Wakurupuka alfajiri, haraka wende kazini Wajutia kuliacha shuka, waogopa kuchelewa Ukifanyacho kimepangwa, mpangaji ni mwajiri Muda ulohisi wako, ukweli si wako Mwajiri kaununua nira kakufungia Wajisifu na ajira? Mwajiriwa akilinda kibarua chake | Picha ya picturesof.net Uhuru ni nini na aliye huru ni nani? Aliyehuru hufugwa na mwingine, ati? Aliye huru yuna muda Cha kufanya akipanga yeye, pa kwenda haamrishwi Huenda atakako kwa hiari ya muda wake Hupata mkate wake pasipo mauzo ya muda wake U huru? Mtumwa aongozwa na bwana wake Hiari na aendako hanayo Kazini ni lazima Ujira huupata kwa kuuza uhuru wake Hana mamlaka na muda alodhani wake Muda wake kauuza kwa mwajiri Nira kakabidhiwa Mabega yote juu, meno yote nje Ajisifu ana ajira! Upendacho kukifanya, huthubutu kukifanya Si wajua hakikupi muamala? Usichopenda ndo' wakifanya kupata mkate wako Kwa gharama ya