Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2006

Ni lini tutajifunza kujifunza?

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) ulikuwa na kasoro kubwa. Kasoro hizi zinaelezwa kujikita kuanzia kwenye utengenezwaji wake (in put) na utekelezaji wenyewe ambao ulileta matokeo yaliyotafsiri mpango mzima kuwa uliharibika. Sirikali ya uwazi (utandawazi) na ukweli ililaumiwa sana kwa kutokuwasikiliza wananchi ambao ndio wadau wakuu wa haya yanayoitwa maendeleo ya elimu. Malalamiko yalielekezwa katika mitaala yenyewe iliyoletwa kinguvu nguvu kwa msukumo wa Bosi wa Elimu wa wakati ule, Yusufu Mungai. Mitaala ambayo mtu unashindwa kuelewa hivi ilikuwa inatetea itikadi gani na kwa maslahi ya nani. Watoto wetu wakafutiwa masomo ya Historia, Uraia na Jiografia. Masomo ambayo yalikuwa yanajaribu kuwajenga moyo wa uzalendo watoto wa Kitanzania. Badala yake likaletwa somo linaloitwa Maarifa ya Jamii ambalo mumo watoto walijazwa maarifa ya mambo yanayohusiana na utandawazi na viwanda vya ulaya na mengine mengine ambayo kimsingi mtoto wa Mtanzania wa kawaida anayaona kuwa ndo