Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2017

Desturi Zetu Zilivyosaidia Malezi Bora ya Watoto -2

Picha
PICHA: The Community Voice NIMEJARIBU kubainisha baadhi ya desturi zilizosaidia kukuza watoto wanaojitambua. Unaweza kusoma makala ya kwanza hapa . Kwa kuanzia, tuliona namna familia zilivyowajibika kumtunza mama aliyejifungua. Mtoto na mama walipata muda wa kutosha kujenga mahusiano ya karibu.

Hakuna Ulazima wa Kushinda Kila Majadiliano

Picha
PICHA: Elly Prior Chukulia mnajadiliana jambo na rafiki yako. Inaweza ikawa ni mtandaoni, nyumbani, ofisini au mahali kwingineko. Katika mazungumzo yenu unabaini hamuelewani. Kile unachoona ni sahihi, sivyo anavyoona mwenzako. Kila mmoja wenu anajaribu kutetea upande wake kuliko anavyoelewa mtazamo wa mwenzake. Unadhani kipi ni sahihi kufanya katika mazingira hayo? Je, ni busara kuendelea kuthibitisha ulivyo sahihi hata kama ni dhahiri mwenzako hayuko tayari kukuelewa? Unajisikiaje mwenzako akikuonesha haukuwa sahihi? Mara nyingi tunafikiri kushindwa na kutokuwa sahihi ni udhaifu. Tunapambana na wasiotuelewa kwa mabishano na majibizana kwa lengo tu la kuonesha tulivyo kwenye upande sahihi. Unazungumza ili kushinda? Nakumbuka siku moja nilishiriki mjadala mmoja kwenye mitandao ya kijamii. Katika mjadala huo, kulikuwepo na pande mbili zinazotofautiana kimtazamo. Kadri mjadala ulivyoendelea, niligundua hapakuwa na jitihada za pande mbili hizo kuelewana. Kila upande

Desturi Zetu Zilivyosaidia Malezi Bora ya Watoto

Picha
PICHA: Huffington Post WAAFRIKA tumekuwa na utaratibu mzuri wa kuwalea watoto wetu. Mila na desturi za jamii nyingi za ki-Afrika zimeyapa malezi ya watoto uzito unaostahili. Malezi yalichukuliwa kama fursa nyeti waliyonayo wanajamii kurithisha utambulisho wa kabila husika kwa kizazi kinachofuata.

Mwalimu Anavyoweza Kukuza Udadisi kwa Wanafunzi -2

Picha
PICHA: The East African MWALIMU anabeba wajibu muhimu wa kuhakikisha mwanafunzi anajenga ari ya kujifunza maudhui kama yaliyoainishwa kwenye mtalaa. Mwalimu aliyeandaliwa vyema na kufuzu kazi ya kutafsiri mtalaa katika maisha ya mwanafunzi, anaweza kuibua na kuchochea udadisi kwa mwanafunzi.  Katika makala ya kwanza tulitumia mfano wa mradi wa Next Generation Leaning (NGL) unaoendeshwa na Shirika la Opportunity Education kujifunza namna mwalimu anavyoweza kuifanya kazi hii kwa ufanisi. Tuliona kanuni mbili. Kwanza, mwalimu anahitaji kumfanya mwanafunzi aone namna gani kile anachofundishwa darasani kinagusa maisha yake ya kawaida. Kujua uhusiano uliopo kati ya maudhui anayojifunza na maisha yake, kunamfanya athamini maudhui husika na hivyo kuwa na ari ya kujifunza. Pili, mwalimu anahitaji kumjengea mwanafunzi uwezo wa kujiuliza maswali ya msingi kuhusu maudhui anayojifunza. Kanuni hii inamsaidia mwanafunzi kupunguza utegemezi kwa mwalimu na hivyo kujenga hali ya kujiamin

Zijue Tabia Nne za Kiongozi Bora Kazini

Picha
Ufanisi kazini, kwa kiasi kikubwa, unategemea uwezo alionao kiongozi. Huyu ni mtu mwenye mamlaka yanayompa sauti ya kuhamasisha watu kujiwekea dira na utaratibu wa kuifikia dira hiyo. Kiongozi anatambulishwa na uwezo wake wa kuwavuta na kuwashawishi watu makini kutumia vipawa , ujuzi na uzoefu walionao katika kuwezesha kufikia malengo mapana ya kampuni, taasisi au kikundi husika.

Unavyoweza Kumrekebisha Mtoto Mjuaji Anayejiona Bora

Picha
PICHA: Psychology Today Kujiona bora ni kujiamini kupindukia. Mtu anayejiamini kupita kiasi, mara nyingi, anaamini anazo sifa ambazo watu wengine hawana. Unapoamini unazo sifa za ziada kuliko wengine ni rahisi kuwa na kiburi. Kuamini watu wengine hawawezi kuwa bora kama wewe kunakufanya uwadharau.

Mwalimu Anavyoweza Kukuza Udadisi kwa Wanafunzi

Picha
PICHA: OBrown & Associates Education Consulting Mara nyingi tumesikia watu wakilaumu mtalaa wetu kwamba unafunga fahamu za wanafunzi wetu. Wenye madai haya wanafikiri bila mtalaa kufanyiwa marekebisho makubwa, haiwezekani elimu yetu ikamnufaisha mwanafunzi. Hata hivyo, tulisema wiki iliyopita, kazi ya mtalaa ni kutoa diraya jumla ya aina ya raia wanaotarajiwa kufundwa kupitia mtalaa husika.

Utaratibu wa Kufuata Unapoachishwa Kazi

Picha
Sheria ya ajira na mahusiano kazini Namba 6 ya mwaka 2004 inaainisha mazingira kadhaa yanayoweza kusababisha mwajiriwa aachishwe kazi na mwajiri. Kwanza, kama mwajiri amefuata masharti ya mkataba yanayohusiana na utaratibu wa kumwachisha kazi. Kufuata masharti ya mkataba kunategemea kama aina ya mkataba. Pale ambapo mkataba ni wa kudumu, mwajiri lazima awe na sababu halali za kuchukua hatua za kusitisha mkataba kwa kufuata utaratibu.

Mafanikio Hayamfanyi Mwanamke Anayejitambua Kuacha Wajibu Wake

Picha
PICHA: RealClearPolitics USAWA wa kijinsia katika dunia ya leo si suala linalohitaji mjadala. Tunakubaliana kimsingi kuwa hakuna jinsia bora kuliko nyingine na pia hakuna jinsia inayohitaji kulipa gharama ya kulinda hadhi ya jinsia nyingine. Mwanamke, anayo haki ya kupata elimu kulingana na uwezo wake, kufanya kazi anayoiweza, kumiliki na hata kurithi mali sawa na mwanaume.

Kumsaidia Mtoto Asiyejiamini, 'Anayeogopa' Watu

Picha
PICHA: Blend Images KUTOKUJIAMINI ni kutokuwa na ujasiri, kutokuwa na imani na uwezo wako mwenyewe. Mtu asiyejiamini anaweza kuwa na uwezo mkubwa wa kufanya vitu. Tatizo lake ni kujishuku. Vijana wa mjini wanaita ‘kujistukia.’ 

Tufanye nini Kukuza Udadisi kwa Wanafunzi Wetu?

Picha
PICHA: Fernando Díez Gallego UDADISI ni uwezo wa kuhoji mazoea. Udadisi ni kiu ya kujiuliza maswali yanayolenga kutafuta majibu ya changamoto zilizopo. Mtu mdadisi lazima atakuwa na uchunguzi ndani yake. Haiachi akili yake itulie. Haridhiki na majibu yaliyozoeleka. Mdadisi hupembua taarifa kumwezesha kuelewa ujumbe uliojificha kwenye taarifa hizo.

Umuhimu wa Mwajiriwa Kuwa na Mkataba wa Ajira

Picha
Waajiriwa wengi, hususani kwenye sekta binafsi, wanafanya kazi bila kuwa na mikataba. Utendaji na usalama wa wafanyakazi hawa, kwa kiasi kikubwa, unategemea hisani na uaminifu wa mwajiri.

Mwanaume Anayejitambua Hatishwi na Mafanikio ya Mwanamke

Picha
PICHA: Ayo Martins Upo ukweli usiosemwa wazi kuwa wanaume wengi wanawaogopa wanawake wenye mafanikio. Wanawake waliosoma, wenye mali na fedha, wenye madaraka makubwa katika jamii, wanakuwa na mtihani mkubwa kuanzisha na kudumisha uhusiano na wanaume.

Ufanye Nini Mtoto Anapokuwa Mkorofi?

Picha
PICHA: JGI/Jamie Grill Pengine una mtoto unayefikiri ameshindikana. Unamwita mtundu, mtukutu, asiyeambilika, mbishi, mkaidi na majina mengine. Kikubwa ni tabia yake ya kupenda kushindana. Katika makala haya tunamwita mtoto mkorofi. Huyu ni mtoto anayeweza kukukatalia kitu bila kupepesa macho na ukajikuta ukifedheheka.