Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2008

Safari zinavyotukutanisha na mengi

Nimekuwa na pilika pilika za hapa na pale. Sehemu kubwa ya muda wangu nikiutumia katika vijiji vyetu. Nilianzia Morogoro. Tukuyu. Kyela. Baridi ile mbaya. Watu wanalima kahawa wa kununua haonekani. Akiwepo basi bei ni ya kutupa. Mtu unajiuliza hivi ni lini wakulima watapata thamani sawa na watu wengine? Mwananchi anahangaika na mashamba ambayo hayamsaidii kujikwamua. Watu wamekata tamaa. Ndugu zangu tuache kufarijiana. Wananchi wamekata tamaa. Majuma kadhaa ya mwezi Julai nimeyatumia Tunduma na Vwawa. Watu wanaishi maisha magumu sana. Wanajua kuwa nchi yao inazo hela, lakini zinaliwa na walafi wachache. Ukitaka kuijua Tanzania, usiishie dasalama. Vwawa na Mbozi panaweza kukupa picha ya nchi yetu. Nikiwa Mbeya mjini nikajaribu kupandisha picha kwenye blogu, ikawa ngumu. Hata sijui palikuwa na nini hapo. Nikiwa Ipogolo Iringa nako sikuweza kukaa na kuandika. Juma moja likaishia Dodoma nikiwa na heka heka nyingi kidogo. Nikadhani nikiwa Singida ningeandika. Wapi bwana. Singida ndio