, unajiweka kwenye hatari ya kujikuta kwenye mazingira ya kufanya maamuzi kwa kuchelewa. Wafanyakazi wengi huamini mwajiri akiwachoka atawaandikia barua ya kuwafuta kazi. Hawajisumbui kujua kusoma ishara mbaya kwa kuamini mwajiri hawezi kuwachoka na akabaki kimya. Unaweza kujiuliza, kama kampuni haikuhitaji kwa nini hawakuambii? Ukweli ni kwamba, wakati mwingine mwajiri huona ni afadhali akuwekee mazingira ya wewe kuondoka mwenyewe kuliko kukuondoa. Mwajiri anapokuondoa anajiweka kwenye mazingira yanayoweza kumletea usumbufu wa kisheria na wakati mwingine wafanyakazi wanaobaki hupatwa na tahayaruki. Ili kuepuka k...

Mbinu za Kukabiliana na Sonona, Hofu Mahali pa Kazi

Picha
Tuchukulie unafanya kazi muhimu inayotakiwa ndani ya masaa mawili yajayo. Wakati ukikimbizana kumalizia kazi hiyo, umeme unakatika. Ofisi haina jenerata na huwezi kutumia kompyuta bila umeme. Unajawa na wasiwasi lakini huna cha kufanya.

Tabia Tano Zitakazokupa Nidhamu ya Muda Kazini

Picha
Mafanikio katika eneo lako la kazi, kwa kiasi kikubwa, yanategemea matumizi ya muda ulionao kwa siku. Kile unachokifanya kati ya saa 6:00 usiku na saa 5:59 usiku wa siku inayofuata, ndicho kinachoamua utekelezaji wa majukumu yako.

Maswali Matano Yatakayokusaidia Kujua Thamani ya Kazi Yako

Picha
Nianze kwa kukuuliza swali rahisi. Kitu gani kinakupa motisha ya kuamka asubuhi na kwenda kazini? Unafikiri nini hasa kinaongeza thamani ya kazi yako? Kwa mujibu wa tafiti, takribani asilimia 80 ya watu wanaofanya kazi za kuajiriwa au kujiajiri hawapati utoshelevu. Kwa hakika mambo mengi yanachangia watu kutokupenda kazi zao. Kuna migororo kazini, kutokufikia matarajio waliyokuwa nayo na wakati mwingine mazingira hafifu ya kazi. Pia, sababu nyingine ni kutokuona namna gani kazi anayofanya mtu inakidhi makusudi mapana ya maisha yake. Katika mazingira haya, ni vigumu kuona thamani ya kazi yake na hivyo itakuwa vigumu kutosheka. Mtu anayependa kazi yake mara nyingi anakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuwa mbunifu, kuwa na bidii zaidi na hivyo kupata matokeo mazuri kuliko mtu anayesukumwa kufanya kitu asichoona thamani yake. Kwa kuzingatia ukweli huo, katika makala haya tunaangazia maeneo matano yanayoweza kukusaidia kuelewa kwanini kazi unayoifanya inaweza kuwa na ...

Mbinu za Kuchagua Kazi Itakayokupa Utoshelevu

Picha
Maamuzi ya kazi gani ufanye ni moja wapo ya mambo ya msingi yanayoathiri maisha ya mtu. Kazi iwe ya kujiajiri au kuajiriwa ndiyo maisha yako. Muda unaoutumia ukiwa kazini unaweza kuwa mwingi kuliko muda unaoutumia ukiwa kwingineko. Maana yake ni kwamba unapofikiri kazi ipi uifanye kimsingi unafanya maamuzi yatakayoathiri mfumo mzima wa maisha yako.

Sababu za Watu Kufanya Uchaguzi Mbaya wa Kazi

Picha
Uchaguzi wa kazi ni maamuzi anayoyafanya mtu kuanzia pale anapopata wazo la kazi anayotaka kuifanya mpaka anapostaafu. Haya ni maamuzi anayoyafanya mtu kutimiza ndoto zake kimaisha tangu anapokuwa masomoni; anapoomba kazi kwa mara ya kwanza na kuipata; anapobadilisha kazi na hata pale anapofikia umri wa kustaafu kazi.