Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Saikojia Tumizi

Mambo Yanayokuza Motisha kwa Wafanyakazi

Picha
Pengine umewahi kufanya kitu kwa sababu tu ulilazimika kukifanya. Moyoni hukusikia msukumo wowote isipokuwa hofu ya kushindwa kufikia matarajio ya mtu mwingine. Lakini pia inawezekana umewahi kufanya kitu bila kusukumwa wala kufuatiliwa. Ndani yako unakuwa na furaha na msukumo unaokuhamasisha kutekeleza jambo si kwa sababu ya hofu iliyotengenezwa na wengine bali shauku ya kufikia kiwango kinachokupa kuridhika.

Jifunze Namna Bora ya Kumzawadia Mwanao

Picha
Watoto wanapenda zawadi. Namna watoto wanavyochukulia zawadi inabadilika kulingana na umri. Katika umri mdogo, mtoto huchukulia zawadi kama haki ya kupata kila akipendacho kwa wakati wowote. Mzazi anaporudi nyumbani jioni, kwa mfano, watoto hutarajia pipi bila kufanya chochote. Lakini kadri mtoto anapoendelea kukua, mtazamo wa zawadi kama haki hupungua. Mtoto huanza kufikiria zawadi kama matokeo ya kufanya kile kinachotarajiwa na mzazi. Mtoto anapofaulu mtihani, mathalani, anatarajia kitu. Unapompa kile anachokitarajia, anajenga hamasa na motisha ya kutia bidii zaidi masomoni.  

Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Anayefanya Vibaya Shuleni

Picha
Si jambo la kufurahisha kwa mzazi unapoona mtoto hajafanya vizuri masomoni. Unapofahamu kuwa maendeleo ya mwanao si kama vile ulivyotarajia, ni rahisi kupatwa na simanzi, wasiwasi na hasira. Ni dhahiri mzazi unatamani mtoto awe na mustakabali mzuri kimaisha. Matumaini hayo yanakufanya uchukulie kushindwa kwake masomo kama kiashiria cha kuharibika kwa maisha yake ya baadae. Hakuna mzazi angependa mtoto awe na maisha yasiyoeleweka.

Mbinu Sita za Kukumbuka Maarifa Unayojifunza

Picha
Mafanikio ya kitaaluma, kwa kiasi kikubwa, yanategemea namna unavyoweza kusoma na kukumbuka kile ulichokisoma. Kusoma kwa bidii na kuelewa unayoyasoma ni muhimu. Lakini kama huwezi kukumbuka ulichokielewa, itakuwa vigumu kufanikiwa. Mitihani, kwa mfano, hupima uwezo wako wa kukumbuka kile unachokijua. Hiyo, hata hivyo, haimaanishi uishie kukumbuka. Unahitaji kuelewa unayojifunza kwa kina lakini pia uwe na uwezo wa kukumbuka.

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke -2

Picha
Katika makala iliyopita , tuliona kuwa mwanamke anahitaji kujua anavyopendwa na mwenzi wake kwa maneno na vitendo. Kadhalika, tuliona mwanamke anatamani kuwa na uhakika wa nafasi ya kwanza kwa mwenzi wake. Hatamani kuona akishindana kwa umuhimu na chochote kile kinachoweza kuchukua nafasi yake kwa mwenzi wake.

Mambo Yanayoweza Kugusa Moyo wa Mwanamke-1

Picha
WANAUME wengi wanaamini wanawake, kwa kawaida, ‘wanapenda hela.’ Kwamba ukiweza kumhakikishia mwanamke 'uhakika wa kiuchumi' unakuwa umemaliza. Ingawa hatuwezi kupuuza ukweli kuwa uhakika wa 'kiuchumi' ni moja wapo ya mahitaji ya mwanamke, lakini si sahihi kuamini kuwa moyo wa mwanamke unaweza kuthamanishwa kwa fedha. Fikra hizi walizonazo wanaume [kuwa anachokihitaji mwanamke ni fedha] zimeleta matatizo mengi katika mahusiano na ndoa. Kwa mfano, wapo wanaume ambao baada ya kuhakikisha wenzi wao wamepata mahitaji ya msingi, basi wanawatelekeza kihisia. Hali hii husababisha upweke mkubwa kwa wanawake hawa wanaojikuta hawana mtu wa karibu kuwasikiliza isipokuwa vitu.

Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Aweze Kushirikiana na Wenzake

Picha
Kushirikiana ni uwezo wa mtoto kuelewa watu wengine wanatarajia nini kwake. Mtoto mwenye ushirikiano na watu, ni mwepesi kutoa alichonacho, ni msikivu, hufanya kazi na wenzake, hucheza kwa ushirikiano na wenzake na huwa na uwezo wa kutafuta suluhu pale anapojikuta katika mazingira ya ugomvi.

Jinsi ya Kumfundisha Mtoto Kuwa Mwuungwana

Picha
Umewahi kumpa mtu kitu anachokihitaji lakini haoni sababu ya kusema, ‘asante’? Mtu anakukosea na hawezi kusema, ‘samahani’, ‘nisamehe’? Wapo wengine hata ufanye vizuri namna gani kusema, ‘hongera umefanya vizuri’ ni kama adhabu na kujishushia hadhi. Hizi ni baadhi ya tabia zinazoweza kuonesha namna mtu asivyo muungwana na zinaweza kumpunguzia thamani yake mbele ya jamii.

Mambo ya Manne ya Kufanya Mtoto Akusikilize, Akuheshimu

Picha
Msomaji mmoja wa safu hii aliniandikia hivi majuzi akidai mwanae hamsikilizi. Kwa mujibu wa mzazi huyu, pamoja na kufanya jitihada za kumwelekeza mwanae mambo muhimu ya kimaisha, bado kijana wake huyo haonekani kusikiliza. Anasema, kadri anavyomwadhibu mwanae, ‘ndivyo anavyozidi kuwa mkaidi…’ Mzazi huyu, inavyoonekana, amepoteza mamlaka yake kama mzazi. Mamlaka kimsingi ni uwezo wa kusema kitu na kikasikika bila kulazimika kutoa adhabu. Unapokuwa na mamlaka maana yake unayo nguvu ya ushawishi inayomfanya mtoto awe tayari kukuiga, kukusikiliza, kukuelewa na kufanya kwa hiari yake yale unayomwelekeza.

Kanuni za Kuongeza Ushawishi wa Hoja Zako

Picha
Kwa nyakati tofauti kila mmoja wetu hutamani kuwa na ushawishi kwa wengine. Ni kawaida, kwa mfano, kutamani hoja tunazozitoa zipokelewe na wale tunaowatumia ujumbe husika. Ili ujumbe upokelewe, inahitajika nguvu inayoweza kuwasukuma wengine kuupenda, kuubali na ikiwezekana kubadilika kwa sababu ya ujumbe husika. Nguvu hii inaitwa ushawishi.

Umuhimu wa Kujenga Tabia ya Kujitolea

Picha
Kujitolea ni kutoa sehemu ya muda wako, ujuzi na maarifa uliyonayo na wakati mwingine nguvu zako kufanya kazi ya watu wengine bila kupata malipo ya moja kwa moja. Kazi unayoifanya kwa kujitolea mara nyingi ungeweza kuifanya kwa kudai ujira lakini unaamua kuifanya bure.  Mathalani, mwajiriwa anayetamani kuleta mabadiliko nje ya ajira yake, anapotumia ujuzi wake kufanya kazi za jamii bila kudai malipo, anakuwa amejitolea. Tuangalie kwa mhutasari kwa nini ni muhimu kujenga tabia ya kujitolea.

Kipimo cha Kujitambua ni Tunavyowatendea Tusiowajua, Wasioheshimika

Picha
Mjema anaandika ripoti inayohitajiwa na mkuu wake wa kazi. Wakati muda wa kukabidhi ripoti hiyo ukikaribia, anapigiwa simu na mtu asiyemfahamu. Mjema hajui ni nani hasa anayemtafuta muda huo hivyo anaamua kupokea simu. Bahati mbaya aliyempigia simu hasikiki vyema. Mjema anahisi labda ni tatizo la mtandao, anaamua kuikata mara moja.

Kujitambua ni Kushinda Ubinafsi, Kujali Mahitaji ya Wengine?

Picha
Tulianza kudodosa suala la kujielewa katika makala yaliyopita . Kama tulivyodokeza, kujielewa kunakwenda sambamba na kuelewa msukumo ulio nyuma ya yale tuyatendayo kila siku. Katika sehemu hii, tutaangalia kwa ufupi kwa nini kujitambua ni zaidi ya ule ‘ubinafsi’ unaoishi ndani yetu.

Tuyafanyayo ni Matokeo ya Tujionavyo

Picha
Ungeulizwa swali, ‘wewe ni nani’ ungejibuje? Wengi tungetaja majina yetu kwa kuamini ‘sisi’ ni majina yetu. Wengine tungetaja kazi zetu kwa sababu kwetu majukumu ndio utambulisho wetu. Sisi ni nani basi? Kwa hakika swali hili si jepesi lakini linatuwezesha kuelewa tabia zetu. Karibu kila tunachofanya ni matokeo ya vile tujionavyo. Katika makala haya, tutaangazia  mitazamo michache inayoweza kutusaidia kutafakari swali hilo. 

Mazingira Manne ya Kimalezi Yanayotengeneza Tabia za Watoto

Picha
Watafiti wa makuzi na malezi wanasema mtoto anahitaji mazingira yanayomchangamsha kihisia, kiakili, kimwili na kimahusiano. Anapochangamshwa vyema, tunaambiwa, mtoto hujisikia utulivu wa moyo unaomfanya awe karibu na wazazi na watu wengine wanaomzunguka. Anapokosa kuchangamshwa, mtoto hujenga uduwavu unaojenga tabia za kujilinda na uchungu wa kujiona anapuuzwa. Katika makala haya, tunaangazia mambo manne yanayoweza kumchangamsha mtoto kihisia na kimahusiano na hivyo kutengeneza tabia na mitazamo yake.

Kuanza Kupotea kwa Desturi ya Ukaribu wa Kifamilia Kunavyoathiri Malezi

Picha
Malezi katika mazingira yetu ya ki-Afrika ni suala nyeti. Kwa kutambua umuhimu wa malezi katika kujenga jamii yenye ustawi, wa-Afrika tumekuwa na desturi ya kuelekeza nguvu zetu nyingi katika malezi ya wanetu. Kwa mfano, tangu mtoto anazaliwa, ilikuwa ni lazima alale kitanda kimoja na wazazi wake kwa muda unaozidi miaka miwili. Mtoto mchanga hakuachwa alale kwenye kitanda chake mapema kwa sababu za msingi zilizokubalika katika jamii zetu.

Madikteta wa Familia Tunaweza Kudai Demokrasia?

Picha
Madai kuwa baadhi ya watawala wetu wa ki-Afrika ni madikteta hayashangazi. Inasemekana watawala hawa  hawasikilizi maoni ya watu wanaowaongoza, hawashauriki wakati mwingine na watu walioteuliwa kuwashauri, wanaminya uhuru wa maoni/kujieleza na kadhalika. Madai haya yanaonekana kuwa ni matamanio ya wananchi kuwa na serikali zinazoheshimu demokrasia -nguvu ya wananchi kushiriki katika uongozi/utawala wa taifa lao kwa kuamua utaratibu gani utatumika kujitawala na nani anaweza kupewa jukumu la kuwaongoza. Haya yote yanadai ushirikishwaji wa wananchi kwa kukuza uhuru wa kila raia kusema/kutoa maoni na kadhalika.

Unaanzisha mahusiano ya ndoa/mapenzi?

Picha
MAZUNGUMZO mengi yanayohusu maandalizi ya ndoa hujikita katika kufanikisha tukio la siku ya harusi. Na wakati mwingine wanaojiandaa kwa ndoa huandaliwa siku chache sana kabla ya tukio hilo. Kwa ujumla, suala la ndoa limerahisishwa kiasi cha kuonekana kuwa yeyote anaweza kukabiliana nalo kwa uzoefu pasipo maandalizi ya kutosha. Hata hivyo, pamoja na wepesi wa maandalizi halisi, na msisitizo uliowekwa na jamii katika 'siku ya harusi', ndoa nyingi huishia kwenye migogoro mingi muda mfupi baada ya tukio la harusi.

Muhtasari na Hitimisho, 'Kanuni zinazoongoza mahusiano na migogoro ya wanandoa'

Picha
TANGU tulipoanza mfululizo wa makala za mahusiano , jambo kubwa nililojaribu kulionesha ni nafasi ya mahitaji ya hisia katika kuimarisha au kuvuruga mahusiano. Na msingi wa haya yote ni kusema kwamba mahusiano hayana miujiza. Mahusiano yanaongozwa na kanuni za kawaida sana ambazo ukifanikiwa kuzitambua na kuzitumia utapunguza kama sio kuondoa matatizo mengi. Kwa mhutasari, ningependa tuyapitie mambo makuu yaliyojitokeza katika mjadala wetu kwa kuyaweka katika makala moja inayojitegemea.

Dhana ya 'mapenzi' kwa mtazamo wa kisaikolojia

Picha
Makala haya yanasaili namna mtazamo wa awali wa watu wanaoamua kuingia katika uhusiano wa kimapenzi unavyoweza kuathiri kwa kiasi kikubwa namna wawili hao watakavyohusiana. Na tunaonesha namna kiwango cha mapenzi kati yao kinatengemea masuala matatu makuu; Ukaribu wa kihisia, tamaa ya mwili na maamuzi yao.