Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Tabia

Ukiigiza Ukatili, Unakaribisha Tabia ya Ukatili

Picha
Kuna wakati unaweza kufikiri unaigiza msimamo na kejeli kwa maumivu ya mtu, unakuwa na maoni yasiyo na haya kwa mateso ya wenzako ukijua unawafurahisha watu fulani lakini hayo maigizo ya kukosa huruma kwa mwenzako yana uwezekano wa kugeuka tabia kweli na ukawa mtu katili kweli kweli. Michezo, dini na siasa visikuchochee kujiona una haki ya kubeza masaibu wanayopitia wenzako kwa sababu mdogo mdogo mizaha hugeuka ukweli.   Mwaka 1971, Philip Zimbardo, mshunuzi na mwalimu wa Chuo Kikuu cha Stanford, alifanya utafiti maarufu kama  #StanfordPrisonExperiment  akilenga kuchunguza nguvu ya mazingira kwenye tabia.    Utafiti ulivyofanyika   Zimbardo alitengeneza gereza la kuigiza hapo chuoni likiwa na seli, mahali mfungwa angekaa mwenyewe, mahali pa wanyarapa kuishi, mahali wafungwa wangetoka na kuteswa na wanyapara. Washiriki walifanyiwa mchujo wa haiba kuona kama ni watu wenye utimamu wa tabia na hisia.    Kwa njia ya nasibu (random assignment) wanafunzi...

Tabia za Mamlaka kwa Wanyonge Zinavyoweza Kuzalisha Uovu

Picha
Umewahi kujiuliza kwa nini watu huweza kupokea na kutekeleza amri hata zile wanazoamini ni kinyume cha maadili, utu na dhamiri zao? Kwa nini mtu anaweza kuambiwa ‘fanya kitu cha kikatili’ na akatii hata kama amri hiyo inamaanisha mtu kuumia na hata kufa?    Mwanzoni mwa miaka ya 1960, Stanley Milgram wa Chuo Kikuu cha Yale alifanya utafiti maarufu kwa jina la  #TheMilgramExperiment . Milgram alitaka kuangalia nini hasa kinachangia mtu kutii mamlaka hata katika mazingira ambayo utii huo unaweza kusababisha madhara kwa binadamu mwenzake.    Kwa lugha nyingine, nini hasa kilifanya watu kama Hitler waliofahamika wazi ni wakatili wawe na wafuasi waaminifu wanaotekeleza maagizo yao kuumiza watu, kutesa na hata kuwaua?   Utafiti ulivyofanyika   Washiriki wa utafiti huo waliaminishwa wanashiriki utafiti wa kuangalia uhusiajo wa kumbukumbu na ujifunzaji na wao wanashiriki kama ‘walimu.’ Jukumu lao lilikuwa ni kusoma swali na kufanya maamuzi ya kumuadhibu mwanaf...