Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2009

Hongera Mzee wa Mshitu

Picha
Mwanablogu Yahya Chaharani (anayesikiliza simu) amepata Shahada ya Uzamili ya Mawasiliano ya Umma ya Chuo Kikuu cha Mt. Augustino, Mwanza. Hongera sana kwa kupiga hatua!Hapo ni katika mahafali yaliyofanyika juma lililopita. Picha kutoka blogu ya Mzee wa mshitu

Fikiri zaidi ya dini yako

Picha
Kitabu hiki nilikipata miezi michache iliyopita. Nimekisoma kwa muda mrefu na kujipatia mwanga adhimu kuhusu dini aina aina. Hapa nilipiga baadhi ya kurasa zake, kukuonesha wewe unayetamani kujua zaidi ya dini yako. Ujue kuna watu hawafikiri kabisa nje ya kiberiti cha dini zao. Kitabu hiki nilikipewa na mdogo wangu Fortunatus kama mchango wake kwenye mijadala ya dini ambayo kimsingi sikupata muda wa kuiendeleza. Upatikanaji wake sina hakika nao lakini nipatapo fursa nitawamegea kidogo kidogo wasomaji wangu.

Public victory: Tatizo letu baya

Picha
Ninaendelea kukisoma kitabu cha Stephen Covey. Nimepata changamoto ambazo idadi yake siijui. Kimsingi anachokisema mwandishi ni umuhimu wa kuanza kujitengeneza wewe mwenyewe kiasi cha kujihakikishia ushindi binafsi (private victory)ndipo ufikiri zaidi ya hapo. Tatizo la watu wengi hufanya makosa. Huanza na kutafuta ushindi wa hadharani (kukubalika, kuhusiana na wengine kwa bidii) kabla ya ushindi binafsi. Huko, kwa mujibu wa Covey ni kupoteza muda!

Ni kukosa muda ama kukosa kipaumbele?

Kimya cha blogu hii hakikutarajiwa ila huenda ni matokeo ya uzembe. Ni wazi bado sijaweza kushika mbili bila kuponyokwa na kimoja. Na nasikitika sana kwamba kinachoniponyoka mara kwa mara ni blogu. Nimekuwa nikifikiri inakuwaje huwa sikosi muda wa kula (na kwa kweli napenda kula) hata kama nimebanwa na vitu kedekede? Kwa nini 'sikosagi' muda wa kuzungumza na marafiki zangu kwa kusingizio cha kubanwa? Hitimisho likawa, huenda ni suala la kipaumbele tu na tabia ya kutokujitimizia ahadi ninazojiahidi. Kwamba inakuwa vyepesi kutimiza ahadi ya nje (na watu wengine) badala ya kutimiza ahadi niliyojiwekea na nafsi yangu. Kwamba kwa nini nisithamini ahadi na nafsi yangu kwanza, ndipo nithamini ahadi na wengine? Kwa nini mtu mwingine akinipa kazi ya kufanya ambayo nina uhakika ina maksi, ninakuwa mwepesi wa kuifanya kwa mazingira yoyote yale (hata ikibidi kujinyima mengineyo kwa uchu tu wa alama za mtihani) and yet nashindwa yale yangu binafsi yasiyo na shinikizo lolote la nje (hi

Mdoti: Mwanablogu wa kufikirisha katua

Nakumbuka miaka ya 2005 na 2006 wakati vugu vugu la blogu likiwa linashika kasi Bongo, ilikuwa ni kawaida kila siku kukutana na 'post' ya kumtambulisha mwanablogu mpya wa kiswahili kwa karibu kila blogu. Kwa sasa, kasi hiyo imepungua sana. Pengine sababu zinaweza kuwa nyingi. Shughuli zimekuwa nyingi na kadhalika. Lakini kwa kutambua umuhimu wake, naomba kumtambulisha mwanablogu mpya Ndugu Mdoti ambaye bila shaka anayo mengi ya kutufikirisha kupitia blogu yake anayoiita tufikiri. Bonyeza hapa kumtembelea mwanablogu huyu , umkaribishe. Ukiweza pia kumtambulisha kwa wasomaji wako kupitia blogu yako, itakuwa poa sana.

Katika hili Mzumbe wana kesi ya kujibu

Kwa muda sasa zimekuwepo shutma (siku hizi zinaitwa kelele nyingi) kuwa Chuo Kikuu Mzumbe kimetengeneza vihiyo wengi. Ni jambo la kusikitisha kwamba shutma hizi, kadri siku zinavyokwenda zinazidi kushika kasi kiasi kwamba sasa jambo hili limechukua ‘urasmi’ fulani hivi ambao kwa hakika si wa kupuuzwa. Juzi tu, mzalendo mmoja alikuja na maelezo yakinifu akidai kwamba kwa utafiti wake, kagundua kwamba ‘kuna matapeli’ kibao ambao wanakula kuku serikalini kwa jina la ‘Dakta’ lakini hawana lolote. Wahusika hawakutujibu (na kwa kweli sikutegemea wajibu kwa sababu) msomaji mfuatialiaji wa mambo atakubaliana nami kwamba habari hizi si za leo. Zimeanza miaka kadhaa iliyopita. Na wahusika hao wanaendelea kudunda mpaka leo. Hivi sasa unaposoma habari hizi, inasemekana baadhi ya ‘madakta’ hawa wamerudi shuleni kwao Mzumbe kurekebisha mambo kimya kimya. Huo ni ushahidi kwamba hata kama wanajidai hawasikii, lakini ‘waimeipata,’ kwamba ujambazi wao wa kitaaluma hatimaye umebainika. Hofu na mas

Tulitembea kabla hatujatambaa?

Watu wengi tunayo mengi sana tunayoyafahamu. Lakini hayo yote tunayoyajua yanakosa namna ya kutusaidia sisi wenyewe, kwa sababu tuliruka hatua muhimu katika maisha. Hatua yenyewe ni kujifahamu sisi wenyewe. Nikirudi nitafafanua.

Kitafute hiki cha Stephen R. Covey

Picha
Kitabu hiki ni kati ya vitabu ambavyo unahitaji kuvisoma kwa faida yako mwenyewe. Sitangazi biashara, natangaza maarifa ya bure ambayo huhitaji kulipia 'tuition fee' kuyapata. Kama wewe ni kati ya watu wanaopenda kuwa na mafanikio ya kikweli kweli, kitabu hiki cha Seven Habits of Highly Effective People si cha kukikosa. Nilikipata Moshi kwa Sh. 22,000.00, sijajua bei yake kwa maeneo mengine.