Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2008

Kwenda mbele kunahitaji kugeuka nyuma?

Ningependa leo tuone ikiwa inatulazimu kuikumbuka jana ili kuweza kuendea kesho. Maana yapo mawazo kwamba ili tuweze kwenda mbele kwa ufanisi, ni vyema kugeuka nyuma kutathmini tulikotoka. Kwamba ni kwa kutumia historia twaweza kubashiri mwelekeo wetu. Tunaambiwa historia hutuelimisha kuhusu mwenendo wetu na namna mwenendo huo ulivyoweza kutufikisha hapa tulipo. Ni kwa kutumia historia hiyo, inasemwa, twaweza kupata maarifa yatakayotusaidia kujikosoa ama kujizatiti kwa faida ya kesho na kuendelea. Wenye mtazamo huu, wanaamini katika nguvu ya historia katika maisha ya mwanadamu. Kwamba maisha yajayo, hayana miujiza. Ni mwendelezo wa mambo yale yale kwa namna isiyotofautiana sana na haya tunayoyajua. Kwamba maisha yatarajiwayo ni kama mwendelezo wa tamthilia ndefu yenye vipande vingi. Vipande hivi vinategemeana. Tukio la kipande kimoja cha tamthlia, hutupa bashiri ya simulizi za vipande vinavyofuata –pamoja na kwamba badiliko dogo laweza kutokea. Katika kujaribu kutanabaisha hiki

Je,nini hasa kinachoongoza mwenendo na tabia yako?

Umewahi kufikiri ni kitu gani hasa kinachoyaongoza maisha yako na namna unavyotekeleza matakwa yako? Kitu gani hasa ambacho ndicho unachoweza kukitaja kwa hakika kwamba ndicho kinachokuongoza. Je, ni mafundisho ya dini yako? Je, ni mtizamo wa watu wanaokuzunguka pamoja na utamaduni wao? Je, ni mambo unayojifunza kwa kuyasoma ama kutazama? Je, ni mtizamo wako/falsafa binafsi? Au ni kitu usichokijua? Nauliza tu. Jielewe.

Kitabu kipya, nimekipata Book Point Arusha jana

Picha
Kitabu kizuri kimeandikwa na Marshall Goldsmith. Kitafute ukisome, kitakufaa.

Kwanini watu huwasema vibaya wenzao?

Binadamu wengi hatupendi tusemwe vibaya. Tunajisikia kuvunjika moyo tunapohisi kuwa yupo mwenzetu anaona fahari kuyasema mapungufu yetu bila staha. Kama wewe si mmoja wapo samahani. Wenzako ndivyo walivyo. Sababu ni kwamba binadamu tunapenda kuonekana wa thamani hata kama mara nyingine thamani hiyo tunayoidai hatunayo. Tunalo hitaji la kuona kuwa wengine wanatuheshimu, kututhamini na kuwa na maoni chanya kutuhusu. Kinachotofautiana, ni kiwango. Hebu fikiria. Mfanyakazi mwenzako anakujia na kuuponda utendaji wako wa kazi uso bin uso. Bila adabu. Bila staha. Ama mwenzi wako anakukosoa mbele za watu kuhusu mambo ambayo yanawahusu ninyi wawili. Ama mkuu wako wa kazi anapokuhamakia kikaoni. Ama rafiki yako anakusemea mbovu mtaani. Kwa wengi wetu, japo katika viwango tofauti, itauma. Sasa ni hivi: Hivyo unavyojisikia ndivyo binadamu wengine wanavyojisikia ukiwaponda. Ni ajabu na kweli. Sisi hawahawa, tunaodai heshima kwa nguvu, ndio hao hao tunaoona raha kuwashushia wenzetu thama

"True confension', mhalifu anapokiri kosa

Picha
Jana nilipita hapa nikakumbuka enzi hizo. Sikumbuki ni idadi gani ya vitabu "nilivichomoa" humu. Enzi hizo nilikuwa mteja wa kudumu humu. Nilikesha ndani ya jengo hili wakati huo wenzangu wakifanya mambo mengine mitaani.

Hasira ina maana gani kwetu?

Hasira si kitu kigeni. Kama hujawahi kuwa na hasira maishani mwako, basi bila shaka mwenzetu unacho kitu fulani ambacho binadamu wenzako wote hawanacho (kasoro?). Hasira ni jambo la kawaida kututokea sisi kama binadamu. Waweza kusababishiwa hasira na watu wengine, vitu ama wewe mwenyewe ukajikasirisha. Bila kujali chanzo chake, ukichunguza vyema utaona ya kwamba karibu mazingira yote yaliwahi kukusababishia hasira yanafanana –fanana kimsingi. Yaani kila jambo fulani akilini mwako lilipoguswa, uliwaka moto kwa hasira. Ulifura. Sasa ningependa tujiulize: Hasira hasa ni nini na ina maana gani kwetu? Inahusianaje na namna tunavyojifikiria? Pengine sijielezi ninavyotaka. Hebu tujaribu hivi: Je, kuna tofauti gani ya kujifikiria wewe mwenyewe kama wewe kabla na wakati wa hasira? Je, kuna tofauti gani ya kuwafikiria wengine (wanaotusababishia hasira) kabla na wakati wa hasira? Je, kwa nini kuna watu hasira huyeyuka kirahisi ilhali wengine hasira ikiacha makovu ya kudumu? Hasira ni kipimo

Ajira milioni moja zilizoahidiwa ndio hizi?

Picha
Hawa ni "waajiriwa" wa Segera. Bila shaka wameingizwa katika kitabu cha ajira. Takwimu mpo? Hapa ni Chalinze. Mkakati wa zile ajira milioni moja umewafikia vijana hawa pia.

Siku nilipokutana na Ojano Kimara

Nakata mitaa Posta mpya. Ni alasiri. Ninakumbuka ahadi ya kwenda kwa rafiki yangu Ojano, Kimara Baruti. Foleni ndefu. Jumlisha joto. Uchovu. Basi nakata tamaa ya kutimiza ahadi yangu hiyo. Ni saa kumi na dakika tano. Ojano anataka kufufua blogu yake. Alianza kublogu miaka miwili iliyopita, bahati mbaya akapumzika bila kuaga. Ni masomo yalipunguza kasi yake hatimaye, yakamnyamazisha kimojaa. Hivi sasa anayo ari ya “kuzaliwa upya”. Anatamani kuanza ukurasa mpya. Ni mawazo hayo yananipa nguvu ya kuingia kwenye ki-haisi. Huyooo naenda Kimara Baruti kumrudusha Ojano kundini. Nyumbani kwake sikujui. Ameahidi kunifuata kituoni. “Vipi umefika wapi?” Ananiuliza. Saa zimeenda. Imekuwa saa kumi na moja na nusu Ubungo kwenyewe sijafika. “Niko njiani…foleni inanichelewesha”. Jiji halifai siku hizi. Idadi ya magari inazidi idadi ya watu. Barabara ni finyu mno. Maelfu ya dakika yanapotelea barabarani kila siku. Siku hizi imekuwa ni sababu tosha ya kujitetea unapochelewa mahali. Urefu wa folen