Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2011

CHANGAMOTO Insha za Jamii - Prof. Mbele

Picha
Natamani sana kukisoma kitabu hiki. Ninakitafuta kwa bidii. Unajua kinakopatikana? Mwandishi Profesa Mbele anasema kakiandika kusahihisha majungu kuhusu Mwalimu Nyerere. Msome hapa halafu uone kama unaweza kujishindia Dola 100! Waweza pia kusoma majadiliano katika Jamii Forums yanayodurusu ikiwa wanaomkosoa Mwalimu Nyerere wana hoja.

Take the Risk cha Ben Carson

Picha
Ndio kwanza nimeanza kukisoma. Take the Risk: learning to identify, Choose and Live with accepatable Risk. Kimeandikwa na Mganga Ben Carson kwa msaada wa Gregg Lewis na kuchapishwa na Zondervan Publishing House mwaka 2008. Kitabu kinaanza na masimulizi ya upasuaji mgumu uliofanyika Julai 2003 kuwatenganisha Ladan na Laleh, mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana sehemu ya vichwa vyao. Mapacha hao hata hivyo walifariki dunia wakiwa na umri wa miaka 29 wakati upasuaji huo ukiendelea huko Singapore. Katika kitabu hiki, mwandishi anajaribu kutupatia somo lilitokana na Upasuaji huo. Ladan na Laleh raia wa Iran muda mfupi kabla ya upasuaji huo uliofanyika Julai 2003.

Elimu pasipo maandishi inawezekana?

Picha
Pamoja na ukweli kuwa wengi wetu tunayakwepa maandishi, lakini hiyo haimaanishi kuwa hatuna kiu ya kujifunza. Pichani, wananchi wa mjini Moshi wakionekana kuvutiwa na matumizi ya video katika kuelimika. Picha: Sayuni Philip

Kuwa mwenye furaha ni uamuzi wako mwenyewe!

Picha
Ni mara ngapi umewahi kukutana na mtu aliyekukwaza kiasi cha kumtupa katika kapu la “watu wa hovyo” wasiostahili heshima kama binadamu? Umewahi kupatwa na tukio ambalo lilibadili kabisa mtazamo wako kuhusu maisha, watu na maisha kwa ujumla? Kwa nini watu kukata tamaa? Umewahi kuwaza kwa nini kinachomkwaza huyu si lazima kimkwaze yule? Umewahi kuonana na mtu anayeshangaa inakuwaje “huyu bwana achukue uamuzi wa ajabu namna ile” wakati kilichotokea kinachukuliwa na wengi kuwa “ni jambo la kawaida”? Natamani ukimaliza kusoma hapa uelewe kwamba sehemu kubwa ya matatizo tunayokabiliana nayo kama binadamu kila siku, tunayasababisha wenyewe. Na kwa yale tusiyo naudhibiti nayo, tunaweza kubadili mtazamo wetu kwayo, na hilo linaloonekana kuwa tatizo ama likawa si tatizo au likabadilika kuwa changamoto. Wengi wetu tunapokumbana na vikwazo (ambavyo mara nyingi huwa ni watu, vile mambo yalivyo na matukio yanayokuwa katika namna tusiyoitegemea) hujenga mawazo kwamba vitu hivyo vi vibaya. Mato

Wanablogu wanasemaje kuhusu utaratibu wa "Kutuzwa"?

Picha
Tangazo lilianzia hapa kwamba kuna mwuungwana -japo hakuwa anafahamika jina lake wala mahali aliko- kapata wazo la kutunuku kazi za wanablogu. Huenda hili bado halijulikani kwa wanablogu wengi kama ilivyokuwa kwangu kabla ya kusoma posti ya mwanablogu matata, Bw. Mubelwa Bandio juma lililopita. Blogu ya mwandaaji wa Tuzo hizo inajinadi kwa maneno haya: "...Our wish is to help bloggers to success, beat the odd and push past their limitation. We believe bloggers can play an important role keeping their places, villages, towns, cities or countries visible. Tanzanian Blog Awards is another opportunity to showcase your blog to the world and get some free traffic and subscribers..." Pamoja na kupongeza wazo hilo (la kuandaa tuzo kwa wanablogu), Mubelwa Bandio alionyesha wasiwasi wake ikiwa zoezi hilo litafanyika katika mazingira ambamo masuala ya msingi kuhusu blogu hayajafanyiwa kazi. Kwamba blogu zinaeleweka vyema kwa wadau (wateuzi na wateuliwa), hilo lilimtia mashak

What religion really means

Picha
Kimeandika yaliyo kinyume na imani yangu. Nakisoma. Mwandishi Karen Armstrong na kuchapishwa na Vintage 2010. Kinauzwa kwa Tsh 19,500.

Wakubwa wetu huko Ufaransa

Picha
Picha hii imechukuliwa kwenye ukumbi wa mijadala wa Jamii Forums ikiwaonyesha watawala wetu walipohudhuria mkutano huko Ufaransa.

Uliwahi kukisoma hiki?

Picha

Padre karugendo na mijadala ya Imani

Picha
Kitabu hiki nilikisoma mara ya kwanza mwaka jana. Yeye mwenyewe alinielekeza mahali pa kukipata baada ya kuwa amesoma mjadala uliomhusu kwenye blogu hii baada ya kusemekana kuwa Padre Karugendo alikuwa "amevuliwa" upadre. Nilijifunza mengi kuhusu dini. Pengine unaweza kujiuliza; Kwa nini aliandika kitabu hiki? Pamoja na kukieleza kisa kizima kilichosababisha yeye "kufutwa" upadre kupitia tangazo la gazetini, Padre Karugendo anasema katika uk. 22: "...lengo zima la kutafakari kwangu na kukushirikisha wewe msomaji, ni kutaka kujenga utamaduni kama ule wa kule zilikotoka dini hizi za kigeni. Utamaduni wa kuamini kitu unachokifahamu vizuri, unachokitafakari, kinachogusa maisha yako ya jana, leo na kesho. Imani inayojenga historia yetu - historia ya Mungu na watu wake wa taifa la Tanzania!" Pamoja na hilo, Padre karugendo anasema kwa sauti kubwa kabisa kwamba, "Si haki Maaskofu kukemea ufisadi ndani ya serikali na kuacha ufisadi unaoendelea ndani y

Ninachokisoma sasa...

Picha

Ninapoahirisha mafanikio yangu kwa "kukwepa" kuamua

Mambo mengi yenye matokeo mazuri, si rahisi kuyafanya. Hasa ikiwa utekelezaji wake unadai utashi, “usilolazimishwa” na mamlaka iliyo nje na mtu mwenyewe. Ugumu wa mambo haya, ni zile zinazoonekana kuwa gharama za papo kwa hapo, zinazoweza kutukwaza tukate tama ya kufanya yale tuyapendayo. Matokeo ya haya yote, ni kujikuta tukiishi maisha yasiyo na utimilifu. Maisha yasiyo yetu. Pengine uliwahi kusoma maneno ya mtu mmoja aitwaye Albert Gray yanayosema: The successful person has the habit of doing things failures don’t like to do. They don’t like doing them either necessarily. But their disliking is subordinated to the strength of their purpose. Nukuu hii imekuwa na maana tofauti kwangu. Kwamba kile ninachokiona kwamba kana kwamba hakivutii kukifanya, ndicho chaweza kufanyika utimilifu wa ninachokikusudia. Mambo gani ambayo unajua ni ya muhimu yafanyike lakini unayaahirisha? Ni mangapi mazuri unayakosa kwa kule tu kukwepa kulipia gharama ya kuyatekeleza hayo unayoyaona kuwa ni

Katuni husema vingi! Tazama hii.

Picha
Kazi ya mchora katuni, Fede wa http://artsfede.blogspot.com

Je, jamii ingekuwaje bila dini?

Picha
Hebu tutafakari ingekuwaje bila dini. Ili kusaili hali hiyo ya kufikirika, hebu tuyasaili masuala haya kuona ikiwa dini inatufaa ama ndilo tatizo linalotukabili. Je, dini zinamsaidia binadamu kumjua Mungu? Je, bila dini tunaweza kuwa na uhusiano na Mungu? Je, dini zinasaidia kujenga jamii ya watu waadilifu na wanyoofu? Je, dini zinawasaidia waumini wa dini moja kuheshimu mitazamo ya waumini wa dini nyingine? Je, dini zinasaidia kujenga upendano katika jamii? Je, dini zinapunguza unafiki katika jamii? Je, dini zinapunguza migongano na misuguano katika jamii? Dini ni nini? Ni kumjua Mungu? Ni chama cha wanaomtafuta Mungu? Dini na imani vinauhusiano? Kwa nini dini? Mimi nafikiri tatizo ni dini zenyewe na sio watu. Wewe unafikiri nini? Tungekuwaje bila dini? Jumapili njema.

Unajua wanyaturu walipangaje uzazi?

Yapo mambo mengi katika jamii zetu yaliyofanyika zamani ambayo tukiyatazama twaweza kujifunza mengi. Mengi ya hayo, si sehemu ya jamii za kisasa hivi leo, lakini yalekuwa na msaada wa namna Fulani kwa jamii. Katika jamii ya asili ya wanyaturu, kabila dogo linalopatika katika wilaya ya Singida (na kidogo manyoni), mahusiano kati ya baba na mama yalikuwa na sura tofauti sana na ilivyo leo. Wakati leo hii, wazazi kulala vyumba tofauti huchukuliwa kama ishara ya kufifia kwa mahusiano baina ya wawili hao, kwa Wanyaturu hiyo ilikuwa na maana tofauti. Kikawaida, wazazi wa Kinyaturu hawakupaswa kukaa nyumba moja (sio chumba kimoja, nyumba moja) ndani ya boma. Katika boma analojenga mwanaume kama himaya ya familia yake, alipaswa kuzingatia uwepo wa nyumba mbili ndnai ya boma moja. Baba ambaye ndiye mkuu wa boma, alilala na wanawe wa kiume katika sehemu maalumu ya nyumba inayojulikana kama "Idemu/Ikumbu". Nyumba hiyo ilijitenga pembeni na nyumba kuu alikoishi mama na wanawe wa

Pedagogy of the oppressed

Picha
Paulo Freire katika sura ya pili ya kitabu chake "Pedagogy of the Oppressed" anazungumzia dhana inayosisimua anayoiita "the banking concept of education" kama chombo kinachotumika kuwakandamiza wanyonge. Kwamba katika hayo yanayoitwa madarasa, wapo waungwana wanaojichukulia kuwa wanajua, hulipwa kwa kuwajaza wenzao "elimu" ambayo kimsingi ni chombo cha kuwakandamiza raia wanaoonewa. Freire anadhani hii si sawa kwa binadamu mwenzako kujiweka juu sana kiasi cha kuamua usome nini, na uache kipi (bila kujali mahitaji yako halisi). Anatoa mfano pale mwalimu anapoweza hata kupendekeza kwamba kitabu fulani kisomwe kuanzia ukurasa wa 10 hadi wa 15! Na eti anadhani anamsaidia mwanafunzi! Kwa mujibu wa Freire, elimu hii haiwezi kumkomboa mnyonge. Je, elimu yetu ina tofauti? Wanafunzi zaidi ya asilimia 50 "walishindwa" mtihani hivi majuzi, ni kweli walishindwa ama ni namna nyingine ya kuwakandamiza vijana wasio na hatia?

Shule zisizo na elimu zifungwe!?

Picha
Ivan D. Illich ni mwanafalsafa aliyezaliwa mjini Vienna mwaka 1926. Katika kitabu chake cha Deschooling Society, Illich anazishambulia taasisi ziinazohodhi wajibu wa kuelimisha jamii. Anasema; “…kwenda shule (tofauti na kuelimika) imekuwa ndio utaratibu wa maisha…shule zimeshindwa kukutana na mahitaji ya mtu mmoja moja, na mbaya zaidi zinaendeleza uongo ule ule kwamba yale yanayoitwa maendeleo yanayotokana na uzalishaji, utumiaji na faida ndicho kipimo cha ubora wa maisha ya mwanadamu. “…Vyuo Vikuu (shule) vimegeuka viwanda vya kutengeneza vibarua kwa ajili ya matajiri, vikiwapa raia vyeti kwa ajili ya kutoa huduma, wakati huo huo vikionekana kuwanyang’anya leseni wale vinavyowadhania kuwa hawafai (waliofeli).” Tafsiri ni yangu. Illich anatoa mapendekezo ya kukomesha mfumo huu wa baadhi ya watu kujipa wajibu wa kuwaelimisha wengine wakati wao wenyewe hawajielimishi. Haoni haja ya kuwa na majengo yanayoitwa shule ambayo kazi yake inaonekana kuishia kutengeneza watumwa wa soko huria

Matokeo Kidato cha IV 2010: Asilimia 89 wamefeli!

Inasikitisha kuwa katika matokeo ya Kidato cha Nne yaliyotangazwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani leo hii, zaidi ya asilimia 50 ya watahiniwa wa mtihani wa kidato cha IV mwaka 2010 wameishia kupata daraja sifuri. Asilimia 39 ya watahiniwa hao (waliozidi 440,000) wameambulia cheti kisicho na tija (yaani Daraja la IV)wakati ni asimilia 11 tu wameweza kupata Madaraja ya I, II na III. Hali hii si ya kufurahia hata kidogo. Je, tuchukue hatua gani kujinusuru na janga hili?

Ajuaye kusoma na hasomi ana nafuu?

Je, kuna tofauti kati ya mtu asiyejua kusoma (illiterate) na yule anayejua kusoma (literate) lakini hasomi?

Pesa bila kufisidi mali ya umma...

Picha
Pesa bila unyonyaji inawezekana? Ninakisoma hiki hivi sasa kwa mara ya pili, cha Napoleon Hill.

Wangapi huzitazama tabia zetu kwa jicho la mabadiliko?

Mwanzo wa mwaka huwa na matumaini tofauti na wakati mwingine wowote wa mwaka. Ni wakati ambapo watu hujisaili, na kutazama wanakoelekea kwa mwaka unaoanza. Ni wakati ambapo watu hujipanga namna ya kupiga hatua katika maeneo muhimu ya kimaisha. Hata hivyo, ni wangapi wetu huweka maazimio ya kubadili tabia zetu? Ni wangapi wetu tunao uwezo wa kuzitazama tabia zetu kwa jicho dhati la mabadiliko? Kwa mfano. kuamua kwamba mwaka huu ninapambana na tatizo la kutokusoma? Kuamua kwamba siwezi kuendelea kuwa mtu nijuaye kusoma lakini sisomi? Ni wangapi wetu hisia hizo za matumaini mapya tunazokuwazo mwanzo wa mwaka, huishia kwa matumaini yayo hayo mwisho wa mwaka? Kwa nini malengo mengi huishia kuwa malengo ya mwaka unaofuata? Kwa nini watu wengi humaliza mwaka kwa masikitiko –wakati wanapojikuta na hali ile ile ama mbaya zaidi ifikapo mwisho wa mwaka? Kumbuka uamuzi wa kufanya badiliko dogo, ambao unauhakika wa kuendelea nao kwa miezi kumi na miwili, ni wa muhimu kuliko kufanya maamuzi

Heri ya mwaka mpya!

Nikutakieni nyote heri ya mwaka mpya 2011. Mwaka wa matumaini mapya. Mwaka wa maendeleo zaidi. Mwaka wenye changamoto chanya zaidi. Na mwaka wa kujielimisha zaidi ya tunavyoelimisha.