Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2009

Kanuni za maumbile na ufahamu wa mwanadamu

Hewa (ambayo nayo tunaambiwa it just happened) ina mchanganyiko wa gesi mbalimbali ambazo zipo kwa uwiano maalumu. Oksjeni lazima iwe kwa asilimia kadhaa, hewa-ukaa nayo iwe asilimia kadhaa na kadhalika. Uwiano huo ukiharibika kwa nukta chache sana, lazima madhara yatokee. Hoja yangu hapa ni iweje hewa hizi ambazo tunaambiwa zilitoke-ga ziwe kwa mpangilio ambao hautakiwi kabisa kuvurugika? Kama ni kwa habari ya by chance, kwa nini itokee kwamba uwiano huo uwe namna ile tu ulivyo? Niliachana na Fizikia miaka kadhaa iliyopita pengine ningekuwa na mifano mingi katika eneo hilo. Lakini hiyo hainifanyi nisahahu kuwa mwenendo wa dunia yenyewe unaonesha kutawaliwa na nguvu ili kuu zaidi. Mfano rahisi ni namna dunia inavyozunguka kwenye mhimili wake. Hakuna kukosea. Njia ni ile ile miaka nenda miaka rudi. Kama dunia ingekuwa imetokea-ga tu basi lingekuwa jambo linalowezekana kuwa siku moja dunia ingepotea njia na kwenda kusikojulikana. Kanuni zinazoongoza mzingo wa dunia zinaonekana kuheshim

Ujuzi wa kanuni za maumbile haumkani Mungu

TUMEKWISHA kuona mifano ya upotoshaji uliofanywa na baadhi ya ‘wanasayansi’ ambao kimsingi walioongozwa na imani kuliko uhalisia. Tukaona kwa ufupi sana nafasi ya sayansi katika kutambua (sio kuvumbua) kanuni za maumbile ambazo kimsingi zilikuwepo kabla ya maarifa haya hayajakuwepo. Hapa tunaendelea pale pale kwa mifano zaidi. **************** Sayansi kwa kuzichunguza kanuni hizo, imeweza kuyabadili maisha ya mwanadamu kwa namna mbalimbali. Kwanza maarifa hayo yameweza kutusaidia kuvumbua nyenzo muhimu zilizotuwezesha kufanya mambo ambayo hapo awali hatukuwa na uwezo nayo. Pamoja na manufaa yote tuliyoyapata kwa maarifa haya ya sayansi, bado yapo maeneo ambayo kusema kweli sayansi imeharibu. Kwanza, kwa matumizi mabaya ya maarifa hayo yamefanya maisha ya viumbe yawe ya wasiwasi zaidi kuliko ilivyowahi kuwa katika kipindi cha nyuma. Kwa mfano, kwa maarifa yaliyopo, zimetengenezwa silaha ambazo kwa kweli kichaa mmoja akipandwa na hasira asubuhi moja na akakosekana wa kumdhiti anawez

Da' Subi kahamia makazi mapya

Naomba nafasi katika blogu yako kuwataarifu wasomaji kuwa tovuti ya mpya ya wavuti.com imechukua nafasi ya iliyokuwa nukta77.com na nukta77.blogspot.comNaomba yeyote aliyekuwa ameweka linki ya nukta77 aihariri na kuweka wavuti.com Karibuni sana kutembelea kwa taarifa za nafasi za masomo na kazi kwa burudani na bila kusahau habari na porojo!Asanteni.wavuti.com ************ Kuanzia sasa pata habari zote kwa kubonyeza hapa . Na kama utapenda kufanya kama nilivyofanya mimi, unaweza kujiandikisha uwe unatumiwa habari kila anapoziweka pale.

Sayansi itufunze kuwa hatujui

Ushahidi mwingine kwamba viumbe hawawezi kuwa wamebadilika kama wanavyodai mashabiki wa nadharia za Darwin upo kwenye stadi za chembechembe hai za viumbe (seli). Kisayansi, ni jambo lililo wazi kwamba msingi wa kiumbe yeyote ni seli. Seli hizi zimeundika kimfumo. (Unakumbuka tafsiri ya mfumo?) Kila seli inayo vipengele vingi vidogovidogo ambavyo hufanya kazi kubwa kuliko kiwanda chochote kinachofahamika kutengenezwa na mwanadamu. Utendaji huu unawezekana kwa sababu kila kipengele kinatengemea kipengele kingine kiasi kwamba kimoja kikiwa na hitilafu hata ndogo sana , hakuna kinachoweza kuendelea. Na hitilafu hii ndogo kwenye seli moja ikiachwa iendelee basi, hatma yake huweza kuwa ‘ugonjwa’ wa kiumbe mzima na hata janga kubwa zaidi. Ni jambo jema kwamba elimu hii ya kujua utendaji muhimu wa kiwango cha seli umewezeshwa na sayansi halisia. Uvumbuzi wa darubini ndio ulimwezesha mwanadamu kuyajua yote haya ambayo hata hivyo yalikuwepo hata kabla ya sisi kuyajua. Mawazo kwamba kiumbe ana

Evolution ni nadharia isiyo ya kisayansi

Wapo watu ambao waliweza kuitumia sayansi vibaya na kuidanganya dunia kwamba ‘maumbile’ (nature) ndio kila kitu. Kwamba kule kuyajua maumbile yanaongoza na kutawala mfumo wa ulimwengu (universe) ni sababu tosha ya kuyaamini maumbile yenyewe. [Mfumo kwa maana hii, ni uhusiano wa vipengele mbalimbali vya kimaumbile vinavyotegemeana kiasi kwamba pakitokea hitilafu katika kipengele kimoja, basi uhusiano wote unaathiriwa.] Watu hawa ni mafisadi wa kisayansi. Na wengine wao nilishajaribu kuwasema zamani kidogo kuonyesha kwamba walitumia sayansi kutuhadaa sisi tutetemekao tusikiapo neno ‘...kwa uchunguzi wa kisayansi...’ Kabla sijaenda mbali, niliseme hili mapema: Sayansi ilivyo ni maarifa ya muhimu sana. Tupo tunaoamini kwamba bila maarifa ya kweli kweli ya kisayansi, tungeishi kwenye dunia tusiyoielewa vizuri (japo hatujafika mahali pa kuielewa kwa maana halisi ya kuelewa) na wala kuelewa namna dhana mbali mbali za kimaumbile zinavyofanya kazi. Kwa hivyo, maisha yetu yangekuwa magumu s

Kwa nini UKIMWI unashika kasi Kusini mwa Jangwa la Sahara?

Hivi sasa ni wazi kwamba UKIMWI ni janga la dunia. Na kwa hakika, dunia yenyewe ni hii ya tatu hasa iliyo kusini mwa Jangwa la Sahara. Sasa hivi, tutakuwa hatujakosea sana tukisema kila familia kwa namna moja ama nyingine imeathiriwa na UKIMWI. Katika kudadisi kiini hasa cha tatizo hili hapa uswahilini, niliwahi kusikia wasomi fulani wakifikia mahali pa kuhisi (na kweli ni kuhisi) kwamba virusi vya UKIMWI vimetengenezwa na waropa kwa lengo kututeketeza sie tuliokolea rangi. Pengine hitimisho hilo lilifikiwa kwa kuangalia msambao wa gonjwa lenyewe. Kwamba tarakimu za waathirika zinaongezeka kwetu,wakati kwa wenzetu tarakimu hizo zinapungua. Hisia hizo niliziona kama jitihada za kawaida za sisi Waafrika kukimbia tatizo. Kila yanapotokea matatizo tunakuwa wa kwanza kukwepa kuwajibika na badala yake tunatafuta mchawi. Huu ni ujinga wa kawaida ambao naamini hatuwezi kuendelea kuuvumilia ikiwa kweli tunataka kuendelea. Chembechembe nyeupe tulizonazo waswahili (zinazoshambuliwa na virusi

Wingi wa siku ndio lengo lako?

Wengi wetu hufanya jitihada kubwa na kutumia muda mwingi kuhakikisha kuwa tunaishi maisha marefu. Tunaepuka kula baadhi ya vyakula na hata kufanya mazoezi si kuwa na furaha bali kuepa magonjwa fulani fulani. Lengo hasa likiwa katika kuzidisha wingi wa siku za kuishi duniani na wala si ubora wa siku hizo. Tungefanya vyema kama tungelijishughulisha kutafuta ubora wa siku chache tulizonazo ili tuweze kuziishi kwa furaha badala ya kuhangaika na kuzirefusha siku zetu ziende mbele pamoja na matatizo yake. Kilichobora si kurefusha siku ambazo zaweza kurefusha matatizo kwa upande mwingine...!

Uhai na mashaka ya chanzo chake

NILIWAHI kujadili kuhusu suala la mkinzano uliopo kati ya sayansi na dini. Sayansi siku hizi haina mvuto kwa vijana wa leo. Unahitaji kuwa mwehu kuijadili. Kimsingi, tangu zamani binadamu amekuwa akijaribu kudadisi asili yake yeye mwenyewe na viumbe wengine. Hilo limekuwa ni mjadala wa binadamu wengi. Kujua hasa ulipotokea uhai na kisa cha kuwa na viumbe wengi kiasi tukionacho leo. Suala hili limejaribu kushughulikiwa kwa njia za kiimani, ambapo wanadamu mwanzoni kabisa waliamini kuwa uhai umeasisiwa na nguvu iliyojuu ya ufahamu unaoelezeka, yaani Mungu. Wafuasi wa imani hii hawahesabiki katika sayari tunayoishi. Ni wengi hata kama si wote katika hawa wanasadiki kiukweli kweli hicho wakiaminicho. Katika hao wachache walishindwa kusaidiki kwa dhati dhana ya uumbaji, jumlisha maendeleo ya ukuaji wa maarifa yenye juhudi za kujua yanayohisiwa kujulikana, wapo binadamu ambao walianza kusita kukubaliana na ‘imani’ hii kwa madai kwamba ‘inalirahisisha mno’ suala gumu kwa maelezo ambayo

Ni wakati wa kukiasi kivuli cha ukweli…

Hutokea mtu akaishi maisha fulani duni sana lakini asijue kabisa kuwa yu duni. Wengine wetu tutakumbuka, angalau wakati ule tukiishi katika umasikini mkubwa wa familia zetu lakini hatukulifahamu hilo. Tuliishi maisha ambayo tunaamini kabisa kuwa hayo ndiyo yalikuwa yenyewe pasi hofu na mashaka. Maisha yalisonga mbele hata kama tulivaa fulana ndefu iliyosaidia kuondoa ulazima wa kuvaa kaputula. Tulipangana kitandani kila mmoja kwa welekeo wake, na bado hatukuuhisi umasikini. Umasikini wetu tulikuja kuujua baadae sana tukiisha kuwa tushahama maisha hayo kwa namna hii au ile. Tukaangalia nyuma na kujisikitikia kwamba “kweli” tulikuwa masikini. Kwa mfano huo, ukweli tulioishi nao ulikuja batilishwa na kugeuka ukweli mwingine tofauti na ule wa mwanzo. Namaanisha, kipindi kile cha umasikini usioonekana, ukweli haukuwa huu tulionao leo kwamba tulikuwa masikini siku zile. Bila shaka unanipata kwa kadiri ninavyotaka unipate, sivyo? Tafakari watu walioishi katika pango lenye giza nene mais

Tovuti bure...wahi!

Nimepata ujumbe kutoka wataalamu hawa wa kutengeneza tovuti. Hivi ndivyo wanavyosema: " Pole na kazi ya kuelimisha na kuburudisha jamii yetu. Tumekuja na huduma mpya ya BURE kwa watanzania tu tunaomba uwafahamishe. Kuzingatia umuhimu wa kuwa na tovuti, na ya kwamba ni gharama sana hapa TZ kupata tovuti, na tena watu wanafanya biashara rasmi kwa barua pepe za bure kama yahuu na giimeili, hii yote inaonesha ukosefu au gharama kubwa ya kupata tovuti. Sisi tumedhamiria kubadili uelekeo mzima wa upepo, na tumepata wasamaria wema na sasa rasmi tumefanikiwa kuleta ufumbuzi na neema kwa waTZ kwa suala la tovuti na anuani rasmi za barua pepe. Na sasa kwa awamu ya kwanza kwa kuanzia tu, WATU 100 WATATENGENEZEWA TOVUTI BURE. Watu 100 kwa maana ya mtu binafsi, kampuni, biashara, shirika, asasi zisizochukua faida (NGO), kikundi, duka, mjasiriamali, saluni, shule ama Saccos n.k. BASI KILA ALIYEDHAMIRIA KUWA NA WEBSITE/TOVUTI ajiunge na utaratibu huu wetu atengenezewe TOVUTI MOJA

Salamu kwako mwanablogu mpenzi

Ni mwaka unakimbia ama ni sisi tunakimbia? Masaa yanakwenda. Majuma yanayakatika. Mwaka huo unayoyomea. Bila kukaa sawa, mtu unajikuta mwaka umekatika ukikuacha unashangaa. Kazi ipo. Mwezi wa kumi huu! Nimeandika kukusalimu ewe mwanablogu. Mie sijambo, nakula asali na maziwa yake kwenye nchi ya ahadi. Ni bukheri wa afya njema.