Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Tafiti

Ukiigiza Ukatili, Unakaribisha Tabia ya Ukatili

Picha
Kuna wakati unaweza kufikiri unaigiza msimamo na kejeli kwa maumivu ya mtu, unakuwa na maoni yasiyo na haya kwa mateso ya wenzako ukijua unawafurahisha watu fulani lakini hayo maigizo ya kukosa huruma kwa mwenzako yana uwezekano wa kugeuka tabia kweli na ukawa mtu katili kweli kweli. Michezo, dini na siasa visikuchochee kujiona una haki ya kubeza masaibu wanayopitia wenzako kwa sababu mdogo mdogo mizaha hugeuka ukweli.   Mwaka 1971, Philip Zimbardo, mshunuzi na mwalimu wa Chuo Kikuu cha Stanford, alifanya utafiti maarufu kama  #StanfordPrisonExperiment  akilenga kuchunguza nguvu ya mazingira kwenye tabia.    Utafiti ulivyofanyika   Zimbardo alitengeneza gereza la kuigiza hapo chuoni likiwa na seli, mahali mfungwa angekaa mwenyewe, mahali pa wanyarapa kuishi, mahali wafungwa wangetoka na kuteswa na wanyapara. Washiriki walifanyiwa mchujo wa haiba kuona kama ni watu wenye utimamu wa tabia na hisia.    Kwa njia ya nasibu (random assignment) wanafunzi...

Tabia za Mamlaka kwa Wanyonge Zinavyoweza Kuzalisha Uovu

Picha
Umewahi kujiuliza kwa nini watu huweza kupokea na kutekeleza amri hata zile wanazoamini ni kinyume cha maadili, utu na dhamiri zao? Kwa nini mtu anaweza kuambiwa ‘fanya kitu cha kikatili’ na akatii hata kama amri hiyo inamaanisha mtu kuumia na hata kufa?    Mwanzoni mwa miaka ya 1960, Stanley Milgram wa Chuo Kikuu cha Yale alifanya utafiti maarufu kwa jina la  #TheMilgramExperiment . Milgram alitaka kuangalia nini hasa kinachangia mtu kutii mamlaka hata katika mazingira ambayo utii huo unaweza kusababisha madhara kwa binadamu mwenzake.    Kwa lugha nyingine, nini hasa kilifanya watu kama Hitler waliofahamika wazi ni wakatili wawe na wafuasi waaminifu wanaotekeleza maagizo yao kuumiza watu, kutesa na hata kuwaua?   Utafiti ulivyofanyika   Washiriki wa utafiti huo waliaminishwa wanashiriki utafiti wa kuangalia uhusiajo wa kumbukumbu na ujifunzaji na wao wanashiriki kama ‘walimu.’ Jukumu lao lilikuwa ni kusoma swali na kufanya maamuzi ya kumuadhibu mwanaf...

Madhara ya Kutoa Ushauri Kienyeji na Kuugeuza Unasihi kuwa Ushauri

Picha
Utamaduni wa (kutoa na kuomba) ushauri umejengeka kwenye misingi ya hekima ya wazee walioona mengi, uzoefu wa mtu mzima unaompa uhalali wa kutoa mwongozo wa kufuata kwa anayemzidi.  Hata tunaposikia unasihi (counselling), aghalabu, mawazo yetu yanaenda kwenye taaluma ya kushauri watu na kuwaambia cha kufanya ili kutatua matatizo yanayowakabili. Wapo, tena wengi, wanaotafsiri ‘counselling’ kama ushauri. Counselling sio ushauri. Katika makala haya, ninajenga hoja kuwa kutoa ushauri ni jambo la hatari na kwamba linaweza kusababisha madhara makubwa kwa anayeshauriwa lakini pia hata anayeshauri.  Kadhalika, ninalenga kuonesha, japo kwa ufupi kuwa hata kwenye unasihi msingi wa kwanza wa kuzingatia kwa mtoa huduma (aliyefuzu) ni kuepuka kabisa kutoa ushauri kwa mtu. Nakusudia kuonesha nini hasa huwa ni malengo ya unasihi. stefanamer/Getty Images Ushauri ni nini?  Unaposema unamshauri mtu unakuwa na maana gani?  Ushauri, kwa kifupi, ni maelekezo mahususi unayompa mtu, maamuz...

Mbinu za Kujenga Ujuzi wa Mwanafunzi

Picha
PICHA: Shutterstock Nakumbuka siku ya kwanza kusikia neno ‘cell’ nikiwa kidato cha kwanza haikuwa kazi rahisi kupata picha kamili. Mwalimu wetu aliandika ubaoni, ‘ cell is a basic unit of life .’ Niliduwaa. Sikujua anamaanisha nini zaidi ya kutazama kamusi kujua maana ya maneno aliyoyatumia. Mwalimu alirudia maneno hayo hayo kuweka msisitizo, na kisha akatafsiri kwa Kiswahili. Alisema, ‘maana yake ni hivi kuna kitu kidogo kisichoonekana kwa macho kwenye miili yetu kinachofanya tuishi. Mmeelewa?’  Kwa kweli hatukuwa na namna nyingine zaidi ya ‘kuelewa’ na tukaitikia, ‘ndiyo!’

Mzazi Ufanyeje Unapompeleka Mwanao Shule ya Bweni?

Picha
PICHA: Paul Jeffrey PAMOJA na changamoto za malezi ya shule za bweni tulizoziona, bado mzazi anaweza kulazimika kumpeleka mwanae kwenye shule hizi. Kwanza, kuna suala la kazi. Wazazi wanaofanya kazi mbali na familia zao wanaweza kuamua kuwapeleka watoto kwenye shule ya bweni ili wasiwe na wasiwasi na uangalizi wao.

Namna ya Kutambua na Kukuza Kipaji cha Mwanao -1

Picha
Kila mtoto ana kipaji. Ingawa ni kweli kuwa watu wengi hawatambui vipaji vyao, hiyo hata hivyo, haimaanishi hawana vipaji. Zipo sababu nyingi zinazofanya watu wasitambue vipaji vyao. Kwanza, ni mfumo rasmi wa elimu unaotumia tafsiri finyu ya uwezo wa kiakili.

Mambo ya Kuzingatia Unapompeleka Mwanao Kwenye Kituo Cha Malezi

Picha
Watafiti wa malezi ya watoto wamejaribu kuangalia namna gani huduma za malezi ya kituoni –day care yanavyoweza kuboreshwa. Moja wapo ya watafiti maarufu katika eneo hili ni   Taasisi ya Marekani ya Mtandao wa Afya ya Mtoto na Maendeleo ya Utafiti wa Malezi ya Watoto (NICHD) . Maswali ya msingi yanayojaribu kujibiwa na tafiti hizi ni ikiwa kuna uhusiano wa ubora wa huduma zinazotolewa na vituo hivi na makuzi ya mtoto katika nyanja za kiakili, kihisia, kimwili na kistadi; aina ya mazingira yanayoweza kuhusianishwa na ukuaji mzuri wa kihisia na kiakili kwa mtoto na kiasi cha masaa kinachopendekezwa kwa mtoto kulelewa katika kituo kwa siku/juma.

Mbinu Nne za Kukuza Ubunifu wa Mtoto

Picha
Ubunifu ni uwezo wa kufikiri, kutafuta majibu au kutatua changamoto kwa namna isiyotarajiwa. Mtu mbunifu hufanya mambo kwa namna isiyo ya kawaida. Hafanyi vitu fulani kwa sababu ameona watu wakifanya. Hafuati mazoea wala uzoefu. Huwa tayari kufanya mambo mapya. Ingawa kuna uhusiano mdogo kati ya ubunifu na uwezo wa jumla wa akili, kwa kawaida, mtu mwenye akili si lazima awe mbunifu. Unaweza kuwa na akili ya kuchambua, kuelewa, kukumbuka na kueleza mambo unayojifunza lakini usiweze kufanya mambo kinyume na mazoea.

Faida, Hasara za Vituo vya Kulea Watoto

Picha
TUMEKUWA tukijadili changamoto zinazowakabili wazazi wanaofanya kazi mbali na nyumbani. Njia kadhaa zinatumika kukabiliana na changamoto hizi. Moja wapo, ni kuwaajiri wasichana wa kazi kwa lengo la kusaidia kuwalea watoto. Tulipendekeza kuwa msingi mkuu wa kupunguza changamoto za huduma hizi zinazotolewa na wasichana wa kazi ni kujenga nao mahusiano mazuri ya kifamilia na kikazi. Mahusiano haya yanawajengea motisha ya kufanya kazi kwa uadilifu na moyo wa kujituma.

Siri za Watu Wanaotekeleza Maazimio ya Mwaka Mpya

Picha
TULIJADILI baadhi ya sababu zinazofanya watu washindwe kutekeleza maazimio wanayoyaweka kila mwaka mpya unapoanza. Tuliona sababu kubwa tatu; kuweka maazimio kwa msisimko tu wa kuingia mwaka mpya usioenda sambamba na tafakari ya kina; kuweka malengo mapana mno yasiyopimika; na pale malengo yanapohusisha mabadiliko ya tabia, kutokujua uliko mzizi wa mabadiliko hayo.

Namna ya Kupunguza Changamoto za Wasichana wa Kazi

Picha
TUMETAJA mambo mawili yanayobadili mfumo wa malezi. Mosi, ni kubadilika kwa majukumu ya kijinsia yaliyozoeleka katika jamii. Mama anapoingia kwenye soko la ajira na kwenda kazini kama ilivyozoeleka kwa baba, changamoto inayojitokeza ni namna wanavyoweza kumlea mtoto wao katika muda wa kazi. Pili ni kufifia kwa utamaduni wa familia tandao unaozorotesha msaada wa kimalezi uliozoeleka kutoka kwa ndugu wa karibu. Mawili haya yanalazimisha familia za sasa kutafuta namna nyingine ya malezi kuwapa fursa wazazi kuendelea na kazi.

Kwa Nini Maazimio Mengi ya Mwisho wa Mwaka Huwa Hayatekelezeki?

Picha
Kila mwaka mpya unapoanza, ni kawaida kwa watu wengi kuweka maazimio fulani ya kutekeleza. Wapo ambao huazimia kubadili tabia wasizozipenda. Wengine huazimia kuanzisha mwenendo mpya wa maisha wanayoyatamani. Wengine hufikiria kutekeleza malengo fulani ya kijamii na kiuchumi yatakayobadili maisha yao kwa mwaka unaoanza. Ingawa ukweli ni kuwa mwaka unapoanza kinachobadilika huwa ni tarehe tu, watu huwa na imani kuwa wanaingia kwenye zama za maisha mapya. Imani hiyo huambatana na jitihada za kujaribu kubadili maisha yao yaendane na zama hizo mpya. Wanasema, ‘mwaka mpya na mambo mapya!’

Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Anayefanya Vibaya Shuleni

Picha
Si jambo la kufurahisha kwa mzazi unapoona mtoto hajafanya vizuri masomoni. Unapofahamu kuwa maendeleo ya mwanao si kama vile ulivyotarajia, ni rahisi kupatwa na simanzi, wasiwasi na hasira. Ni dhahiri mzazi unatamani mtoto awe na mustakabali mzuri kimaisha. Matumaini hayo yanakufanya uchukulie kushindwa kwake masomo kama kiashiria cha kuharibika kwa maisha yake ya baadae. Hakuna mzazi angependa mtoto awe na maisha yasiyoeleweka.

Mbinu za Kushinda Maswali ya Usaili wa Kazi - 1

Picha
Kama tulivyoona katika makala yajuma lililopita , usaili ni hatua ya mwisho kuelekea kupata kazi. Sehemu kubwa ya usaili ni maswali na majibu yanayolenga kupima uwezo wako wa kukabiliana na changamoto halisi za kazi. Ingawa yapo maswali yanayoweza kukupa wasiwasi wa nia ya mwuulizaji, fahamu kuwa hakuna swali linaulizwa kwa nia mbaya au kwa bahati mbaya. Kila swali linaloulizwa linalenga kutafuta uthibitisho kuwa wewe ni mtu sahihi kwa kazi unayoomba.

Mambo ya Kuzingatia Unapoandika Wasifu wa Kazi (Curriculum Vitae)

Picha
Katika mchakato wa kuomba ajira baada ya kuona tangazo la kazi, mambo matatu ni dhahiri. Mosi, huombi kazi hiyo wewe mwenyewe. Wapo watu wengi wanaoandika maombi na hivyo kuongeza ushindani wa nani atapata. Pili, nyaraka unazotuma kwa mwajiri mtarajiwa ndizo zinazojenga utambulisho wako kabla wewe mwenyewe hujafahamika. Tatu, afisa mwajiri hatatumia muda mrefu kusoma maelezo yako. Katika hali ya kawaida, atatumia dakika moja kuamua ikiwa amevutiwa na maelezo yako ama la.

Mambo Sita ya Kufanya Unapotafuta Kazi

Picha
Kutafuta kazi ni kuingia kwenye soko la ajira ambalo kimsingi ni uwanja unaowakutanisha watu wenye mahitaji makubwa ya aina mbili. Upande mmoja, wapo watu wenye ‘bidhaa’ ya ujuzi na weledi, lakini wenye hitaji la kujipatia kipato kwa kutumia ujuzi na maarifa waliyonayo. Hawa wanaitwa watafuta kazi.

Unaweza Kumfundisha Mtoto Adabu Bila Kumchapa

Picha
Mjadala wa fimbo na malezi una historia ya mjadala mkali. Fimbo, kwa hakika, zimekuwa kama sehemu ya maisha yetu . Takwimu zinathibitisha hali hii. Kwa mfano, asilimia zaidi ya 80 ya wazazi wa nchi zinazoendelea wanatumia fimbo angalau mara moja kwa mwezi. Ndio kusema, vipigo kwa watoto vimekuwa sehemu ya malezi katika nchi zetu hizi. Matumizi haya makubwa ya fimbo kwa kiasi fulani yanatokana na imani waliyonayo wazazi kuwa bila mtoto kusikia maumivu hawezi kurekebisha tabia wala kuwa msikivu. Ingawa hakuna ushahidi wowote kuwa viboko vinasaidia kujenga nidhamu kwa watoto, bado wazazi wengi wanaamini adhabu ya fimbo ndiyo jibu la kumnyoosha mtoto.

Mambo ya Manne ya Kufanya Mtoto Akusikilize, Akuheshimu

Picha
Msomaji mmoja wa safu hii aliniandikia hivi majuzi akidai mwanae hamsikilizi. Kwa mujibu wa mzazi huyu, pamoja na kufanya jitihada za kumwelekeza mwanae mambo muhimu ya kimaisha, bado kijana wake huyo haonekani kusikiliza. Anasema, kadri anavyomwadhibu mwanae, ‘ndivyo anavyozidi kuwa mkaidi…’ Mzazi huyu, inavyoonekana, amepoteza mamlaka yake kama mzazi. Mamlaka kimsingi ni uwezo wa kusema kitu na kikasikika bila kulazimika kutoa adhabu. Unapokuwa na mamlaka maana yake unayo nguvu ya ushawishi inayomfanya mtoto awe tayari kukuiga, kukusikiliza, kukuelewa na kufanya kwa hiari yake yale unayomwelekeza.

Kanuni za Kuongeza Ushawishi wa Hoja Zako

Picha
Kwa nyakati tofauti kila mmoja wetu hutamani kuwa na ushawishi kwa wengine. Ni kawaida, kwa mfano, kutamani hoja tunazozitoa zipokelewe na wale tunaowatumia ujumbe husika. Ili ujumbe upokelewe, inahitajika nguvu inayoweza kuwasukuma wengine kuupenda, kuubali na ikiwezekana kubadilika kwa sababu ya ujumbe husika. Nguvu hii inaitwa ushawishi.

Makundi Manne ya Tabia za Watoto Kitabia

Picha
Ingawa ni kweli tunazaliwa na sehemu ya tabia tulizonazo, upo ukweli wa kiutafiti unaothibitisha kwamba mazingira ya kimalezi yana nafasi kubwa katika kujenga tabia za mtu. Ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili, mathalani, unatawaliwa zaidi na uasili ambao kwa kiasi kubwa hatuna mamlaka nao. Hata hivyo, ukuaji wa kihisia na kimahusiano unatawaliwa zaidi na mazingira ya kimalezi ambayo tayari tuliyaona kwenye makala iliyopita .