NI UKWELI kwamba katika suala la malezi, hakuna kitu unachoweza kukiita 'the obvious'. Hakuna uzoefu. Na tunahitaji kujifunza kwa wengine. Ndivyo anavyofanya mzazi mmoja nchini Panama, Joel Silva Díaz , anayeandika uzoefu wake wa kimalezi katika blogu yake . Lengo lake ni kushirikisha wasomaje wake kile anachodhani kinaweza kuwasaida watu wenye kiu ya kujifunza. Anasema, Sikumbuki kuwa na mazungumzo ya zaidi ya mistari mitano na baba yangu. Ni miaka kumi na zaidi imepita. Kwa matukio ya hapa na pale kati yangu na baba yangu, naweza kusema tu ni kwamba angalau nilikuwa na baba. [...] Na hicho ndicho ninachotaka kukifanya vizuri zaidi, nataka kuwa baba anayefanya bila hata kutambua, nataka kuwakumbatia, kuwabusu, kuwapa fursa bora za kufanya maamuzi bora na kuwasaidia wanapokuwa hawajafanya chema, sichelewi kuwonyesha upendo na kuwajali, hata kama kuna nyakati naweza kweli kuwafinya. [...] Kama mzazi, nisingependa niwe mtu wa kuwachungulia wanangu kila baada ya ma...