Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2010

Posti bora ya mwaka 2009

Kabla sijapotea kwenye blogu (kwa siku mbili tatu nne)nitakushirikisha posti bora kabisa nilizozisoma kwa mwaka mzima 2009 ambazo kwa hakika zilinipa mtazamo mpya wa mambo. Nitarudi kama Shaka Ssali anavyosema-ga "Don't go away!", naja.

Blogu bora kwa mwaka 2009!

Mwaka jana umepita kwa namna yake. Namshukuru Mwenyezi Mungu amenifikisha mwaka huu salama. Japo sikuwa hewani mwishoni mwa mwaka, lakini nimekuwa nikitafakari kidogo namna mwaka ule ulivyoenda katika maeneo kadhaa ya maisha yangu. Mafanikio kwa Matatizo. Furaha kwa huzuni. Kupanda na Kushuka. Kupiga hatua mbele katika eneo moja na kurudi nyuma kwingineko. Yote yamekuwa sehemu yangu kwa mwaka uliopita. Nimekuwa msomaji wa blogu karibu zote zilizo hai. Na kwa kweli nimejifunza maarifa mengi makubwa bila kuyagharimia. Waandishi wake waliyagawa bure na uone ilivyo ajabu, maana waliweza kujibizana na wasomaji wao kwa lengo la kupanua mjadala. Na ni hakika kwamba hivi sasa blogu zimeanza kuchukua nafasi ya magazeti na televisheni, au angalau kupambana na vyombo hivyo vikongwe. Umaarufu wa magazeti ya kununua taratibu unaanza kupotea. Katika blogu za Kiswahili jambo la tofauti hivi sasa ni maudhui aina aina yanayoandikwa. Nakumbuka miaka mitatu au minne iliyopita, karibu kila blogu ilik

Mwisho wa mwaka Singida

Picha
Hapa ni sehemu ya mji wa Singida kama ilivyokuwa Krismas ya mwaka huu. Wengine ni Bw. Albert William, mhadhiri msaidizi DUCE (huyu aliwahi kublogu hapa miaka kadhaa iliyopita, bila shaka atarejea tena. Mwingine ni mkewe Krissie, mtafiti wa bayoteknolojia, Mlimani aliyewahi kublogu hapa na kuitelekeza blogu hiyo kwa muda. Na huyo mwingine (mwenye kaki) ni kilaza, mimi.